Nashauri Spika Ndugai ajiuzulu
Huo ni msamiati wa Ulaya na siyo Afrika.
Afrika unafukuzwa hakunaga kujiuzulu
 
Umeomba msamaha na imeonekana kwamba huko ndani ya chama tayari pazia lilishapasuka na moto ulishakolea , hakuna aliekuelewa je utaendelea kulamba miguu mtu mzima mwanaume na heshima yako , unalidhaliliaha bunge. Hukupaswa kuomba msamaha lakini ulidhani ni uungwana kumbe wenzio ni watu wa ghubu.
Ukiondoka hapo utatengeneza heshima kubwa sana hasa kwa sisi wanaume na tunaweza tukakuelewa ukirudi tena 2025 lakini kuishi miaka 4 zaidi kwa kujipendekeza , asee utakuwa umechemka , hatutakuelewa na utakuwa pengine umeiua heshima yako yote uliyoijemga katika mbio zako za kisiasa mpaka leo.
Kuna viumbe kuviruhisu vikupandie kichwani ni laana, hilo kosa mlilifanya wenyewe na mwendazake na leo hii linawacost, naamini mnajutia wote kosa hilo kwa sasa.
Nchi yote imejaa mipasho na marumbano, hela zinategemewa za kuombaomba , kazi zimesimama, ni kuitana ikulu kupeana mipasho , huu ni upuuzi na umama uliotawala nchi nzima kwa sasa, ni aibu,
Muache awatoe hao mawazori, njooni pembeni tuunde chama ili turudishe heshima ya wanaume ndio heshima ya taifa hili.
HAKUNA MWANAMKE ANAEJUA VITA.









 
Ukifuatilia hili fukuto utaona CCM wanajichanganya pakubwa sana na hilo linaonekana kwenye kauli zao...

Ishu ndogo tu ya kutoa ufafanuzi wa namna nchi inavyokopa na kulipa deni, kila mtu mwenye tija nalo huko serikalini kaibuka na kuzungumza yake...

Pia, Rais na Mwigulu kama hawapo tayari kwa Rais kuwa labelled kwamba sio 'Rais anakopa fedha' bali serikali ndio yenye kukopa, basi wawe tayari kuomba msamaha wananchi pale ambapo fedha ya matumizi inapotolewa na serikali kwenda kufanya maendeleo halafu wao kuiwekea mapambio ya 'Rais katoa kiasi fulani cha fedha kujenga hiki n kile'
 
RAIS NA KIONGOZI WA MHIMILI MWINGINE 'HANA IMANI'
SPIKA AMEPOTEZA IMANI YAKE KWA BUNGE NA CHAMA

Jana Jumatatu Spika wa Bunge la JMT Mh Ndugai alifafanua kauli ya 'mikopo na mnada wa nchi'

Spika alijitokeza baada ya 'kushukiwa vikali' na makundi ya chama na viongozi wa serikali

Spika alisema 'amenukuliwa vibaya, kipande cha video kinachozunguka si sahihi kwa alichosema'

Mwisho wa ufafanuzi ,Spika alimuomba radhi Mh Rais na Wananchi kwa ''usumbufu'' uliojitokeza bila ufafanuzi ikiwa atawachukulia hatua gani waliosambaza kipande cha video.

Mh Spika hakukana sauti ya video au kutilia shaka iwapo video imechezewa
Alichosema imepotoshwa bila kuonyesha wapi na kwa vipi.

Swali linafuata, je, alichukua hatua gani dhidi ya vyombo husika? na kwanini ilimchukua muda mrefu kujibu hoja yenye hisia kama ilivyo?

