Napendekeza iundwe Tume Huru ya kuchunguza kifo cha Hayati Magufuli

Napendekeza iundwe Tume Huru ya kuchunguza kifo cha Hayati Magufuli

Kauli ya Nyere aliwahi kusema kuwa " Uraisi ni mzigo mzito sana"

kazi ya uraisi sio lele mama haswa kama kweli umeamua kupambana kwa manufaa ya Taifa lako lkn kama umeamua kula starehe sio kazi nzito hata kidogo.

njia pekee ya kuchunguza kifo chake ni kufanya kazi kwa bidiii, kulinda Rasilimali za nchi yetu kwa masilahi ya wananchi, kwa kufanya hayo tunaweza kuwabaini walio husika.
 
Habar watanzania lengo langu la kuanzisha huu uzi si kwa Nia Mbaya ila nikutaka tu Kumaliza Maswali ya Watanzania wengi wanao shuku kua Hayat kafanyiwa hujuma.

Baada ya kuona mambo mengi Yanayo endelea kwenye mitandao ya kijamii na mitaani. ni wazi kabisa Baadh ya watanzania walio wengi Wana shuku kifo cha Hayat Magufuli na kudhan kua kifo chake kina Hujuma.

Serikal iheshimu mawazo ya watanzania tunao tilia shaka kifo cha Rais wetu na izingatie kwa kuunda Tume huru ya uchunguzi.

Mimi Binafsi nikikumbuka Tukio la ule Moshi uliomfata Hayat Magufuli Mtwara alipokua kwenye Gari bila kujulikana wapi umetokea na kuzua Taharuki nazid kua na mashaka kua Huenda zile zilikua baadhi ya mbinu za kutaka kujaribu na zilishindwa Lakini waliojaribu hawakuacha.

Huwezi kusema ule ulikua uchawi sababu hakuna uchawi na wala siamini uchawi kama upo.

Sasa ili kujiridhisha Basi serikal ifanye uchunguzi na uchunguzi uwe wa wazi ili kufuta hii shauku ya Baadhi ya watu kwani ikiendelea ivi na serikal kukaa kimia huwezi jua Baadaye itakua na madhara gani pia huto jua maadui baadae wanaweza kuutumia huu uvumi kama silaha so nibora serikal ilimalize kwanza ili swala kwani kila siku mambo yanazid kupamba moto.

Video ya tukio la moshi hio apo chini.


Huo uchunguzi unaoutaka una maslahi gani kwako na kwa taifa?
Je, una tija yoyote kiuchumi?
Unataka kuwasahihisha madaktari waliomhudumia au Mungu?
Kama huna majibu ya maswali haya, Basi jinyamazie na kukupa tumaini la kuishi huku ukimaliza na kibwagizo Cha " kazi ya Mungu haina makosa kwani bwana alitoa na bwana ametwaa na jina lake lihidimiwe"!
 
Yaaah na ndo wapiga kura halisi, pia wahudhuriaji kampeni, safari hii 2025 huyu mama atapiga kampeni sijui wapi na chama chake.

Ni heri aanze kusafisha kwa kutembelea wananchi.
Mjinga gani kakuambia CCM wanashinda sababu wanafanya kampeni?
 
Naunga mkono hoja! Halafu Luhaga Mpina awe Mwenyekiti na Biswalo Mganga awe Makamu wake!

Livingstone Lusinde awe Mjumbe, Joseph Kasheku Msukuma awe Mjumbe, Ole Sabaya awe Mjumbe, Chalamila awe Mjumbe, Jenister Mhagama awe Mjumbe, Tulia awe Mjumbe, na Phillipo Mpango awe ndiye mlezi wa hiyo Tume.
Wape na hadidu za rejea na wapi wapeleke hiyo ripoti ya uchunguzi! Na pia muongezee na Bashiru na polepole pamoja na musiba ili kuweka mizania sawa!
Sijui mnatumia kilevi gani kinachaharibu ubongo wenu enyi binadamu!
Ikikupendeza wachunguze vifo vya watu wote kabla na baada ya magu kufariki!
 
Nakuunga mkono mwazo yako na serikali inashauri isipuuze mkangaiko huu vinginvyo ijiandae kuadhibiwa. Hii sauti hatonyamazishwa kwa vitisho kamwe.

Wasikilizeni wanaolalamika wana hoja yenye mashiko ili mbaki salama jisafisheni hakuna namna ya ujanja wa matamko ya kisiasa.

Waziri mkuu, mkuu wa mkoa wa Mbeya, Balozi wa Tanzania Namibia na weza kuwatetea sio kosa lao.

