Nape: Kampuni za simu haziibi vifurushi vya intaneti vya wateja

Nape: Kampuni za simu haziibi vifurushi vya intaneti vya wateja

Na kwa hakika wizi unafanyika namna hiyo kwa kuuzia watu bando fake unaambiea GB 5 kumbe ni GB 3 na hapo ugumu unakuja kwenye kujua kama hili bando ni kweli ni GB 5 au lah.....
Huwezi jua sababu wameseti meseji unayopata wewe ikuoneshe umepokea 5GB ila kimsingi umeibiwa.

Kifurushi changu cha sasa nilijiunga Voda cha buku 5 ni GB 3 za week nzima naona wamenipa GB halisi maana Zantel nao wamekuwa wezi sikuhizi Unajiunga elfu 2 kila siku 1.3GB za week ila hazitoboi
 
Nape ameshatulizwa na makampuni ya mitandao ya simu
Kashalambishwa 100G ya bakshishi atafanya nini tena?

Hapo ni mwendo wa kukinga posho kila mwezi wanammegea 100M yake kila kampuni la simu hutakaa usikie tena yale mambo ya fine walizokuwa wanapigwa na Magufuli.
 

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema Bungeni kuwa Serikali inaendelea kuchambua malalamiko ya matumizi ya Bundle kwenye simu.

Amefafanua, "Malalamiko kwamba kuna Bundle zinawekwa kwenye Simu, zinatumika bila Mtumiaji kuzitumia yamekuwepo, yamefikishwa Mamlaka husika na Uchambuzi umefanyika. Matokeo yanaonesha hakuna wizi uliotokea, isipokuwa kuna tatizo la matumizi ya simu za kisasa".

Ameongeza, "Matatizo hayo yamejikita kwenye maeneo mawili; 1) Hizi simu za kisasa wakati mwingine hata ukiwa hutumii kuna baadhi ya Applications zinaendelea kufanya kazi nyuma ya simu. 2) Simu hizi unaweza kuweka Bundle lako ukawasha 'Hotspot' kinachoruhusu mtu mwingine kutumia Data uliyonayo".

Kupitia Twitter Waziri Nape ameandika.

"YEYOTE ANAYEAMINI KAIBIWA KIFURUSHI KABLA HAJATUMIA AKAKUTA KIMEISHA, ALETE USHAHIDI TUTAFANYA UCHAMBUZI KWA KUTUMIA VIFAA VYA KISASA NATUTAWEKA HADHARANI KUONYESHA TATIZO LILIPO. Lakini mpaka leo malalamiko yote yaliyopokelewa tatizo limekutwa ni uelewa wa matumizi ya simu JANJA"
Namuunga mkono asilimia mia moja waziri. Kuna uelewa mdogo wa watumiaji wa smart phones, hicho anachokisema ni sahihi kwa sababu binafsi kuna wakati nilihisi bundle langu linaisha bila kuelewa lina isha vipi.

Nilichofanya nili install app ya ku track all my internet usage, hii app inakuonesha kabisa una bundle lenye mb ngapi na jinsi linavyoenda likiisha. Pia hii app ilikua ina list apps zote kwenye simu ikianza ile inayotumia bundle zaidi, mfano ticktock, instagram, twiter, telegram etc.

Kwa hili nikaja kujua nini kinamaliza bundle langu. Hii app nilikuta inatumia hadi mb 12 saa nyingine wakati hata sijaifungua. Nilifanya maamuzi ya kuitoa kwenye simu yangu, tokea hapo bundle linatumika vizur.

Kwa hiyo ni kweli, hakuna anayesema anaibiwa bundle ataweza kuleta ushaidi wa hilo, sana sana tu mtu ana back ground apps zinazo run na kumaliza bundle lake na hazijui.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema Bungeni kuwa Serikali inaendelea kuchambua malalamiko ya matumizi ya Bundle kwenye simu.

Amefafanua, "Malalamiko kwamba kuna Bundle zinawekwa kwenye Simu, zinatumika bila Mtumiaji kuzitumia yamekuwepo, yamefikishwa Mamlaka husika na Uchambuzi umefanyika. Matokeo yanaonesha hakuna wizi uliotokea, isipokuwa kuna tatizo la matumizi ya simu za kisasa".

Ameongeza, "Matatizo hayo yamejikita kwenye maeneo mawili; 1) Hizi simu za kisasa wakati mwingine hata ukiwa hutumii kuna baadhi ya Applications zinaendelea kufanya kazi nyuma ya simu. 2) Simu hizi unaweza kuweka Bundle lako ukawasha 'Hotspot' kinachoruhusu mtu mwingine kutumia Data uliyonayo".

Kupitia Twitter Waziri Nape ameandika.

"YEYOTE ANAYEAMINI KAIBIWA KIFURUSHI KABLA HAJATUMIA AKAKUTA KIMEISHA, ALETE USHAHIDI TUTAFANYA UCHAMBUZI KWA KUTUMIA VIFAA VYA KISASA NATUTAWEKA HADHARANI KUONYESHA TATIZO LILIPO. Lakini mpaka leo malalamiko yote yaliyopokelewa tatizo limekutwa ni uelewa wa matumizi ya simu JANJA"
Huyu kashapewa rushwa tayari, application zinafanya kazi hata kama umezima bando?
 
Namuunga mkono asilimia mia moja waziri. Kuna uelewa mdogo wa watumiaji wa smart phones, hicho anachokisema ni sahihi kwa sababu binafsi kuna wakati nilihisi bundle langu linaisha bila kuelewa lina isha vipi.

