Nape: Kampuni za simu haziibi vifurushi vya intaneti vya wateja

Nape: Kampuni za simu haziibi vifurushi vya intaneti vya wateja

Huku huja sms umetumia 75% ya GB zako baada ya sekunde kadhaa hata hiyo 25% haipo tena
Halotel hao, wakikwambia umetumia 75% ujue bando limeisha. Huu mtandao umekuwa wa kihuni sana sikuhizi, nafikiri ni kwasababu unamilikiwa na mabepari wa kitz.
 
Huku huja sms umetumia 75% ya GB zako baada ya sekunde kadhaa hata hiyo 25% haipo tena
Mie bado hawajaanza kunitapeli! Jana wamentumia hio ya 75% ila nina zaidi ya siku 4 toka nijiunge
 
Mimi nina case study tofauti.
Laini yangu kuu ni HALOTEL. Ndg yangu mmoja siwezi kumpata kwa Halotel kila nikimpigia inatumika tuu... tena kwa laini zake mbili.
Ndipo nikaamua kuweka salio kwenye voda yangu.
Niliweka 500 nikanunua kifurushi chenye dakika 30 kwa siku. Papo hapo nikampigia tukaongea kwa 20mn kifurushi kikaisha. Nikanunua tena nikaongea 20mn tena kikaisha.
Ukiuliza salio linaonysha lipo lakini ukipiga unaambiwa huna salio.

Kuna shida mahali. Huyu jama tayari yuko compromised.
Kwa sababu nimegundua mtandao ambao bado hauna shida sana ni TTCL kwa hiyo ukiwa huko underground apps hazisomi internet??
 
Kiongozi kama hujui kitu, kukaa kimya ni busara na hekima. Maana hata Biblia inasema hata mpumbavu akikaa kimya huonekana mwenye hekima.
 
Huwezi jua sababu wameseti meseji unayopata wewe ikuoneshe umepokea 5GB ila kimsingi umeibiwa.

Kifurushi changu cha sasa nilijiunga Voda cha buku 5 ni GB 3 za week nzima naona wamenipa GB halisi maana Zantel nao wamekuwa wezi sikuhizi Unajiunga elfu 2 kila siku 1.3GB za week ila hazitoboi

Ndio maana nasema Nape Nnauye alitakiwa atwambie au awambie watanzania wao kama serikali wamehakikisha vipi kujua kuwa huduma inayotolewa imeendana na thamani ya pesa iliyosemwa? Nape amejuaje kuwa ni kweli tumepewa G 3 kwa elfu tatu na sio Gb 1? Mtu anasimama anasema watakuwa hawajui kutumia simu sijui anafikiri watu ni wajinga wajinga kama yeye?
 
Mie bado hawajaanza kunitapeli! Jana wamentumia hio ya 75% ila nina zaidi ya siku 4 toka nijiunge
Unabahati mkuu jana ilibidi niwatwangie na kukoroma kidogo kwahiyo toka walipo tuma sms imebaki 25% saa 9:37 alasiri hadi sasa bado halija ishaa
 
Ukilinganisha na upupu wa network providers wengine, atleast hao wana unafuu.
Mkuu nina line 4(Voda, Airtel, Halotel na Tigo) hakuna penye unafuu, kila line huwa najitahidi kuweka elfu 10 kwa mwezi lakini hazitoboi hasa upande wa bando angalau dak zinatoboa
 
Unabahati mkuu jana ilibidi niwatwangie na kukoroma kidogo kwahiyo toka walipo tuma sms imebaki 25% saa 9:37 alasiri hadi sasa bado halija ishaa
Mie mpaka sasa pia bado hawajanikatia umeme!

Toka jana saa 12 naona wanajiheshimu sikuhizi maana sijawahi kutumia bando lao!

Nilijiunga 12GB za mwezi zimekaa week 1 na nusu tu!😅 japo nilizifuja ila nahisi zile zilikuwa GB 8 za uhalisia tu
 
Mimi nina case study tofauti.
Laini yangu kuu ni HALOTEL. Ndg yangu mmoja siwezi kumpata kwa Halotel kila nikimpigia inatumika tuu... tena kwa laini zake mbili.
Ndipo nikaamua kuweka salio kwenye voda yangu.
Niliweka 500 nikanunua kifurushi chenye dakika 30 kwa siku. Papo hapo nikampigia tukaongea kwa 20mn kifurushi kikaisha. Nikanunua tena nikaongea 20mn tena kikaisha.
Ukiuliza salio linaonysha lipo lakini ukipiga unaambiwa huna salio.

Kuna shida mahali. Huyu jama tayari yuko compromised.
Kwa sababu nimegundua mtandao ambao bado hauna shida sana ni TTCL kwa hiyo ukiwa huko underground apps hazisomi internet??
Nape kapewa Rushwa yake safi ametulia
 
Namuunga mkono asilimia mia moja waziri. Kuna uelewa mdogo wa watumiaji wa smart phones, hicho anachokisema ni sahihi kwa sababu binafsi kuna wakati nilihisi bundle langu linaisha bila kuelewa lina isha vipi.

Nilichofanya nili install app ya ku track all my internet usage, hii app inakuonesha kabisa una bundle lenye mb ngapi na jinsi linavyoenda likiisha. Pia hii app ilikua ina list apps zote kwenye simu ikianza ile inayotumia bundle zaidi, mfano ticktock, instagram, twiter, telegram etc.

Kwa hili nikaja kujua nini kinamaliza bundle langu. Hii app nilikuta inatumia hadi mb 12 saa nyingine wakati hata sijaifungua. Nilifanya maamuzi ya kuitoa kwenye simu yangu, tokea hapo bundle linatumika vizur.

Kwa hiyo ni kweli, hakuna anayesema anaibiwa bundle ataweza kuleta ushaidi wa hilo, sana sana tu mtu ana back ground apps zinazo run na kumaliza bundle lake na hazijui.

Sent using Jamii Forums mobile app

Pamoja na uelewa mdogo wa watumiaji wa smart phone lakini haiondoi ukweli kuwa makampuni ya simu wanafanya wizi sana tena sana....

Yani mnataka kusema watanzania wote wanao lalamika basi hawajui kutumia smart phone hahahaha
Yani yeye Nape ndio anajua kutumia smart phone kuliko watanzania wengine?
 
Back
Top Bottom