Narudi zangu kijijini, maisha ya mjini siyataki tena

Narudi zangu kijijini, maisha ya mjini siyataki tena

Kweli mkuu, simu ni kisababishi namba moja kilichosababisha kupungua kwa upendo katika jamii; imeondoa ile dhana ya kutembeleana na kusaidiana.​
Simu ni mtihani mkubwa sana kwa jamii
Kuna watoto wa shule ulaya waliulizwa mmoja mmoja kuwa je unatumia simu masaa mangapi kwa siku?
Yaani wengine mpaka masaa 7 kwa siku
Watu wazima ndio kabisa
Mtu unamkuta anawasiliana na ndugu kwa simu ilhali anaweza kwenda na kukaa nao hata saa moja
Maadili yamekufa kisa simu
Simu ni mpango mzima wa kuwafanya wengi wasiwe wabunifu
Kutwa jitu linacheka na simu badala ya ku socialize na wenzie
Ukiuliza unaweza kuiacha simu kwa siku ngapi bila kuigusa wengine wanakuambia eti ntakufa ndio uhai wangu 😄
Ukimuuliza tena inakuingizia sh ngapi anakenua meno
 
Unaenda kijijini kwenda kudinya nyama kwa nyama??
Unaenda kijijini ambako wahatumii mafuta ya kula zaidi ya mawese??

Kila la heri ila cha msingi Katie mimba za kutosha ndio mtaji wa kwanza wa mwanakijiji.
Na kule wapo..
kir.jpg
 
Kuna vijiji vina mandhari nzuri sana, hatujazaliwa ili tukue,tuzeeke, na tufie sehemu zenye msongo wa mawazo; kubadili mazingira ni muhimu.
Kabisa mkuu maisha ya dar kero nyingi hewa Chafu hulali vizuri kelele za bar na vigodoro ni shida tupu ukitaka kwenda sehemu hujui utafika saa ngap kero tupu maisha ya dar nilikimbia mda sana
 
Nimeamua nikazeekee kijijini kwa sababu zifuatazo:-​
  • Kule kijijini nitapata hewa safi isiyokuwa na mchafuko​
  • Kule kijijini nitapata majirani wema wasiokuwa na choyo​
  • Kule kijijini tutakuwa tunatembeleana bila chuki​
  • Kule kijijini tutakuwa tunakunywa togwa pamoja​
  • Kule kijijini tutapunguza msongo wa mawazo​
  • Kule kijijini tutaingia shamba lolote kuchuma matunda na kula​
  • Kule kijijini tutakuwa tunasikia milio ya ndege na viumbe mbali mbali​
  • Kule kijijini tutafurahia uoto wa asili​
  • Kule kijijini tutakuwa tunaenda kuwinda kama sehemu ya michezo​
  • Kule kijijini tutapata marafiki wengi ambao sio wanafiki​
  • Kule kijijini tutakuwa tunatembeleana panapotokea mmoja wetu anaumwa.​
  • Kukaa kwenye nyumba ya nyasi yenye hewa safi na ya kuvutia​
  • Kula vyakula vilivyopikiwa kwenye vyungu na kuwa na ladha nzuri​
  • Kendwa kuogelea mitoni na kuvua samaki kama sehemu ya michezo na uwindaji​
Kwa ujumla maisha ya kijijini yatakuwa ni mazuri sana

View attachment 3121969

Kwa nyie mnaobaki mjini, nawaachia mpambane na:-​
  • Majungu na fitina zenu​
  • Mchafuko wa hali ya hewa​
  • Jua kali​
  • Msongamano wa watu​
  • Makelele ya baa na kumbi za starehe zinazoharibu utulivu wa ubongo​
  • Misongo ya mawazo kutokana na changamoto za kimazingira​
  • Kudharauliwa na vijana​
  • Kununua kila kitu; nyanya, yai ,mchicha n.k​
  • Kutokuwa na marafiki wa kweli​
  • Kila mmoja kumuona mwenzie fursa​
  • Kuzeeka kabla ya umri wako​
  • Kupata magonjwa ya moyo na presha n.k​
  • Kula vyakula vyenye kemikali katika kukuzia au usindikaji​
View attachment 3121971

Fanya maamuzi mapema; njoo kijijini tukawinde kanga pori, sungura, n.k pamoja na kuongeza miaka mingi ya kuishi.
Sawa
 
Back
Top Bottom