Nimeamua nikazeekee kijijini kwa sababu zifuatazo:-
Kule kijijini nitapata hewa safi isiyokuwa na mchafuko
Kule kijijini nitapata majirani wema wasiokuwa na choyo
Kule kijijini tutakuwa tunatembeleana bila chuki
Kule kijijini tutakuwa tunakunywa togwa pamoja
Kule kijijini tutapunguza msongo wa mawazo
Kule kijijini tutaingia shamba lolote kuchuma matunda na kula
Kule kijijini tutakuwa tunasikia milio ya ndege na viumbe mbali mbali
Kule kijijini tutafurahia uoto wa asili
Kule kijijini tutakuwa tunaenda kuwinda kama sehemu ya michezo
Kule kijijini tutapata marafiki wengi ambao sio wanafiki
Kule kijijini tutakuwa tunatembeleana panapotokea mmoja wetu anaumwa.
Kukaa kwenye nyumba ya nyasi yenye hewa safi na ya kuvutia
Kula vyakula vilivyopikiwa kwenye vyungu na kuwa na ladha nzuri
Kendwa kuogelea mitoni na kuvua samaki kama sehemu ya michezo na uwindaji
Kwa ujumla maisha ya kijijini yatakuwa ni mazuri sana
View attachment 3121969
Kwa nyie mnaobaki mjini, nawaachia mpambane na:-
Majungu na fitina zenu
Mchafuko wa hali ya hewa
Jua kali
Msongamano wa watu
Makelele ya baa na kumbi za starehe zinazoharibu utulivu wa ubongo
Misongo ya mawazo kutokana na changamoto za kimazingira
Kudharauliwa na vijana
Kununua kila kitu; nyanya, yai ,mchicha n.k
Kutokuwa na marafiki wa kweli
Kila mmoja kumuona mwenzie fursa
Kuzeeka kabla ya umri wako
Kupata magonjwa ya moyo na presha n.k
Kula vyakula vyenye kemikali katika kukuzia au usindikaji
View attachment 3121971
Fanya maamuzi mapema; njoo kijijini tukawinde kanga pori, sungura, n.k pamoja na kuongeza miaka mingi ya kuishi.