Nashauri Spika Ndugai ajiuzulu
Ni wazi kauli ya Mheshimiwa Rais Samia huyu Spika Ndugai hakutaka Rais Samia Suluhu Hassan achukue madaraka baada ya kifo cha mwendazake.

Spika Ndugai ameliendesha bunge kwa kutofata katiba kwa mfano wa wabunge Covid19 kuwa pale bungeni. Kumyima Mheshimiwa Tundu Lissu haki zake zote pamoja na yeye kujua yaliyompata (kushindwa pia kutoa wazi ripoti ya kamati ya bunge chini ya Adadi Rajabu iliyochunguza kupigwa risasi Mheshimiwa Tundu Lissu).

Spika Ndugai alikuwa na kauli ya kifedhuli na vitisho kwa mfano dhidi ya Assad na Jenerali Ulimwengu.

Ndugai Must Go kwani hawezani na Serikali ya awamu ya sita
 
Kumwondoa Ndugai ni kukata tawi ukitegemea mzizi wa uvunjwaji wa katiba na haki za binadamu utang'oka pia, lakini pia ukitegemea kupata mfumo sahihi wa uendeshwaji na usimamizi wa Serikali automatically.

Hakuna ushahidi kwamba Ndugai hakkutaka Mama aongoze nchi. La sivyo asingewapigia kampeni 2015 na 2020.

Uendeshwaji wa bunge, usiokuwa na mtengamano upo siku zote tangu siasa ya vyama vingi iingie nchini. Tofauti ni hekima na viwango vya ugandamizaji. Ndugai amefanya ugandamizaji kwa kiburi, pasipo busara, heshima wala aibu, na kiwango kimekuwa cha juu kwa kuwa huko awali hatukuona Speaker akienda mbali kiasi cha kutaka kuthibiti hata haki za kuishi za wapinzani. Mtakumbuka kipindi cha "Wanaoafiki ni wengi wameshinda..", hata pale ilipobainika vinginevyo, lakini hatukuona personal and personality attacks.

Lakini pia, ufahamu kwamba kazi ya Bunge siyo UNAFIKI wa kujenga urafiki ama kuendana na Serikali. Kazi ya Bunge ni kuisimamia serikali na kuhakikisha inatembea katika njia sahihi. Kitu ambacho mwandishi amezoea ni ile hali ya bunge kupiga makofi kila kitu kinacholetwa na serikali bila kukichambua na kukitathimini kitaalam. Labda hapa ndipo hitaji la kubadili katiba kuhusu sifa za wagombea wa Ubunge.

Kwa mtazamo wa agenda iliyoko mezani, Ndugai kama amefunguka macho na kuona kuna madudu mengi yanayofanyika ama yaliyopitishwa na bunge, ama yasiyofuata utaratibu kama ambavyo ccm imezoea akiwemo yeye mwenyewe na mihimili yote; alipashwa kuonyesha ukomavu wa kifikra, na kiuongozi.

a) Ni kweli hakutakiwa kunyamaza kwa sababu kufanya hivyo ni kuendelea kulihujumu taifa makusudi.

b) Hakupashwa kuongea mitaani kama mtu asiyekuwa na namna ya kutatua hizo ndivyo sivyo.

c) Alipashwa kupeleka agenda hizo bungeni zikajadiliwa kwa kina na yeye kama kiongozi wa Bunge, kama anavyoweze kuinfluence uvunjaji wa katiba na wabunge wasihoji, (matibabu ya LIsu, wabunge 19 wasio wateule wa rais, na wasio na vyama, n.k), bila shaka angeinfluence michango makini ya kuchambua tatizo lililopo, kiwancho chake, athari zake na suluhisho la muda mfupi na la muda mrefu. Hata kama ccm waliozoea uovu wasingempenda, Watanzania na dunia ingemwelewa sana.

