Nashauri nafasi ya Urais tumpe Mzungu ili atuletee maendeleo

Nashauri nafasi ya Urais tumpe Mzungu ili atuletee maendeleo

Sahihi sana,aweke miingizi yake.

NGO nyingi sana ,wako vizuri sanaaa
 
Ndugu zangu Watanzania napendekeza Wazungu wagombee nafasi ya Urais ili watuletee maendeleo,tumeona katika shughuli za kimaendeleo tumewapa bandari ndugu zetu DP World,tumefanikiwa, Tanesco napo panasua sua tumwongezee DP World aweze kuleta Umeme wa uhakika wakikataa tuwaite tena Net Solution ili watuendeshee shirika letu la Umeme,bado tuna idara nyingi pia zimedorora kama idara za maji zote za mijini na vijijini nchi nzima kama nyongeza,baada ya hapo wapewe na hospitali/zahanati/vituo vya afya vyote nchi nzima kama bonus ila nimeona tunazunguka bure tufanye kama walivyofanya Zimbabwe,wamewaita tena Wazungu waje walime kwenye mashamba makubwa plantations maana Wazimbabwe hawawezi kulima,Wazungu wameitikia wito wamekuja na wameanza kulima, Zimbabwe imeanza kuwa ya kijani badala ya jangwa,kwa nini sisi Watanzania tusiwaite Wazungu waje wagombee urais na chawa wawapigie kampeni washinde urais na nchi yetu iongozwe tena na mzungu,tuanze kula nyama za kwenye kopo,tufufue kile kiwanda cha Tanganyika Packers, tufufue Ceramic kiwanda cha vyombo vya Udongo pale Morogoro,Tufufue viwanda vya nguo Polyester na Mwatex,Viwanda vya kutengeneza magari aina ya Nyumbu,viwanda vya kutengeneza viatu kama Moro Shoes,Wazungu walete ofisi zao kubwa kubwa za UN na NGO's makubwa tuongee kiingereza kama Kenya,hatutaongea kiswahili tutaongea kiingereza,mnaonaje Watanzania!?
Kinachotunyima maendeleo na kinachosababisha wizi serikalini katika taifa hili ni UBAGUZI WA RANGI , KIKANDA na HATA UDINI NA UKABILA!
MUNGU hakuruhusu bahati mbaya tuchangamane damu, wako wahindi, wazungu,machotara , waarabu na wengine weeengi wazawa wa sampuli nikizotaja hapo! Tatizo ni fikra mbovu iliyojijenga katika falsafa ya majina kama wanyonge, mabeberu, wanyonyaji, wakoloni ! Ni sawa ilikuwa sawa kutumia falsafa hizi kipindi cha ukombozi wa bara la afrika! Lakini kwa sasa tunapigania ukombozi upi!!? Ukombozi wa nyakati zile ulikuwa wa kukataa mabavu, kwasasa ni mtu akikuzidi akili uchange vizuri zako ukatae au ukubali akutawale kimikataba! Hatuna uwezo wa kuliendesha taifa kwa kutegemea genetics moja ya mzunguko wa vizazi wa wanasiasa tuliokuwa nao na tunaoendelea nao! Nilazima kwa fikra zisizo za kibinafsi tujichanganye kama taifa stars tupambanie taifa!
Lazima tuanze kuwa na wanasayansibwa kivita, matibabu, kilimo , biashara , madini bila kutegemea kuwakodisha kutika nje maana tunao ila ndio hivyo kwa fikra za ukombozi wa kutoka kwa mkoloni dhambi ya ubaguzi inatutafuna kwa pigo la umasikini na kulibariki jina la WANYONGE!
Lazima tubuni uchumi wetu kama brands hili linawezekana kabisa! Mifumo ya elimu ya kukarirusha watoto mambo yasiyo na tija katika kujiajiri nayo yafutwe!
Siasa za tanzania kwa 60% ni fitna 40% taifa linabebwa na mfumo wa dunia na rasilimali zetu ambazo kwa namna moja au nyingine lazima zifuatwe na wateja ama walaji kutoka nje na mikopo! Tatizo hizi 60% za siasa zingetumika katika siasa kazi , siasa ubunifu , siasa uchumi hakika Tanzania ingekuwa mbali mara 50 kuliko Afrika ya kusini hata Nigeria ama Egypt! Tatizo ni mfumo wa mzunguko wa aina ya wanao endesha siasa za taifa hili! Siwalaumu, wanamchango, ila tuchangamane tulipiganie Taifa!
Ni maoni tu!
 
