Nataka kujiunga na Upadre ila kuna ufafanuzi ambao sijaupata

Nataka kujiunga na Upadre ila kuna ufafanuzi ambao sijaupata

Habari za wakati huu wanajamii.

Moja kwa moja kwenye swali langu la msingi.

Nahitaji kujiunga na Updare wa Kanisa Katoliki, ila kuna baadhi ya maswali sijaweza kupata ufafanuzi wake.

1.Ni umri gani unakuwa mwisho wa kujiunga na upadre?

2.Je ni elimu kiwango gani kinakubalika ili kuendelea na masomo ya Upadre?

3.Je kama nilikuwa na mahausiano ambayo sikufunga Ndoa Kanisani, baadae mahusiano yakafa na tumeshapata Mtoto inakuaje?


Nakuombeni ufafanuzi wa kina wandugu.
Jambo la kwanza u padri ni wito, mchakato wake una mambo mengi kuanzia ukuaji wako, uhusiano wako na kanisa nk.

Ushauri. Kila Jimbo lina mkurugenzi wa miito waweza kufika kwa paroko wako kwa hatua za awali kisha yeye atakupa mwongozo sahihi.

Tumsifu Yesu Kristo.
 
Habari za wakati huu wanajamii.

Moja kwa moja kwenye swali langu la msingi.

Nahitaji kujiunga na Updare wa Kanisa Katoliki, ila kuna baadhi ya maswali sijaweza kupata ufafanuzi wake.

1.Ni umri gani unakuwa mwisho wa kujiunga na upadre?

2.Je ni elimu kiwango gani kinakubalika ili kuendelea na masomo ya Upadre?

3.Je kama nilikuwa na mahausiano ambayo sikufunga Ndoa Kanisani, baadae mahusiano yakafa na tumeshapata Mtoto inakuaje?


Nakuombeni ufafanuzi wa kina wandugu.
1. Hakuna umri wa mwisho kuwa padre, hata uzeeni unaweza pewa daraja takatifu
2. Unapata malezi ya kuendana na elimu uliyonayo. Malezi yataanzia pale ulipoishia wewe.
3. Ukishajiweka chini ya malezi salama majibu yote yatapatikana. Hii ni nia njema, unahitaji kuanza malezi mara moja
 
Huo ni utume, Watumwa wa utume huo WANAO WITO... Swali la kwanza je, wewe una wito huo au UNATAKA?

WITO huu unahakikiwa kuanzia seminary ndogo mpaka juu huko, sio rahisi kuchukua "Hoehae/mangumblu" toka mtaani.. Je, wewe umewahi kupita kwenye malezi ya kitume?

UNATAKA (Kadiri ya maandishi yako) kujiunga upadre, je washirika/jimbo?

Haloo, SIKUKATISHI TAMAA, LAKINI una asilimia 0.98% za KUUPATA.

Mimi sijui lolote, NIMELOPOKA TU.
Usimvunje moyo mwenzako.
 
Jambo la kwanza u padri ni wito, mchakato wake una mambo mengi kuanzia ukuaji wako, uhusiano wako na kanisa nk.
Hiyo ndio inaitwa vetting kwa wale mliouliza vetting ni kitu gani kwenye kujiunga upadri

Vetting yake sio ya kitoto

Utachimbwa ndani nje
 
Kama unataka upadre wa jamii forum basi subiri majibu ya wadau ila kama una nia ya kweli ni vyema ukaenda kanisani na kukutania na padre wa miito ambaye atakujibu maswali yako yote bila wasiwasi.
Hapa hapa pia kuna majibu mazuri. Ni kuchambua tu jema na baya. Amefanya vizuri na atapata msaada anaouhitaji
 
Ukifika darasa la Saba unafanya mitihani ya seminari ili kukuandaa kuingia kidato cha kwanza ,ukifaulu kwa alama wanazotaka basi unapewa fomu ya kujaza ,unalipa ada zao na ndipo tunaanza kidato cha kwanza ,suala la umri ukiingia kidato cha kwanza unasoma pre_form one mwaka mmoja,mpaka unamaliza sekondari unakuwa umetumikia miaka mitano lakini pia kuna mitihani ambayo unafanya hiyo mitihani ukipata chini ya alama 50 unarudishwa nyumbani kwa maana umeshindwa kuendelea na shule hivyo kama ulianza na miaka 14 utamaliza na miaka 19 ,mwaka wa mwisho wa masomo unachagua masomo yako matatu pamoja na Bible knowledge huku ukichagua shule za kidato cha tano ambazo zinahusika na seminari za kikristo pia unatakiwa ufaulu kwa kiwango cha division one au two zile za mwanzo hivyo ukifaulu unakwenda kusoma kwa miaka miwili yaani five na six ,jumlisha miaka 19 na hii miwili inakuwa miaka 21 baada ya hapo ukifaulu unakwenda chuo kwa miaka kama 6 hivyo mpaka unamaliza unakuwa na miaka 27,28,30 na ndani ya hiyo miaka 6 ndipo unaambiwa hakuna kuona wewe utahudumia jamii tu
Seminari kuu sio miaka 6,ni miaka 8 hadi 9, Miaka mitatu (3) Ni Falsafa, Miaka minne (4) ni Teolojia, Mwaka mmoja (1)wa Uchungaji.Sometimes km kuna shida Ktk ufaulu au nidhamu huweza kwenda miaka ,8 hadi 9 na sometimes 10.
 
