Nape: Kampuni za simu haziibi vifurushi vya intaneti vya wateja

Nape: Kampuni za simu haziibi vifurushi vya intaneti vya wateja


Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema Bungeni kuwa Serikali inaendelea kuchambua malalamiko ya matumizi ya Bundle kwenye simu.

Amefafanua, "Malalamiko kwamba kuna Bundle zinawekwa kwenye Simu, zinatumika bila Mtumiaji kuzitumia yamekuwepo, yamefikishwa Mamlaka husika na Uchambuzi umefanyika. Matokeo yanaonesha hakuna wizi uliotokea, isipokuwa kuna tatizo la matumizi ya simu za kisasa".

Ameongeza, "Matatizo hayo yamejikita kwenye maeneo mawili; 1) Hizi simu za kisasa wakati mwingine hata ukiwa hutumii kuna baadhi ya Applications zinaendelea kufanya kazi nyuma ya simu. 2) Simu hizi unaweza kuweka Bundle lako ukawasha 'Hotspot' kinachoruhusu mtu mwingine kutumia Data uliyonayo".

Kupitia Twitter Waziri Nape ameandika.

"YEYOTE ANAYEAMINI KAIBIWA KIFURUSHI KABLA HAJATUMIA AKAKUTA KIMEISHA, ALETE USHAHIDI TUTAFANYA UCHAMBUZI KWA KUTUMIA VIFAA VYA KISASA NATUTAWEKA HADHARANI KUONYESHA TATIZO LILIPO. Lakini mpaka leo malalamiko yote yaliyopokelewa tatizo limekutwa ni uelewa wa matumizi ya simu JANJA"
Daaaaaaah
 
Nape pamoja na watanzania walio wengi hawawezi kuwa na ubongo wa kuweza kuyajua hayo, wao husubiri tu zile sms za "umetumia 75 ya bando lako"

Yeye anafikiri tunaposema tunaibiwa anafikiri hatupati hizo sms anazo subiri! Hawa makampuni wanatakiwa wawe wanaangaliwa kujua kweli kama wanachotoa kinaendana na walichosema.....

Sisi tutujuaje kuwa ni GB 5 na sio tatu? Kama Nape anategemea asubiri sms ndio kujua ukweli basi ni mtupu sana kichwani yani haya makampuni waibe kirahisi hivyo? Hawa watu wana akili sana awawezi kuiba kwa njia rahisi ni lazima wakubandike Gb 5 hewa kumbe GB 2 sasa swali kwa TCRA na Nape Nnauye wanawezaje kutambua vifurushi hewa?

Kama watu wanakwenda kwenye vituo vya mafuta wanawekewa hewa tupu halafu mtambo unasoma umeweka lita 10 kumbe 3 ni hewa ...sasa hawa wamitandao watashindwa vipi kutupa vifurushi hewa?
 
Wizi ni pale unaponunua bando kisha unapangiwa siku za kutumia kwa kawaida unaponunua kitu hutakiwi upangiwe muda wa kutumia bando la siku la wiki la mwezi huu ni wizi waache bando mpaka liishe
 
Hii nchi only vitukuu vyetu labda baada ya kutucheka ancestors wao watajaribu kusahihisha wakati kizazi chote cha walafi na wanamtandao kimeisha!
 
Mitandao ya simu imekaa kiwizi wizi sana kwahiyo kuitetea na kutuona sisi wananchi ndo washamba nikutukosea heshima.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Watanzania wengi hawajui matumizi sahihi ya bando. Kuna watu wanaruhusu apps kuji-update na ku-run at the background hivyo kupelekea bando kutumika.
How do you shut down those self updating apps and background running apps.
 

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema Bungeni kuwa Serikali inaendelea kuchambua malalamiko ya matumizi ya Bundle kwenye simu.

Amefafanua, "Malalamiko kwamba kuna Bundle zinawekwa kwenye Simu, zinatumika bila Mtumiaji kuzitumia yamekuwepo, yamefikishwa Mamlaka husika na Uchambuzi umefanyika. Matokeo yanaonesha hakuna wizi uliotokea, isipokuwa kuna tatizo la matumizi ya simu za kisasa".

Ameongeza, "Matatizo hayo yamejikita kwenye maeneo mawili; 1) Hizi simu za kisasa wakati mwingine hata ukiwa hutumii kuna baadhi ya Applications zinaendelea kufanya kazi nyuma ya simu. 2) Simu hizi unaweza kuweka Bundle lako ukawasha 'Hotspot' kinachoruhusu mtu mwingine kutumia Data uliyonayo".

