Nashindwa kabisa kurudia tendo kwa mwanamke mmoja; lakini wakiwa tofauti naweza kwenda hadi mara nne. Nina tatizo?!!!

Kudoba wepo baaah

Senior Member
Joined
May 12, 2024
Posts
155
Reaction score
461
Habarini wakuu!
Kama kichwa kinavyojieleza hapo juu. Nina changamoto hiyo; siwezi kamwe kurudia tendo nikiwa na mwanamke mmoja......yaani nakuwa mtu wa bao moja tu chali hata nifanye au anifanyie nini mwanamke. Yupo aliyenipenda na kutumia usiku mzima kunijaribu kwa kila hali ikiwemo kuloweka kabisa huku akinigusa kila sehemu yenye hisia lakini wapi! Wanawake nilioshirikiana nao wote wananijua kama mtu wa hivyo (bao moja chali) na, kama mnavyojua mambo ya wanawake, heshima inapungua.

Lakini ajabu na kitu wasichokijua ni kwamba nikitoka kwa mwanamke mmoja kwenda kwa mwingine basi naweza kurudia bila shaka. Nimefanya utafiti huo mara kadhaa; nilianza na mmoja, nikaja wawili, watatu mpaka wanne ili muradi tu wawe tofauti kwa kila tendo. Nilifanya hivyo katika kujipima.

Wakuu nimeleta kwenu hii hoja ili mnisaidie mawazo kama inawezekana kwani nina wakati mgumu sana katika umri wangu huu wa ujana wa miaka 27;
-naogopa kuanzisha mahusiano ya kudumu (kwa hofu kwamba ni mke gani atavumilia hali hiyo kwa aina ya wanawake wa sasa wanaokesha mitandaoni na kuweka wazi jinsi wanavyohusudu 'mashine'?); hivyo masuala ya familia hayaeleweki mpaka sasa,
-hii hali ya kupitia wanawake tofauti ni hatarishi kwa afya yangu na mustakabali wangu wa maisha kwa ujumla.....kupungukiwa baraka, kuvurugwa, gharama n.k.

Nawasilisha!
 
Acha punyeto kijana
 
Acha hofu dogo...Unaenda ukiwa na hofu kama utaweza kwenda next round ndio maana huwezi alafu acha kuangalia Porn
 
Acha punyeto kijana
Hapo punyeto inasingiziwa tu.

Huyo akimaliza game atoke kitandani azunguke zunguke hata kidogo humo ndani ya nyumba.

Alafu asiwaze kabisa ishu za kurudia tendo maana akiliwaza atakumbuka hawezi, hofu itamjaa mwishowe hatoweza kabisa.

Lingine aache kujisafisha/kuoga/kunawa kwa maji ya baridi baada ya tendo.

Anywe maji mengi kabla ya tendo, ili aweze kukojoa mkojo baada ya kumaliza tendo. Kuna kitu iyo hali itamsaidia.

Mwisho wa yote ale vizuri na kufanya mazoezi hasa ya kata tumbo na muguu iwe walau na misuli sio nyama uzembe. Aache/apunguze kunywa energe drinks pia.

Nyongeza; akapime ugonjwa wa kisukari.
 
Akiwa,na kisukari afanyeje,ili uume urudi kama zamani?
 
Cha muhimu mkojoze mwanamke kabla hujamaliza, sio tako 5 na wewe unakuwa umemaliza. Kama utatumia hata dk 10 hiyo fresh tu
 
Nilitaka kusema sex is not for everyone.Sema acha kuhalalisha umalaya kijanja, tafuta mtu mnaependana nakuijua vizuri hali Yako, Kaa nae kwa wiki au miezi kadhaa huku ukiendelea na dozi ya ndizi, karanga, parachichi n.k.
 
Mwisho wa yote ale vizuri na kufanya mazoezi hasa ya kata tumbo na muguu iwe walau na misuli sio nyama uzembe. Aache/apunguze kunywa energe drinks pia.

Nyongeza; akapime ugonjwa wa kisukari
Nakazia ushauri huu hapa.

Ila 27 n mapema mno.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…