Naona wazazi wangu wamenichoka, ni muda sasa nami nianze kujitegemea

Naona wazazi wangu wamenichoka, ni muda sasa nami nianze kujitegemea

Sikiliza mdogo wangu,
Mzazi hawezi badilika bila Sababu za msingi,lazima Kuna sehemu utakuwa unamkwaza,kaa tafakari njia zako hapo nyuma na za sasa utajua tatizo Nini!
Kama mzazi anajaribu kukuweka kwenye njia iliyo sahihi,humu utashauriwa mengi,tafadhali yachuje Kabla hujafanya maamuzi.

Haya unakwenda kupanga chumba source of income ya kulipia Kodi na kula,kulipia bili za umeme na maji,vitanda na godoro ,vyombo unazitoa wapi?unafanya kazi?
Kuhusu pesa kulipia kodi na mambo mengi we niachie mimi nitajuwa namna ya kuyashughulikia ila kikubwa mwisho wa mwezi huu niwe nimeshasepa home
 
At 21 unahama unaenda wapi, nina bro ana 26 na yupo bado home

Fanya hivi wewe jali mishe zako, msalimie tu then pita kule usiwaongeleshe ongeleshe

Usitoke home mpaka pale utakopojiweza
Mimi nimeshajitahidi sana kujali mishemishe zangu nakuishi na wazazi wangu ila tabia ya bimkubwa kunifokea kwa sauti kubwa kwakweli nimeshamvumilia vyakutosha sasa ni muda wangu wa kuwa huru na kelele za bimkubwa. Kuhusu umri wangu 21, najua utashangaa kwanini naondoka home ila ndio hivo mkuu kelele za bimkubwa ndio zinanifanya niondoke nyumbani
 
Mwaya mdogo wangu,
Nenda kapambane huko duniani, wengine tulianza kujitegemea hata huo umri wako ni mkubwa,

Ila aga nyumbani kwa amani, maana hujui siku utakayorudisha mpira kwa kipa, wewe ni wa kiume hivyo usiuogope mtaa, jitafutie kakitu kako kadogo ka kuingiza shilingi mbili tatu unakuwa unaenda home mara chache kuwasalimia, unawapelekea japo mafuta na mchele,

Mama atakuheshimu tu, asikudanganye mtu, wamama wetu wengi wanawaheshimu zaidi wale watoto wanaowa support..!!
 
Jiweke kama mtu anayestahili kuheshimiwa, mwenye Akili,
Fanya wanaokuzunguka wakuogope, yaani MTU akitaka kukutuma kazi anajifikiria mara tatutatu!

Wengine tulizaliwa hivyo,
Ndio naanza sasa kujitafutia heshima hasa kwa wazazi wangu naona nikiendelea kukaa hapa nyumbani zarau zitakuwa nyingi na nataka niwaonyeshe kwamba naweza kuishi bila wao ili heshima iwepo
 
Najua sikuhizi nimebadilika nahisi hata wazazi wanalijua hili na kubadilika kwangu nikutoka na majukumu niliyonayo sasa hasa ukizingatia masomo chuoni nakosa muda wa kufanya kazi hasa katikati ya wiki na pia kuchelewa kurudi nyumbani sio kwamba nimeanza uhuni??hapana ni majukumu tu ya chuo yananifanya nifanye hivi maana huwa na baki mpaka saa 4 usiku na muda huo nautumia kujisomea chuoni maana kusoma home jau sana ukizingatia kelele za bimkubwa uwezi kuwa na utulivu. Sasa ndugu yangu kwa mabadiliko haya hivi ni kweli maza aanzee kukuchukia bila sababu za msingi
Polesana
 
