Natafuta Santuri (CD kubwa za zamani aina ya Gramophone)

Natafuta Santuri (CD kubwa za zamani aina ya Gramophone)

Bongo ilikuwa ni RTD redio TANZANIA pia sera ya Nyerere ilikuwa ni lazima nyimbo ziwe edited na basata,matusi yanaimbwa kimafumbo sio siku hizi live hadi mtoto wa tumboni anajua hilo ni tusi.
BASATA kazi yake sasa hazielewek, yani mpaka watu wapige kelele kwanza ndio nyimbo ifungiwe. Kisheria kila mtu anatakiwa apeleke nyimbo yake basata kabla ya kuiachia kwa sababu za hati miliki na vitu vingine.
 
Gramaphone zilikuwa na speaker yake hapo hapo
IMG-20170429-WA0018.jpg
 
Zamani enzi za wazee wakoloni waliotoka zao vitani ndio walikuja na hizi record player au ukanunue Kenya likuwa ni bora uchezee kitu kingine na sio kugusa hiki kifaa au CD zake utahamu mji, walikuwa wakali Sana wazee wa zamani.
Hizi bado sio za zamani, ni za miaka ya 70 hivi. Hizi ninazozungumzia ni za zamani zaidi kipindi kile cha ukoloni. .
 
Hizi player zamani vijijini zilikuwa zinaendeshwa na daina moo ya baiskeli soo unanyonga baiskeli ndo betri then rekodi player inaplay sauti ni speaker za Ahuja zile kubwa za msikitini inafungwa juu ya mti, usiku vijana mbalimbali toka vijiji mbalimbali ndio disco watu pori kwa pori wanakatiza maporini usiku Wana mapanga na marungu wanakutana na wanyama mfano fisi, chui, simba wanafata mziki kilometa 10 usiku sauti ufika mbali sana. Wanakula mziki usiku kucha alfajiri wanawahi kurudi majumbani kuwahi namba shuleni viboko vinakusubiria saa moja kamili viboko vinakuhusu. Mingi ilikuwa ni miziki ya misibani.
Hahaha wazee wetu walikuwa wanatumia science ila hawakujua jinsi inavyofanya kazi vyema. Science ya dynamo ya baiskeli ni science ya kitoto kabisa ila hata leo mashuleni hakuna science kwenye majaribio. .

Kuna player na kuna gramaphone, ila gramaphone ya mwanzo kabisa player ndo hizi ambazo zimekuja sasa hivi. .
 
Dah jamaa kweli ni collector. Sahani 1000+ ni nyingi sana babu. Ntakuja unigawie na mimi ila napenda za waimbaji wa mbele sana sana Jazz, R&B, na hiphop kama unazo.
Nakusanya nyimbo za kiafrica tu sikusanyi nyimbo za nje. Hizi za nje ziko kibao ila sinazo kabisa. Nitapost santuri zangu hapa watu waone ni nyingi kweli kweli. .
 
Aisee mbona kama unajichosha sana kutafuta hayo masanturi ya zamani! Hizo nyimbo za zamani baada ya kuzipata unazifanyia nini?

Au una kipindi cha redio unakiendesha?
Mimi nilininunua wakati fulani nadhani ni kupitia huu uzi..nilitengeneza art work moja nzur sana.....nimetundika ukutani....inapendeza sana kwa watu wanaojua hiyo kitu!!
Screenshot_20211103-155849_Instagram.jpg
 
Mimi nilininunua wakati fulani nadhani ni kupitia huu uzi..nilitengeneza art work moja nzur sana.....nimetundika ukutani....inapendeza sana kwa watu wanaojua hiyo kitu!!
Kuna kijana nimekutana nae yuko Arusha anatengeneza artwork za kuchora ila zinakuwa inspired na santuri. Kazi zake nzuri sana aisee, kuna watu wana vipaji. Ila sasa yeye hauzi art work zake akiniruhusu nije nipost nitakuja kuweka hapa mzione. .
 
Kuna kijana nimekutana nae yuko Arusha anatengeneza artwork za kuchora ila zinakuwa inspired na santuri. Kazi zake nzuri sana aisee, kuna watu wana vipaji. Ila sasa yeye hauzi art work zake akiniruhusu nije nipost nitakuja kuweka hapa mzione. .
Naomba (contacts) namba yake ya simu!!
 
Mkuu, mashine kama yako nitapata wapi na kwa bei gani ? Pia ni vyema ukiniambia bei za player zingine
Hii machine ni mpya sio za kizamani, zile za kizamani unaweza pata mitaani huko kama mtu alikuw nazo ila zile sikushauri kwa sababu nyingi zinaharibu santuri zake. .
 
Inasikitisha pale mtu anapoahidi kukutafuta kuhusu santuri kisha anapotea mazima, natafuta santuri kama mnauza nazinunua. .
 
Inasikitisha pale mtu anapoahidi kukutafuta kuhusu santuri kisha anapotea mazima, natafuta santuri kama mnauza nazinunua. .
 
26 October 2022
Bado natafuta santuri. .
Wish you good day
On my side watching Ancient Aliens on history channel😊
 
27th October 2022
Bado nanunua santuri za zamani. .
 
Back
Top Bottom