Naona wazazi wangu wamenichoka, ni muda sasa nami nianze kujitegemea

Naona wazazi wangu wamenichoka, ni muda sasa nami nianze kujitegemea

Boom linakuchanganya dogo.
Wazazi hawapendezwi na tabia zako tangu umeanza chuo.
Vijana wa kariba yako huwa ni jeuri msiopenda kukosolewa(wasomi uchwara), kuna kazi mnahisi mnadhalilishwa, mahisi mmekua hivyo mzazi hapaswi kukukoromea( elewa kua baadhi ya wazaz mtoto hata awe na 50 yrs kwao bado ni mtoto tu)..

Timiza majukumu uliyopangiwa, bado upo kwao fuata yanayokupasa, jeuri haitokusaidia.

Maisha yakikukaba koo huko ulikopanga, utaandika uzi kua wazazi wako hawakujali.

Kama unaenda kupanga basi kapange mkiwa na hali nzuri wewe na wazee wako. Waambie mpango wako wa kupanga ukiwa tayari umejirekebisha.
Comment bora kabisa...dogo anajiona kakua, anadanganywa na kadegree uchwara...aje kitaa sasa maji ataita mmaaa
 
Mara nyingi ukiaanza kukua utaanza kuona kama wazazi wanakunyanyasa.
Lakini kuna siku utaelewa kuwa wazazi walikuwa hawakunyanyasi na wala hawana nia mbaya na wewe. Bali wanakuweka katika mstari ulionyooka
 
Nazania ni wakati sahihi wa yeye kujitegemea sasa,
Ila anatakiwa aondoke nyumbani vizuri,na asikate tamaa kabisa,siku akikwama aweze rudi na wakampokea(asiweke akilini mentality ya kurudi ama kushindwa,ikifika hatua amerudi imebidi na hamna namna tena,ila kwa changamoto ndogo ndogo apambane nazo,anatakiwa awathibitishie wazazi wazo lake la kujitegemea ni sahihi,mana ukirudi tena home na huna kitu hali itakuwa mbaya zaidi ya mwanzo)

Sijui lakin kama ananielewa.
Mimi nimekuelewa vizuri tu mkuu kuaga ni nitaaga vizuri bila shida. Ila huko niendako naimani Mungu atanipigania
 
Nimecheka sana unaposema eti umemvumilia sana. [emoji28][emoji28][emoji28]

Mpaka umri huo, nani kamvumilia mwenzie sana?. Narudia kukwambia mdogo wangu, nyumbani hutakiwi kuondoka kwa hasira. Na siku utakayoamua kuondoka, make sure umejipanga, wahenga waliposema "Ukitaka kuruka, Agana na nyonga" walikuwa na maana yao kubwa sana.

At 21, bado sana mdogo wangu. Tena kibongo bongo ndio kabisaaa. Tumia hizo hasira ulizo nazo kujipanga namna ya kuondoka hapo home. Kama Unaona huwezi kuendelea kukaa hapo mpaka utakapo graduate, basi atleast jiwekee deadline, then anza mipango ili kumeet hiyo deadline.

Unga kilo 2200, nyumba za kupanga hata huwe na taa moja tu ndani malipo ni 10000/=. Usije ukasoma story za watu waliosurvive kitaa zikakupa mori, mwaka mmoja una siku 365, na siku moja ina masaa 24. Haya masaa 24 ni mengi sana, hasa ukiyapitisha bila kupata proper meals.

Humu JF Ushawahi kusoma story ya yule jamaa aliyeondoka kwao kwa jeuri ya boom? Matokeo yake mambo yalikuwa tight ikafikia hatua giza likiingia anapanda juu ya mparachichi anakula Yale majani, then anaenda kushushia na maji bombani?