Mh Spika anasema alikuwa mgonjwa na kutoweza kujitokeza, hata hivyo ofisi ya Spika ni kubwa ingeliweza kutoa taarifa za awali ikisubiri hali ya Mh kuimarika. Hili halikutokea

Kabla ya mkutano mitandaoni kulikuwa na mazungumzo kwamba atapojitokeza atasema 'amenukuliwa vibaya' Huu ni utamaduni wa viongozi wanapokwepa kukiri au kuomba msamaha kwa matendo au kauli zao

Jumanne ya leo ndani ya Ikulu kulifanyika hafla ya taarifa ya utekelezaji wa mpango wa serikali unaohusiana na pesa za mkopo unaozungumziwa kwa utata

Viongozi wote wa serikali na chama walisomeka kwa kauli zao 'kumshambulia' Mh Spika

Mh Rais alionekana kukereka na ukweli kwamba 'taarifa za mikopo zinapita katika nyumba ' na kisha mtu anasema yaliyosemwa

Mh Rais anasema nguvu yake ni kutokana na kuungwa mkono na Wananchi katika sakata hili
Na kwamba ''wanaotazama 2025' waondoke wakajiandae vizuri

Ukifuatilia kwa undani msamaha wa Mh Spika haukupokelewa na mhimili wa serikali achilia mbali Chama chake

Mh Spika alikuwa na machaguo mawili.
Kwamba asimame na kile alichosema akiamini ni maoni yake, au
Kutoomba radhi asubiri kutetea hoja zake kwa mantiki bila kujali nini kitafuata

Kitendo cha kutochukua hatua dhidi ya ''wapotoshaji' na kitendo cha kuomba msamaha kinamwacha na chaguo moja 'Ajiuzulu'

Mh Spika atakuwa amepoteza ''vote of confidence' kutoka ''Caucus'' ambayo ni asilimia 90+

Mh Spika amepoteza 'Vote of confidence' katika Chama kufuatia matamko ya viongozi

Mh Spika amepoteza 'vote of confidence' kwa kiongozi wa Mhimili mwingine, hakusimama na kauli yake

Katika nchi nyingine hili la mihimili kutofautiana ni la kawaida, kwa nchi yetu ambako kuna mihimili imejichimbia, hili si la kawaida na linamwcha pagumu

Katika mazingira hayo Mh Spika hana pa kusimama tena kwa maana ya kwamba haungwi mkono na sehemu yoyote ya jamii japo kwa uwazi na amebaki kisiwani

Spika alipaswa kufanya alichofanya Waziri wa fedha enzi hizo bwana Edwin Mtei.
Mtei alipotofautiana na Mwl Nyerere kuhusu sera za nchi kwendana na matakwa ya IMF na WB, alijiuzulu. Miaka mingi baadaye ilibainika Mtei alikuwa Sahihi kwa maamuzi

Hadi leo Mzee Mtei anabaki heshima yake na ''role model'' ya namna gani viongozi wanapaswa kusimama na hoja zao kwa kuamini kile wanachoamini

Spika Ndugai hana uungwaji mkono ,hata kama ataendelea, kazi itakuwa ngumu sana

Kila kauli yake itakuwa sawa na kutembea juu ya miba.
Hii italiacha Bunge kupoteza nguvu zake zote kwasababu Spika ni 'symbol' ya Bunge

Mh Spika ni wakati wa Kujiuzulu, hakuna ajuaye nini kitatokea ndani ya chama chako.

Ikitokea vinginevyo aibu itakuwa kubwa kuliko ilivyo sasa.
Ni wakati ufanye tathmini na uchukue uamuzi mgumu

Jiuzulu, usimame na kile unachoamini , siyo dhambi wala kosa! ni ukomavu na ubaki mbunge

Sehemu II tutaangalia ufafanuzi wa deni na kauli za nchi duniani zinakopa

Tusemezane

Why ajiuzuru? Kwani yy amewekwa na Rais?
 
Na hili litapita kama yapitavyo mengine...

Ingawa kwangu cha maana na chenye tija kwa Taifa ni kuzungumzia hii mikopo na kinachofanywa / hakifanyiki na mikopo hio (Kwa kutokuunga mkono wanaohoji na kukubaliana kwamba ni sahihi kumuacha mtu ajenge nchi au atupeleke yeye binafsi anapoona ni sawa kwa mtaji wa Pesa zetu; sio Sahihi hata Kidogo....