Kuna kikundi kilishika hatamu ya ghafla baada ya hayati kufariki kisha huenda wakawa wanatoa mwongozo nini cha kusema kuzuia taharuki maana JPM alikuwa anatisha wakati akiwa na pumzi na walikuwa na hofu huenda pumzi ikamrudia ndio walitumia muda mrefu kujiridhisha kweli uhai umeondoka vinginevyo ingekuwa balaa, watu wangetamani ardhi iwameze kukwepa rungu lisilo na huruma.
Ni jukumu la serikali kuchunguza na kupata taarifa juu ya kifo hiki sio jukumu la raia kusema eti leteni taarifa tuzifanyie kazi huyo raia anajipenda apeleke hizo taarifa? utauliwa haraka sana. Kwanza hii issue tunaodai uchunguzi kuweni makini watu wana watu wao humu wana wachora tu. Uliona wapi Rais anaenda kutibiwa Mzena hospital ? hii ni hospital ambayo mimi ndo niliisikia muda huo, hata hospitals za wilaya zina hadhi zaidi ya mzena, labda hadhi yake sawa na zile za kata.
 
Naunga mkono hoja! Halafu Luhaga Mpina awe Mwenyekiti na Biswalo Mganga awe Makamu wake!

Livingstone Lusinde awe Mjumbe, Joseph Kasheku Msukuma awe Mjumbe, Ole Sabaya awe Mjumbe, Chalamila awe Mjumbe, Jenister Mhagama awe Mjumbe, Tulia awe Mjumbe, na Phillipo Mpango awe ndiye mlezi wa hiyo Tume.

Mweka hazina awe Doto James
 
Mtaani JPM amefahamika kauwawa,

Mnakaa kwenye AC huku hamjui kinachoendelea sababu furaha yenu imepatkana mnasahau wananchi, sijui 2025 watawaangaliaje mtaani.
Inaonekana una taarifa sahihi na kwa kuzipeleka hupajui! Hapa sio mahali pake. Zipeleke kwa igp au rpc aliye jirani na ulipo atazipokea na kuzifanyia kazi na majibu utayapata!
Nikutahadharishe tu kuwa; hili kosa la kutishia amani na usalama wa nchi adhabu yake unaijua? Sijakutisha Bali nimekusaidia kukupa elimu na kukuambia kuwa, " umejificha katikati ya uwanja wa Mpira yaani katikati ya dimba"! Wanakuona ujue!
 
,,,Huna mda mchfu we na nani, eti uvae barakoa huy mamako mwenyeweumemuona anavo vaa barakoa ?,,, ni mpumbavu
Heh! Tena? Maneno hayo waweza kumtamkia mamako? Basi huwezi Basi ufanye mkono wako uwe na break ya kuyaandika yasiyoandikika kwa watu wazima Tena mama zetu! Tafadhali usirudie Tena nakusihi!
 
Kuna wakati niliandika uzi kuhusu serikali kuweka wazi kuhusu kifo cha Magufuli na si kutupaka mafuta kwa mgongo wa chupa. Uzi haukumaliza dakika hata moja ulifutwa. Sielewi kwanini. Nitasema hata tufiche ukweli ipo siku ukweli utajulikana.

Tumejenga utamaduni kwa kuwa kimya watu hawataki kuhoji. Ukihoji ni matusi. Lakini serikali ikiruhusu uchunguzi itasaidia kuondoa hayo yanayosemwa.
Mhe. Rais, alikataza kusiwe na uvumi bali watu wenye ushahidi wapeleke la sivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa.

Ni majuzi tu yule mwanaharakati Msiba alitamka wazi kuwa Magufuli aliuliwa. Mbona serikali ipo kimya haija mhoji msiba atoe ushahidi kuhusu tuhuma za Magufuli kuuwawa. Rais Samia anasema madaktari walitoa taarifa kafa kwa ugonjwa wa moyo, hivyo tusihoji kwa kua madaktari wamesema.

Rais anatufunga mdomo. Kwani mara ngapi madaktari udai mtu kafa kwa hiki, lakini uchunguzi ukifanyika unakuta ni tofauti. Mfano Yasin Arafat taarifa ya madaktari ilikuja kutofautiana na uchunguzi ulofanyika. Ikaonekana aliuwawa kwa sumu.

Nachojiuliza ni kwanin serikali ilificha kuumwa kwa Magufuli, na hata siku alokufa inadaiwa si hiyo. Haya yalisemwa wazi na Tundu Lissu pamoja na Lema.
Wakishirikiana na vyombo vya habari vya Kenya. Lissu katika twiter aliongea magufuli tayari kafa. Lakini vyombo vya ndani vilibaki kimya na serikali pia, ilificha.
Na viongozi walikanusha hasa Waziri Mkuu alidai Rais Magufuli alikuwa mzima na anachapa kazi. Baadae aliye kuwa mkuu wa mkoa Mbeya alisema kaongea na Rasi Magufuli yupo mzima anachapa kazi.

