Napinga kwa nguvu zote baadhi ya member humu kuwaona walimu kama "special group"

Napinga kwa nguvu zote baadhi ya member humu kuwaona walimu kama "special group"

Kuna harakati nimezikuta toka najiunga jamii forum na bado zinaendelea kwa baadhi ya member kuwadharau na kuwakejeli walimu wa nchi hii

Napinga kwa nguvu zote za kuwafanya walimu kama marginal group kwa kigezo cha mshahara na maisha kiujumla

Nakataa unyanyasaji huu wa kifikra kwa walimu eti kisa some of them walienda kwa olevel certificate

Hata kama imefika wakati walimu wakawa wengi mtaani kwa sababu ya kimfumo bado haiwafanyi walimu wadharauliwe kwani kada nyingi bado zinasota kwenye suala la ajira

Nchi hii hakuna mwenye afadhali tukija suala la maslahi hasa walio halmashauri na tukija kwenye mishahara bado utakuta mfumo unaotumika kulipa watumishi ni kulingana na kiwango chao cha elimu kwa kada zote

Kuhusu hali ya kimaisha ngazi ya halmashauri wote ni wagaa gaa na upwa wanakula wali bila mchuzi dharau zinatoka wapi?

Tukija superiority ya kada michepuo ya kada zingine na ualimu mtiririko ni uleule either mtu aende olevel certificate, advance certificate au chuo moja kwa moja

Kwanini walimu wadharauliwe? Kwanini tuwakejeli? Nchi hii tunategemeana hii ni ecosystem bila mwalimu bila dactari na kada zingine hakuna mtiririko wa uendeshaji nchi tuheshimiane
Sawa mwalimu,somesha watoto wako wote ualimu,mnyororo wa umaskini utakuwa nawe daima, nakutakia umaskini mwema amina
 
Kwani moderators wa JF uwa wanafurahia mada za kila siku za kuwakejeli walimu ndiyo maana uwa hawazifuti? Wenyewe wakiguswa kidogo tu wanafutilia mbali nyuzi zake muda huo huo.
 
Ukiwa unakasirika na kila maoni yanayotolewa humu JF utawehuka bure... Hili ni jukwaa la fikra huru, humu kuna kila aina ya watu...
Kimsingi maoni yote yana mantiki ukiona kilichoandikwa na mwenzako hukielewi maana yake hujakomaa kifikra...
Sasa unakuta kuna Mwl anapokea million 1 kwa mwezi halafu kuna mimi nipo private sector napokea laki3 ila kilasiku nawatukana walimu humu, unadhan nani mgonjwa wa akili?
Walimu wanatucheka sana tunavyo waona cheap, nilichogundua Mwl anapokea mshahara ila kwa siku anafanya kazi masaa yasiyozidi 4, hapo kama akiwa ana vipindi kama hana wengi hawaendi kazini wanafanya mambo yao binafsi...🙄

WaTz wengi tuna kufa mapema kwasababu ya chuki wivu makasiriko husda vinyongo na roho mbaya...
Una akili sana.Kazi zote huwa ziko hivi,ama ikupe fedha nyingi lakini itakunyima muda wa kupumuzika,au ikupe fedha za kawaida tu,lakini itakupa pia muda wa ziada wa kupumuzika.
Think about this.Mwalimu ana muda mwimgi wakutokuwepo kazini(wanafunzi wakifunga).Pia muda wake wakuwa kazini ni mfupi.Mwalimu mwenye akili ataugeuza muda wote huo wa kuwa huru kuwa fedha.Advantage nyingine ni kuwa ni rahisi kwa mwalimu kupanda madaraja kiutumishi na kufikia kiwango cha juu cha mshahara,kuliko kada zingine.
Walimu wenye akili wameshaona hiyo fursa ya muda mwingi wa ziada,na sasa wanatafuta tu pesa.Off course hawakosi walimu wasioona fursa waliyonayo,kama ilivyo kwenye kada zingine pia.Sio wafanyakazi wote wa TRA kwa mfano wana maisha mazuri.Wengine wanaishi kawaida tu.
WALIMU POPOTE MLIPO,MSIFADHAISHWE NA KEJELI ZA WATU HUMU.WENGI WAO WANAOWAKEJELI HAWANA HATA NUSU YA MAISHA MNAYOISHI.


KWA MEMBERS WENGINE HUMU,UJUMBE WANGU KWENU NI KUWA,NI MTU MPUMBAVU TU ANAWEZA KUKEJELI KAZI YA UALIMU,PAMOJA NA WALIMU WETU.KEJELI ZOZOTE KWA WALIMU ZINAONYESHA JINSI GANI HAUJITAMBUI NA ULIVYO LIMBUKENI TU
 
Back
Top Bottom