Nataka kumiliki Scania R450. Je, pesa itarudi baada ya muda gani?

Nataka kumiliki Scania R450. Je, pesa itarudi baada ya muda gani?

Mafuta yana faida ila kwa mtaji wa roli moja au mawili usijaribu.Mafuta ni risk na short zikitokea wakati wa kushusha ni hasara ya transporter, bei za tela za tenki zipo juu.

Ukitaka upate ahueni kama una gari chache kubali kufanya joint venture na kampuni kubwa zenye tenda ili na wewe uingize gari zako na kupata mafuta ya kupeleka nje(Transit)

Kama unavutiwa kusafirisha mafuta upate tenda za ndani(local) kwenye sheli za mikoani za watu binafsi ambayo hawana gari.
 
Thanks[emoji120]
Mafuta yana faida ila kwa mtaji wa roli moja au mawili usijaribu.Mafuta ni risk na short zikitokea wakati wa kushusha ni hasara ya transporter, bei za tela za tenki zipo juu.

Ukitaka upate ahueni kama una gari chache kubali kufanya joint venture na kampuni kubwa zenye tenda ili na wewe uingize gari zako na kupata mafuta ya kupeleka nje(Transit)

Kama unavutiwa kusafirisha mafuta upate tenda za ndani(local) kwenye sheli za mikoani za watu binafsi ambayo hawana gari.
 
Sio muandishi mzuri bali naomba nichangie kidogo kwa uzoefu niliopata baada ya kuamua kuingia kwenye hiyo biashara 2011 to 2015.
1. Nilisajili kampuni na kupata investor Exemption TIC, unapata break kubwa ya kodi na zoezi likaanza.

2. Tuliagiza gari 4 na tela 4 Daf XF 3 flatbed trailer na 124 moja yenye tela ya tiper. 124 ilikuja single excel ikaongezwa hapa bongo kwa gharama ya 5M kila kitu.

3. Kazi ikaanza mwaka wa kwanza ulikuwa sio mbaya kazi zilikuwepo na madereva wa mwanzo walikuwa wanajielewa ikawa angalau si haba dola zilikaa mkononi. Shida ikaanza baada ya kuondoka kurudi ninapoishi nje ya Tanzania hapo madereva na wasimamizi ikaanza shughuli nzito madereva wakaondoka na kuanza na madereva vishoka hali ikawa tete nikaamua kuuza Daf zote nikabaki na 124 tipper nikatafuta kampuni ya ujenzi nikaingia now mkataba wa kazi na kuacha majukumu kwa mtu wa kusimamia hiyo tu.
My point.
Gari ya kuanza nayo kama unataka kusogea tafuta 124L haitakuangusha kama utaihudumia vizuri, unawezanunua single excel ukaongeza excel bongo maana kununua single ni bei chini na zipo nyingi europe.
Pia kama unataka kuingia kwenye hii biashara ni kweli pesa ipo sana ila unahitajika kujitoa kwenye hiyo biashara 120% hakikisha gari imepakia mzigo bandarini usimuamini agent, Ukiweza safiri mpaka nchi za jirani kutana na ma agent na jenga nao ukaribu na muaminiane sana.
Dereva makini ndio mtaji na mafanikio yako ,kama ukipata dereva mzuri basi mtunze na muhudumie kama nyumba ndogo yako sababu utapata return kwake ya kuhudumia chombo kinachompa mazuri yote unayompa.
Mwisho Nasisitiza hili. Muda wako wote ujitoe kwenye hiyo kazi na uwepo wako ndio mafanikio yako.
Mimi ilinishinda kutokuwepo sehemu ya tukio ila kwa biashara ni nzuri sana ,ingawa sasa hivi kidogo ina misukosuko ya hapa na pale lakini muda utapita itarudi kama zamani.
Nipo njia kuirudia 2026 kunapo uhai.
Asanteni.
 
Biashara magari labda uwe dereva mwenyewe, hakuna watu hatari kama Madereva. Watakufilisi.

Kama alivyopata hasara yule Mama wa roli moja lililotumbukia mto Wami.
Ni uzembe wa dereva kuto kuhakiki mfumo wa Upepo ktk hilo lori.

Kama alikuwa na mtaji mdogo ndo keshafirisika hapo.
Madereva afadhali na ugonjwa wa Corona.
 