Huo ni utume, Watumwa wa utume huo WANAO WITO... Swali la kwanza je, wewe una wito huo au UNATAKA?

WITO huu unahakikiwa kuanzia seminary ndogo mpaka juu huko, sio rahisi kuchukua "Hoehae/mangumblu" toka mtaani.. Je, wewe umewahi kupita kwenye malezi ya kitume?

UNATAKA (Kadiri ya maandishi yako) kujiunga upadre, je washirika/jimbo?

Haloo, SIKUKATISHI TAMAA, LAKINI una asilimia 0.98% za KUUPATA.

Mimi sijui lolote, NIMELOPOKA TU.
Yesu alichukuwa watu hoe hae kina Mtume Petro na wakawa bonge ya mitume...
 
Seminari kuu sio miaka 6,ni miaka 8 hadi 9, Miaka mitatu (3) Ni Falsafa, Miaka minne (4) ni Teolojia, Mwaka mmoja (1)wa Uchungaji.Sometimes km kuna shida Ktk ufaulu au nidhamu huweza kwenda miaka ,8 hadi 9 na sometimes 10.
Mwaka mmoja wa malezi sijauona apoa,wazee wa kipalapala ntungamo,na segerea
 
Habari za wakati huu wanajamii.

Moja kwa moja kwenye swali langu la msingi.

Nahitaji kujiunga na Updare wa Kanisa Katoliki, ila kuna baadhi ya maswali sijaweza kupata ufafanuzi wake.

1.Ni umri gani unakuwa mwisho wa kujiunga na upadre?

2.Je ni elimu kiwango gani kinakubalika ili kuendelea na masomo ya Upadre?

3.Je kama nilikuwa na mahausiano ambayo sikufunga Ndoa Kanisani, baadae mahusiano yakafa na tumeshapata Mtoto inakuaje?


Nakuombeni ufafanuzi wa kina wandugu.
Tafuta kuonana na mkurugenzi wa miito jimbo katoliki ulilopo
 
Habari za wakati huu wanajamii.

Moja kwa moja kwenye swali langu la msingi.

Nahitaji kujiunga na Updare wa Kanisa Katoliki, ila kuna baadhi ya maswali sijaweza kupata ufafanuzi wake.

1. Ni umri gani unakuwa mwisho wa kujiunga na upadre?

2. Je, ni elimu kiwango gani kinakubalika ili kuendelea na masomo ya Upadre?

3. Je, kama nilikuwa na mahausiano ambayo sikufunga Ndoa Kanisani, baadae mahusiano yakafa na tumeshapata Mtoto inakuaje?


Nakuombeni ufafanuzi wa kina wandugu.
Number 3 imekuengua..... wewe ni mlei
 
Habari za wakati huu wanajamii.

Moja kwa moja kwenye swali langu la msingi.

Nahitaji kujiunga na Updare wa Kanisa Katoliki, ila kuna baadhi ya maswali sijaweza kupata ufafanuzi wake.

1. Ni umri gani unakuwa mwisho wa kujiunga na upadre?

2. Je, ni elimu kiwango gani kinakubalika ili kuendelea na masomo ya Upadre?

3. Je, kama nilikuwa na mahausiano ambayo sikufunga Ndoa Kanisani, baadae mahusiano yakafa na tumeshapata Mtoto inakuaje?


Nakuombeni ufafanuzi wa kina wandugu.
Kwanza hakuna masomo yanaitwa masomo ya upadre. Upadre ni Sakramenti. Pili umeshafeli kabla hata hujaanza jitihada zako. Upadre sio wa kombania. Njia sahihi muhimu na ya kwanza ni kuonana na paroko wa mahali husika uliopo.
 
Habari za wakati huu wanajamii.

Moja kwa moja kwenye swali langu la msingi.

Nahitaji kujiunga na Updare wa Kanisa Katoliki, ila kuna baadhi ya maswali sijaweza kupata ufafanuzi wake.

1. Ni umri gani unakuwa mwisho wa kujiunga na upadre?

2. Je, ni elimu kiwango gani kinakubalika ili kuendelea na masomo ya Upadre?

3. Je, kama nilikuwa na mahausiano ambayo sikufunga Ndoa Kanisani, baadae mahusiano yakafa na tumeshapata Mtoto inakuaje?


Nakuombeni ufafanuzi wa kina wandugu.
Swali la kwanza Hakuna mwisho wa umri kujiunga na upadri.

Kuhusu elimu ukitoa kidato cha sita,siyo chini ya miaka 10 ya kusoma vyuo vikuu ukisomea huo upadri.HAIPUNGUI MIAKA KUMI.

Swali la tatu,Kwa kuwa ulishakuwa na mtoto hili ni kikwazo kwako.Ila sina hakika na hili.

Hayo mengine ndivyo ilivyo.

ILA UPADRI NI WITO SIYO KAZI.HILO ULIJUE.

PIGIA MSTARI NENO WITO.WITO.

UKIWA HUNA. WITO UTAKWENDA KUTEMWA TU AU UTAJITEMQ MWENYEWE .
 
Kwanza hakuna masomo yanaitwa masomo ya upadre. Upadre ni Sakramenti. Pili umeshafeli kabla hata hujaanza jitihada zako. Upadre sio wa kombania. Njia sahihi muhimu na ya kwanza ni kuonana na paroko wa mahali husika uliopo.
Alichomaanisha masomo ya theolojia,malezi ñk
 
Back
Top Bottom