Huo ni msamiati wa Ulaya na siyo Afrika.
Afrika unafukuzwa hakunaga kujiuzulu
 
Umeomba msamaha na imeonekana kwamba huko ndani ya chama tayari pazia lilishapasuka na moto ulishakolea , hakuna aliekuelewa je utaendelea kulamba miguu mtu mzima mwanaume na heshima yako , unalidhaliliaha bunge. Hukupaswa kuomba msamaha lakini ulidhani ni uungwana kumbe wenzio ni watu wa ghubu.
Ukiondoka hapo utatengeneza heshima kubwa sana hasa kwa sisi wanaume na tunaweza tukakuelewa ukirudi tena 2025 lakini kuishi miaka 4 zaidi kwa kujipendekeza , asee utakuwa umechemka , hatutakuelewa na utakuwa pengine umeiua heshima yako yote uliyoijemga katika mbio zako za kisiasa mpaka leo.
Kuna viumbe kuviruhisu vikupandie kichwani ni laana, hilo kosa mlilifanya wenyewe na mwendazake na leo hii linawacost, naamini mnajutia wote kosa hilo kwa sasa.
Nchi yote imejaa mipasho na marumbano, hela zinategemewa za kuombaomba , kazi zimesimama, ni kuitana ikulu kupeana mipasho , huu ni upuuzi na umama uliotawala nchi nzima kwa sasa, ni aibu,
Muache awatoe hao mawazori, njooni pembeni tuunde chama ili turudishe heshima ya wanaume ndio heshima ya taifa hili.
HAKUNA MWANAMKE ANAEJUA VITA.









 
Ukifuatilia hili fukuto utaona CCM wanajichanganya pakubwa sana na hilo linaonekana kwenye kauli zao...

Ishu ndogo tu ya kutoa ufafanuzi wa namna nchi inavyokopa na kulipa deni, kila mtu mwenye tija nalo huko serikalini kaibuka na kuzungumza yake...

Pia, Rais na Mwigulu kama hawapo tayari kwa Rais kuwa labelled kwamba sio 'Rais anakopa fedha' bali serikali ndio yenye kukopa, basi wawe tayari kuomba msamaha wananchi pale ambapo fedha ya matumizi inapotolewa na serikali kwenda kufanya maendeleo halafu wao kuiwekea mapambio ya 'Rais katoa kiasi fulani cha fedha kujenga hiki n kile'
 

Why ajiuzuru? Kwani yy amewekwa na Rais?
 
Na hili litapita kama yapitavyo mengine...

Ingawa kwangu cha maana na chenye tija kwa Taifa ni kuzungumzia hii mikopo na kinachofanywa / hakifanyiki na mikopo hio (Kwa kutokuunga mkono wanaohoji na kukubaliana kwamba ni sahihi kumuacha mtu ajenge nchi au atupeleke yeye binafsi anapoona ni sawa kwa mtaji wa Pesa zetu; sio Sahihi hata Kidogo....

Anayehoji anastahili maelezo na sio kejeli wala shinikizo
 
Tulia Akson Mwanjala ameshaanza kupasha misuli moto.Lolote linaweza kutokea.
 
Huyu kashajiuzulu tayari....nafikiri kuna utaratibu wa bunge kutangaza.
 
Mods unganisheni hizi NYUZI sasa imekuwa kero kila mmoja ananzisha uzi content ni zile zile.
 
Usijiuzulu hata wazo hilo usiwe nalo. Kutoa maoni yako ni haki ya kikatiba
 
Zimafutwa na kuunganishwa nyingi tuu lakini wanazidiwa
Wanajitahidi sana, naona wameshaunganisha huu uzi sasa. Ni kero kila ukiingia JF unakutana na habari zinazofanana.
Ahsanteni sana MODS.
 
Yaani mtu kutoa mawazo yake ndio ajiuzuru? una akili za ovyo sana wewe
Inategemea na mtu mwenyewe,
huyu anaeongelewa ni mgogo pia ni spika pia alikubali kuwa kibaraka wa muhimili mwingine!

Mama alisema clear kbs,

"nyumba yake ndio inapitisha hiyo mikopo"

Kimsingi huyu mgogo hajui yuko pale kwa ajili gani, na ndo anaetumika kuumiza watanzania kupitia bunge la micjongo!

Ni huyu hakutaka watanzania wajue kinachoongelewa bungeni

Wacha aning'inizwe tu"
 
Why ajiuzuru? Kwani yy amewekwa na Rais?

'Mtu mzima na akili yake...'' hili ni neno kubwa sana likhusisha akili , umri na kufikiri kwa Mh Spika
Ni kwamba Wananchi wamepewa dondoo za kutathmini uwezo wa kifikra wa Spika wao

Well, si lazima ajiuzulu kama watu wanavyoshauri hata hivyo ni wakati atathmini kama ana heshima tena mbele ya Bunge na jamii kwa ujumla. Jana pale Ikulu wenzake walitueleza mengi kuhusu yeye na kubwa zaidi ni uwezo wake wa kufikiri
 

Tunatumia mazoea ndio shida, but kama akiamua anaendelea kukaa na bado kama kiongozi wa mhimili akawa anampinga Rais wake

Ni kawaida Sana inchi zingine,

Kama akijiuzulu means hakuna mtu anapaswa kuongea anything tofaut na mawazo ya rais
 
Tunatumia mazoea ndio shida, but kama akiamua anaendelea kukaa na bado kama kiongozi wa mhimili akawa anampinga Rais wake

Ni kawaida Sana inchi zingine,

Kama akijiuzulu means hakuna mtu anapaswa kuongea anything tofaut na mawazo ya rais
Hapa lazima uelewe hoja ni nini
Kumpinga Rais kama kiongozi wa mhimili mwingine si jambo geni au baya.
Alichozungumza si kibaya au kigeni

Tatizo ni hili, kusingizia alinukuliwa vibaya
Kuomba msamaha kwa aliyosema kwa maana hajui alisema nini au alikusudia nini
Kuzungumzia miswada iliyopita mikononi mwake kinafiki
Kuhojiwa uwezo wake ''kiakili'' na Viongozi wote wakuu wa nchi

Heshima yake haipo kwasasa mbele ya jamii. Ajiuzulu tu
 

Mpaka ndugai ameomba msamaha ujue kuna kikao kilifanyika, otherwise angechuna
 
Mpaka ndugai ameomba msamaha ujue kuna kikao kilifanyika, otherwise angechuna
Yes lakini hiyo haitaondoa ukweli kuwa popote atakapokaa, simama au kutembea watu watahoji swali moja, mkuu wa nchi alitilia shaka utimamu na umri wa Ndugai.

Hana heshima popote pale.
Juzi kasingizia media leo anaomba msamaha , huyu hana maana hata akibali Spika heshima yake haipo. Suala hapa si kuondoka au kubaki, tunahoji heshima yake , heshima ya Uspika na heshima ya Bunge.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…