Nataka kuuza nyumba, viwanja, gari na vitu vyote vya ndani nirudi bara kuanza upya kutoka Zanzibar

Nataka kuuza nyumba, viwanja, gari na vitu vyote vya ndani nirudi bara kuanza upya kutoka Zanzibar

Tanga na Zanzibar Ni kama Kitu kimoja..
Mimi Mzaliwa wa Zanzibar na Nimekulia Tanga..
Nilihamia Tanga mwaka 1987..

Wengi wa Tanga Sana sana Pangani wanajiita wazanzibar..
Na zanzibar Mara Nyingi wanadai Tanga iko.kwao na Bagamoyo...

Watu wa Tanga Wengi Nikiwemo Mimi Tuna familia Huko zenji na ndugu pia..
Ni kweli kabisa na baadhi ya maeneo ya Bagamoyo
 
Ndugu wana JF poleni na kazi na mihangaiko ya maisha.

Mimi ni kijana wa miaka 29 mzaliwa wa Morogoro na kukulia DSM hasa maeneo ya Tandika! Nilipohitimu masomo yangu pale UDSM 2017 nilikuja Unguja mwezi wa 7 mwaka huo huo kujaribu bahati yangu, kilichonileta ni soka na alieniunganisha na hio timu ni rafiki yangu. Lkn ligi ya Unguja hailipi kwa mwaka huo ilikuwa ni kujitolea tu.

Mwishowe nikaongea na mwenye timu kuwa maisha ya soka yamenishinda narudi nyumbani, yule tajiri aliuliza kinachonisibu na mimi nikamueleza, Lkn alishangaa sana kusikia mimi ni muhitimu wa chuo kikuu na nimekosa kazi mpaka nimeamua kuja kucheza mpira ili nipate kula.

Yule tajiri alitokea kunielewa sana, akanambia nisiondoke na pale kwenye nyumba ya timu mtaani atanihamisha nitakaa peke yangu na atanitafutia kazi na kweli alitimiza, Mwaka uliofata yaani 2018 mwezi wa 8 niliajiriwa kwenye taasisi moja inayojishughulisha na masuala hapa Unguja.

Ile taasisi ilinibadilishia maisha yangu sana kwani ndani ya muda mchache nilikuwa miongoni mwa wafanyakazi tegemezi pale kwenye taasisi, elimu yangu ikanisaidia kupata nafasi nzuri na mshahara mzuri zaidi kwani wengi wa waajiriwa walikuwa hawana elimu kubwa na wengi ni mabeach boy tu wa mtaani.

Maisha yalibadilika sana ndani ya muda mfupi safari za Dar, Arusha, Zenji kwa mwewe ilikuwa kawaida sana kwangu, nilipata pesa nyingi pia nje ya mshahara wangu, Nyingi zikiwa ni tips toka kwa wageni tukiwa safarini.

Mimi napenda sana watoto na wageni wengi wenye watoto walikuwa hawawezi kuniacha hivi hivi maana watoto wao walinipenda kwa muda mfupi na mara nilipojua hili shimo nililishikilia kweli kweli japo corona ilifanya taasisi ikayumba kidogo na baadhi ya wafanyakazi kupunguzwa lkn nashukuru sikuwa miongoni mwao.

Wakati wa corona mabosi walishindwana (Nasema mabosi kwa kuwa taasisi ni share older ya watu watano), Baadhi walitaka kampuni ifungwe kupisha janga la corona na wengine walisisitiza kazi ziendelee hata kama ni kwa hasara Ila jina la kampuni liwe midomoni mwa watu, Mvutano huu ulipelekea muanzilishi mmoja wa kampuni kujitoa na kudai share zake na akapatiwa na kuletwa share holder mwingine (Huyu aliyejitoa ndio aliyenipa kazi baada ya kuuganishwa na yule jamaa mwenye timu)

Kutokana na changamoto ya corona, mshahara ulipunguzwa sana na tukawa tunalipwa kama posho tu. Hali hii ilifanya niingie bank kucheki balance yangu na nikakuta nina namba nzuri tu kwenye account zote mbili (Ya Tsh na Dolar) nikaamua kununua viwanja vitatu hapa Unguja, nikanunua Alphard pia nikampa mtu aifanye private hire na nikawa nampa wageni wa pale kazini wanaotaka usafiri kwa siri kubwa maana hairuhusiwi taasisi ina magari yake pia inakodisha. Nilibakiwa na pesa kidogo sana kwenye acc kw ajili ya kula na matumizi madogo madogo maana ardhi ni ghali sana Unguja hasa maeneno jirani kama Kisauni, Mbweni, Kiembe Samaki, Chukwani, Fuoni, Kwerekwe nk!

