"If I wasn't on some shit, I'm getting on it"
Jadakiss - "Kiss of Death"....
Uganda haina utamaduni wa marais kuheshimu term limits.
Tanzania tangu aondoke Nyerere marais wote wameheshimu term limits.
Na hata Magufuli amesema hatazidisha muhula wake.
Sasa huu mchecheto wa kusema Magufuli ataongeza muda unatokea wapi?
Hata kama humuamini Magufuli, unatakiwa kutomuamini kimantiki.
Ama sivyo, unaweza kubakia unajadili speculations za ajabu...
Hilo shairi la Jadakiss ni fasihi, sasa kama huelewi fasihi, kuelewa ni vigumu.
Hapa kuna mambo mawili.
1.Speculation/ ubashiri
2. Fact
Kwenye speculation na ubashiri hakuna mpaka, unaweza kutunga lolote.
Unaweza kusema 2025 tutagundua Magufuli ni mumiani aliyetoka sayari ya Zuhura.
Hakuna anayeweza kupinga hili kwa fact, kama ambavyo huwezi kuthibitisha kwa fact.
Kwa sababu hatujafika 2025.
Halafu kuna facts.
Tuna facts gani za kuonesha Magufuli ataendelea na urais baada ya 2025?
Magufuli amesema hilo? Hapana. Alichosema ni kukanusha hilo.
Magufuli ameanzisha mchakato huo? Hakuna ushahidi wowote.
Sasa mchecheto huu kuhusiana na hadithi zisizo na msingi unatokea wapi?
Kama unakubali kirahisi hivyo uchaguzi wa 2020 ushapita, hata kama Magufuli akijiongezea muda wa urais 2025 hutafanya kitu.
Utasema tu uchaguzi wa 2025 ushapita.
Na kuanza kulalamika "Magufuli atajiongezea muda tena 2030".
Kelele zote ni bure tu.
Imepita hiyoooo.Magufuri hatomaliza huu muhula akiwa madarakani.....!!!
Mark my words
Hao wapambe mbona walikuwepo tangu utawala wa Nyerere.
Nyerere alitoa hotuba moja akasema kila alipokuwa akitaka kujiuzulu, wapambe wakawa wanamuambia, Mwalimu, usituache, taifa linakuhitaji sana.
Akawa anaongeza miaka mitano, anasema hii ya mwisho.
Ikiisha, wapambe wanamwambia "Mwalimu, usituache, taifa linakuhitaji sana".
Mwisho akastuka. Akagundua kwamba issue si kwamba taifa linamuhitaji.
Issue ni kwamba hao wapambe walikuwa wanamuhitaji kwa faida zao binafsi. Walikuwa hawajui rais anayekuja atakuwa nani na atakuja na watu gani.
Akawakatalia, akajiuzulu.
Kwa hiyo hizi kelele za wapambe zipo tu.
Lakini je, rais mwenyewe anataka nini?
Rais kashasema hataongeza muda.
Na hakuna factual evidence kwamba ataongeza.
Ni speculations tu.
Huyu kiranga amekuwa snitch kama goodluck haule"Speculation"?
Ni 'facts' zipi zinazokufanya wewe uamini hatajiongezea muda? Ziweke hapa tuzione.
Mtu akija kwako akope halafu asilipe, keshokutwa anakuja tena kukulaghai juu ya 'favor' nyingine unaendelea kuamini kwamba mtu huyo ni 'dependable na kumtimizia matakwa yake bila kuwa na wasiwasi wowote juu yake, wewe utakuwa na sababu zako za kuamini ushawishi wake huo mpya...
Watz hawana chochote cha maana ndio majambazi ya ccm yanawapora chochote yanayojisikia kuporaSiku zote ktk maisha muogope Sana MTU asie ongea huyo muogope Sana.
Inawezekana pia kesho jua lisichomoze, kwa kuchoka kuwaka.Kumbe inawezekana! Ni jambo la kutisha sana.
Term limits is the least of your worries, do you understand that?Hata China kabla ya Xi kulikuwa na utamaduni wa kuheshimu term limits,lolote linawezekana.
Even more reason to prioritize things.Lolote linawezekana, hakuna mahali pa kuchora mstari kwa sasa.
Hapa ndipo penye jambo la msingi.Ni kweli kelele zote ni bure
Tanzania hatuna katiba tena wala utawala wa sheria.Kila mtu anafanya anavyojiskia.Ni gangster country.Uchaguzi ni dhuluma na wizi mwanzo mwisho. Katiba inavunjwa mchana kweupe watu wanashangiliaNatabiri yakuwa jaribio lolote la kubadili katiba na kurefusha ukomo wa Rais litazuwa Moto wa kisiasa ambao haukuwahi kutokea tangu kuwepo kwa Taifa hili...
Nyerere ana makosa yake.Aliwakatalia wapambe baada ya kukaa zaidi ya miaka 20 madarakani.
Wenyewe washajua kumchinja kobe timing.Itakuwa hivyo kama ndani ya CCM hawatakubali wenyewe wenye connection na deep state.
Shida karata ya kupoteza control ndio itakayokuwa mwanzo wa anguko.
Nyerere ana makosa yake.
Lakini, tafadhali usimfananishe Nyerere na vitu vya kijinga anavyofanya au anavyoweza kufanya Magufuli...
Ukisema hivyo unaweza kusema jua halijachomoza jana. Bila hata kujisumbua kutoa ushahidi.Historia daima huandikwa na washindi.
Kama Oscar Kambona na bibi Titi wangekuwa washindi hatujui wangeandika historia gani na wao.