Nataka kumiliki Scania R450. Je, pesa itarudi baada ya muda gani?

Nataka kumiliki Scania R450. Je, pesa itarudi baada ya muda gani?

Basi itakuwa biashara zote za usafirishaji zina changamoto Sana, me sikuwahi kuwa na gari kubwa la biashara Ila nimewahi miliki Bajaj na pikipiki kadhaa, aiseee aisikwambie mtu.....yaani ni pasua kichwa vby mno!
Mkuu mie nakushauri anza na Fuso Tandam ndio utapiga pesa zaid. Ninakushauri hvo kwa kuwa hapa home tuna Scania tatu na Fuso mbili ila Fuso ndio zinapiga kazi kuliko Scania.

Na pia km ni Scania kwa wewe unaeanza sikushauri kwa kuwa ni sumbufu sana hasa ikishaanza kuchoka. Scania za kukutoa umaskini ni zile model za kizaman.

Na pia wanaokushauri kuhusu magari ya abiria naomba usiwasikilize kabisaa, maana yana changamoto nyingi sana. Mie binafsi nina Nissan Caravan mbili ila ni kichefu chefu kitupu.

NB: nimekushauri kutokana na uzoefu wangu wa kuishi na hayo magari kwa muda mrefu.
 
Nimepata kama mil 100 baada ya kuvuna vanila huko Bukoba. Sasa nahitaji nijiingize kwenye biashara ya usafirishaji na wazo langu ni kununua scania kama kwenye picha

Nimepanga kuanza na moja kutokana na kiasi nilicho nacho

Naomba wenye uzoefu, kama biashara ikienda vizuri, kwa mwezi naweza ingiza kiasi gani?
View attachment 1484199
Kabla hujanunua nenda cheki na wazoefu wa logistics kama golden fleet ujiingize kwenye michongo yao nje ya hapo utalia kilio ambacho hujawahi kulia maisha yako
 
Kama kilimo kimekupa pesa hizo nakushauri uendeleze tu kilimo ongeza hekta na pia nunua matrekta ya kulimia na kuvunia you dnont need kuivest kwenye biashara za watumia ndago. ... ila kwa Sound yako unaonehsa mtu wa Fix na Mipango mingi isiyotekelezeka... Alamsiki.
 
Kama kilimo kimekupa pesa hizo nakushauri uendeleze tu kilimo ongeza hekta na pia nunua matrekta ya kulimia na kuvunia you dnont need kuivest kwenye biashara za watumia ndago. ... ila kwa Sound yako unaonehsa mtu wa Fix na Mipango mingi isiyotekelezeka... Alamsiki.
Ulianza vizuri sana, mwishoni umeongea madudu.
 
Inaelekea huna taarifa sahihi. Ndago iko kwenye kilimo.
Hakuna biashara inayolipa kwa sasa kama ya usafirishaji.
Kama ipo naomba iwekwe hapa tuichambue.
Kama kilimo kimekupa pesa hizo nakushauri uendeleze tu kilimo ongeza hekta na pia nunua matrekta ya kulimia na kuvunia you dnont need kuivest kwenye biashara za watumia ndago. ... ila kwa Sound yako unaonehsa mtu wa Fix na Mipango mingi isiyotekelezeka... Alamsiki.
 
Tofautisha changamoto za biashara na usimamizi mbovu ukianzia jinsi unavyowapata na kuwalipa madereva.
Basi itakuwa biashara zote za usafirishaji zina changamoto Sana, me sikuwahi kuwa na gari kubwa la biashara Ila nimewahi miliki Bajaj na pikipiki kadhaa, aiseee aisikwambie mtu.....yaani ni pasua kichwa vby mno!
 
Hayo ni maneno tu. Biashara ya mkaa ipo ya aina 2. Kuutoa porini na kuja nao mjini na kuupakia vituo maalum kuuleta mjini. Hii ya 1 inaua gari na hii ya 2 inalipa. Mfano kuutoa mkaa njombe kuja dar ni biashara kubwa.
Kwanini kubeba mkaa? Nifumbue hapo
 
Gari ambazo nina uzoefu nazo ni Howo na Shacman.

Ngoja nianze na Howo .
Howo ni miongoni mwa Gari za Kichina nzuri sana hasa kwenye utumiaji wa mafuta .Ukitaka kununu gari kama hii ni vema ukanunua Brand new .Maana bei ya mpya inashabiana na Bei za Scania used.Faida ya Howo mpya ni kuwa ina utumiaji mzuri wa mafuta hasi kulingana Horse Power (HP) yake ni 371. Katika biashara ya magari kitengo cha mafuta ni chagamoto so unapoata gari inayokula mafuta vizuri inapungiza gharama za uendeshaji. Pili Howo ikiwa mpya na ukapata dereva mzuri na mzoefu itakuchukua muda mrefu sana kupata hitilafu za mara kwa mara.Kwa kifupoi haina breakown za mara kwa mara na itakuchukua miaka Mitano mpaka 8 kuanza kusumbua.Kwa hiyo miaka kama utakuwa umeitumia vizuri utakuwa umeshrushisha hela yako na umeshanunua nyingine tena .
Upatikanaji wa spare ni rahisi kwa Tanzania ka sasa kuna mawakala wengi wa SINOTRUCK hapa Bongo so spare si tatizo.Pia spare zake bei affordable

