October man
JF-Expert Member
- Nov 23, 2017
- 3,635
- 5,012
Aisee
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Aisee
Ndugu yangu hilo ni jina tu.Ukiweza niajiri kwenye Kampuni yako.
Kwa huduma ya Kufwatilia Gari na Mafuta tuwasiliane inbox hutajuta na utapunguza gharama kwa kiasi kijubwa sana.View attachment 1485446View attachment 1485447View attachment 1485448
Usimpe matumaini hayo kaka utanuingiza katika shida kwa rut ipi aweke m 8 kwa mwezi hata siku mojaWastani ni mil 8 (ila itategemea na mizunguko yako pia,) ngoja wataalamu waje
Usimpe matumaini hayo kaka utanuingiza katika shida kwa rut ipi aweke m 8 kwa mwezi hata siku moja
Sent using Jamii Forums mobile app
Hili neno naunga mkono kwanza kabisa unakua huna presha daily unaiona gar yako na ndo biashara nzur na kama wewe mwenyewe huna kaz unaendesha mwenyewe tu income inazid zaidNunua mende ya mchanga.. Iweke Dar.. Nadhani kipande ni laki tatu kwa siku.. Usisahau kukatia bima kubwa.. Tafuta gari iliyo chini ya kilomita laki saba.View attachment 1484231
Bei ni hadi gari husika ikaguliwe na kupimwaAsante kwa taarifa mtaalam. Je bei ikoje kwa tani 10 na tani 16.
Huo ni ukweli mtupu, biashara ya magari na umalaya havikai pamoja. Hili sio tu kwa wamiliki hata madereva. Ukitaka kufilisika au kukutana na majanga/ajali zisizoisha changanya izo mambomkuu hapo kwenye wanawake naomba urudie kwanza mana itanisaidia siku na mimi nikiwa na wazo kama la huyu baharia
Capo Dei Capi
Route za hapa ndani tu unaipata , hiyo ni wastan kabisa , normalKama transit hio anapata hata na zaidi
Kwanini kubeba mkaa? Nifumbue hapoWakuu,
Niseme machache.
Marehamu Rugemalila Mutahaba aliwai kusema maneno haya, naomba kumnukuu" Ukifanya biashara na haikupi changamoto basi hiyo biashara haina faida achana nayo"
Akaenda mbali tena, Mjasiriamali wa kweli ni yule anayebadilika badilika huwez kukomaa na biashara ya aina moja tu kwa wakati wote, Mwisho wa nukuu.
Hii biashara ina changamoto zake lakini ina pesa, sehemu yeyote yenye changamoto pesa inapatikana hapo.
Scania 113M ni horse nzuri lakini ina mapungufu yake, hii gari haitumii umeme mwingi na ulaji wake wa diseal ni mkubwa, lakini pia haina Kitanda.
Kwa mfano trip ya Dar -Lubumbashi, halafu Lubumbashi - Dar hiyo gari inatumia diseal lita 2400 na muda mwingine mpaka 2500 wakati scania 114L, 124L inakula lita 2200.
Kwa ushauri wangu, unaweza kuanza na scania 114L yenye horse power 380 cabin ndogo. Au ukishindwa sana basi chukua DAF XF 95 manual, (camis engine)
View attachment 1484869
View attachment 1484870
Kama nilivyosema awali, Dereva ndiye mtu muhimu sana atakaye kutoa hapo ulipo mpaka sehemu uliyopanga wewe kufika. Tatizo kubwa kwenye hii biashara wamiliki wengi wanamchukulia dereva kama barmaid.
Dereva mzuri unampataje? Madereva wazuri siku zote wanaibwa kutoka kwenye makampuni mengine.
Tengeneza mofolojia ya kazi yako vizuri, kwa mfano kuna kampuni X inamlipa dereva mileage ya kwenda Lubumbashi na kurudi dar TSHS 1milion
Kiaje? Dereva anapewa shs 500k kwenda Lubumbashi na anavyoingia Mgodini kupakia copper unampatia dola 100, akirudi dar unampa shs 300k kama return mileage. Sasa dereva kama huyo kwanini asiheshimu kazi na kutunza gari lako vizuri..!
Kwenye hii kazi reporting ni muhimu sana, mwenye mzigo wake anataka kujua gari iko wapi na imelala wapi? Sasa ili uweze kwendana na hii ari huna budi kutengeneza Kanuni ambayo itakuwa kama katiba ya kazi ofisini kwako.
Dereva aanze safari saa moja asubuhi na ikifika saa kumi na mbili jioni apaki gari atafute guest alale na atume ujumbe kwako kukupa report. ( Kuwa mkali sana kwa dereva anayepuuzia hili)
Madhara ya kutembeza gari usiku ni makubwa sana na yanaweza kukufilisi kabisa na ukajuta kwanini uliingia kwenye hii biashara ya magari kama wanavyoelezea wadau hapo juu.
Breakdown, jitahidi sana kuepuka hitilafu za njiani, funga spare za uhakika ambazo utaweza zipata sub-scania au kwenye maduka mengine ambayo yako vizuri.
Na unapopata breakdown najua kichwa kinawaka moto na pressure inakuwa juu, jitahidi sana kujicontrol, pokea simu ya agent aliyekupakilisha mzigo au mteja mwenyewe mwambie ukweli na umpe uhakika wa usalama wa mzigo wake na uhakika wa kutoka hapo ulipo nasa.
Kutokupokea simu za hao watu kutakuharibia sana na siku nyingine utashindwa aminiwa na ukizingatia ndiyo kwanza unaanza.
Kwenye hii biashara tuna utatu mtakatifu, ambao ni Dereva, Agent / Wakala wa mizigo na Fundi wako wa gari, Hawa watu ishi nao vizuri, kuwa nao karibu kushindwa mchepuko wako.
Chonde chonde usiruhusu lori lako kubeba mkaa, (kama ni kagunia kamoja basi akamwagie maji ndiyo akabebe)
Rate za mizigo sokoni huwa zinabadilika kutoka na ari ilivyo kwa wakati huo na kabla ya kumpatia agent nyaraka zako za gari basi jiridhishe kwa kufanya utafiti kidogo wa bei maana nao ni watafutaji kama wewe.
Shukrani sana!
Muwe na jumapili njema iliyobarikiwa
Je gharama kwa kawaida huwa ni kiasi gani?Bei ni hadi gari husika ikaguliwe na kupimwa
Chonde chonde usiruhusu lori lako kubeba mkaa, (kama ni kagunia kamoja basi akamwagie maji ndiyo akabebe)
Mkuu ujue kuna mda mizigo ya local hua inatafutwa kwa tochi lakiniRoute za hapa ndani tu unaipata , hiyo ni wastan kabisa , normal
Tatizo zinakula sana mafuta.113 na 124 ni roho ya paka.alafu hazina mambo mengi kwenye mifumo yake kwenye injini.
Hiyo bei inafanana na fuso used nje tani 4 , manake naona zina range dolla 5000-7000 Ukiweka na kodi nadhan unaangukia kwenye hiyo price
Kama una coaster usinge uliza game la Scania.. Wacha utani nasi!Coaster ninayo, ipo barabarani