Nilichofanya nili install app ya ku track all my internet usage, hii app inakuonesha kabisa una bundle lenye mb ngapi na jinsi linavyoenda likiisha. Pia hii app ilikua ina list apps zote kwenye simu ikianza ile inayotumia bundle zaidi, mfano ticktock, instagram, twiter, telegram etc.

Kwa hili nikaja kujua nini kinamaliza bundle langu. Hii app nilikuta inatumia hadi mb 12 saa nyingine wakati hata sijaifungua. Nilifanya maamuzi ya kuitoa kwenye simu yangu, tokea hapo bundle linatumika vizur.

Kwa hiyo ni kweli, hakuna anayesema anaibiwa bundle ataweza kuleta ushaidi wa hilo, sana sana tu mtu ana back ground apps zinazo run na kumaliza bundle lake na hazijui.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa hiyo hata kama umezima data application zinafanya kazi?
 
Shida ya watawala hapo ajili ya maslahi ya umma ni ajili ya maslahi ya familia zao, huyu kavuta rushwa zake
 
Watanzania wengi hawajui matumizi sahihi ya bando. Kuna watu wanaruhusu apps kuji-update na ku-run at the background hivyo kupelekea bando kutumika.
Mkuu huko kutokujuwa kwa watz kumeanza juzi? Simu janja zimekuja juzi nchi hii ni kwanini hayo malalamiko hayakuwepo before? Kiungwana unapaswa kuwataka radhi watz.
 
Huwezi jua sababu wameseti meseji unayopata wewe ikuoneshe umepokea 5GB ila kimsingi umeibiwa.

Kifurushi changu cha sasa nilijiunga Voda cha buku 5 ni GB 3 za week nzima naona wamenipa GB halisi maana Zantel nao wamekuwa wezi sikuhizi Unajiunga elfu 2 kila siku 1.3GB za week ila hazitoboi
Voda wapo vema. Hakuna kama voda. Nipo Eyateli nimetumia GB 15 kwa SIKU 4 ni ajabu ila kwa VODA GB 3 WIKI NZIMA NA DATA SIZIMI
 
Voda wapo vema. Hakuna kama voda. Nipo Eyateli nimetumia GB 15 kwa SIKU 4 ni ajabu ila kwa VODA GB 3 WIKI NZIMA NA DATA SIZIMI
Yeah niliweka line yao kwa ajili ya Mpesa tu ila sasa ntakuwa najiungia bando humu.
 
Ndio nimewaambia hawa jamaa wanacheza na lines of command tu! Ni condition statements tu wanacheza nazo. Huwezi ukakaa ujue haya hata uwe Samia Suluhu ila watu wa IT wanajua huu mchezo.

IF (Kajiunga 1GB)
then (Mpe MB 600)
Print (Umepokea 1GB za kutumia kwa masaa 24)
Else (Salio lako halitoshi)
1 gb ya zamani ndiyo 500 mb ya sasa, kwa matumizi yaleyale.
 
1 gb ya zamani ndiyo 500 mb ya sasa, kwa matumizi yaleyale.
Exactly, ndio wanachofanya yani! Sababu mb500 zinadumu hasa zikiwa ni halisi zikiwa mara 2 yake ndio kabisa kunakuwa hamna kipengele
 
Na kwa hakika wizi unafanyika namna hiyo kwa kuuzia watu bando fake unaambiea GB 5 kumbe ni GB 3 na hapo ugumu unakuja kwenye kujua kama hili bando ni kweli ni GB 5 au lah.....
Ukitaka kulijua baada ya kupokea hiyo txt ya kuwa umepata GB5, ingia instagram , youtube au kama sio mpenzi wa hizo sites ingia twitter au jf kisha baada ya nusu saa omba kujua salio lako.

Ukiomba salio baada ya kulitumia bando watakuletea kiasi sahihi (tofauti na kile cha geresha) hapo sasa ndo utashangaa unambiwa una 3gb.
 
Ndio nimewaambia hawa jamaa wanacheza na lines of command tu! Ni condition statements tu wanacheza nazo. Huwezi ukakaa ujue haya hata uwe Samia Suluhu ila watu wa IT wanajua huu mchezo.

IF (Kajiunga 1GB)
then (Mpe MB 600)
Print (Umepokea 1GB za kutumia kwa masaa 24)
Else (Salio lako halitoshi)

Huu ndio mchezo na ninacho jiuliza Nape ametumia mbinu gani kufanya hitimisho hili?
 
Ukitaka kulijua baada ya kupokea hiyo txt ya kuwa umepata GB5, ingia instagram , youtube au kama sio mpenzi wa hizo sites ingia twitter au jf kisha baada ya nusu saa omba kujua salio lako.

Ukiomba salio baada ya kulitumia bando watakuletea kiasi sahihi (tofauti na kile cha geresha) hapo sasa ndo utashangaa unambiwa una 3gb.
😂😂😂😂😂😂😂 jamaa wahuni mno mzee ila wamejificha kwenye kichaka cha background apps.

Na sahizi android na iphone OS zao wamekupa user u admin uruhus app zipi zitumie data sio kama zamani kuwa zinajidokolea data kimya kimya.

Kwahio amna app inakula data background pasipo wewe kuiruhusu.
 
Ukitaka kulijua baada ya kupokea hiyo txt ya kuwa umepata GB5, ingia instagram , youtube au kama sio mpenzi wa hizo sites ingia twitter au jf kisha baada ya nusu saa omba kujua salio lako.

Ukiomba salio baada ya kulitumia bando watakuletea kiasi sahihi (tofauti na kile cha geresha) hapo sasa ndo utashangaa unambiwa una 3gb.
Huku huja sms umetumia 75% ya GB zako baada ya sekunde kadhaa hata hiyo 25% haipo tena
 
Back
Top Bottom