d) Alikuwa na uwezo wa kukaa na viongozi wa mihimili mingine akawapa tahadhari ama akapata ufafanuzi wa hayo na kutoa ushauri yakini. Kama angeliona kuna undani usio mwema, bado alikuwa na nafasi nzuri ya kupambania haki za Watz kwa njia bora kwa sababu nafasi yake imempa access nyingi, ambazo naomba nisi list hapa.

e) Lakini pia ifahamike kwamba aliyosema, amesema mambo ya maana sana ambayo yanapashwa kuzingatiwa kama hayakuwa yakizingatiwa na diyo sababu hakuomba radhi kwa maneno aliyosema bali kwa hali iliyotokana na kusema kwake. Mwenye akili na afahamu.

f) Na kwamba si kila analolisema Ndugai, ni ofisi ya speake imesema. Kumbuka ni binadamu ambaye kama yeye anayohaki ya kuwaza, kusema na kuona kama anavyotaka bila kuunganishwa na ofisi yake. Nalazimika kuamini kwamba yote ameyazungumza kama Ndugai na si kama speaker wa bunge.

g) Visasi si mfumo wa kutoa ama kupata haki kwa jamii ya watu wastaarabu. Ndugai asishambuliwe kwa lengo la kumlipiza visasi, ama kumtweza kwa maslahi ya binafsi ya watu, bali lengo liwe kutengeneza msingi imara wa uendeshaji wa vyombo ya umma, uhuru na democrasia ya kujieleza na kutoa maoni ya watu, na kujenga Uhuru wa watu kukosoa Mamlaka zinapokosea bila kuvunja heshima ya viongozi ama kuwadhalilisha.

h) Kudhalilisha wakuu wanchi ni kuwadhoofisha na kuwafanya wasitumikie wananchi kwa morali kitu ambacho ni hasara ya kila mtu. NATEGEMEA KWA KUSEMA HIVI NITAELEWEKA SIFURAHII NA HAIFAI HATA KIDOGO pale watu wanapomtukana Mwl Nyerere, Hayati Mkapa na Hayati Magufuli bila kuelewa kwamba wale walikuwa icon za nchi yetu na kuwadhalilisha ni kudhoofisha taasis ya urais ambako mwisho wake ni dhiki kwa watu wote.

i) Ccm acheni kujigundisha kwenye taasisi ya urais kwa sababu si nafasi yenu. Sasa kwa ajili ya mambo yenu ya hila na misuguano yenu na ndani, mnataka kutuharibia nchi kwa kuanzisha marumbano na taasis ya Urais. Hatutaki. Mambo yenu huko kwenye chama lakini Serikali iacheni ifanye kazi ya kuwatumikia wananchi.
 
Tunajua hakuna utamaduni wa kuwajibika kwa matendo au kauli

Tunachosema hapa ni kwamba hata akiendelea Heshima yake ipoje?
Hivi atasema nini au atasimama wapi na kubaki na heshima
Tayari ni mtu mnyonge kama aliyetupwa kisiwani

Ni wakati sasa aangalie masilahi mapana ya Taifa!
Mkuu Ndugai amefanya na hata kusema mengi sana yenye kuutweza Utu na heshima yake kwenye Jamii na bado maisha yakaendelea.

Kupiga mpinzani wake na Gongo.
Suala la Wabunge 19, wasio na Chama.
Suala la Prof. Assad.
Kujiita Chizi ndani ya Bunge.
Kuunga mkono mada ya kuongeza muda kwa Mwendazake.
Suala la Bandari ya Bagamoyo.
N.k n.k n.k

Kwa hili la kusigana na Rais, tujiandae soon kuona amealikwa Ikulu kwenda kunywa chai. Na akitoka hapo inakuwa ni mwendo Wa kuunga Mkono na kusifia kila atakachokisema Mama.

Atasema nilikuwa sijui, ila nimeenda Ikulu nikaonana na Wataalamu Wa Uchumi wamenielewesha vizuri sana faida za Mikopo..