Kupitia Twitter Waziri Nape ameandika.

"YEYOTE ANAYEAMINI KAIBIWA KIFURUSHI KABLA HAJATUMIA AKAKUTA KIMEISHA, ALETE USHAHIDI TUTAFANYA UCHAMBUZI KWA KUTUMIA VIFAA VYA KISASA NATUTAWEKA HADHARANI KUONYESHA TATIZO LILIPO. Lakini mpaka leo malalamiko yote yaliyopokelewa tatizo limekutwa ni uelewa wa matumizi ya simu JANJA"
Wizi mkubwa uko hapa,unaweka kifurushi,speed ya inakuwa kubwa kama nusu saa,baada ya hapo inashuka kwa kiwango cha kobe,inaendelea kusumbua hivyo mpaka kifurushi kinaisha,na jinsi inavyotumia muda mrefu kutafuta mtandao bila mafanikio unakuja tu kushtukia Mb zimeisha,hivyo kukulazimisha ununue tena kifurushi...
 
Mkuu huko kutokujuwa kwa watz kumeanza juzi? Simu janja zimekuja juzi nchi hii ni kwanini hayo malalamiko hayakuwepo before? Kiungwana unapaswa kuwataka radhi watz.
Simu janja zimekuwepo muda, lkn matumizi ya mb yamepanda hv karibuni kwa watanzania walio wengi.

Siku za nyuma watu walikuwa wanaingia Facebook tu na wakawa wanatambiashiana kupost picha huko
 
Wewe acha kuropoka tuu hii mitandao ni wezi haiwezekani kila mtu akawasingizia hivi unafikiri huyo Nape wako anajua nini kuhusu matumizi ya simu na vifurushi ambacho watu wote wanao lalamika hawajui au sisi hatujui? Hebu twambie Nape au na wewe unajua nini ambacho watu wengine hawajui? Kila siku visingizio ni kusema oooh apps ziko on na data umeacha on ....
Labda atakuwa ndiye Nape mwenyewe
 

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema Bungeni kuwa Serikali inaendelea kuchambua malalamiko ya matumizi ya Bundle kwenye simu.

Amefafanua, "Malalamiko kwamba kuna Bundle zinawekwa kwenye Simu, zinatumika bila Mtumiaji kuzitumia yamekuwepo, yamefikishwa Mamlaka husika na Uchambuzi umefanyika. Matokeo yanaonesha hakuna wizi uliotokea, isipokuwa kuna tatizo la matumizi ya simu za kisasa".

Ameongeza, "Matatizo hayo yamejikita kwenye maeneo mawili; 1) Hizi simu za kisasa wakati mwingine hata ukiwa hutumii kuna baadhi ya Applications zinaendelea kufanya kazi nyuma ya simu. 2) Simu hizi unaweza kuweka Bundle lako ukawasha 'Hotspot' kinachoruhusu mtu mwingine kutumia Data uliyonayo".

Kupitia Twitter Waziri Nape ameandika.

"YEYOTE ANAYEAMINI KAIBIWA KIFURUSHI KABLA HAJATUMIA AKAKUTA KIMEISHA, ALETE USHAHIDI TUTAFANYA UCHAMBUZI KWA KUTUMIA VIFAA VYA KISASA NATUTAWEKA HADHARANI KUONYESHA TATIZO LILIPO. Lakini mpaka leo malalamiko yote yaliyopokelewa tatizo limekutwa ni uelewa wa matumizi ya simu JANJA"
Ni heri angenyamaza tu kwanza hana hadhi ya kuwa Waziri ni mpigaji mbobezi
 
"YEYOTE ANAYEAMINI KAIBIWA KIFURUSHI KABLA HAJATUMIA AKAKUTA KIMEISHA, ALETE USHAHIDI TUTAFANYA UCHAMBUZI KWA KUTUMIA VIFAA VYA KISASA NATUTAWEKA HADHARANI KUONYESHA TATIZO LILIPO. Lakini mpaka leo malalamiko yote yaliyopokelewa tatizo limekutwa ni uelewa wa matumizi ya simu JANJA"
Wanaochambua ni wataalamu wa IT, Nape si mtaalamu wa IT ni mtaalam wa majukwaa ya siasa, nitamuelewa kama atasema anakwenda kufanya uchambuzi yeye binafsi lakini siyo kuwatumia watu wengine ambao hatujui wanainterest gani
 
Back
Top Bottom