Fikiria upya mkuu. Then jipange
Majani ya mparachichi? Hebu nitag huo uzi[emoji16][emoji16][emoji16]
 
Mkuu usihame home, tumia kufokewa ka morali ya kupambana, tumia kama morali ya kusoma umakize chuo vizuri

Itumie kama morali tu usisahau mama naye ni binadamu

Sema mimi mama angu akinifokea heeh waga namwambia ndo unanifokea sasa, ndo unanifokea [emoji23][emoji23][emoji23] hata ka nimekosea by then
Mi wazazi wangu kitu kidogo tu eti ntakupa laana hasa Maza anapenda sana hii misemo[emoji848][emoji848]
 
Kuna mdau huko juu kasema maza atakua hana maelewano mazuri na mshua so hasira anahamishia kwako hiyo ni truee kabisa,na kubwa kabisa mzee itakua above 50 bimkubwa below 40 hapo mzee hapigi show tu,nakumbuka nilipanga nyumba moja k/nyama mama mwenye nyumba alikua anawatukana watoto wake mitusi mizito anasimama uwanjani hadi majirani wanasikia alikua hana mume,baada ya muda akatokea mzee mmoja anampiga mashine kelele zote zikaisha anaongea kwa upole tu so hapo mchawi mshua mwambie ampige mashine maza atatulia tu,tafuta lugha ya kuongea na mshua aelewe hilo jukumu.
[emoji38][emoji38][emoji38]
 
Mkuu hayomaisha kwangu mimi naona kawaida mkuu maana nilishawahi kushindia mkate na maji tena nilishawahi kutembea kwa mguu kutoka home mpaka chuo wiki nzima kipindi hicho boom lilichelewa kutoka nikawa nashida maji na mkate chuoni so kwangu maisha kama mimi nimeshayazoe hivo usinitishie maisha
Hivi dogo unaujua mtaa au unahadithiwa?

Life litakuchapa mpaka ujinyee[emoji16][emoji16]
 
Dah mimi ndio mkubwa na nina mdogo wangu moja nae ni wakiume ila dogo yupo la pili so me ndio nakuwa house girl na house boy home maana maza washaniifanya niwe hivi ukiwaambia ndugu unaoneka una jeuri kwa wazazi mara umeanza zarau. Basi naamua kukaa nayo moyoni
Mdogo wako yuko la pili?? Duuh bonge la gap[emoji848]
 
K
Hapana mkuu unajua kuna maneno mzazi akiyaongea unajua kabisa hapa mzazi anakunyanyasa hivi kweli mimi na umri wangu huu niachae mavi chooni hebu mkuu think twice, sikuwahi kuambiwa hivi hapo nyuma. Na suala la kuanza kupanga chumba tayari nimeshaweka mipango yangu fresh nina akiba yangu ya boom kama 200k nahisi itanitosha kabisa kuanzia maisha
Kumbe una boom... Jiongeze kijana.. kukaa Kwa wazaz Kwa umri huo piah ni changamoto coz utaona Kama unaonewa... Yawezekana bi mkubwa anasema huyu mbna anaboom na anakula nyumbani na vitu vingne... Pia mzazi muda mwingne kwake unabaki mtoto bo matter umefikia wapi
 
Inaweza Kuwa mzazi anashindwa kukuelewa ama ulishajiona matawi,na pia ni namna aliyoiona mzazi akubane ili aweze hakikisha mabadiliko ya tabia yako ama yapo yanayokuzuzua.Pia kwa jinsi ulivyo react na mwelekeo wa nia ya maamuzi yako.Inaonyesha inashinda ambayo imepelekea hali hiyo kwa mzazi [emoji848]
Huyu dogo kanikumbusha kaka angu alivyotimiza miaka 19 akaanza kuwala wadada na mimba juu, hee akawa kiburi, Maza akimsemesha anawaka...Maza nae akawa anamla mboko za mgongo mbele za watu mbona alinyooka[emoji848]
 
Comment bora kabisa...dogo anajiona kakua, anadanganywa na kadegree uchwara...aje kitaa sasa maji ataita mmaaa
Nguvu ya boom hiyo, wala asijione kua kajitambua sana.
Akifanikiaa kusolve hilo na wazazi wake hapo ndo atakua matured na atafute chumba sasa.

Yaani unamkasirikia mama kabisaa, bora angekua mshua ila sio mama.
 
Yaani we upo chuo mdogo wako la pili?ndio maana unaona hutaki kugombezwa,yaani kifupi hujazoea maisha Hayo gap Kati yako na Dogo ni kubwa sana so inaonyesha uliishi Maisha ya kuendekezwa sana ulipokuwa mwenyewe Kabla Dogo hajazaliwa
Exactly [emoji122][emoji122]
 
Back
Top Bottom