Napendekeza iundwe Tume Huru ya kuchunguza kifo cha Hayati Magufuli

Napendekeza iundwe Tume Huru ya kuchunguza kifo cha Hayati Magufuli

Sankara aliuwawa kwa bunduki. Huyu alikuwa mgonjwa tangu alipokuwa mbunge na pengine kabla ya hapo.

Umeshajiuliza ni kwanini hakupanda ndege kwenda Ulaya hata mara moja?. Fanya kazi ndogo tu kuliko kulialia hapa jukwaani.

Nenda hospitali ya Mzena na omba taarifa za kuugua mpaka kufa kwa mheshimiwa JPM. Mengine yote unayoyaandika ni hisia tu za jumla jumla.

Mimi na Wewe tutakufa hakuna aliyeandikiwa na Mungu maisha ya milele.
Kuuwa ni kuuwa tu, iwe umeuwa kwa risasi, uwe umeuwa kwa sumu yote ni mauaji. Pia soma sheria za uchunguzi wa vifo zinasemaje. Uwezi nambia mie niende mzena, sihusiki na uchunguzi. Ila nahusika kudai haki kufanyika.
Naamini ipo siku inakuja, iwe miaka zaidi ya kumi ijayo. Ila haki haipotei. Na msimamo wangu hautabadiliswa. Nasimamia kuundwa tume hata usemeje.
 
Kama ikifahamika Mungu ndiye aliyefanya hivyo mtafanyaje?
 
Ok, kaunde tume ya vifo vya ma-Rais waliotangulia basi. Unajitia ujuaji na hujui lolote, serikali ina namna yake bora kabisa ya kuchunguza na kutoa taarifa na bahati nzuri taarifa ya chanzo cha kifo tumeshapewa, sijui unataka uchunguzi wa nini!!?? Kama umeumia sana nenda Chato kachunguze.
Weye ndo unaejitia ujuaaji hata ujui taratibu za kuchunguza kifo cha utata unadai mimi ndo nichunguze inaonesha ambavyo unaupungufu wa uelewa bali umejawa ushabiki.
 
Kuuwa ni kuuwa tu, iwe umeuwa kwa risasi, uwe umeuwa kwa sumu yote ni mauaji. Pia soma sheria za uchunguzi wa vifo zinasemaje. Uwezi nambia mie niende mzena, sihusiki na uchunguzi. Ila nahusika kudai haki kufanyika.
Naamini ipo siku inakuja, iwe miaka zaidi ya kumi ijayo. Ila haki haipotei. Na msimamo wangu hautabadiliswa. Nasimamia kuundwa tume hata usemeje.
Hayo unayoyaongea yalisikika mwaka 1984 baada ya Sokoine kufa kwa ajali pale Morogoro na mpaka leo hakuna habari yoyote ya nani haswa alihusika na kifo chake.

Hayati JPM alikuwa ni binadamu kama wewe, mwenye matatizo ya kiafya ambayo kiungwana hatupaswi kuyasema humu jukwaani.

Kifo chake ni sawa na vifo vingine vingi tu, ni sisi tuliyempenda sana ndio tunaamini katika uwepo wa nadharia za ajabu.
 
Habar watanzania lengo langu la kuanzisha huu uzi si kwa Nia Mbaya ila nikutaka tu Kumaliza Maswali ya Watanzania wengi wanao shuku kua Hayat kafanyiwa hujuma.

Baada ya kuona mambo mengi Yanayo endelea kwenye mitandao ya kijamii na mitaani. ni wazi kabisa Baadh ya watanzania walio wengi Wana shuku kifo cha Hayat Magufuli na kudhan kua kifo chake kina Hujuma.

Serikal iheshimu mawazo ya watanzania tunao tilia shaka kifo cha Rais wetu na izingatie kwa kuunda Tume huru ya uchunguzi.

Mimi Binafsi nikikumbuka Tukio la ule Moshi uliomfata Hayat Magufuli Mtwara alipokua kwenye Gari bila kujulikana wapi umetokea na kuzua Taharuki nazid kua na mashaka kua Huenda zile zilikua baadhi ya mbinu za kutaka kujaribu na zilishindwa Lakini waliojaribu hawakuacha.

Huwezi kusema ule ulikua uchawi sababu hakuna uchawi na wala siamini uchawi kama upo.

Sasa ili kujiridhisha Basi serikal ifanye uchunguzi na uchunguzi uwe wa wazi ili kufuta hii shauku ya Baadhi ya watu kwani ikiendelea ivi na serikal kukaa kimia huwezi jua Baadaye itakua na madhara gani pia huto jua maadui baadae wanaweza kuutumia huu uvumi kama silaha so nibora serikal ilimalize kwanza ili swala kwani kila siku mambo yanazid kupamba moto.

Video ya tukio la moshi hio apo chini.


Tume ya korona inatosha kwa jambo hili wanajua ukweli.
 
Upumbavu acha weye unae ongea bila kujua nini maana ya uchunguzi. Kwanini kuumwa kwa Rais kuligichwa? Leo ndo tunaambiwa kafa kwa matatzio ya moyo.
Ndo maana tunataka uchunguzi.
Pia uwe na ababu kama ukufundishwa adabu na wazazi wako. Na nikwambie tu mimi sitishwi na kutukanwa. Ni mtu wa misimamo. Kutukana kwako walaa hakunitishi au kunikatisha tamaa. Na mtu anae tukana anaonesha kaishiwa hoja. Na pia malezi yake alopata yana mushikheri.
Hunipotezei muda tena, nishajua najibishana na mtu wa aina gani. Pole nawapa wazazi, ndugu na familia yako, wanavumilia sana kuishi na wewe. Bye.
NB: ukianza uchunguzi uniambie nikusaidie usafiri wa Chato.
 