Penye rizki hapakosi fitna wahenga walisema, kuondoka kwa yule bosi mmoja ikiwa kama kinga niliyokuwa nayo pale kwenye taasisi imeondoshwa na hapo nikaanza rasmi kuoneshwa mm sistahili kuwa pale, kwanza nikondolewa nafasi niliyopewa kwa kigezo kuwa mimi sijasomea masuala ya utalii japo hakuna yeyote aliyesomea wengi wamesomea lugha tu Kifaransa, Kipoland, Kirusi, Kitalina nk, kuondoshwa kwa hiki cheo kukafanya nibaki nategemea mshahara tu though haukuwa mdogo mana ni tarakimu 7 lkn nilipoteza pesa nyingi nilizokuwa napata kwenye kuandaa safari za ndege, hotel, chakula, sehemu wanazotembelea wageni nk

Wageni wengi walinizoea na walikuwa wanatoa recommendation nzuri dhidi yangu hiyo hata ofisini nikawa sikosi mia mia nje ya mshahara, lkn kadri muda ulivyokuwa unaenda nilianza kuona visa na mikasa, ubaguzi wa wazi wazi dhidi yangu! Mtu anakuchokoza kwa kukuita kafiri kisa tu muda wa kuswali umefika na wewe hujaenda kuswali ama hujasitisha huduma, wengine wanakuita ukawa timu pinzani, wengne wanasema aliyekuleta kaondoka wewe unafanya nini ilimradi tu ujibu ukatwe mshahara ama usimamishwe kazi nk

Haya tote yalianza kunikinaisha na ile kazi maana sasa nilikuwa simalizi miezi 6 bila adhabu kusimamishwa bila malipo ama kukatwa mahahara hata “Akijamba Mwantumu naambiwa nanuka mm” hii hali ilinikera sana. Lkn mtoto wa maskini hadeki niliendelea kuhustle kama kawaida nikijituma huku na kule na mwaka jana mwanzoni nilifanikiwa kujenga nyumba kwenye moja ya viwanja vyangu, Nyumba ya vyumba vinne viwili vikiwa ni master, jiko sebule na dining na stoo nikaipiga fence tamu sana nikaiacha ikiwa inahitaji finishing ndogo sana za ndani lkn rangi madirsha milango tiles mafeni gypsum tyr kifupi ni complete house

“Barabara hata iwe ndefu vipi haikosi kona kona, mwaka Jana mwez wa 6 yule dereva wangu nilimpa wageni 7 wanataka kuzunguka shamba (Shamba ni eneo nje ya mji hapa Unguja, Huko kuna mahotel na starehe nyingine nyingi) wale wageni wakaomba waongozane na mmoja wa mwenzetu pale ofisini, Hapo ndo kitumbua kiliingia mchanga kwani wakiwa njiani yule mwenzangu aliisifia gari kuwa inatunzwa vizuri iko fresh sana na yule dereva wangu ndipo akaropoka kuwa gari ya boss wako X hii.

Jamaa akachimbwa na yule mwanamke akamfungukia kuhusu nyumba na mengne mengi anayoyajua kuhusu mimi. Kesho yake nikaitwa na boss kuulizwa kwanini wageni hawakodi magari ya ofisi na badala yake gari fulani linaonekana kubeba sana wageni wa kampuni hasa wale wanaopita kwenye mikono yangu!

Nilijitetea sana kwamba yule jamaa bei zake ni nusu ya zetu na wageni wengi ni vishuka (hawana pesa) ndo maana nampa yeye kuiepusha taasisi na hasara lkn maelezo yangu hayakufaa kitu! Boss alikuwa anajua kila kitu na mwsho akanipa barua ya kunisimaisha kunifukuza kazi. Nilimsihi sana anisamehe lkn haikufua dafu sana alisistiza nilipokula na kuihujumu taasisi pametosha.

Wakati huu sikuwa na akiba yoyote bank maana ndo nilitoka kumalizia ujenzi nikabaki nasubiri pesa za kwenye gari niwe nakula lkn jamaa nae akwa analalamika kukosa wageni hivyo pesa ikazidi kuwa ngumu na tayari nilikuwa nawasaidia ndugu zangu wengi hivyo nikaanza kuona pengo sasa.