Hasara za Howo.
Life span ya hizi gari ni fupi ukiliganisha na gari kama Scania .So ni vizuri kuitunza vizuri ili na yenyewe ikutunze pia.Service za mara kwa mara ni muhimu .
Ni muhimu ni kuwa mafundi wazuri na wanajua gari si bora fundi. Ikupendeza mara moja moja uwaite wenyewe wachina waicheki.
Gari za Shacam.
Ni gari ngumu na zenye nguvu sana, Nguvu kubwa inatoka kuwa na Horse Power kubwa kuna za 420HP na 440 HP .HP kubwa inasababisha ulaji mkubwa wa mafuta .
Fiada za Shacman ni pamoja na kuwa na nguvu kubwa gari kama hiii ni ngumu kukwama sehemu za rough Roads.Hii inaweza kupita sehemu ngumu kwa mfani mvua inanyesha huko migodini ni ngumu sana kukwama.
Inawe uwezo wa kubeba mzigo mikubwa kwa mfano inaweza kuungwa na trailer ya Lowbed na ikabeba mzigo heavy sana.

Hasara ya Shacman
Utumiaji mkubwa wa mafuta huchangia gharama za kiu edeshaji kuwa kubwa.
Life span yake pia si ndefu kama ilivuo gari nyingi za kichina.
Mkuu tunaomba bei zake kuanzia kipisi mpka flatbed
 
Hahahaha kwamba akina luhuye, hunge, Texas, sigori, mwanza huduma na wenzao wanafanya ujinga kutembea tupu?

Wale gari zao ni kwa ajili ya mizigo yao na wameridhika na pesa wanayopata kwenye cement mkuu..

Ukiona gari imebeba cement ujue tajiri amekunja 11m, na unaeza kuta hata gari 4 zinapeleka sehem moja!

Hayo mambo ya madagaa dere ndo na yeye anajitafutia ugali

Sent from my SM-J105H using JamiiForums mobile app
Mwanza huduma sio mdogo yule, niliongelea hawa wanao chipukia
 
Kuna kampuni kama sikosei ni Overland walikuwa wakitoka Zambia kama wanarudi tupu basi gari moja itabeba horse za gari 2, na nyingine itabeba tela za gari 2.

Hapo atakuwa amepunguza hesabu ya gari 4 kurudi tupu, na zitahesabika ni gari 2 zimerudi tupu.
Kampuni kubwa nyingi wanafanya hivyo, wanaokoa wese
 
Jamani mnampoteza. Yeye sio kampuni hivyo mifano ya kampuni haitamsaidia.
Anachonitaji ni mbinu tunazotumia watu binafsi kwenye biashara ya malori katika kuajiri, kutengeneza gari, kutafuta mizigo na kusimamia biashara ya malori.
Kampuni kubwa nyingi wanafanya hivyo, wanaokoa wese
 
Jamani mnampoteza. Yeye sio kampuni hivyo mifano ya kampuni haitamsaidia.
Anachonitaji ni mbinu tunazotumia watu binafsi kwenye biashara ya malori katika kuajiri, kutengeneza gari, kutafuta mizigo na kusimamia biashara ya malori.
Tunampoteza wapi? hakuna mtu amemwambia afanye hilo , lakn pia kwakua tunategemea biashara ikue si vibaya tukajua hawa wakubwa wao wanafanyaje
 
Mkuu sina uhakika na bei ila niongelee upande wangu huwa tunanunua Fuso ya kawaida yan single diff ambayo inakuwa bado nzma kabsa kuanzia milion 22 hadi 28, halafu tunaipeleka garage Moshi kwenda kuongeza chassis na kuwa Tandam.

Pia inarembwa na kufanyiwa kila kitu hadi ikitoka hapo inakuwa km mpya. Cost zote inaweza kusimamia milion 42 hadi 50 na gari inakuwa imesimama balaa

NB: hyo cost ya milion 42 had 50 ni kuanzia gharama ya kununua gari hadi kufanyia kila ktu.
Natumaini umekosea kidogo au takwimu zako ni za miaka mingi nyuma.
Kiuhalisia na kikawaida huwezi kuipeleka fuso ya mil 25 eti ukaiwekee tandem kwani hiyo ni bei ya fuso iliyochoka.