Kwa local naomba nikusahihishe route ya Dar-Mza ni $43 to $47 per ton unless uwe inabeba mizigo ya international company ndio unaweza kupata $70..... Which is also rare for the owner of single truck.
 
Kuna kampuni kama sikosei ni Overland walikuwa wakitoka Zambia kama wanarudi tupu basi gari moja itabeba horse za gari 2, na nyingine itabeba tela za gari 2.
Horse ndio nini?

Nimesikia brigedia general aliyeopoa Scania la Mama mto Wami anasema engine na Cabin vimepotea, chasis na horse vimepatikana. Horse ni nini? Thanks.
 
Horse ndio nini?

Nimesikia brigedia general aliyeopoa Scania la Mama mto Wami anasema engine na Cabin vimepotea, chasis na horse vimepatikana. Horse ni nini? Thanks.

Horse au Tractor Unit ni kichwa cha roli kinachotumika kuvuta tela la mzigo.
Cabin ni sehemu ya kuendeshea na dereva kupata kupumzika au kulala.
Hiyo chini ni Horse ya Scania yenye Day Cabin. Cabin hii haina kitanda cha kulala.
 

Attachments

  • images (2).jpeg
    images (2).jpeg
    20.2 KB · Views: 29
  • images (2).jpeg
    images (2).jpeg
    20.2 KB · Views: 29
Horse au Tractor Unit ni kichwa cha roli kinachotumika kuvuta tela la mzigo.
Cabin ni sehemu ya kuendeshea na dereva kupata kupumzika au kulala.
Hiyo chini ni Horse ya Scania yenye Day Cabin. Cabin hii haina kitanda cha kulala.

Horse haiwezi kuwa ndio tractor unit au kichwa kinachovuta trela kama unavyodai kwa sababu:

Mkuu wa kamandi za wahandisi wa kijeshi kikosi cha NYUMBU PROJECT, aliyeagizwa na Mkuu wa Majeshi ya Wananchi kwenda kuopoa Scania la Mama wa mto Wami, Brigedia Generali Mhandisi Mwandamizi Hashim Yusuph Komba, amesema wamefanikiwa kuokoa CHASIS na HORSE lakini ENGINE na CABIN vimezolewa na mto, havikupatikana!

Na Cabin ndimo mule mbele anamolala dereva, na ndio kichwa..

KICHWA cha Scania kimepotea.
HORSE imepatikana.
Kwa hiyo KICHWA sio HORSE.

HORSE ni nini ???


 
Horse haiwezi kuwa ndio tractor unit au kichwa kinachovuta trela kama unavyodai kwa sababu:

Mkuu wa kamandi za wahandisi wa kijeshi kikosi cha NYUMBU PROJECT, aliyeagizwa na Mkuu wa Majeshi ya Wananchi kwenda kuopoa Scania la Mama wa mto Wami, Brigedia Generali Mhandisi Mwandamizi Hashim Yusuph Komba, amesema wamefanikiwa kuokoa CHASIS na HORSE lakini ENGINE na CABIN vimezolewa na mto, havikupatikana!

Na Cabin ndimo mule mbele anamolala dereva, na ndio kichwa..

KICHWA cha Scania kimepotea.
HORSE imepatikana.
Kwa hiyo KICHWA sio HORSE.

HORSE ni nini ???


Maelezo ya Offshore yako sahihi 100%
 
Horse haiwezi kuwa ndio tractor unit au kichwa kinachovuta trela kama unavyodai kwa sababu:

Mkuu wa kamandi za wahandisi wa kijeshi kikosi cha NYUMBU PROJECT, aliyeagizwa na Mkuu wa Majeshi ya Wananchi kwenda kuopoa Scania la Mama wa mto Wami, Brigedia Generali Mhandisi Mwandamizi Hashim Yusuph Komba, amesema wamefanikiwa kuokoa CHASIS na HORSE lakini ENGINE na CABIN vimezolewa na mto, havikupatikana!

Na Cabin ndimo mule mbele anamolala dereva, na ndio kichwa..

KICHWA cha Scania kimepotea.
HORSE imepatikana.
Kwa hiyo KICHWA sio HORSE.

HORSE ni nini ???


huenda mkuu wa kamandi za uhandisi alipitiwa tu kidogo japokuwa tamko lake halibadili ukweli juu ya maana ya horse!

Horse ni combination ya cabin na complete chassis mahususi kwa ajili ya kuvuta semi trailer/interlink(tela zisizo na ekseli mbele).