Ila kujiuzulu?
Tusahau kwa sasa.
 
Mkuu Ndugai amefanya na hata kusema mengi sana yenye kuutweza Utu na heshima yake kwenye Jamii na bado maisha yakaendelea.

Kupiga mpinzani wake na Gongo.
Suala la Wabunge 19, wasio na Chama.
Suala la Prof. Assad.
Kujiita Chizi ndani ya Bunge.
Kuunga mkono mada ya kuongeza muda kwa Mwendazake.
Suala la Bandari ya Bagamoyo.
N.k n.k n.k
Mengi kati ya hayo yalikuwa na ' baraka'
Kwa hili la kusigana na Rais, tujiandae soon kuona amealikwa Ikulu kwenda kunywa chai. Na akitoka hapo inakuwa ni mwendo Wa kuunga Mkono na kusifia kila atakachokisema Mama.
Itakuwa ni vema kwake, na watakaofanya hivyo watakuwa 'mataulo'
Atasema nilikuwa sijui, ila nimeenda Ikulu nikaonana na Wataalamu Wa Uchumi wamenielewesha vizuri sana faida za Mikopo..
Kwa Tanzania ya leo hili linaweza kutokea! si la kulikataa sana tukijua tumepoteza sehemu kubwa ya uwezo wa watu kifikiri. Possible!
Ila kujiuzulu?
Tusahau kwa sasa.
Tunachosema hapa ni kuwa kwa yaliyotokea jana aliposhika kipaza suati na kulia lia, na ya leo Ikulu ni ngumu sana kumuona kama ana kivazi kilichobaki mwilini. Mh anaweza kugoma kujiuzulu , swali ni moja kwake hivi kuna kingine tena kilichobaki katika sanduku la heshima yake?
 
Speaker ana more info za madeni na uwezo wa kulipa kushinda tunavyodhani.

Based on the following info:

Mama Samia: Mwigulu akanipigia simu usiku nimelala kuniambia mama kuna madeni yame mature, ila kuna mkopo wa concession akanishauri tuukakate tulipe madeni. Nikaoana hii akili.

Kwa wenye kuelewa maswala ya public debt there is a problem kwenye makusanyo.

Mateja wanaita chasing the dragon ni muda tu kabla moto aujawaka.

Nilichojifunza based on mama Samia speech; speaker ana info ni kiasi gani serikali inashida ya kulipa madeni yake based on collections za sasa ndio maana ya kutoa kauli yake.

Mama moto auko mbali you’are chasing the dragon.

Hakuna mkosoaji anaetaka mama ashindwe; the woman needs to revert back quickly to how things were under JPM.

Jumba linawaka hilo soon kwa sisi tunaoweza analyse mambo. Dah mpaka namuhurumia huyu mama wengine ukosoaji wetu sio wa chuki bali kurekebisha aipeleke nchi sawa.

Moto waja soon, kwanini watu wenye tamaa wamemuingiza huyu mama mkenge kwa kutoridhika kwao.

Watch this space tupo pabaya. Dah again kuna watu wana roho mbaya why are they exploiting this woman.

Very sad, sina tabia ya kuongopa; nawaambia kwa kumsikiliza Mama Samia mwishoni kabla ya kumuwakia speaker kinachofuata ni mshtuko wa mushroom bomb, na tatizo sio yeye bali wahuni.

Not trying to be the prophecy of doom but watch what’s next. It’s a pity to mama.

Kumsaidia tu mama uombaji msamaha wa speaker alishaonywa what you were about to say; watu wamejipanga kupambana na wahuni. Busara ni mama Samia kuirudisha nchi alipoipokea.
 