Inatakiwa na inashauriwa ununue fuso yako kinanda yaani saaafi kabisa agiza hata ya mil 60 sasa ndo uipeleke gereji ikafanyiwe mambo, ikitoka hapo tayari thamani yake inakua kwenye million 80-100 hivi. Huu ndo uhalisia wa SASA mwaka 2020
 
Hapana Tandam ipo juu ya kipisi, kwa maana kipisi kilichosimamia kucha unachukua kuanzia milion 25 hadi 32.

Hali kadhalika Tandam kuna wengne wananunua hadi million 70, 80, had 90.
Kipisi cha million 25????? Itakua napitwa na mengi, naomba uniunganishe na muuzaji wa hivyo vipisi vya bei hiyo kiongozi vinahitajika vitatu chap viwe 113, 93 au 94 poa tu
 
Japo sipo kwenye mood ya kuandika, lakini nikipita kimya nitakua sijakutendea vema wala kuitendea vyema nafsi yangu.
Nina uzoefu niseme wa kutosha kuweza kutoa 'expart opinions' kwa mtu anyetaka kuanza biashara ya usafirishaji kwa kumiliki malori.
Nawapongeza wachangiaji wenzangu kwenye uzi huu, ila kuna mawili matatu nimegundua toka kwa hao wenzangu japo kuu hasa ni hili.
-Wengi hawana taarifa kamili na sahihi juu ya bei na uhalisia wa aina anuai za magari pia uhalisia katika sekta nzima ya usafirishaji hapa nchini.
Wengi wameshauri na umeonesha kuridhika na ushauri juu ya kuanza na Fusi-tandam. Mimi kwa uzoefu wangu sikushauri kuanza na tandam kwa sababu zifuatazo;
+ Gharama. Ununuaji na ubireshaji wa tandam huweza kufika 80-100mil hii ni gharama kubwa sana kwa gari ya tandam ukilinganisha na performance yake barabarani.
+Matunzo. Tandam ina gharama kubwa sana katika matunzo hasa hasa engine. Ukumbuke ile ni engine yenye HP kama 200 hivi lakini inabebeshwa tani 18 hivyo injini huchoka haraka na kuhitaji kubadilishwa. Ni kawaida kwa life span ya injini kwenye tandam kuwa miaka minne japo mara nyingine huweza kujikongoja hadi 8 kutokana na nidhamu yako ya kuibebesha mzigo
+Mifumo ya uendeshaji. Tandam nyingi hasa hasa nikiwa ni mzigo hata tani 12 tu ujue haina uwezo wa breaking za ghafla so katika kipengere hiki tegemea neema ya Mungu na kuthibitisha hili fuatilia ajali za tandam kugonga gari nyingine kwa nyuma utaambiwa sababu.

Kama utaamua kuanza na gari toka ukoo wa mzee Mitsubishi basi achana na tandam ila chukua fuso kipisi beba tani zako 7au 8 baas. We mwenyewe jiulize tu gari ulikua designed kubeba tani 5 ila Bongo Pasua Kichwa Engineering wanaifanya ibebe tani 18.
USHAURI WANGU SASA.
Kwa mtaji wa milion 100, anza na gari ambayo gharama ya manunuzi yake hadi kuingia road yaani horse na trailer yake isizidi 80ml.
Hapa utaona kipi rahisi kwako either kuagiza used ulaya au used ya kibongo bongo, ambapo kwangu naona ni sawa tu japo hakikisha kama ni used ya kibongo bongo usichukue iliyoingia nchini zaidi ya miaka miwili nyuma.
Hapo ukitaka kuagiza ni vema ukaanza na gari ambazo ni rafiki kwa mafundi na vipuri vyake mara ipatapo faida. Nashauri Scania series 4 yoyote kati ya 114 au 124 horsepower yoyote hamna shida najua hiyo hadi inakaa road itakugharimu kwenye 60ml hivi na trela lake ni 20ml tu.
Anza na safari za local na kwa kuwa wewe ni mgeni basi kichwa chako ni halali ya Dalali na atakupiga sana katika miezi mitatu ya kwanza hadi kichwa kikukae sawa utengeneze wateja wako. Route zinatofautiana na msimu kwani kuna wakati nyanda za juu kubalipa na kuna wakati kanda ya ziwa kunalipa.

Oya nimechoka kutype, ntaendelea kesho
 
Natumaini umekosea kidogo au takwimu zako ni za miaka mingi nyuma.
Kiuhalisia na kikawaida huwezi kuipeleka fuso ya mil 25 eti ukaiwekee tandem kwani hiyo ni bei ya fuso iliyochoka. Inatakiwa na inashauriwa ununue fuso yako kinanda yaani saaafi kabisa agiza hata ya mil 60 sasa ndo uipeleke gereji ikafanyiwe mambo, ikitoka hapo tayari thamani yake inakua kwenye million 80-100 hivi. Huu ndo uhalisia wa SASA mwaka 2020
Hujakosea mkuu, ila tu gari ambayo wewe unainunua kwa milion 30 mie naweza kuipata kwa milion 20.
 
Back
Top Bottom