Nikauza kiwanja kimoja mwak jana mwezi 10 ili nijitafute lkn imeshindikana ile pesa nimeishia kuila tu na kusaidia ndugu! Sasa nimebakiwa na kiwanja kimoja ambacho nilikinunua 18M thamani kwa sasa inaweza kufika 25M mpk 22M, 20M ikawa bei ya chap kwa haraka, nina Alphard japo biashara haiendi nimechoka kugombana na madereva, na nina nyumba ambayo thamani yake inaweza kufika 100M kwa hapa Unguja.

Wazo langu ni kuuza hv vyote walau nipate 150M to 140M Kisha nikanunue nyumba 3 Tandika za 15M each, 2 nizipangishe na moja niifanyie ukarabati niweke flem zangu Tatu nifungue duka la chakula na mahitaji yote ya nyumbani na nje niweke genge, flemu ya pili nifungue glosary ya kawaida ya mtaani na nje niweke chips na flem ya Tatu nifungue mama lishe!

Hili ni wazo langu naomba ushauri zaidi hata ulio nje ya huu wana JF.

NAWASILISHA.
Usiuze ulichonacho, endelea kupambana upate kingine.

Chukua arphard yako endesha mwenyewe uku ukisikilizia mchongo.

Hiyo 150m itaungua na uwe chizi.
 
Kijana usiuze nyumba wala gari.Nyumba yako ifanye kuwa bnb au itangaze huku bara am sure watu wengi tu wanakuja huko weekend unawakodishia gari chukua wageni wakifika unawachaji kuwapeleka kwako na nyumba unawachaji kwa siku watakazo kaa huwezi kulala njaa hapo hizo nyumba unazotaka kununua tandika hela yake utaipata kupitia hio nyumba ya zbar na gari .
 
Kijana usiuze nyumba wala gari.Nyumba yako ifanye kuwa bnb au itangaze huku bara am sure watu wengi tu wanakuja huko weekend unawakodishia gari chukua wageni wakifika unawachaji kuwapeleka kwako na nyumba unawachaji kwa siku watakazo kaa huwezi kulala njaa hapo hizo nyumba unazotaka kununua tandika hela yake utaipata kupitia hio nyumba ya zbar na gari .
Mkuu Asante sana. Nakupm unipange zaidi
 
Mkuu naona kama homesick inakusumbua umepakumbuka sana nyumbani si ndiyo?

Ushauri wangu fanya yote ila usije kuthubutu kuuza hio nyumba coz nyumba zanzibar zina thamani sana kutokana na ufinyu wa ardhi

Ni bora ukakomaa na hyo gari huku unaangalia upepo unavuma vipi! Kurudi huku bara halafu mambo yakuharibikie hata hao ndugu zako unaowasaidia watakukimbia
Ushauri mzuri ila asipoufata ipo siku ataukumbuka...
 
Mkuu pole kwa maswahibu, nina rafiki wakike mtu wa bara, ambaye ana gari ya kawaida tu, amepanga mbweni na ana kikampuni cha mfukoni tu japo ana vibali vyote hence analipa kodi, kazi yake anapokea watalii na kuwapangia safari, na hii kazi amejifunza mwenyewe bila msaada wa yeyote, mwaka wa 4 huu yuko kwenye game. Changamoto gari yake ni ya kawaida/ haiko licensed kubeba abiria/wageni, lakini anakomaa nayo tu, hata akikamatwa na matrafiki “yanazungumzika”.

Wewe ambaye umetoka kwenye reputable organization, una experience nzuri, una support system (your former Boss) una gari nzuri, naona uko kwenye nafasi nzuri zaidi ya kufanya vizuri, unless una tatizo lingine au umepamiss kwenu.

Wazanzibar hawa ni wakuishi nao hivyo hivyo tu, samaleko nyingi ilimradi yako yanaenda.

Usikate tamaa, binafsi naona ukiamua kukomaa utafanikiwa, tena una pakuishi kabisa. Labda kuna mengine haujayasema.
 
Mkuu pole kwa maswahibu, nina rafiki wakike mtu wa bara, ambaye ana gari ya kawaida tu, amepanga mbweni na ana kikampuni cha mfukoni tu japo ana vibali vyote hence analipa kodi, kazi yake anapokea watalii na kuwapangia safari, na hii kazi amejifunza mwenyewe bila msaada wa yeyote, mwaka wa 4 huu yuko kwenye game. Changamoto gari yake ni ya kawaida/ haiko licensed kubeba abiria/wageni, lakini anakomaa nayo tu, hata akikamatwa na matrafiki “yanazungumzika”.