Anayehoji anastahili maelezo na sio kejeli wala shinikizo
 
Wadau Watanzania Wote Tumeusikia na kuutazama MPAMBANO baina ya MIHIMILI Miwili yaani SERIKALI NA BUNGE.Mpambano huo Unatokana na Serikali kuamua Kutekeleza Bajeti iliyopitishwa na BUNGE iliyohusisha UKOPAJI.
Kwa Mshangao MKUBWA Spika wa Bunge Alihutubia Wagogo Wenzake na KUIPONDA SERIKALI kwa KUKOPA na Kudai Huenda NCHI ikapigwa MNADA.Kutokana na KAULI hiyo ya SPIKA
Mh.RAIS amehitimisha MPAMBANO LEO.
USHAURI kwa SPIKA
Nichukue Nafasi kumtaka SPIKA NDUGUI Atumie UUNGWANA aliouonyesha Jana KUOMBA MSAMAHA KUTANGAZA "KUJIUZULU" kwani "HATAAMINIKA TENA"
Tulia Akson Mwanjala ameshaanza kupasha misuli moto.Lolote linaweza kutokea.
 
Huyu kashajiuzulu tayari....nafikiri kuna utaratibu wa bunge kutangaza.
 
IMG-20220105-WA0064.jpg
 
Mods unganisheni hizi NYUZI sasa imekuwa kero kila mmoja ananzisha uzi content ni zile zile.
 
Ndugu zangu wa JF

Nitoe maoni yangu kama Mtanzania Mzalendo kufuatia kauli ya Ndugai kubeza kitendo cha Rais Samia kuendelea na Sera ya kukopa Fedha nje ya Nchi kugharamia miradi ya Maendeleo

Kauli ya Mheshimiwa Ndugai sio tu inabeza na kudharau mamlaka ya Rais bali inalenga kuhujumu jitihada za makusudi za Rais Samia kukamilisha miradi mikubwa ya maendeleo inayohitaji Fedha nyingi sana kuikamilisha

Mheshimiwa Ndugai akiwa Kiongozi wa Bunge ameshindwa kuonyesha uwajibikaji wa pamoja wa kidola na ameamua kwa makusudi kutumia nafasi yake vibaya kwa maslahi binafsi

Ieleweke Rais Samia anakopa fedha kwa maslahi ya Nchi yetu na amekuwa muwazi kwenye suala hili

Ieleweke kuwa Fedha za Tozo haziwezi kugharamia miradi yote mikubwa ya kimkakati na haiwezi kuwa mbadala wa kukopa Fedha

Mheshimiwa Ndugai angeliweza kuomba kuonana na Rais Samia na kumshauri aonavyo badala ya njia aliyoitumia ya kuropoka HADHARANI!

Kwa maoni yangu kauli ya Mheshimiwa Ndugai likusudia kukwamisha juhudi za Rais wetu kukamilisha miradi mbalimbali ya Maendeleo kama ilivyoelekezwa kwenye Ilani ya CCM

Nashauri Mheshimiwa JOB NDUGAI ajiuzulu mara moja wadhifa wake wa Uspika na akishindwa kufanya hivyo mamlaka husika zimchukulie hatua za kumvua uanachama wa CCM kwani kwa sasa sio Mwenzetu tena

Tumpe ushirikiano Rais Samia

KaziIendelee
Usijiuzulu hata wazo hilo usiwe nalo. Kutoa maoni yako ni haki ya kikatiba
 
Zimafutwa na kuunganishwa nyingi tuu lakini wanazidiwa
Wanajitahidi sana, naona wameshaunganisha huu uzi sasa. Ni kero kila ukiingia JF unakutana na habari zinazofanana.
Ahsanteni sana MODS.
 
Yaani mtu kutoa mawazo yake ndio ajiuzuru? una akili za ovyo sana wewe
Inategemea na mtu mwenyewe,
huyu anaeongelewa ni mgogo pia ni spika pia alikubali kuwa kibaraka wa muhimili mwingine!