Una hoja japo umewasilisha bandiko kimzaha sana.
Naona ndugu yangu fisadi wamekukatisha tamaa kabisa. Maana fisadi ni mawakala wa hao wazungu kwa hivyo wewe unaona bora tuwape wazungu hadi urais. Japo tukate gharama ya hawa wakala wazungu wenyewe wapate chao kweupe😂🤣...au sio bhana🤣🤣
 
Mkoloni arudi tu, Bora mkoloni mweupe kuliko huyu mweusi mwenzetu.
 
Naona ngugu yangu fisadi wamekukatisha tamaa kabisa. Maana fisadi ni mawakala wa hao wazungu kwa hivyo wewe unaona bora tuwape wazungu hadi urais. Japo tukate gharama ya hawa wakala wazungu wenyewe wapate chao kweupe😂🤣...au sio bhana🤣🤣
was
 
Akili ya mwanadamu ni ileile isipokuwa ubadirika kulingana na wale inaowaongoza, wanaongozwa wakikubali kuongozwa kipumbavu naye aliyoko juu atakuwa mpumbavu tuu.Akija mzungu naye anaweza kutopea katika ufisadi hadi ukashangaa, lkn ujinga huohuo hawezi kuufanyia kwao.Uliwahi kuona wapi katka nchi za kiafrika wananchi wakiandamana kupinga mtoto wa kiongozi kusafiri bure kwenye usafiri wa uma kama ndege.Ni kama alivyo kocha wa mpira.
 
Ndugu zangu Watanzania napendekeza Wazungu wagombee nafasi ya Urais ili watuletee maendeleo,tumeona katika shughuli za kimaendeleo tumewapa bandari ndugu zetu DP World,tumefanikiwa, Tanesco napo panasua sua tumwongezee DP World aweze kuleta Umeme wa uhakika wakikataa tuwaite tena Net Solution ili watuendeshee shirika letu la Umeme,bado tuna idara nyingi pia zimedorora kama idara za maji zote za mijini na vijijini nchi nzima kama nyongeza,baada ya hapo wapewe na hospitali/zahanati/vituo vya afya vyote nchi nzima kama bonus ila nimeona tunazunguka bure tufanye kama walivyofanya Zimbabwe,wamewaita tena Wazungu waje walime kwenye mashamba makubwa plantations maana Wazimbabwe hawawezi kulima,Wazungu wameitikia wito wamekuja na wameanza kulima, Zimbabwe imeanza kuwa ya kijani badala ya jangwa,kwa nini sisi Watanzania tusiwaite Wazungu waje wagombee urais na chawa wawapigie kampeni washinde urais na nchi yetu iongozwe tena na mzungu,tuanze kula nyama za kwenye kopo,tufufue kile kiwanda cha Tanganyika Packers, tufufue Ceramic kiwanda cha vyombo vya Udongo pale Morogoro,Tufufue viwanda vya nguo Polyester na Mwatex,Viwanda vya kutengeneza magari aina ya Nyumbu,viwanda vya kutengeneza viatu kama Moro Shoes,Wazungu walete ofisi zao kubwa kubwa za UN na NGO's makubwa tuongee kiingereza kama Kenya,hatutaongea kiswahili tutaongea kiingereza,mnaonaje Watanzania!?
Kweli, na alete wazungu wenzie wacharaze viboko weusi wavivu wote.
 
Mwanzo tulidhani jamaa alitutukana kumbe alikuwa sahihi
Wenye akili kubwa huangalia mbali zaidi kuliko wenye akili ndogo.Botha alikuwa akili kubwa viongozi wachache kama wakina Mandella waliliona hilo,ndio maana mpaka Leo Makaburu wapo South Africa.

Robert Mugabe kujifanya akili kubwa ameacha Zimbabwe iko vibaya na katika kundi hili hata yule wa Butiama anaingia.
 
Back
Top Bottom