Sent from my SM-J105H using JamiiForums mobile app
 
Wakuu,

Niseme machache.

Marehemu Rugemalila Mutahaba aliwai kusema maneno haya, naomba kumnukuu" Ukifanya biashara na haikupi changamoto basi hiyo biashara haina faida achana nayo"

Akaenda mbali tena, Mjasiriamali wa kweli ni yule anayebadilika badilika huwez kukomaa na biashara ya aina moja tu kwa wakati wote, Mwisho wa nukuu.

Hii biashara ina changamoto zake lakini ina pesa, sehemu yeyote yenye changamoto pesa inapatikana hapo.

Scania 113M ni horse nzuri lakini ina mapungufu yake, hii gari haitumii umeme mwingi na ulaji wake wa diseal ni mkubwa, lakini pia haina Kitanda.

Kwa mfano trip ya Dar -Lubumbashi, halafu Lubumbashi - Dar hiyo gari inatumia diseal lita 2400 na muda mwingine mpaka 2500 wakati scania 114L, 124L inakula lita 2200.

Kwa ushauri wangu, unaweza kuanza na scania 114L yenye horse power 380 cabin ndogo. Au ukishindwa sana basi chukua DAF XF 95 manual, (camis engine)

View attachment 1484869

View attachment 1484870

Kama nilivyosema awali, Dereva ndiye mtu muhimu sana atakaye kutoa hapo ulipo mpaka sehemu uliyopanga wewe kufika. Tatizo kubwa kwenye hii biashara wamiliki wengi wanamchukulia dereva kama barmaid.

Dereva mzuri unampataje? Madereva wazuri siku zote wanaibwa kutoka kwenye makampuni mengine.

Tengeneza mofolojia ya kazi yako vizuri, kwa mfano kuna kampuni X inamlipa dereva mileage ya kwenda Lubumbashi na kurudi dar TSHS 1milion

Kiaje? Dereva anapewa shs 500k kwenda Lubumbashi na anavyoingia Mgodini kupakia copper unampatia dola 100, akirudi dar unampa shs 300k kama return mileage. Sasa dereva kama huyo kwanini asiheshimu kazi na kutunza gari lako vizuri..!

Kwenye hii kazi reporting ni muhimu sana, mwenye mzigo wake anataka kujua gari iko wapi na imelala wapi? Sasa ili uweze kwendana na hii ari huna budi kutengeneza Kanuni ambayo itakuwa kama katiba ya kazi ofisini kwako.

Dereva aanze safari saa moja asubuhi na ikifika saa kumi na mbili jioni apaki gari atafute guest alale na atume ujumbe kwako kukupa report. ( Kuwa mkali sana kwa dereva anayepuuzia hili)

Madhara ya kutembeza gari usiku ni makubwa sana na yanaweza kukufilisi kabisa na ukajuta kwanini uliingia kwenye hii biashara ya magari kama wanavyoelezea wadau hapo juu.

Breakdown, jitahidi sana kuepuka hitilafu za njiani, funga spare za uhakika ambazo utaweza zipata sub-scania au kwenye maduka mengine ambayo yako vizuri.

Na unapopata breakdown najua kichwa kinawaka moto na pressure inakuwa juu, jitahidi sana kujicontrol, pokea simu ya agent aliyekupakilisha mzigo au mteja mwenyewe mwambie ukweli na umpe uhakika wa usalama wa mzigo wake na uhakika wa kutoka hapo ulipo nasa.

Kutokupokea simu za hao watu kutakuharibia sana na siku nyingine utashindwa aminiwa na ukizingatia ndiyo kwanza unaanza.

Kwenye hii biashara tuna utatu mtakatifu, ambao ni Dereva, Agent / Wakala wa mizigo na Fundi wako wa gari, Hawa watu ishi nao vizuri, kuwa nao karibu kushindwa mchepuko wako.

Chonde chonde usiruhusu lori lako kubeba mkaa, (kama ni kagunia kamoja basi akamwagie maji ndiyo akabebe)

Rate za mizigo sokoni huwa zinabadilika kutoka na ari ilivyo kwa wakati huo na kabla ya kumpatia agent nyaraka zako za gari basi jiridhishe kwa kufanya utafiti kidogo wa bei maana nao ni watafutaji kama wewe.

Shukrani sana!

Muwe na jumapili njema iliyobarikiwa
Kwanini asibebe mkaa????????????
 
Back
Top Bottom