Nashauri Spika Ndugai ajiuzulu
Ki ukweli watanzania walio wengi mitandaoni wamefurahishwa na kitendo cha mama kumchamba Yustino, hata baada ya kuomba msamaha…


Yustino ajitafakari..
 
Yustino kaomba msamaha, mama kampa za utosini..

Sabaya alikwenda clouds kujisafisha na kumsifia mama, mama akamla kichwa..

Connect Dots..
 
WAZIRI MWIGULU , WANAODAIWA NI WALIPA KODI SI SERIKALI

Laiti Ndugai angesimama na hoja yake kungelikuwa na mjadala mzuri na endelevu

Kwa mfano, Mawaziri na watu wanaosema nchi zote zinakopa hawaelezi ukweli ulivyo

Nchi kama Marekani inakopa lakini deni lao linakuwa ''monitored'' na Mabunge
Mara zote utasikia mgogoro wa 'debt ceiling' kwa maana ukomo wa kukopa

Hatuwezi kukopa bila kuwa na utaratibu na hapa Spika Ndugai ana hoja

Hoja yake inajijibu, mikopo na Bajeti zinapita mikononi mwake, mbona hakuyasema Bungeni? Hii haimaanishi hana hoja, ipo lakini amejivuruga vuruga sana kwa njia nyingi

Hakulaumu Bunge kupitisha miswada ya pesa! hakuongelea mikopo bungeni
Huko nje alipoongelea amekenguka na kuomba misamaha

Leo Waziri Mwigulu kasema hakuna Mtanzania atakayegongewa au kuchukuliwa ng'ombe kwa ajili ya kulipa deni. Deni linalipwa na serikali.Kauli ya Waziri ni upotoshaji mkubwa.

Serikali haina chanzo kingine cha mapato isipokuwa Wananchi.
Japo hawatogongewa hodi milangoni , watagongewa hodi za kulipa madeni kupitia Miamala, sukari, mabati, chumvi, dawa n.k. Hivyo wananchi wanalipa deni na si serikali

Hoja nyingine ya Waziri Nchemba ni kuhusu watu kumsingizia Rais kwamba anakopa.
Waziri kasema Rais hakopi ni serikali. Hili ni kweli kabisa kwamba serikali ndiyo inayokopa

Anachosahau Waziri Nchemba ni kuwa Viongozi ndio wanamsingizia Rais pale wanapowaambia wananchi Rais katoa pesa za madawati, vyumba, Hospital n.k na kwamba Wamshukuru yeye si Serikali.

Sasa inakuwaje tabu au tatizo kwa watu wale wale wanaoamini kuwa Rais kawaletea kitu fulani kutoamini Rais huyo kaenda kukopa?

Viongozi wanambebesha Rais mzigo huu unaoitwa ''kukopa' badala ya serikali kwasababu viongozi hao kwa kujipendekeza husema ''Rais kawaletea abcd au katoa pesa abcd''

Kauli zote za kujichanganya ni katika kumjibu Spika Ndugai na hoja ya kukopa
Kwa bahati mbaya wengi hawajibu hoja wanajibu kisiasa, lakini Spika ajilaumu kwa ''kuuza ghala la silaha'' kwa kuomba msamaha kwa jambo lenye tija, hana pa kusimama anapigwa kutoka kona zote, anadhalilishwa na kabaki tu kama Spika lakini heshima hakuna

Katika sintofahamu hii hakuna namna nyingine ni Spika ajiuzulu
Kawavuruga wenzake na msamaha wake '' hajapokelewa'

Spika Ndugai it's time to go!

Alinda
 
Spika Ndugai it's time to go!
Mkuu Nguruvi3, kama kuna watu ndani ya taifa hili ambao nafasi walizoshika zinawazidi kimo ni huyo Job Ndugai. Ilikuwakuwaje hadi mtu mhuni kama huyo akazawadiwa nafasi nyeti kama hiyo...aah, eti ukada? Hebu msikilize tu anavyotamba hapa...



Hakuna jambo baya kama ulevi wa madaraka. Wakati anazawadiwa uspika, sifa pekee aliyokuwa nayo ni ile ya kutembeza bakora baada ya kumtandika fimbo kichwani mgombea mwenzake, Dr. Chilongani, hadi kulazwa hospitali.

Ndugai atembeza bakora. (2).jpg
 
Mag3 Mkuu tulijua Spika alikuwa na matatizo mengi
Mfano ni jinsi alivyo handle suala la Wabunge COVID-19

Baada ya kauli ya mikopo, Wenyeviti wa CCM wamemshukia kuhusu COVID-19 na gharama za matibau. Leo wakiwa Ikulu, Rais alifarijika na 'waliomjibu Spika Ndugai' na kusema hao ndio waliomtia moyo aendelee, kwa maana aliridhia tuhuma dhidi ya Spika Ndugai

Kubwa zaidi ni pale Rais ambaye ni mwenyekiti wa chama anapotilia shaka ''Akili ya Spika'' hapo kuna jambo zito. Leo uongozi wa nchi umemshukia na Spika hana pa kushika tena