Mama alisema clear kbs,

"nyumba yake ndio inapitisha hiyo mikopo"

Kimsingi huyu mgogo hajui yuko pale kwa ajili gani, na ndo anaetumika kuumiza watanzania kupitia bunge la micjongo!

Ni huyu hakutaka watanzania wajue kinachoongelewa bungeni

Wacha aning'inizwe tu"
 
Why ajiuzuru? Kwani yy amewekwa na Rais?

'Mtu mzima na akili yake...'' hili ni neno kubwa sana likhusisha akili , umri na kufikiri kwa Mh Spika
Ni kwamba Wananchi wamepewa dondoo za kutathmini uwezo wa kifikra wa Spika wao

Well, si lazima ajiuzulu kama watu wanavyoshauri hata hivyo ni wakati atathmini kama ana heshima tena mbele ya Bunge na jamii kwa ujumla. Jana pale Ikulu wenzake walitueleza mengi kuhusu yeye na kubwa zaidi ni uwezo wake wa kufikiri
 
'Mtu mzima na akili yake...'' hili ni neno kubwa sana likhusisha akili , umri na kufikiri kwa Mh Spika
Ni kwamba Wananchi wamepewa dondoo za kutathmini uwezo wa kifikra wa Spika wao

Well, si lazima ajiuzulu kama watu wanavyoshauri hata hivyo ni wakati atathmini kama ana heshima tena mbele ya Bunge na jamii kwa ujumla. Jana pale Ikulu wenzake walitueleza mengi kuhusu yeye na kubwa zaidi ni uwezo wake wa kufikiri

Tunatumia mazoea ndio shida, but kama akiamua anaendelea kukaa na bado kama kiongozi wa mhimili akawa anampinga Rais wake

Ni kawaida Sana inchi zingine,

Kama akijiuzulu means hakuna mtu anapaswa kuongea anything tofaut na mawazo ya rais
 
Tunatumia mazoea ndio shida, but kama akiamua anaendelea kukaa na bado kama kiongozi wa mhimili akawa anampinga Rais wake

Ni kawaida Sana inchi zingine,

Kama akijiuzulu means hakuna mtu anapaswa kuongea anything tofaut na mawazo ya rais
Hapa lazima uelewe hoja ni nini
Kumpinga Rais kama kiongozi wa mhimili mwingine si jambo geni au baya.
Alichozungumza si kibaya au kigeni

Tatizo ni hili, kusingizia alinukuliwa vibaya
Kuomba msamaha kwa aliyosema kwa maana hajui alisema nini au alikusudia nini
Kuzungumzia miswada iliyopita mikononi mwake kinafiki
Kuhojiwa uwezo wake ''kiakili'' na Viongozi wote wakuu wa nchi

Heshima yake haipo kwasasa mbele ya jamii. Ajiuzulu tu
 
Hapa lazima uelewe hoja ni nini
Kumpinga Rais kama kiongozi wa mhimili mwingine si jambo geni au baya.
Alichozungumza si kibaya au kigeni

Tatizo ni hili, kusingizia alinukuliwa vibaya
Kuomba msamaha kwa aliyosema kwa maana hajui alisema nini au alikusudia nini
Kuzungumzia miswada iliyopita mikononi mwake kinafiki
Kuhojiwa uwezo wake ''kiakili'' na Viongozi wote wakuu wa nchi

Heshima yake haipo kwasasa mbele ya jamii. Ajiuzulu tu

Mpaka ndugai ameomba msamaha ujue kuna kikao kilifanyika, otherwise angechuna
 
Mpaka ndugai ameomba msamaha ujue kuna kikao kilifanyika, otherwise angechuna
Yes lakini hiyo haitaondoa ukweli kuwa popote atakapokaa, simama au kutembea watu watahoji swali moja, mkuu wa nchi alitilia shaka utimamu na umri wa Ndugai.

Hana heshima popote pale.
Juzi kasingizia media leo anaomba msamaha , huyu hana maana hata akibali Spika heshima yake haipo. Suala hapa si kuondoka au kubaki, tunahoji heshima yake , heshima ya Uspika na heshima ya Bunge.
 
Back
Top Bottom