Mimi nimeshajitahidi sana kujali mishemishe zangu nakuishi na wazazi wangu ila tabia ya bimkubwa kunifokea kwa sauti kubwa kwakweli nimeshamvumilia vyakutosha sasa ni muda wangu wa kuwa huru na kelele za bimkubwa. Kuhusu umri wangu 21, najua utashangaa kwanini naondoka home ila ndio hivo mkuu kelele za bimkubwa ndio zinanifanya niondoke nyumbani
Umejaribu kuongea na mzaziwako wa kiume umsikie anasemaje huenda Kuna changamoto wazazi wanapitia hivo wanadhindwwa kuzuia hasira zao Kwa watu wengine kujitegemea na kusoma naona haviend pamoja waulize hata ambao walifnya hivo wengi waliishi Kwa shida sana
 
heshimu wazazi
ni hayo tu. acha kiburi, mzazi hawezi kumnyanyasa mwanae
tena ukome kabisa kwa maneno uliyotumia
Mkuu tatizo wewe hayajakukuta, hao wazazi unaowatetea sametimes tabia zao huwezi kuzivumilia. Ni wazazi najua ila sio kwamba wanahaki ya kuwa sahihi muda wote kuna wazazi wanakosea hasa jinsi ya kuongea na mtoto huwezi kumfokea mtoto tena kwa sauti kubwa kwangu mimi hili hapana kama heshima wazazi nawapa ila wao mbona mimi hawanipi heshima yangu
 
Mkuu we unaongea tu ila mimi nimeshajitahidi kufanya kazi za nyumbani kama kuosha vyombo naosha deki pia napiga hata jana pia nilipiga deki na maza akafoka ananiambia napiga deki vibaya sijui maji niliopigia ni machafu wakati maji ni masafi tu hayana shida. Na mimi kwenda kupanga nimeamua ili niepuke na kero za bimkubwa maana yeye ni mtu wa kufokea fokea bila sababu za msingi sasa naona kama kanichoka
Huko kufoka kaanza lini au wewe humjui maza ako??
Maana huyo sio mke kusema eti mmekutana ukubwani, umekua unamuona, au hujaishi nae muda mrefu??
 
Umejaribu kuongea na mzaziwako wa kiume umsikie anasemaje huenda Kuna changamoto wazazi wanapitia hivo wanadhindwwa kuzuia hasira zao Kwa watu wengine kujitegemea na kusoma naona haviend pamoja waulize hata ambao walifnya hivo wengi waliishi Kwa shida sana
Yaani Dogo angejua mtaani Sio poa,angetulia.,labda Kwa vile wanasemaga wenzetu ni wanaume
 
Mwaya mdogo wangu,
Nenda kapambane huko duniani, wengine tulianza kujitegemea hata huo umri wako ni mkubwa,

Ila aga nyumbani kwa amani, maana hujui siku utakayorudisha mpira kwa kipa, wewe ni wa kiume hivyo usiuogope mtaa, jitafutie kakitu kako kadogo ka kuingiza shilingi mbili tatu unakuwa unaenda home mara chache kuwasalimia, unawapelekea japo mafuta na mchele,

Mama atakuheshimu tu, asikudanganye mtu, wamama wetu wengi wanawaheshimu zaidi wale watoto wanaowa support..!!
Kabisa mkuu nami nataka nifanye hivo hivo nijitafutia hata kibiashara kidogo au vibarua ili niweze kukidhi mahitaji yangu then kingine nitakachokipata nipeleke home ili nipate heshima yangu
 
Mkuu me nimeshamvumilia sana bimkubwa na nimehmshajitahidi kumweka sawa (yaani asinichukie) ila kila nikijaribu kufanya kazi za hapa home maza bado anafoka nimeshajitahidi kuvumilia maisha ya hapa nyumbani ila sina amani wala furaha.

Hali hii inanifanya mimi nisishinde hapa nyumbani nakaa zangu chuoni mpaka saa 4 usiku na weekend naamua kusepa home nikawacheki wana ilimradi niyakwepe maneno ya bimkubwa mimi kumvumilia nimeshindwa mkuu mwisho wa mwezi huu nimeshapanga nasepa home potelea mbali changamoto za mtaani
Nimecheka sana unaposema eti umemvumilia sana. 😅😅😅

Mpaka umri huo, nani kamvumilia mwenzie sana?. Narudia kukwambia mdogo wangu, nyumbani hutakiwi kuondoka kwa hasira. Na siku utakayoamua kuondoka, make sure umejipanga, wahenga waliposema "Ukitaka kuruka, Agana na nyonga" walikuwa na maana yao kubwa sana.