Caucus ya CCM ni dhahri itamkataa , Bunge lote ni la CCM kwa maana Bunge halina imani naye

Kuacha wadhfa wa Uspika si jambo rahisi au jepesi. Utamu wa cheo unamtia upofu hata pale panapohitaji maamuzi magumu kama leo. Ndugai anahitaji ushauri wa ndugu haraka sana

Kinachoendelea leo ni njia nyepesi ya kumwambia 'hawamtaki'' akikomaa kamati kuu itaitwa kumjadili na utakuwa mwanzo wa mwisho katika siasa za Tanzania kwa J. Ndugai

Lipo dirisha moja lililowazi, Kujiuzulu kabla ya mauza uza ambayo ni lazima yanakuja

Rais hawezi kuwa disappointed kiasi kile akiwa na hasira tena baada ya kuombwa msamaha halafu mtu akadhani ' ni upepo utapita''.

Spika Ndugai, maamuzi mengine ni magumu lakini ni muhimu. Hili la kujiuzulu halina mbadala

Spika Ndugai JIUZULU umepoteza kila kitu hata marafiki wanakumbia leo hii.

Tusemezane
 
Coup zote huwa ziko hivyo, hawaitashia na Spika tu, wakitoka hapo Jeshini, Usalama, na mwishowe uraiani.
It’s a purge …
 
..kuna mambo rais ssh ameyasema yamenishangaza kidogo.

..unakumbuka kauli ya Gavana wa BOT kwamba tuko vizuri deni sio tatizo?

..sasa leo rais ssh katoboa siri kwamba mh.mwigulu alimpigia simu usiku mkubwa akiwa na stress kuhusu madeni ya serikali!!

..raisi akaendelea kusema kwamba sehemu ya mkopo wa 1.3 trillion imetumika kulipa madeni / mikopo ambayo ime-mature.

..tunahitaji kuzungumzia deni la taifa kwa umakini zaidi. miaka michache iliyopita tulikuwa sehemu ya nchi zilizoitwa Highly Indebted Poor Countries, tukabembeleza ili tusamehewe madeni. Leo rais anazungumzia serikali kuchukua mkopo kulipia mkopo. Je, tuko salama huko tunakoelekea?

..baada ya hayo machache, sasa naomba tuendelee na mjadala kama Spika Ndugai anao "udhu" wa kuendelea ktk nafasi hiyo.
 
Hatakuwa na hoja ya kumshtaki Rais kwasababu keshauza 'ghala la silaha' kwa kuomba msamaha

Laiti angesimama na kauli yake pengine angeungwa mkono na mpambano ungekuwa na mantiki

Kabla ya kuitisha 'hoja hiyo'' kamati kuu itamwita na kumfyekelea mbali.
Kumbuka cheo cha Uspika hakina qualification ni fadhila tu ya chama

Heshima yake ipo sehemu moja, Ajiuzulu
Hapo cha-cha
 
baada ya hayo machache, sasa naomba tuendelee na mjadala kama Spika Ndugai anao "udhu" wa kuendelea ktk nafasi hiyo.

Huu ndio wakati wa Ndugai kujua nani ni marafiki wake wa kweli na nani ni marafiki wa wakati wa kula bata tu! Marafiki wa kweli watamshauri aachie ngazi ili kulinda heshima , lakini hao wengine watamdangaya kuwa akomae tu na angoje kusikia kwa wabunge watakaporudi kwani wanadhani wengi watamuunga mkono!! Ukweli ni kwamba hakuna mbunge atakayemuunga mkono hivi sasa watamkimbia kana kwamba ana ukoma!! Ni juu yake na wake zake watunze heshima yao kwa kumsihi ajiuzulu huo uspika kabla hawajakosa kila kitu. Hiyo ndio busara iliyobaki kwake kwa wakati huu.
 
Hii nchi ngumu sana ukitofautiana na serikali.serikali iko radhi ukifanya Madudu wakuache.ili siku umetofautiana nao ndo hapo kaburi linafukuliwa.yale makosa yanaanza kuzungumzwa utadhani kile kipindi hawakuona mf wabunge COVID-19.....ngoma nzito kila mwana ccm anatafuta atatoa tamko ajulikane yuko na nani.watz kwa unafiki namba moja
 
Huu ndio wakati wa Ndugai kujua nani ni marafiki wake wa kweli na nani ni marafiki wa wakati wa kula bata tu! Marafiki wa kweli watamshauri aachie ngazi ili kulinda heshima , lakini hao wengine watamdangaya kuwa akomae tu na angoje kusikia kwa wabunge watakaporudi kwani wanadhani wengi watamuunga mkono!! Ukweli ni kwamba hakuna mbunge atakayemuunga mkono hivi sasa watamkimbia kana kwamba ana ukoma!! Ni juu yake na wake zake watunze heshima yao kwa kumsihi ajiuzulu huo uspika kabla hawajakosa kila kitu. Hiyo ndio busara iliyoki kwake kwa wakati huu.
Ni kweli kabisa, option moja pekee iliyobaki, baada ya "kuvuliwa nguo" na Rais ni kwa Mheshimiwa Spika kujiudhuru. Full Stop
 
Kubwa zaidi ni pale Rais ambaye ni mwenyekiti wa chama anapotilia shaka ''Akili ya Spika'' hapo kuna jambo zito. Leo uongozi wa nchi umemshukia na Spika hana pa kushika tena
MH SPIKA JOBU NDUGAI TAFADHARI ZINGATIA USHAURI HUU Rais hana imani tena na wewe Ndugu yangu Spika. Hivyo kuna mambo mawili ambayo unapaswa kuyafanya.