Sisi Watanzania hatuhitaji uchunguzi wowote juu ya kifo cha Mwendazake, Maana kifo chake hakina utata lakini pia tunaomba uchunguzi katika vifo vyenye utata kama Kifo cha Ben Saanane, Azory Gwanda, Lwajabe nk.

Naomba kuwasilisha kwa niaba ya Watanzania Walio wengi.
 
Kitendo cha kuwambia mtoa hoja kwamba aende Chato akachunguze, inathibitisha umetumwe kuja kuleta vitisho.

Mziki huu sio kidogo jidanganyeni na kadri siku zinavyoenda ndivyo moto utazidikupamba moto beyond control
Fanya kazi wewe, acha kubwabwana mtandaoni. Haya unayoandika yatakugharimu muda si mrefu. Hatuwezi kuwafumbia macho wapumbavu wachache wanaotaka kuichonganisha serikali na wananchi wake, HATUWEZI.
 
Kweli kabisa wanyonge huwezi kuwakuta humu. Wale waliotandika nguo zao barabarani hao ndiyo wanashauku .humu utawakuta wahujumu uchumi, waliotumbuliwa ,vyeti feki, mafisadi n.k
Wewe ni nani kati ya hao? Ni fisadi, mtumbuliwa au...?
 
Watanzania hao wenye shuku na uchunguzi juu ya kifo cha mpendwa wetu JPM huwezi kuwakuta JAMII FORUM au TWITTER tuko wachache

Wengi sana hawana ACCESS ya hii mitandao miwili.
Kwani mlikua hamjui anategemea Mashine ya mzungu kusukuma damu? Yye anawachochea muwachukie wazungu huku yye anapumua kwa msaada wa beberu. Sasa mashine ikifeli unatafuta mchawi? Kejeli zote zile hta kutengeneza mashine ya kusukuma damu humi nchi alishindwa?

Mnafurahisha
 
Hayo unayoyaongea yalisikika mwaka 1984 baada ya Sokoine kufa kwa ajali pale Morogoro na mpaka leo hakuna habari yoyote ya nani haswa alihusika na kifo chake.

Hayati JPM alikuwa ni binadamu kama wewe, mwenye matatizo ya kiafya ambayo kiungwana hatupaswi kuyasema humu jukwaani.

Kifo chake ni sawa na vifo vingine vingi tu, ni sisi tuliyempenda sana ndio tunaamini katika uwepo wa nadharia za ajabu.
Sasa hiyo tabia ya kukaa kimya kwa vifo vya viongozi ndo tunataka yaishe. Na ipo siku yataisha. Uchunguzi utaanza kufanyika. Haijalishi kiongozi kafa lini uchunguzi ufanyika tu.
 
Naunga mkono hoja! Halafu Luhaga Mpina awe Mwenyekiti na Biswalo Mganga awe Makamu wake!

Livingstone Lusinde awe Mjumbe, Joseph Kasheku Msukuma awe Mjumbe, Ole Sabaya awe Mjumbe, Chalamila awe Mjumbe, Jenister Mhagama awe Mjumbe, Tulia awe Mjumbe, na Phillipo Mpango awe ndiye mlezi wa hiyo Tume.
Minong'ono ni Mingi Sana,,,,, JPM ameuumiza Sana moyo wangu
 
Unadhani mie sijui mtu nae ongea nae ni wanamna gani. Familia yangu haikuhusu. wewe leta hoja zako hapa siyo kuingiza mambo ya familia. Mtu akikoswa hoja ndo matatizo chochote anaropoka.
Kajisomee sheria ya uchunguzi wa vifo inasemaje ndo uje uropoke hapa.
 
Sasa hiyo tabia ya kukaa kimya kwa vifo vya viongozi ndo tunataka yaishe. Na ipo siku yataisha. Uchunguzi utaanza kufanyika. Haijalishi kiongozi kafa lini uchunguzi ufanyika tu.
Mpaka hiyo tabia ya kukaa kimya itakapokuwa imeisha mimi na wewe tutakuwa tumeshafukiwa.

Acha kupoteza muda kwa kutawaliwa na dhana nyingi potofu.
 
Mpaka hiyo tabia ya kukaa kimya itakapokuwa imeisha mimi na wewe tutakuwa tumeshafukiwa.

Acha kupoteza muda kwa kutawaliwa na dhana nyingi potofu.
Mie sipotezi muda. Binadamu tumezaliwa na makusudi hapa duniani. Na kila mtu ana vision na maono yake. Maono yako hayawezi kuwa yangu wala yangu kuwa yako.
Na uchunguzi wa kifo si dhana potofu la sivyo kusingekuwa na hizo sheria. Hata kama sinto kuwepo Kifo cha Magufuli kikachunguzwa katika nafsi ya kiroho nitakuwa mwenye furaha kwani kila jambo linasehemu ya kuanzaia.
Sinto nyamaza, nitaongea. Ila nachoamini ipo siku. Nayo inakuja.
 
Back
Top Bottom