Naona ipo siku nitaiacha hii kazi ya ualimu ni wakati Sasa wa Kutengeneza mifumo

Naona ipo siku nitaiacha hii kazi ya ualimu ni wakati Sasa wa Kutengeneza mifumo

Pole sana Mwalimu.
Umelaumu sana uongozi wako lakini inaelekea hujui namna ya kujitoa kwenye chama chako. Epuka sana lawama. Ungeeleweka sana kama ungeomba kujua utaratibu wa namna ya kujitoa kwenye chama cha wafanyakazi mf. CWT.
Walimu msijishushe sana hadi mkaeleweka vibaya. Tunawategemea sana sanaaa, nyinyi ni watu muhimu sana katika jamii

Ukitaka kujitoa fanya hivi:
Andika notisi ya siku 30 kwa DED ukimtaarifu kuwa unatarajia kujitoa CWT; nakala peleka kwa Katibu CWT wilayani kwako.
Baada ya siku 30 makato ya 2% yatasitishwa.
Then ukitaka kujiunga na chama kingine utajaza fomu maalum baada ya kuelimishwa. Ukiridhika nao mwandikie DED wako ukimtaarifu kuwa akate kiasi fulani kwenye mshahara wako kwenda chama kipya. Ambatisha hiyo fomu.
Fanya hivyo Mwalimu,ni haki yako.
Lakini ni vizuri chama ndicho nikufuate kukubembeleza.
Sorry, huu si uzi mpya. Namtetea mwalimu wetu.
 
Pole sana Mwalimu.
Umelaumu sana uongozi wako lakini inaelekea hujui namna ya kujitoa kwenye chama chako. Epuka sana lawama. Ungeeleweka sana kama ungeomba kujua utaratibu wa namna ya kujitoa kwenye chama cha wafanyakazi mf. CWT.
Walimu msijishushe sana hadi mkaeleweka vibaya. Tunawategemea sana sanaaa, nyinyi ni watu muhimu sana katika jamii

Ukitaka kujitoa fanya hivi:
Andika notisi ya siku 30 kwa DED ukimtaarifu kuwa unatarajia kujitoa CWT; nakala peleka kwa Katibu CWT wilayani kwako.
Baada ya siku 30 makato ya 2% yatasitishwa.
Then ukitaka kujiunga na chama kingine utajaza fomu maalum baada ya kuelimishwa. Ukiridhika nao mwandikie DED wako ukimtaarifu kuwa akate kiasi fulani kwenye mshahara wako kwenda chama kipya. Ambatisha hiyo fomu.
Fanya hivyo Mwalimu,ni haki yako.
Lakini ni vizuri chama ndicho nikufuate kukubembeleza.
Sorry, huu si uzi mpya. Namtetea mwalimu wetu.
Asante.

Nilifanya hivyo mwaka Huu mwezi wa pili, niliandika barua ya kumtaarifu DED kujiondoa uanachama wa CWT nakala nyingine nikapeleka kwa karibu CWT wilaya (copy zote ninazo), Nikaandika barua nyingine ya kujiunga na chakuhawata ambapo wamenikata kwa muda Sasa, Lakini Cha kushangaza mwezi uliopita nikaona makato ya CWT (chama ambacho nilishajiondoa kabla)..kitendo Cha kwenda kufatilia na kuuliza kwanini nimekatwa chama ambacho nilishajiondoa na fomu nilimuachia katibu wa CWT? Ndio naona danadana zikipigwa, mkuu wa idara utumishi ananiambia niende CWT waniandikie kwamba nimeshajitoa, CWT wanasema wenyewe hawawezi kuniandikia nirudi utumishi ndio wenye uwezo wa kunitoa.
 
Fikiria hupo chama Cha chakuhawata alafu inatokea tu chama kingine (CWT) wanapitisha makato yako na umeshajitoa, Unaenda kwa afsa utumishi ( Hapo umeshamtafuta mwezi mzima hayupo ofsini) anakujibu short tu kwa dharau kwamba nenda huko CWT wakuandikie kwamba wewe sio Mwanachama wao uniletee hapa nikutoe, anasema hivyo anajua fika wewe kwenda CWT sio jukumu lako maana huo ni mshahara wako sio wa CWT na anajua fika kwamba CWT hawawezi kukusaidia kitu, unaenda huko CWT hawakupi ushiriakiano wowote, unarudi kwa afsa utumishi anakujibu Sasa "Mimi nifanyaje/nikusaidiaje?"

Unarudi shuleni na mawazo. Nafundisha physics na Mathematics form one mpaka form four, nitapata morale ya kufanya kazi? Itoke wapi? Mimi ni mtaaluma majukumu ya kitaaluma nitayatimizaje huku nikiwa na mawazo?

Dharau! Dharau! Dharau sio kitu kizuri, ukimletea mtu dharau sehemu ambayo anaona ni haki yake basi jiandae kuchukua matokeo ya dharau. Huyo Afsa utumishi anadharau kwa sababu Sina power,Sina hela na Sina heshima ndio ni ukweli, Ukiwa maskini lazima udharililike tu. Mshahara wa kwangu Mimi ndio na mamlaka nijiunge chama a au b, mtu anakataa kukuondoa kwa faida gani? Yeye anafaidika kwa lipi mtumishi kukatwa vyama viwili?