Ni wazi kauli ya Mheshimiwa Rais Samia huyu Spika Ndugai hakutaka Rais Samia Suluhu Hassan achukue madaraka baada ya kifo cha mwendazake. Spika Ndugai ameliendesha bunge kwa kutofata katiba kwa mfano wa wabunge Covid19 kuwa pale bungeni. Kumyima Mheshimiwa Tundu Lissu haki zake zote pamoja na yeye kujua yaliyompata (kushindwa pia kutoa wazi ripoti ya kamati ya bunge chini ya Adadi Rajabu iliyochunguza kupigwa risasi Mheshimiwa Tundu Lissu)
Spika Ndugai alikuwa na kauli ya kifedhuli na vitisho kwa mfano dhidi ya Assad na Jenerali Ulimwengu.
Ndugai Must Go kwani hawezani na Serikali ya awamu ya sita
Naheshimu mtazamo wako Great Thinker ila kuna Lawama zingine hapa Yeye unamuonea bali zinaenda pia Serikalini na katika System ya Taifa letu.

Kuhusu Kujiuzuru Kwake kutokana na hii Sintofahamu aliyoiibua naungana mkono nawe ( na tena Spika Ndugai alifanye hili upesi ) kwani kwa Kauli tu ya Mheshimiwa Rais Samia jana ni dhahiri kuwa hamuamini tena na hata Ndugai nae Kisaikolojia hatokuwa vizuri kwani alijua Msamaha wake ungezaa Matunda ila Mama ( Mheshimiwa Rais Samia ) ndiyo Kashindilia kabisa Msumari wa Moto.
 
Aende wapi tena, keshaomba msamaha
20220105_070952.jpg
 
Kauli alizotoa spika wa Bunge dhidi ya Mikopo ya maendeleo serikali awamu ya sita zinazotafsiriwa kama ni za kutaka kukwamisha jitihada za maendeleo ya wananchi anazofanya Rais ambaye ni na mwenyekiti wa chama chake ka kaulinza Rais leo juu ya alichofanya Ndugai anapaswa kujiuzuzu kwani inaonyesha Hatoshi.
 
Things were under JPM????????? Aisee unachekesha. Sasa jpm si ndo alikopa % 99 ya deni lote kwa miaka chini ya 6. Alikopa kwenye banks zinohitaji high returns, hakushirikisha cabinet. Alifanya haya peke ake na tunajua kabisa jpm hakuaga na hata basic knowledge ndogo ya macro economy
Ni hivi wao wenyewe kupitia Mwigulu na Dr Mpango wameongelea topics za public debt management appraisals.

Kwa lugha yako under Magufuli serikali ilikuwa inayumudu regardless ya alichokopa.

Alichokosea mama ni kuongelea simu ya Mwigulu siku zote wengine tumekuwa tukisema hana washauri wa uchumi. Watu makini wangemwambia asiongelee hiyo siri.

Moshi unafuka na moto waja, dah mpaka namuhurumia.

Kuna watu wamejipanga kuirudisha nchi ilipokuwa inaelekea chini ya Magufuli; ata mama anaweza ifanya hiyo kazi akijitoa kwa wahuni. Vinginevyo atoboi 2025 jamaa wamedhamiria.
 
Mengi kati ya hayo yalikuwa na ' baraka'

Itakuwa ni vema kwake, na watakaofanya hivyo watakuwa 'mataulo'

Kwa Tanzania ya leo hili linaweza kutokea! si la kulikataa sana tukijua tumepoteza sehemu kubwa ya uwezo wa watu kifikiri. Possible!

Tunachosema hapa ni kuwa kwa yaliyotokea jana aliposhika kipaza suati na kulia lia, na ya leo Ikulu ni ngumu sana kumuona kama ana kivazi kilichobaki mwilini. Mh anaweza kugoma kujiuzulu , swali ni moja kwake hivi kuna kingine tena kilichobaki katika sanduku la heshima yake?
He has nothing to loose.
Hana hiyo heshima ya kuilinda.
Hana mapenzi yeyote kwa Taifa.
Kikubwa ni atajishusha kwa Mamlaka ili mambo yake yaende, na amalizie muda wake..
 