1.Wewe ni CCM kabla hujawa Mbunge wala kabla hujawa Spika. Mh Rais ni Mwenyekiti wa CCM hivyo waweza kujiuzulu kwa kumueshimu Mh Mwenyekiti wa CCM na kwa Maslahi makubwa ya CHAMA. Au 2.Usubiri Bunge likuondoe kupitia Katiba ya JMT Ibara 84-.

(7) Spika atakoma kuwa Spika na ataacha kiti cha Spika litokeapo lolote kati ya Mambo yafuatayo- (d)Ikiwa mtu huyo ataondolewa kwenye madaraka ya Spika kwa azimio la Bunge lililoungwa mkono na wabunge ambao idadi yao haipungui theluthi mbili ya Wabunge wote;

Ukisubiri hoja hiyo ya pili utaibua na mambo mengine maana Wabunge watapata muda wa kukuchambua kwanza kabala ya kukuazimia na kama hujuavyo kila mmoja wakati huu anataka kuonekana mbele ya Boss kwahiyo watakufanya uwanja wa fujo kisha watakutupa.

Chanzo: twitter
1641347545743.png
 
..kuna mambo rais ssh ameyasema yamenishangaza kidogo.
Rais SSH alikuwa 'ameghadhabika' na kauli za Spika Ndugai. Hakuwa katika hali ya kawaida
..unakumbuka kauli ya Gavana wa BOT kwamba tuko vizuri deni sio tatizo?
Hili ndilo tatizo la viongozi wetu, kwamba, ni lazima azungumze 'kupendeza' hata kama kufanya hivyo ni kusema uongo! Viongozi hawana ujasiri wa kusema hapa sivyo!!.
..sasa leo rais ssh katoboa siri kwamba mh.mwigulu alimpigia simu usiku mkubwa akiwa na stress kuhusu madeni ya serikali!!
..raisi akaendelea kusema kwamba sehemu ya mkopo wa 1.3 trillion imetumika kulipa madeni / mikopo ambayo ime-mature.
Kaeleza ukweli kinyume na Gavana. Hivi kwani ilikuwa lazima Gavana wa BoT aseme jambo!
..tunahitaji kuzungumzia deni la taifa kwa umakini zaidi.
Pengine Spika ana point, lakini kuna maswali mengi;

Miswada ya mikopo si ilipita mikononi mwake! Ilikuwaje hakuhoji au kuanzisha mjadala huo.

Juzi kasema, siku iliyofuata kasingizia media bila kuchukua hatua mwisho kaomba msamaha.

Kila mahali duniani deni linazungumzwa kwa masilahi mapana ya Taifa, hapa nyumbani majibu ni rahisi tu '' kila nchi inakopa'
miaka michache iliyopita tulikuwa sehemu ya nchi zilizoitwa Highly Indebted Poor Countries, tukabembeleza ili tusamehewe madeni. Leo rais anazungumzia serikali kuchukua mkopo kulipia mkopo. Je, tuko salama huko tunakoelekea?
Tulisamehewa na Paris Club chini ya uongozi wa PM CD Msuya.
Hoja ya nchi za HIPC ni kuwa madeni ni makubwa na kinachopatikana katika nchi hizo kinalipia Riba na si madeni na madeni yanaongezeka. Paris Club ikasamehe madeni yote.
..baada ya hayo machache, sasa naomba tuendelee na mjadala kama Spika Ndugai anao "udhu" wa kuendelea ktk nafasi hiyo.
Mkuu kwa hali ilivyokuwa leo ni suala la kumwambia sasa ni 'najisi ' .

Kuambiwa ''mtu mzima na akili.....'' inatosha .

Rais wa nchi anapohoji uwezo wa fikra za kiongozi mwenzake inatosha.
Mkuu wa nchi ana stara zake, ameongea kiungwana

Marafiki wa karibu ni wakati wa kumfikia Spika Ndugai na kumweleza ukweli, ajiuzulu

Wazee wa CCM msaidieni Mwenyekiti na mzigo huu, nendeni mumwambie Ndugai inatosha

Mh Ndugai, ''mtu mzima na akili ..'' utaongozaje tena! wewe ni ndege aliyekatwa mabawa

Usisubiri kamati kuu ikae, hutapewa onyo kwasababu Spika atakuwaje katika kipindi cha 'uangalizi' kama Mh Pole2?

Muda umefika, JIUZULU ondoke kwa amani si kwa heshima kwasababu sijui leo wenzako kama wamebakiza hata ya kijiko cha chai! JIUZULU
 
Back
Top Bottom