Nataka kumiliki Scania R450. Je, pesa itarudi baada ya muda gani?

Nataka kumiliki Scania R450. Je, pesa itarudi baada ya muda gani?

Mkuu
Fuso ni biashara ya dereva na sio mwenye gari. Uliza maswali ya msingi kwenye biashara.
Mfano.
1. Wewe unalenga kupata faida kiasi gani kwa mwezi?
2.Hiyo milioni 100 ni pikipiki ngapi na hesabu yake ni kiasi gani kwa mwezi1?
3. Je ni bajaji ngapi? Hesabu kwa mwzi je?
4. Taxi. Ngapi ? Mapato kwa mwezi?
5. Fuso za mchanga je.
6. Fuso za mizigo?
7. Trucks za tani 10? Mfano scania 94? 93 etc
8. Scania za tani 30 ? Nk

Utaona bei za Fuso tandam inafikia .ilioni 80 wakati hiyo ni 124. Hesabu zao kwako tajiri ni mbingu na nchi, pia matengenezo ya fuso ni makubwa.
Hata bima kubwa ya fuso iko juu sababu ya risk ya fuso.

Vinginevyo jenga nyumba pangisha ila kipato cha nyumba ya 100m kwa mwaka ni kipato cha 124 cha mwezi !

SHINDANISHA HUO MTAJI USIUTUPE TUU KWA MASIFA.
Mkuu, ushauri nimeuvhukua na ufanyia kazi
 
Kuna mdau kaeleza kwenye huu uzi jinsi wanavyo nunua na kuzibadilisha.
Mmenishawishi kuhusu Tandam fuso,,sasa swali zinauzwa bei gani na pia Tandam fuso ndo inakuaje?.
Najua kipisi,pulling,semi,boxboard,,ila kwenye Tandam fuso niko gizani
 
Tanzania yapo magari mangapi?? yote yametumbukia ? biashara zote zina risk mkuu, na zote zina risk za kuhatarisha na kuua mtaji wote , ndio maisha yalivyo, tuna options mbili tu either tufanye au tusifanye
Muhimu ni kukata bima kubwa.
 
Kumiliki sania ni issue ndogo. Kazi ni kupata dereva mtulivu na anaeielewa gari. Pili ni nani na wapi pa kutengeneza gani lako na tatu unaifanyaje hiyo biashara. Ziko aina 4 za mfumo wa biashara ya malori hapa Tz.
1. Unaoperate kama kampuni, yaani unatafuta mzigo wewe, unantuma tu dereva na unampa mileji yake. Pesa zote unalipwa wewe tajiri.
2. Unasafirisha mizigo yako ya biashara zako. Hii ni kama una hardware etc.
3. Unakaa kushoto...unatembea na gari. Unapatana kila kitu wewe na kszi ya dereva ni kuendesha tu.
4. Hesabu. Unamkabidhi gari dereva, mnakubaliana route na unampa mtaji wa mafuta. Dereva anakuletea hesabu kwa mzunguko wa kwenda na kurudi. Wewe unabaki na matengenezo makubwa, service na tairi. Humlipi posho.

Kila moja ina faida na hadara zake.
Nimeifanya hiyo kwa miaka zaidi ya 30 sasa.

Ushauri.
Unapotaka kununua gari la biashara angalia bei za vipuri na upatikanaji wa mafundi wazuri eneo lako. Usikimbilie magari ya kisasa au ya nyuma sana au lenye milleage nyingi sana.
Scania ni chaguo zuri. Ushauri baki kwenye 124
Vichwa vinazidi kuja sasa.
Ushauri makini sana huu.
 
Mkuu
Fuso ni biashara ya dereva na sio mwenye gari. Uliza maswali ya msingi kwenye biashara.
Mfano.
1. Wewe unalenga kupata faida kiasi gani kwa mwezi?
2.Hiyo milioni 100 ni pikipiki ngapi na hesabu yake ni kiasi gani kwa mwezi1?
3. Je ni bajaji ngapi? Hesabu kwa mwzi je?
4. Taxi. Ngapi ? Mapato kwa mwezi?
5. Fuso za mchanga je.
6. Fuso za mizigo?
7. Trucks za tani 10? Mfano scania 94? 93 etc
8. Scania za tani 30 ? Nk

Utaona bei za Fuso tandam inafikia .ilioni 80 wakati hiyo ni 124. Hesabu zao kwako tajiri ni mbingu na nchi, pia matengenezo ya fuso ni makubwa.
Hata bima kubwa ya fuso iko juu sababu ya risk ya fuso.

Vinginevyo jenga nyumba pangisha ila kipato cha nyumba ya 100m kwa mwaka ni kipato cha 124 cha mwezi !

SHINDANISHA HUO MTAJI USIUTUPE TUU KWA MASIFA.


Yaani sijui kwanini biashara za vyombo vya Moto zinaboa...Jana Kuna Bajaj kazi yake kusomba maji..Yan dogo anasema siku biashara ikichanganyia anauza trip8!@16000 ambazo ni dumu40@400!

