Nape aanza nyodo kwa wananchi. Anatoa majibu ya shombo

Nape aanza nyodo kwa wananchi. Anatoa majibu ya shombo

Sexless

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2017
Posts
23,683
Reaction score
55,898
Nape anashiba na kusaza awamu hii. Mama alishamtoa wasiwasi Nape na mawaziri wengine kwamba hatowatumbua hata wakikosea. Hivyo hawana hofu tena.

Nape anaulizwa kuhusu TOZO mpya za miamala ya kibenki anajibu kwa nyodo. Majibu yake yananuka shombo la ulevi wa madaraka.

Nchi hii jamani! Acha tu.

20220818_164602.jpg
 
Kama sio kumharibia Bi Samia ni nini? maana yake ni usilete fyokofyoko kwenye hiyo picha.

Sasa tofauti yake na ile ya Polepole kutukatia mauno ni ipi?
 
Maana ya huo ujumbe wa Picha ni "Msilete fyoko fyoko" au aliathiriwa na yule mbeba Bastola wa Makonda?
 
Hajawahi kuacha nyodo, unavyosema ameanza tena unakosea. Ule upole wao huwa wanauleta kumdanganya mtawala awape ulaji, wakishapata cheo dharau lazima zianze.

Huwa nawashangaa hawa viongozi wetu, kutwa kushinda kwenye mitandao ya kijamii wakati wanajijua hawana "guts" za kuvumilia matokeo ya kushinda huko.

Hawa jamaa sasa wanatuonesha viburi vya wazi, wanajua hatuna cha kuwafanya kwani mama yao anawapenda sana anawalinda; na hata kama uchaguzi mwingine ukifanyika wanajua watachakachua warudi tena ulingoni, wanajiamini, wameshatuona watanzania wajinga hatuna chakuwafanya zaidi ya kulalamika tu.

Sasa wanajua vizuri inyeshe mvua, liwake jua, hata serikali ijayo watakuwepo uongozini, kwanini wawe na hofu kwa kondoo wanaowatawala?
 
Itafika mahali tutaelewana tu.
Baadhi ya viongozi wa sasa ni walamba asali. Hawajali wananchi wa kawaida aka maskini!

Nape ana dharau sana. Namfahamu na wala si kwa kuambiwa bali kwa kuthibitisha. He is not humble. He is very harsh!

Ila ipo siku atajifunza kuwa maisha ni watu na hapaswi kuwabagua hata kama wana hadhi ya chini kuliko aliyonayo.
 
Nape anashiba na kusaza awamu hii. Mama alishamtoa wasiwasi Nape na mawaziri wengine kwamba hatowatumbua hata wakikosea. Hivyo hawana hofu tena.

Nape anaulizwa kuhusu TOZO mpya za miamala ya kibenki anajibu kwa nyodo. Majibu yake yananuka shombo la ulevi wa madaraka.

Nchi hii jamani! Acha
Si mlimwoonesha huruma wakati akinyooshewa bastola kutoka kwa kibano cha mpapuro mkafikiri ni mwenzenu sasa oneni wenyewe kwa macho na masikio yenu msikie wenyewe kwamba yeye ni nani na hakuna mu wa kumfanya chochote. Msikimbilie kuunga mkono mtu kwa matendo ya gizani msiyoyajua dhidi ya mtu fulani.

Wote waliomkashifu JPM wako madarakani kwa sasa na nyodo hizo ndio uthibitisho walifanya nini.......bado mengine yatatokea ya ajabu na kusikitisha lakini hatolewe pale........wana hati miliki ya nchi
 
Rais Samia kwanini unawakumbatia Mwigulu, Makamba na Nape? Mbona hawafai kabisa yaani wanakuhujumu wazi wazi. Tunamlilia Dkt Magufuli, angekuwepo gharama za maisha zingekuwa chini na watu hawa wasingekuwepo kabiaa kwenye safu za uongozi.
 
Rais Samia kwa nini unawakumbatia Mwigulu, Makamba na Nape????? Mbona hawafai kabisa yaani wanakuhujumu wazi wazi. Tunamlilia Dkt Magufuli, angekuwepo gharama za maisha zingekuwa chini na watu hawa wasingekuwepo kabiaa kwenye safu za uongozi.
Watu wanalamba asali.
Samia yupo kwapani mwa mafisadi hana ubavu.
Huyu hapaswi kupewa 2025 mtaliangamiza taifa.
 
Back
Top Bottom