Uchaguzi 2020 Nasimama na Dkt. John Pombe Magufuli, Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM

Uchaguzi 2020 Nasimama na Dkt. John Pombe Magufuli, Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM

Ukimuona mwanasheria anamtetea Magufuli basi ujue ni walewale! Yani kwa kumtetea Magufuli huna sifa ya uanasheria
Jamani tuwe waelewa japo kidogo, huyu naye ana familia, mtaani pagumu.

Ccm huwa inawapa ajira wanasheria wanakuwa wanadheria wa chama wanalipwa mishahara, mimi simlaumu kwa kweli.

Kuwa wakili wa kujitegemea kwa kutegemea kuwaandikia watu Affidavit na kuwagongea mihuri kwa tozo ya buku kumi tu hivi unadhani huyu mwenzenu hata Toyota IST ataendesha mwaka gani?

Mzee Yusuf tu mwenyewe njaa imemkimbiza kwa mungu ndio sembuse huyu wakili wa kawaida?
 
Nilitabiri humu na ikawa kweli kuwa Wagombea wakuu wa uchaguzi mkuu wa Rais mwaka huu ni Wakili Msomi mwenzangu Tundu Lissu (Upinzani/CHADEMA) na Dr. John Pombe Magufuli (CCM). Ni katika andiko langu hili: Uchaguzi 2020 - Utabiri wangu 2020: Ni Dr. John Pombe Magufuli (CCM) na Wakili Msomi Tundu Antipas Lissu (Upinzani) Urais. Tuwafuatilie; tuwachambue na tuwachague!. Katika andiko langu hilo, niliahidi mgombea wa kusimama naye katika kuelekea uchaguzi mkuu huu.

Wengi wetu tunajua kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeshakamilisha uteuzi wa wagombea wa Urais. Pia, tunafahamu kuwa kampeni za Urais zinaanza leo ambapo CHADEMA watazindua kampeni zao Mbagala, jijini Dar es Salaam. Kesho itakuwa zamu ya CCM kuzindua kampeni zao huko jijini Dodoma. Wapo wagombea wengi katika ngazi ya Urais. Lakini, Dr. John Pombe Magufuli, Rais wa sasa wa Tanzania na mgombea wa CCM pamoja na Wakili Msomi Tundu Antiphas M. Lissu wanabaki kuwa wagombea wanaofuatiliwa Zaidi.

Ndiyo kusema, katika ngazi ya Urais, mchuano mkali utakuwa kati ya wagombea hao wawili. Kama mtanzania wa kawaida, mfuatiliaji wa siasa na nisiye mwanachama wa chama chochote cha siasa hapa Tanzania na kwingineko, nawiwa kusimama na Dr. John Pombe Magufuli, mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM. Naahidi kumuunga mkono katika kampeni zake atakazozianza kesho na kumuombea kura pale itakapobidi kwa nafasi yangu. Sababu za kumuunga mkono nitazieleza katika siku zijazo humuhumu JF zikichagizwa na yatakayosemwa kwenye kampeni.

#Nasimama na JPM kwa miaka mitano mingine!
Nimeipenda hiyo mtni umeamua kuwa muwazi. Hata mimi nimeona jamaa zetu wa CDM wameamua kuwa kama wachekeshaji tu sioni chochote wanachokisema naona wameamua kuazima style ya Trump
 
Nilitabiri humu na ikawa kweli kuwa Wagombea wakuu wa uchaguzi mkuu wa Rais mwaka huu ni Wakili Msomi mwenzangu Tundu Lissu (Upinzani/CHADEMA) na Dr. John Pombe Magufuli (CCM). Ni katika andiko langu hili: Uchaguzi 2020 - Utabiri wangu 2020: Ni Dr. John Pombe Magufuli (CCM) na Wakili Msomi Tundu Antipas Lissu (Upinzani) Urais. Tuwafuatilie; tuwachambue na tuwachague!. Katika andiko langu hilo, niliahidi mgombea wa kusimama naye katika kuelekea uchaguzi mkuu huu.

Wengi wetu tunajua kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeshakamilisha uteuzi wa wagombea wa Urais. Pia, tunafahamu kuwa kampeni za Urais zinaanza leo ambapo CHADEMA watazindua kampeni zao Mbagala, jijini Dar es Salaam. Kesho itakuwa zamu ya CCM kuzindua kampeni zao huko jijini Dodoma. Wapo wagombea wengi katika ngazi ya Urais. Lakini, Dr. John Pombe Magufuli, Rais wa sasa wa Tanzania na mgombea wa CCM pamoja na Wakili Msomi Tundu Antiphas M. Lissu wanabaki kuwa wagombea wanaofuatiliwa Zaidi.

Ndiyo kusema, katika ngazi ya Urais, mchuano mkali utakuwa kati ya wagombea hao wawili. Kama mtanzania wa kawaida, mfuatiliaji wa siasa na nisiye mwanachama wa chama chochote cha siasa hapa Tanzania na kwingineko, nawiwa kusimama na Dr. John Pombe Magufuli, mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM. Naahidi kumuunga mkono katika kampeni zake atakazozianza kesho na kumuombea kura pale itakapobidi kwa nafasi yangu. Sababu za kumuunga mkono nitazieleza katika siku zijazo humuhumu JF zikichagizwa na yatakayosemwa kwenye kampeni.

#Nasimama na JPM kwa miaka mitano mingine!
Vyeo vimejaa Mkuu, pole
 
Post yangu kwa pasco na Mselewa ni utani, mara nyingi, lakini nawaheshimu sana. Kwa mfano mimi na wewe tupo hapa kwa majina ya bandia, lakini hawa jamaa wapo kwa utambulisho wao halisi! Na kwa taarifa yako, tunao jua kusoma between the lines, hawa jamaa tunawaelewaga!
Asante kunielewesha. Kumbe mawazo yetu yanalingana.
 
Back
Top Bottom