At 21, bado sana mdogo wangu. Tena kibongo bongo ndio kabisaaa. Tumia hizo hasira ulizo nazo kujipanga namna ya kuondoka hapo home. Kama Unaona huwezi kuendelea kukaa hapo mpaka utakapo graduate, basi atleast jiwekee deadline, then anza mipango ili kumeet hiyo deadline.

Unga kilo 2200, nyumba za kupanga hata huwe na taa moja tu ndani malipo ni 10000/=. Usije ukasoma story za watu waliosurvive kitaa zikakupa mori, mwaka mmoja una siku 365, na siku moja ina masaa 24. Haya masaa 24 ni mengi sana, hasa ukiyapitisha bila kupata proper meals.

Humu JF Ushawahi kusoma story ya yule jamaa aliyeondoka kwao kwa jeuri ya boom? Matokeo yake mambo yalikuwa tight ikafikia hatua giza likiingia anapanda juu ya mparachichi anakula Yale majani, then anaenda kushushia na maji bombani?

Fikiria upya mkuu. Then jipange
 
Habarini wakuu! Ni mimi kijana wenu humu jamiiforums nina miaka 21, kama mnavyojuwa umri huu bado nipo masomoni chuo flani hivi apa dar na bado nipo home.

Sasa tuludi kwenye mada, unajua nini hapa home sipaelewi sikuhizi nimekuwa nikichukiwa pasipo na sababu za msingi, hasa bi mkubwa amekuwa mtu wakunifokea fokea hadi majirani huwa wanasikia jinsi ninavyofokewa. Majuzi kati hapa niliambiwa sikuhizi hapo home sifanyi kazi na ninachelewa kurudi nyumbani, nikiwauliza wazazi wangu ni kazi gani wanataka mimi nizifanye hapa nyumbani naambiwa nioshe vyombo, mara nifyeke majani na mikazi mengine kibao.

Okay siku na kipingamizi kwasababu hawa ni wazazi wangu hivo ni wajibu kuwasikiliza na sio kwamba siku za nyuma nilikuwa sifanyikazi? Hapana ni kutokana na majukumu ya masomo huku chuoni yananibana sana hivo nakuwa mtu sio wakushinda nyumbani maana mda wote na huku chuoni huwa na baki mpaka saa 3 au nne usiku ndio narudi home. Nafanya hivi ili nikimbie majukumu ya nyumbani ila baadae nahisi wazazi wangu walinishukizia.

Anyway sasa kila nikifanya kazi za hapa nyumba bado maneno yanakuwa mengi mara uwambie urudie kuosha vyombo mara mbili wakati apo vyombo ushaosha na vinan'gaa bila shida , ukitoka hapo mara uwambiwe chooni unaachafua mara hausafishi mara unaingiza mchanga mara uwambiwe uliacha mavi leo asubuhi yaani maneno yanakuwa mengi halafu bimkubwa anaongea kwasauti kubwa hadi majirani wanasikia

Mimi hali hii sipendezwi nayo, naona wazazi wangu kama wameanza kunichoka, hapa nafanya mpango mwisho wa mwezi huu nichomoke hapa home najua mwanzo wa kujitegemea huwa mgumu ila potelea mbali siwezi kuendelea kukaa home huku nikidharirishwa na maneno ya bimkubwa.

Anyway natafuta chumba bei iwe 50k maeneo kuanzia ubungo kibo, kona mpaka kimara korogwe. Kama unaona au unasikia kuna chumba kinapangishwa maeneo hayo anipange sasa. Wakuu #natanguliza shukuran
Pole Sana kak haya maisha nimewai ishi unagombezwa bila sababu yoyote ile

Kuna chumba kipo pale kibo nilikuwa nakaaga wakt nasoma hapo chuo

Hvyo ukifika kibo uliziaa bar ya daga daga kisha nitexr pm nikupe maelekezo

Ujingwa sna kunyanyaswa bila sababu za msingi sijapenda hilo
 
Back
Top Bottom