Narudi zangu kijijini, maisha ya mjini siyataki tena

Narudi zangu kijijini, maisha ya mjini siyataki tena

Vyote hivyo haviji hivi hivi bila kushika jembe na shoka sharo wew unaweza
Mimi ni muwindaji mzuri sana, tutakuwa tunaenda kuwinda
wind.jpg
 
Kijijini maisha sio marahisi kama unavyofikiri.

Utajuta na kutamani kurudi mjini.

1. Hospitali zipo mbali.

2. Baadhi ya maeneo hakuna maji safi na salama.

3. Ushirikina uliopitiliza.

4. Wivu uliopitiliza.

5. Barabara za vumbi.

6. Kukaa gizani ni kawaida .

7. Huduma za kifedha zipo mbali.
 
Nimeamua nikazeekee kijijini kwa sababu zifuatazo:-​
  • Kule kijijini nitapata hewa safi isiyokuwa na mchafuko​
  • Kule kijijini nitapata majirani wema wasiokuwa na choyo​
  • Kule kijijini tutakuwa tunatembeleana bila chuki​
  • Kule kijijini tutakuwa tunakunywa togwa pamoja​
  • Kule kijijini tutapunguza msongo wa mawazo​
  • Kule kijijini tutaingia shamba lolote kuchuma matunda na kula​
  • Kule kijijini tutakuwa tunasikia milio ya ndege na viumbe mbali mbali​
  • Kule kijijini tutafurahia uoto wa asili​
  • Kule kijijini tutakuwa tunaenda kuwinda kama sehemu ya michezo​
  • Kule kijijini tutapata marafiki wengi ambao sio wanafiki​
  • Kule kijijini tutakuwa tunatembeleana panapotokea mmoja wetu anaumwa.​
  • Kukaa kwenye nyumba ya nyasi yenye hewa safi na ya kuvutia​
  • Kula vyakula vilivyopikiwa kwenye vyungu na kuwa na ladha nzuri​
  • Kendwa kuogelea mitoni na kuvua samaki kama sehemu ya michezo na uwindaji​
Kwa ujumla maisha ya kijijini yatakuwa ni mazuri sana

View attachment 3121969

Kwa nyie mnaobaki mjini, nawaachia mpambane na:-​
  • Majungu na fitina zenu​
  • Mchafuko wa hali ya hewa​
  • Jua kali​
  • Msongamano wa watu​
  • Makelele ya baa na kumbi za starehe zinazoharibu utulivu wa ubongo​
  • Misongo ya mawazo kutokana na changamoto za kimazingira​
  • Kudharauliwa na vijana​
  • Kununua kila kitu; nyanya, yai ,mchicha n.k​
  • Kutokuwa na marafiki wa kweli​
  • Kila mmoja kumuona mwenzie fursa​
  • Kuzeeka kabla ya umri wako​
  • Kupata magonjwa ya moyo na presha n.k​
  • Kula vyakula vyenye kemikali katika kukuzia au usindikaji​
View attachment 3121971

Fanya maamuzi mapema; njoo kijijini tukawinde kanga pori, sungura, n.k pamoja na kuongeza miaka mingi ya kuishi.
Umenikumbusha kupiga hodi mtoni tulipokuwa tunaenda kuoga mtoni
 
Maisha ya mjini kila siku ni mateso, muda mwingi unaupoteza bara barani; achilia mbali stress za hapa na pale
Kuna jamaa yangu tulikutana baada ya miaka kadhaa kukatika ananiuliza dogo umekuwa mlevi halafu mbona unazeeka hivi wakati hata bia sinywi ila nilikuwa nauza ndani ya vingunguti

Ujue ikiwa unachelewa kulala na unaamka mapema ngozi inafubaa unapoteza mvuto hata akili inapunguza ubora wake wa kufikiri, kumbukumb n.k
 
Kuishi mjini haswa dar kuna hitaji uwe na moyo mgumu, sisi tusiopenda heka tulikimbia muda sana aisee, na hiyo hali ya hewa ilivyo ngumu nduo balaaa... Karibu karne ya tisa mkuu, huku tunaishi kijamaa mjini ni ubepari.
Mjini mkikutana mtaani mnakuwa kama hamjuani, kila mmoja ana changamoto zake
 
Back
Top Bottom