Ndugai alidhamiria kumuua kisiasa mama Samia. Badala yake kauwawa yeye na wale mawaziri watakao toswa. Take my words!
 
Kauli alizotoa spika wa Bunge dhidi ya Mikopo ya maendeleo serikali awamu ya sita zinazotafsiriwa kama ni za kutaka kukwamisha jitihada za maendeleo ya wananchi anazofanya Rais ambaye ni na mwenyekiti wa chama chake ka kaulinza Rais leo juu ya alichofanya Ndugai anapaswa kujiuzuzu kwani inaonyesha Hatoshi.
Madaraka yanaweza kufanya ujisahau na kuvimba.
 
Kauli alizotoa spika wa Bunge dhidi ya Mikopo ya maendeleo serikali awamu ya sita zinazotafsiriwa kama ni za kutaka kukwamisha jitihada za maendeleo ya wananchi anazofanya Rais ambaye ni na mwenyekiti wa chama chake ka kaulinza Rais leo juu ya alichofanya Ndugai anapaswa kujiuzuzu kwani inaonyesha Hatoshi.
Mimi nilidhani mpaka Asubuhi hii nikiamka nitaanza kusikia Breaking News kuwa Job Ndugai resigns kumbe Jamaa bado tu ni defiant kwa Bunge, Wabunge, Mheshimiwa Rais na hata kwa Sisi Watanzania wa Kawaida?
 
Mimi nilidhani mpaka Asubuhi hii nikiamka nitaanza kusikia Breaking News kuwa Job Ndugai resigns kumbe Jamaa bado tu ni defiant kwa Bunge, Wabunge, Mheshimiwa Rais na hata kwa Sisi Watanzania wa Kawaida?
Mkuu waafrika tuna njaa Sana ndicho kinachotuua ama kutumaliza.
Mana ndo tunatoka Zama za kuishi mapangoni tunaingia kwa tembe house later mud walled house and glass thatched.

Unadhani angekuwa mjukuu wa Trump angekubali adhalilishwe kwa lipi.
Mie ndo Mana sipendi kuwa chini ya mtu.yaani kuelekezwa mie Cha kuongea ama kusema siwezi.
Ni aheri niishi kawaida kwa viazi na mchicha Ila niwe na furaha ya moyo kuliko Julia kuku kule Serena Ila u me wangu hauna kazi
 
Kauli alizotoa spika wa Bunge dhidi ya Mikopo ya maendeleo serikali awamu ya sita zinazotafsiriwa kama ni za kutaka kukwamisha jitihada za maendeleo ya wananchi anazofanya Rais ambaye ni na mwenyekiti wa chama chake ka kaulinza Rais leo juu ya alichofanya Ndugai anapaswa kujiuzuzu kwani inaonyesha Hatoshi.
Mkuu kama unakimbizwa chukua maficho kwanza uandike vizuri.
 
Ni wazi kauli ya Mheshimiwa Rais Samia huyu Spika Ndugai hakutaka Rais Samia Suluhu Hassan achukue madaraka baada ya kifo cha mwendazake. Spika Ndugai ameliendesha bunge kwa kutofata katiba kwa mfano wa wabunge Covid19 kuwa pale bungeni. Kumyima Mheshimiwa Tundu Lissu haki zake zote pamoja na yeye kujua yaliyompata (kushindwa pia kutoa wazi ripoti ya kamati ya bunge chini ya Adadi Rajabu iliyochunguza kupigwa risasi Mheshimiwa Tundu Lissu)
Spika Ndugai alikuwa na kauli ya kifedhuli na vitisho kwa mfano dhidi ya Assad na Jenerali Ulimwengu.
Ndugai Must Go kwani hawezani na Serikali ya awamu ya sita
Ndugai ni mpuuzi lakini ccm na serekali ni wapuuzi zaidi
 
Back
Top Bottom