Natabiri jaribio lolote la kubadilisha Katiba na ukomo wa Rais litaibua mazito

Natabiri jaribio lolote la kubadilisha Katiba na ukomo wa Rais litaibua mazito

Hata China kabla ya Xi kulikuwa na utamaduni wa kuheshimu term limits, lolote linawezekana.
Uganda haina utamaduni wa marais kuheshimu term limits.

Tanzania tangu aondoke Nyerere marais wote wameheshimu term limits.

Na hata Magufuli amesema hatazidisha muhula wake.

Sasa huu mchecheto wa kusema Magufuli ataongeza muda unatokea wapi?
 
Lolote linawezekana, hakuna mahali pa kuchora mstari kwa sasa.
Hata kama humuamini Magufuli, unatakiwa kutomuamini kimantiki.

Ama sivyo, unaweza kubakia unajadili speculations za ajabu...
 
Circumstantial evidence
Hilo shairi la Jadakiss ni fasihi, sasa kama huelewi fasihi, kuelewa ni vigumu.

Hapa kuna mambo mawili.

1.Speculation/ ubashiri
2. Fact

Kwenye speculation na ubashiri hakuna mpaka, unaweza kutunga lolote.

Unaweza kusema 2025 tutagundua Magufuli ni mumiani aliyetoka sayari ya Zuhura.

Hakuna anayeweza kupinga hili kwa fact, kama ambavyo huwezi kuthibitisha kwa fact.

Kwa sababu hatujafika 2025.

Halafu kuna facts.

Tuna facts gani za kuonesha Magufuli ataendelea na urais baada ya 2025?

Magufuli amesema hilo? Hapana. Alichosema ni kukanusha hilo.

Magufuli ameanzisha mchakato huo? Hakuna ushahidi wowote.

Sasa mchecheto huu kuhusiana na hadithi zisizo na msingi unatokea wapi?
 
Ni kweli kelele zote ni bure
Kama unakubali kirahisi hivyo uchaguzi wa 2020 ushapita, hata kama Magufuli akijiongezea muda wa urais 2025 hutafanya kitu.

Utasema tu uchaguzi wa 2025 ushapita.

Na kuanza kulalamika "Magufuli atajiongezea muda tena 2030".

Kelele zote ni bure tu.
 
Aliwakatalia wapambe baada ya kukaa zaidi ya miaka 20 madarakani.
Hao wapambe mbona walikuwepo tangu utawala wa Nyerere.

Nyerere alitoa hotuba moja akasema kila alipokuwa akitaka kujiuzulu, wapambe wakawa wanamuambia, Mwalimu, usituache, taifa linakuhitaji sana.

Akawa anaongeza miaka mitano, anasema hii ya mwisho.

Ikiisha, wapambe wanamwambia "Mwalimu, usituache, taifa linakuhitaji sana".
Mwisho akastuka. Akagundua kwamba issue si kwamba taifa linamuhitaji.

Issue ni kwamba hao wapambe walikuwa wanamuhitaji kwa faida zao binafsi. Walikuwa hawajui rais anayekuja atakuwa nani na atakuja na watu gani.

Akawakatalia, akajiuzulu.

Kwa hiyo hizi kelele za wapambe zipo tu.

Lakini je, rais mwenyewe anataka nini?

Rais kashasema hataongeza muda.

Na hakuna factual evidence kwamba ataongeza.

Ni speculations tu.
 
"Speculation"?
Ni 'facts' zipi zinazokufanya wewe uamini hatajiongezea muda? Ziweke hapa tuzione.

Mtu akija kwako akope halafu asilipe, keshokutwa anakuja tena kukulaghai juu ya 'favor' nyingine unaendelea kuamini kwamba mtu huyo ni 'dependable na kumtimizia matakwa yake bila kuwa na wasiwasi wowote juu yake, wewe utakuwa na sababu zako za kuamini ushawishi wake huo mpya...
Huyu kiranga amekuwa snitch kama goodluck haule
 
Kumbe inawezekana! Ni jambo la kutisha sana.
Inawezekana pia kesho jua lisichomoze, kwa kuchoka kuwaka.

Hilo linatisha zaidi kama unalielewa.

Lakini je, kwa sayansi tunayoijua sasa, tukianza kujadili hilo na kuhamanika, tutakuwa sawa?
 
Lolote linawezekana, hakuna mahali pa kuchora mstari kwa sasa.
Even more reason to prioritize things.

