Natafuta mji mtulivu wa kwenda kupumzika kwa mwezi mmoja

Natafuta mji mtulivu wa kwenda kupumzika kwa mwezi mmoja

Umofia kwenu wakuu!

Ambao mna uzoefu mkubwa na maeneo (miji midogo) ya nchi hii. Naomba ushauri au mapendekezo, ni mji gani mdogo naweza kwenda kukaa kwa muda wa mwezi mmoja (brain recharging)

Uwe ni mji mdogo, uliotulia kwa mandhari na hali ya hewa, ambao jioni naweza enjoy evening walk, uwe ni mji salama, na wenye vyakula vizuri vya asili, kwa mfanano mzuri think of somewhere like Lushoto (Lushoto ndio kwetu so don't mention)

Binafsi nimewaza kwenda Tarakea Rombo, lakini naona ni vyema nipate mawazo kwa wadau. N.B, iwe ni sehemu yenye nyumba za wageni ambazo ni classic.
Asanteni.
View attachment 1412207
Bukoba pako poa sana mkuu chakula cha asili mpaka chips wanatengeneza kwa mayai ya kienyeji samaki fresh kabisa. Nyama choma kuku wa kienyeji na bei yake ni rafiki pia kuna hotel na lodge nzuri bei poa hari ya hewa na beach fresh, Pia ni wakarimu boda boda mpaka 500. Usalama unaweza kutembea kwa mguu mpaka asubuhi na usikutane kibaka wala jambazi kama alivosema mdau hapo juu. Nitarudi tena Bukoba
 
Mkuu nenda moshi eneo linaitwa HIMO. nikuzuri sana..nimeenda Mara nyingi..utafurahi..pia MARANGU kuzuri itafurahi

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Himo pale jua kali Sana na joto la kutisha utafikiri uko kwenye Jangwa la Kalahari, pia kuna harufu chafu sana throughout the year inayotoka kwenye kiwanda cha ngozi cha Woisso. Himo hapafai hata kwa nukta moja bora Marangu...japo kwa mujibu wa mleta Uzi sehemu inayomfaa kwa mtazamo wangu ni Bukoba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimeeeecheeekaaaa eti boda boda jero

Sent using Jamii Forums mobile app
Hata usicheke ndugu ule mjini ni mzuri mno japo watu wengi hawaufahamu, hata uteremke stend SAA saba usiku unaweza kushangazwa na bei za bodaboda, mfno sehemu ambapo ungepelekwa hata kwa elf tano au saba utashangaa unaambiwa book moja au mia tano na ukienda mbali sana utashangaa haizidi elf moja na mia tano. Bukoba niliipenda sana kuliko sehemu yoyote hapa Tanzania, changamoto ya mji wa Bukoba ni kwamba hadi mjini katikati lugha ya Kihaya inatumika sana, Wahaya wanapenda sana lugha yao na wala hawana tabia ya kuongeaongea kiswahili km sehemu nyingine. Nadhan wanaweza kuwa ndo kabila pekee hapa Tanzania linalo tumia kilugha kuliko kabila lolote hapa nchini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bukoba pako poa sana mkuu chakula cha asili mpaka chips wanatengeneza kwa mayai ya kienyeji samaki fresh kabisa. Nyama choma kuku wa kienyeji na bei yake ni rafiki pia kuna hotel na lodge nzuri bei poa hari ya hewa na beach fresh, Pia ni wakarimu boda boda mpaka 500. Usalama unaweza kutembea kwa mguu mpaka asubuhi na usikutane kibaka wala jambazi kama alivosema mdau hapo juu. Nitarudi tena Bukoba
Hii Bukoba lazima ni nzuri,kila mtu anaizungumzia. Tatizo ni km 1000+ from Dar na utalii wa ndani unanoga kuendesha
 
Hii Bukoba lazima ni nzuri,kila mtu anaizungumzia. Tatizo ni km 1000+ from Dar na utalii wa ndani unanoga kuendesha
Sio mchezo utaenjoy sema kutoka dar ni safari kweli ila kama una private car utafanya utalii wa ndani mana unapita mikoa kama 6 Pwani,Morogoro,Dodoma,Singida,Tabora,Shinyanga,Geita then ndo Kagera yenyewe.
 
Unashangaa nini.ndo maana route nyingi za daladala mjini bukoba zimestop Kwa sababu ya bodaboda.


Unaweza hata kwenda 5km Kwa jero mfano mjini kashai,mjini rwamishenye, mjini migera bodaboda huwa ni jero.


NB. Biashara ya bodaboda Kwa tz imeanzia bukoba

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli ilianzia bukoba wakiiga kutoka Uganda na safari mpaka ya karibu km 6 ni jero
 
Hata usicheke ndugu ule mjini ni mzuri mno japo watu wengi hawaufahamu, hata uteremke stend SAA saba usiku unaweza kushangazwa na bei za bodaboda, mfno sehemu ambapo ungepelekwa hata kwa elf tano au saba utashangaa unaambiwa book moja au mia tano na ukienda mbali sana utashangaa haizidi elf moja na mia tano. Bukoba niliipenda sana kuliko sehemu yoyote hapa Tanzania, changamoto ya mji wa Bukoba ni kwamba hadi mjini katikati lugha ya Kihaya inatumika sana, Wahaya wanapenda sana lugha yao na wala hawana tabia ya kuongeaongea kiswahili km sehemu nyingine. Nadhan wanaweza kuwa ndo kabila pekee hapa Tanzania linalo tumia kilugha kuliko kabila lolote hapa nchini.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli wanapenda kuongea lugha yao.
 
Unatuzingua wewe...mwenda kupumnzika huqa amepanga na hana mbwembwe...nyie wenye vijihela vya nyanya kwa mbwembwe[emoji125]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unatuzingua wewe...mwenda kupumnzika huwa amepanga na hana mbwembwe...nyie wenye vijihela vya nyanya kwa mbwembwe[emoji125]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom