Natafuta mji mtulivu wa kwenda kupumzika kwa mwezi mmoja

Natafuta mji mtulivu wa kwenda kupumzika kwa mwezi mmoja

Nenda Bukoba utafurahi maisha kuna beach nzuri sana zenye mvuto was kipekee, kuna Bunena Beach, beach ya asili yenye mawe mazuri sana, unakaa juu ya maweza unausikilizia upepo mwanana kutoka ziwa Victoria hakuna kelele wala nini, vilevile kuna beach ya Kiloyera in nzuri hakuna mfano, kuna beach ya Bukoba Club hakika huu mji unapendeza sana. Halafu mjini katikati hamna cha foleni wala nini vyakula vya asili vipo vya kutosha na gharama ni za kawaida sana.

Binafsi hayo mazingira niliyapenda sana zaidi ule mji una amani na usalama kuliko miji yote niliyowahi kutembelea hapa Tanzania. Bukoba na viunga vyake hata usiku wa manane unatembea bila shida yoyote ile. Tatizo wanapenda sana kuongea kihaya kuliko lugha yoyote ile.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naunga mkono hoja ule mji hauna heka heka plus kuna sehemu kibao za evening walk.
Huwa napenda pia kwenda kuna beach hotel mbili napenda kushinda hapo.
Wish nitume picha nikiwa hapo [emoji12]
Hakika.
Bukoba ni mji ambao una mandhari nzuri sana, kijani karibu muda wote wa mwaka, hali ya hewa ni safi, Watu wa bukoba ni waungwana sana(japo wanapendana zaidi wao kwa wao..ukitaka wakuelewe ujue lugha yao😜)
Pia huo mji hauna watu wengi (msongamano). Bei ya vyakula ni ya chini..ila hawajui kupika lol.

Kwa ujumla Bukoba ni sehemu nzuri ya ku-refresh mind.
 
Bukoba club pale kuku wa kuchoma balaaa kiroyera nyingine nimeisahau beach hotel.
Plus anaweza kuvuka maji akaenda kutalii.
Halafu Bukoba raha sana ukiwa na laki tu Don wewe, msosi sasa hadi raha.
Eyce i wish nitume picha nikiwa huko.
I really enjoyed the place.
Naipenda ile sehemu. B
Wishes zimekuwa nyingi sasa. Emu tuma tuone labda na sisi tutakuwa inspired
 
Nenda Bagamoyo ukishidwa kwenda huko basi nenda Bukoba.
 
Umofia kwenu wakuu!

Ambao mna uzoefu mkubwa na maeneo (miji midogo) ya nchi hii. Naomba ushauri au mapendekezo, ni mji gani mdogo naweza kwenda kukaa kwa muda wa mwezi mmoja (brain recharging)

Uwe ni mji mdogo, uliotulia kwa mandhari na hali ya hewa, ambao jioni naweza enjoy evening walk, uwe ni mji salama, na wenye vyakula vizuri vya asili, kwa mfanano mzuri think of somewhere like Lushoto (Lushoto ndio kwetu so don't mention)

Binafsi nimewaza kwenda Tarakea Rombo, lakini naona ni vyema nipate mawazo kwa wadau. N.B, iwe ni sehemu yenye nyumba za wageni ambazo ni classic.
Asanteni.
View attachment 1412207
jaribu kwenda Pemba mkuu
 
Bukoba club pale kuku wa kuchoma balaaa kiroyera nyingine nimeisahau beach hotel.
Plus anaweza kuvuka maji akaenda kutalii.
Halafu Bukoba raha sana ukiwa na laki tu Don wewe, msosi sasa hadi raha.
Eyce i wish nitume picha nikiwa huko.
I really enjoyed the place.
Naipenda ile sehemu. B

Em mtendee haki Depal kwa kutuma picha 😊😊
 
Back
Top Bottom