Makamu wa Rais akiwa ziarani Tanga, nae alisema Rais Magufuli hajambo na anawasalimia wananchi. Baadae akatoa kauli mtu ni kawaida kusumbuliwa na mafua ya hapa na pale.
Hii kauli ilileta utata!

Kesho yake Makamu wa Rais akatangaza msiba wa kitaifa. Kuwa Rais Magufuli kafariki.
Huu mtililiko unaleta mashaka na inaonesha serikali ilikuwa inaficha jambo. Kuanzia Rais Samia, Waziri Mkuu na alie kuwa RC Mbeya waombe masamaha kwa kupotosha jamii.

Pia serikali itueleze kwa nini Magufuli alikuwa anaumwa lakini ilifichwa. Wananchi walikosa haki ya kumuombea.
Haya yote yanafanya uhalali kuwa iundwe tume huru kuchunguza kifo cha Magufuli. Haya mambo ya kunyamazishana si haki. Kwanini serikali haitaki uchunguzi? Wakiguswa wanakuwa wakali?
Kunasiku watu watakwenda mahakamani kudai haki ya kuundwa tume huru kuchunguza kifo cha Magufuli.

Hatuwezi kuwa tunanyamaza wakati viongozi wa Taifa wanakufa, pasipo hata kujiridhisha?
Ifikie wakati kuwe na uchunguzi.
Rais Samia, leo watakupamba usifanye uchunguzi, lakini kikulacho siku zote ki nguoni mwako. Kuwa makini, usidhani kushabikiwa na kupigiwa makofi ndo kupendwa.
Je wewe umewahi kujiridhisha na vifo vya ndugu zako au unajitutumua tu.


Mimi nashauri iundwe TUME HURU YA UCHAGUZI
 
Kuna wakati niliandika uzi kuhusu serikali kuweka wazi kuhusu kifo cha Magufuli na si kutupaka mafuta kwa mgongo wa chupa. Uzi haukumaliza dakika hata moja ulifutwa. Sielewi kwanini. Nitasema hata tufiche ukweli ipo siku ukweli utajulikana.

Tumejenga utamaduni kwa kuwa kimya watu hawataki kuhoji. Ukihoji ni matusi. Lakini serikali ikiruhusu uchunguzi itasaidia kuondoa hayo yanayosemwa.
Mhe. Rais, alikataza kusiwe na uvumi bali watu wenye ushahidi wapeleke la sivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa.

Ni majuzi tu yule mwanaharakati Msiba alitamka wazi kuwa Magufuli aliuliwa. Mbona serikali ipo kimya haija mhoji msiba atoe ushahidi kuhusu tuhuma za Magufuli kuuwawa. Rais Samia anasema madaktari walitoa taarifa kafa kwa ugonjwa wa moyo, hivyo tusihoji kwa kua madaktari wamesema.

Rais anatufunga mdomo. Kwani mara ngapi madaktari udai mtu kafa kwa hiki, lakini uchunguzi ukifanyika unakuta ni tofauti. Mfano Yasin Arafat taarifa ya madaktari ilikuja kutofautiana na uchunguzi ulofanyika. Ikaonekana aliuwawa kwa sumu.

Nachojiuliza ni kwanin serikali ilificha kuumwa kwa Magufuli, na hata siku alokufa inadaiwa si hiyo. Haya yalisemwa wazi na Tundu Lissu pamoja na Lema.
Wakishirikiana na vyombo vya habari vya Kenya. Lissu katika twiter aliongea magufuli tayari kafa. Lakini vyombo vya ndani vilibaki kimya na serikali pia, ilificha.
Na viongozi walikanusha hasa Waziri Mkuu alidai Rais Magufuli alikuwa mzima na anachapa kazi. Baadae aliye kuwa mkuu wa mkoa Mbeya alisema kaongea na Rasi Magufuli yupo mzima anachapa kazi.

Makamu wa Rais akiwa ziarani Tanga, nae alisema Rais Magufuli hajambo na anawasalimia wananchi. Baadae akatoa kauli mtu ni kawaida kusumbuliwa na mafua ya hapa na pale.
Hii kauli ilileta utata!

Kesho yake Makamu wa Rais akatangaza msiba wa kitaifa. Kuwa Rais Magufuli kafariki.
Huu mtililiko unaleta mashaka na inaonesha serikali ilikuwa inaficha jambo. Kuanzia Rais Samia, Waziri Mkuu na alie kuwa RC Mbeya waombe masamaha kwa kupotosha jamii.