Walimu wanapambana sana kazi wanazozifanya ni nyingi mnoo, hawana allowance zozote, wanakaa Shule mpaka saa 11:30 jioni kwa malipo ya elfu 3-6 (remidial) yote ni kwa ajili ya kutimiza majukumu yao, ni sawa hatuna shida na hizo allowance tumeshakubali, Lakini? Wapeni malimbikizo yao ya mishahara (mshahara wangu wa kwanza sijawahi kulipwa Hadi Leo), Wapande madaraja kwa wakati, wakienda huko halmashauri/manispaa na matatizo yao wajibiwe kwa staha na ustaarabu maana huko halmashauri ndio sehemu pekee ya kutatuliwa changamoto, Lakini ajabu ni kwamba walio kwenye position ya kukusaidia hawakusaidii (hawaoni umuhimu wa kukusaidia) kumbuka hata hao Ma-afsa utumishi walikua walimu kabla wakaenda kujiendeleza.

Nimegundua huku ni changamoto kwakweli na Sioni kama nitakuepo kwa muda huku, hiki kijiti nitawaachia wengine wakikimbize na kulijenga taifa. Lakini WAJUE walimu wote sio fairule, tulifaulu vizuri form six tumezaliwa kwenye umaskini mkubwa sana tumekimbilia huku atleast tuanze kujitegemea mapema. Sasa ni wakati wa kuandaa mifumo kwa hasira kubwa na umakini mkubwa hata hiyo siku ikifika isiwe majuto bali ni ushindi.
Wewe kama unataka kuacha ualimu ni vizuri uache, sasa hapa unampigia kelele nani? Ulivyoandika humu ni pumba na ujinga mtupu! Kama hutaki kazi ya ualimu ondoka haraka sana kwani nani alikuingiza kwenye kazi hiyo!
 
Asante.

Nilifanya hivyo mwaka Huu mwezi wa pili, niliandika barua ya kumtaarifu DED kujiondoa uanachama wa CWT nakala nyingine nikapeleka kwa karibu CWT wilaya (copy zote ninazo), Nikaandika barua nyingine ya kujiunga na chakuhawata ambapo wamenikata kwa muda Sasa, Lakini Cha kushangaza mwezi uliopita nikaona makato ya CWT (chama ambacho nilishajiondoa kabla)..kitendo Cha kwenda kufatilia na kuuliza kwanini nimekatwa chama ambacho nilishajiondoa na fomu nilimuachia katibu wa CWT? Ndio naona danadana zikipigwa, mkuu wa idara utumishi ananiambia niende CWT waniandikie kwamba nimeshajitoa, CWT wanasema wenyewe hawawezi kuniandikia nirudi utumishi ndio wenye uwezo wa kunitoa.
Muone Afisautunishi wa walimu,Katibu wa TSC wilaya yako.
Mueleze kila kitu,yataisha.
 
Jaribu kutumia mamalaka nyingine pia kupata haki yako. Unaweza kwenda hata kwa viongozi wa kisiasa kama Mkuu wa Wilaya na mbunge wa eneo husika, naamini watakusaidia kutatua changamoto unayoipitia
Hakuna wa kukusaidia kwenye hii Dunia isipokuwa ni wewe mwenyewe, aache kazi akapambane kitaa atatoboa tu. Kazi ya ualimu ya kisenge sana
 
We unataka kuacha kazi kwa hasira? Utatoka apo utaenda kujinyonga bure maana mawazo mengi yatakujaa, utaanza kuwategemea watu na kuona ni wabaya,

Sikia Hiko kidgo unachokipata Kuna watu hawana kbsaa, na Kuna wengine wanapata kama wewe na Bado wanafurahia maisha,
Life is not always sweet, Kuna vingine vichungu hata kama ungekua mbunge au rais , shubiri ipo,
We si unasema huna kazi Kuna mwl wa s/m haja ajiriwa 6yr now,

Hapa ni Tz sio ULAYA Wala sio mbinguni
so dance according to the beat , wakipigia lege cheza lege wakiweka buzuki pita nalo,

Makasiliko hayajawahi muacha mtu salama kila sector Ina udhaifu ,

Acha kazi kama umeanzisha shule yako au ushajitengenezea sehem for the purpose to employee your self lakin sio kwa hasira hizo hutavuna kitu,
Nyie ndo walimu waoga waoga, ukienda jinga jinga lina miaka Sita linasubiri kuajiriwa hilo ni jalimu pumbavu lisilojitambua. Walimu wote wana kasoro kubwa sana kwenye ubongo
 
Unarudi shuleni na mawazo. Nafundisha physics na Mathematics form one mpaka form four, nitapata morale ya kufanya kazi? Itoke wapi? Mimi ni mtaaluma majukumu ya kitaaluma nitayatimizaje huku nikiwa na mawazo?
Pole sana, Ndugu. Weka mipango na mikakati, utafanikiwa nje ya ajira ya Ualimu.
-
Nimepita huko, nafahamu na naelewa unachopitia.
 
Back
Top Bottom