Lakini eti kipande ni 15000!..! Tena kiangaszi biashara ndo nzuri Balaa..hw come umpe tajiri 15?ati oh mafuta na service juu yangu nikaona bado wizi mtupu
 
Mfumo wako wa biashara ni upi? Au unamuachia dereva ndio akuamulie? Wengi wanaanza biashara bila maamuzi ya uendeshaji wa biashara. Wananaachia madereva wawaamulie.
Mfano.
Biashara ya pikipiki na bajaji na teksi kwa sasa ina mifumo 2 mikubwa.
1. Mkataba. Unamnunulia, mnakubaliana hesabu kwa wiki na muda, say mwaka na nusu baada ya hapo chombo kinakuwa chake. Wakati wote kinakuwa kwenye bima kubwa.
2. Hesabu kwa siku ila malipo kwa wiki. Hapa chombo ni chako hivyo matengenezo ni juu yako. Hapa unachochochunga vi hesabu na uzima wa chombo.

Ukiwa tajiri wa chombo cha moto kama dereva anatunza chombo na analeta hesabu usimuonee wivu.
Matajiri wengi hawaki kumuona dereva akibadilika hata kama kila kitu kiko sawa.
Kila mtu anahitaji maendeleo. Ni pamoja na dereva wako.
 
Mkuu sina uhakika na bei ila niongelee upande wangu huwa tunanunua Fuso ya kawaida yan single diff ambayo inakuwa bado nzma kabsa kuanzia milion 22 hadi 28, halafu tunaipeleka garage Moshi kwenda kuongeza chassis na kuwa Tandam.

Pia inarembwa na kufanyiwa kila kitu hadi ikitoka hapo inakuwa km mpya. Cost zote inaweza kusimamia milion 42 hadi 50 na gari inakuwa imesimama balaa

NB: hyo cost ya milion 42 had 50 ni kuanzia gharama ya kununua gari hadi kufanyia kila ktu.
Hiyo 22 unanua used from Japan au hapa bongo
 
Mkuu, ungeelezea gharama za huduma hiyo. Pia ungeelezea changamoto za magari hayo na gharama za kukarabati.
Gharama za kazi hii hutofautiana kulingana na kazi itakayofanywa kwa gari hisika. Fuso zote za tani 3 huitajiwa kuwekewa double chasis ili ziweze kubeba tani 10 kwa single au 16 kwa tandam
 
Mkuu,

Nikupongeze sana kwa uthubutu huu.

Hii biashara ni nzuri ila ina changamoto zake za hapa na pale ila ina pesa.

Ili uweze kutoboa kwenye hii biashara jitahidi kumudu jazba zako kwa dereva wako tena hasa akiwa porini , Dereva ndiye mtu anayeweza kukufanya ufanikiwe na kukufanya ufeli mazima.

Trailer zipo za aina mbili,

Flatbed na Skelton

Kwa vile wewe ndiyo unaanza basi nakushauri uchukue flatbed kwa sababu kazi zote utabeba. Vilevile uchukue Trailer yenye (axles za BPW).

Kampuni zinazozalisha hizo trailer zipo nyingi hapo mjini, Superdoll, Simba na wengineo, Nashauri ununue trailer za mtumba.

Kikazi,
Kuna trip za local( za ndani)
Kuna trip za transit ( Nje ya nchi)

Trip za ndani sikushauri uzifanye kwasababu zinachosha gari na magurudumu. Ni bora ufanye hizo za Transit tu, tena za Dar - Lubumbashi tu.

Trip za Dar - Lubumbashi hazichoshi gari ingawa gari inachukua mwezi mzima au zaidi lakini pesa yake unaiona, Gari inaenda na mzigo na inarudi na mzigo (Copper)

Sasa ili uweze kufanya hizo trip za transit kwa mtu wa gari moja, nakushauri ufanye joint venture na mtu mwingine ambaye ana gari nyingi ili uweze kupata c28 ya TRA na hii itakusaidia kujikusanya na kujifunza mchezo.

Kwanini nasema hivyo, sijajua mfuko wako ukoje ila kuna mlolongo wa makadirio ya kodi, kukata vibali vya Zambia na mambo mengine, kwa gari moja ni story tu.

Mkuu, Magurudumu ya gari yako hakikisha umenote zile serial number na uwe mfwatiliaji wa kuyakagua kila baada ya trip.

Dereva mtaji wake ni Diseal na Magurudumu, akiishiwa huko njiani anayanywa fasta na yanauzika sana hapo Tunduma au huko Mpika.

Punguza wanawake (Mademu) magari ni kama Majini hayapendi uchafu wa mwili, na pia dereva asikuzooee sana maana wanakuwaga na vinasaba vya kiswahili unaweza kujikuta yeye ndiye kawa boss na wewe ukawa mfanyakazi wake. Zingatia Services ya gari, usifuge magonjwa kwenye gari!

Naomba niishie hapa,
Cheza na dola mkuu.

Shukrani
Mkuu hapo kwenye wanawake naomba urudie kwanza mana itanisaidia siku na mimi nikiwa na wazo kama la huyu baharia

Capo Dei Capi
 
Back
Top Bottom