Maana, manweza kudhibiti term limits, halafu, ajaye akaleta maanguko mara 100 ya Magufuli.

There are bigger fish to fry. Term limits is the least of your worries.

Do you understand that?
 
Ni kweli kelele zote ni bure
Hapa ndipo penye jambo la msingi.

Hata tukikubali kifalsafa tu, kama experiment.

Tuseme Magufuli anataka kujiongezea muda wa urais.

1. Kuna mkakati gani wa kumzuia yeye binafsi kufanya hilo.
2. Kuna mkakati gani wa kumzuia yeye binafsi kufanya hilo, na kumzuia yeye binafsi asipachike kibaraka wake kuwa rais ajaye?
3. Kuna mkakati gani wa kuzuia rais yeyote wa Tanzania asitumie vibaya nguvu za kirais na kusababisha taifa kwenda mrama?

Nimeuliza maswali haya mara nyingi, sijapata majibu.

Watu wamekwama kwenye kumtazama Magufuli mtu, badala ya kuangalia urais kama taasisi ambayo itaendelea kuwepo hata Magufuli akifa kesho.
 
Mambo mangapi watanzania tunashikwa makalio na jiwe na hatufanyi chochote.Hakuna kipya, jiwe ameshajua makalio yetu malaini ndio maana anayashika anavyotaka
 
Natabiri yakuwa jaribio lolote la kubadili katiba na kurefusha ukomo wa Rais litazuwa Moto wa kisiasa ambao haukuwahi kutokea tangu kuwepo kwa Taifa hili...
Tanzania hatuna katiba tena wala utawala wa sheria.Kila mtu anafanya anavyojiskia.Ni gangster country.Uchaguzi ni dhuluma na wizi mwanzo mwisho. Katiba inavunjwa mchana kweupe watu wanashangilia
 
Aliwakatalia wapambe baada ya kukaa zaidi ya miaka 20 madarakani.
Nyerere ana makosa yake.

Lakini, tafadhali usimfananishe Nyerere na vitu vya kijinga anavyofanya au anavyoweza kufanya Magufuli.

Nyerere alijiuzulu Uwaziri Mkuu January 1962.Wiki sita baada ya Tanganyika kupata Uhuru.

Ili aende kuimarisha chama.Ile move haijawahi kurudiwa dunia nzima mpaka leo, sijawahi kusikia mfano mwingine wa mtu kupewa nchi, kuiweka mikononi mwa mtu mwingine ili yeye aimarishe mambo ya msingi, halafu mtu huyo kurudi kwenye uongozi wa nchi huku akikubalika sana tu.

Alimuachia nchi Rashid Mfaume Kawawa.Kawawa akaongoza nchi kama Waziri Mkuu.

Nyerere alivyomaliza kuimarisha chama, akarudia uongozi wa nchi kama Head of State.

Kiongozi wa Nigeria alivyosikia habari hii, alisema "nileteeni huyo Kawawa nimfanye awe mwanangu, maana utiifu huo Nigeria hapa usingewezekana".

Hivyo, ukimtuhumu kwamba alipenda kuongoza nchi bila kuachia madaraka, anaweza kukujibu kwamba yeye madaraka aliyaachia wiki sita tu baada ya kupewa nchi.
 
Itakuwa hivyo kama ndani ya CCM hawatakubali wenyewe wenye connection na deep state.

Shida karata ya kupoteza control ndio itakayokuwa mwanzo wa anguko.
 
Historia daima huandikwa na washindi.
Kama Oscar Kambona na bibi Titi wangekuwa washindi hatujui wangeandika historia gani na wao.
Nyerere ana makosa yake.

Lakini, tafadhali usimfananishe Nyerere na vitu vya kijinga anavyofanya au anavyoweza kufanya Magufuli...
 
Historia daima huandikwa na washindi.
Kama Oscar Kambona na bibi Titi wangekuwa washindi hatujui wangeandika historia gani na wao.
Ukisema hivyo unaweza kusema jua halijachomoza jana. Bila hata kujisumbua kutoa ushahidi.

Weka ushahidi wa vinginevyo tuuchunguze.

Hata wewe unakaribishwa kubadili historia ya Nyerere kujiuzulu Uwaziri Mkuu January 1962.

Nywrere nu mshindi. Kaandika historia.

Ukitaka kutufahamisha zaidi ya yaliyoandikwa kuhusu yeye, yaandike hapa.

Vinginevyo, you are worse than an illiterate.

Kwa sababu hutaki kuandika unayofahamu.
 
Back
Top Bottom