Kidini miongozo hii hapa:
4 Mtazifanya hukumu zangu, nanyi mtazishika amri zangu, ili mwenende katika hizo; mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.
Mambo ya Walawi 18:4
5 Kwa ajili ya hayo mtazishika amri zangu na hukumu zangu; ambazo mtu akizitumia ataishi kwa hizo; mimi ndimi Bwana.
Mambo ya Walawi 18:5
6 Mtu ye yote aliye wa kwenu asimkaribie mwenziwe aliye wa jamaa yake ya karibu ili kumfunua utupu; mimi ndimi Bwana.
Mambo ya Walawi 18:6
7 Utupu wa baba yako, wala utupu wa mama yako, usifunue, maana ndiye mama yako; usifunue utupu wake.
Mambo ya Walawi 18:7
8 Utupu wa mke wa baba yako, usifunue; maana, ni utupu wa baba yako.
Mambo ya Walawi 18:8
9 Utupu wa umbu lako, binti ya baba yako, au binti ya mama yako, kwamba alizaliwa nyumbani mwenu au kwamba alizaliwa kwengine, utupu wa hao usifunue.
Mambo ya Walawi 18:9
10 Utupu wa binti ya mwanao mume, au wa binti ya binti yako, utupu wao hao usifunue; kwa kuwa ndio utupu wako mwenyewe.
Mambo ya Walawi 18:10
11 Utupu wa binti ya mkewe baba yako, aliyezaliwa na baba yako, yeye ni umbu lako, usifunue utupu wake.
Mambo ya Walawi 18:11
12 Usifunue utupu wa umbu lake baba yako; maana, yeye ni jamaa aliye karibu.
Mambo ya Walawi 18:12
13 Usifunue utupu wa umbu la mama yako; maana, yeye ni jamaa ya mama yako ya karibu.
Mambo ya Walawi 18:13
14 Usifunue utupu wa ndugu ya baba yako, usimkaribie mkewe huyo; yeye ni shangazi lako.
Mambo ya Walawi 18:14
15 Usifunue utupu wa mkweo mwanamke; yeye ni mke wa mwanao; usifunue utupu wake huyo.
Mambo ya Walawi 18:15
16 Usifunue utupu wa mke wa nduguyo; maana, ni utupu wa nduguyo.
Mambo ya Walawi 18:16
17 Usifunue utupu wa mwanamke na binti yake; usimtwae binti ya mwanawe mume, au binti ya binti yake, ili kufunua utupu wake; hao ni jamaa ya karibu; ni uovu mkuu.
Mambo ya Walawi 18:17
18 Wala usitwae mwanamke pamoja na nduguye, awe mtesi wake, na kufunua utupu wake, huyo wa pili atakapokuwa yu hai.
Mambo ya Walawi 18:18
19 Nawe usimkaribie mwanamke kufunua utupu wake wakati wa kutengwa kwa ajili ya unajisi wake.
Mambo ya Walawi 18:19
20 Usilale na mke wa mwenzio, ukajitia unajisi naye.
Mambo ya Walawi 18:20
22 Usilale na mwanamume mfano wa kulala na mwanamke; ni machukizo.
Mambo ya Walawi 18:22
23 Wala usilale na mnyama ye yote, ili kujitia unajisi kwake; wala mwanamke asisimame mbele ya mnyama ili kulala naye; ni uchafuko.
Mambo ya Walawi 18:23
Kisayansi:
Ukioana na ndugu wa karibu upo uwezekekano wa genes ambazo ni hatari kujitokeza na kuleta madhara kwa kiumbe atakayezaliwa hususani koo zenye hizo genes( lethal genes).
NAOMBA KUWASILISHA.