Pia serikali itueleze kwa nini Magufuli alikuwa anaumwa lakini ilifichwa. Wananchi walikosa haki ya kumuombea.
Haya yote yanafanya uhalali kuwa iundwe tume huru kuchunguza kifo cha Magufuli. Haya mambo ya kunyamazishana si haki. Kwanini serikali haitaki uchunguzi? Wakiguswa wanakuwa wakali?
Kunasiku watu watakwenda mahakamani kudai haki ya kuundwa tume huru kuchunguza kifo cha Magufuli.

Hatuwezi kuwa tunanyamaza wakati viongozi wa Taifa wanakufa, pasipo hata kujiridhisha?
Ifikie wakati kuwe na uchunguzi.
Rais Samia, leo watakupamba usifanye uchunguzi, lakini kikulacho siku zote ki nguoni mwako. Kuwa makini, usidhani kushabikiwa na kupigiwa makofi ndo kupendwa.

Well
Si wewe pekee uliefutiwa uzi wa aina hio humu nakumbuka kuna mshiriki mmoja alikuja na mada " Utata juu ya kifo cha Magufuli " pia waliufuta ule uzi, alielezea vyema sana na utata wenyewe uligusia kwenye ;

1. Hujuma katik kifaa cha pacemaker
2. Ujio wa wageni kutoka china
3. psu ndani ya psu

Au tutegemee kuna utata zaidi ambao haukuzungumwa hapo

Matukio yanayozalisha maswali ( ? ) ni mengi ikiwemo hilo taarifa za mgonjwa kuvuja hata kabla ya kifo na mbaya zaidi circle yake ( PM, Makamu, Wakuu wa mikoa nk ) haikua na taarifa na kama walipewa basi ni za uongo.

Hivi unadhani ni kweli Chalamila, Majariwa na Makamu walikua wanajua kuwa mzee amefariki ? ALAFU wao wakaamua tuu kusema yuko anapiga kazi ama yupo nimewasiliana nae. Inawezekana ?

Mbaya zaidi mtu tuu wa nje kabisa ya mfumo yuko full detailed na anatoa dhihaka juu ( Lema, Lissu na wengineo )

Mpaka taarifa za hayati kusafirshwa kwenda kenya walilijua and sishangai Kigogo kuwa na kibendera cha kenya kwenye account yake, hakipo kwa bahat mbaya

Kuna mambo mengi kweli yana leta utata.

Kuna umuhimu wa kuundwa Tume ituletee majibu, Lakin question comes what if they will lie ?
 
Serikali ilishatoa sababu ya kifo cha marehemu! Uchunguzi wa nini tena? Lakini hilo halitoshi, Rais Mpya naye alisema kama watu wana ushahidi, basi waupeleke kwenye vyombo usika kwa ajili ya uchunguzi!

Hivyo kama una wasiwasi, anzisha uchunguzi wako wa chini kwa chini ili huo ukweli ubainike. Ila sisi wengine, tumeshakubali matokeo.
Mimi si serikali, Ningekuwa serikali ningefanya. Nachoongelea hapa kwanini kumekuwa na utata, toka anaumwa ilifichwa. Matamshi ya kuambiwa tu na madaktari hatuhitaji. Kama walitundanganya wakati anaumwa, ni kipi tutaamini. Tunachotaka ni uchunguzi huru.
Kuambiwa tupeleke ushahidi, ni maneno matamu ya kutaka kuchunguzi usifanyike. Swala Rais aunde Tume huru, watu watakuwa huru kupeleka huo ushahidi.
Uwezi mwambia mtu apeleke ushahidi, bila huyu mtu kutojua apeleke wapi, na je usalama wake utakuwa vipi?
Swala unda tume huru uone kama watu hawatopeleka ushahidi.
Watanzania si watoto sasa kuelezwa kauli za kudanganywa na kutishiwatishiwa.
 
Je wewe umewahi kujiridhisha na vifo vya ndugu zako au unajitutumua tu.


Mimi nashauri iundwe TUME HURU YA UCHAGUZI
Siwezi ingia hapa kuweka mambo binafsi ya familia, maswala ya familia umalizwa kifamilia. Na sijaongelea maswala ya kifamilia.
Naongelea maswala ya kitaifa. Alie kufa ni Rais wa Jamhuri ya muungano. Alilipwa mshahara na kutunzwa kwa kodi za watanzania. Kikubwa alikuwa mzalendo wa Taifa hili. Uchunguzi wa kifo chake ni muhimu. Kinakuuma nini uchunguzi ukifanyika?
 
Back
Top Bottom