Wewe ambaye umetoka kwenye reputable organization, una experience nzuri, una support system (your former Boss) una gari nzuri, naona uko kwenye nafasi nzuri zaidi ya kufanya vizuri, unless una tatizo lingine au umepamiss kwenu.

Wazanzibar hawa ni wakuishi nao hivyo hivyo tu, samaleko nyingi ilimradi yako yanaenda.

Usikate tamaa, binafsi naona ukiamua kukomaa utafanikiwa, tena una pakuishi kabisa. Labda kuna mengine haujayasema.
Hizi Dini tumeletewa tu na wala hakuna Dini itakayompeleka mtu mbinguni, kwanza asilimia kubwa hatujachangua Dini tuliyopo tumefata Dini za wazazi wetu Mimi nikifika maeneo Kama hayo na nikaona salama yangu ni kubadili Dini Hata sijiulizi Mara mbili.
 
Pole Mkuuu, bora uishi Urusi au Ujerumani ubaguzi wao una kipimo. Usithubutu kuishi na hawa Ndugu zetu Wavaa Vipedo. Baada ya kuishi Zanzibar na kuona Visa vyao na ubaguzi na Unyanyasaji wao nilliapa sijji kucheka na ngedere. Wakiwa bara wanajifanya kujichekesha kinafiki na sisi, lkn deep down ni vichomi, watu wenye hila na hawafai kwa chochote. Tupa kule kabisa, rudi nyumbani mkuu achana nao Mungu atakuongoza tu.
Sijapenda hapo tu uliposema "wavaa vipedo" kwa kuwa unabagaza imani za watu lakini ni ukweli usio na shaka wazanzibar (wengi wao) ni wabaguzi na haubaguliwi kwa kuangaliwa dini yako tu bali unabaguliwa kutokana ubara wako.
 
Pole sana kwa maswahibu mdogo wangu.

Hongera yako angalau wewe una kitu sema ni changamoto tu za dunia zinakusibu, pambana nazo.

Nakushauri usiweke hela zote katika biashara moja..

Uza hivyo vitu vyako ila usije ukajiingiza kwenye makundi yasiyo na maana
 
Katika kitu ambacho kimefichwa kwa ajili ya kuboresha muungano wetu ni hiki:

unwritten law : law based chiefly on custom rather than legislative enactments​


wewe njoo na NIDA kama hupati ardhi hapa Zanzibar!
Na kitambulisho cha Mzanzibari atapewa bila usumbufu. Wengi wa watanganyika wanavyo.
 
Pambania gari Yako beba wagenj utateleza sana ila utasimama....hakuna kazi rahisi tunajikausha tu....
 
Yah nimefanya research kabla na nimekulia sana maeneo Yale! Thow izo nyumba hazina finishing nzuri lkn ndo zilivyo nyumba nyingi za Dar hasa maeneo ya uswazi
Mwanangu unaenda kuuziwa nyumba za udongo wewe! Labda kama nia ni kupata kiwanja!
 
Mkuu pole kwa maswahibu, nina rafiki wakike mtu wa bara, ambaye ana gari ya kawaida tu, amepanga mbweni na ana kikampuni cha mfukoni tu japo ana vibali vyote hence analipa kodi, kazi yake anapokea watalii na kuwapangia safari, na hii kazi amejifunza mwenyewe bila msaada wa yeyote, mwaka wa 4 huu yuko kwenye game. Changamoto gari yake ni ya kawaida/ haiko licensed kubeba abiria/wageni, lakini anakomaa nayo tu, hata akikamatwa na matrafiki “yanazungumzika”.

Wewe ambaye umetoka kwenye reputable organization, una experience nzuri, una support system (your former Boss) una gari nzuri, naona uko kwenye nafasi nzuri zaidi ya kufanya vizuri, unless una tatizo lingine au umepamiss kwenu.

Wazanzibar hawa ni wakuishi nao hivyo hivyo tu, samaleko nyingi ilimradi yako yanaenda.

Usikate tamaa, binafsi naona ukiamua kukomaa utafanikiwa, tena una pakuishi kabisa. Labda kuna mengine haujayasema.
Hapana mkuu hakuna ambalo sijasema, hakuna nililoficha. Asante sana kwa ushauri. Nimeupokea
 
Ila ku supply nako changamoto saivi.....suppliers washakuwa wengi
Kila sehem ni mapambano. Dunia uwanja wa vita! Uzuri wa Zanzibar uchumi wake ni hybrid yani sio wa kitanzania Moja kwa Moja. Huyu akirudi dsm anaenda kupambana na uchumi wa mtanzania halisi... Kabla ya yote kwanza atafute mganga
 
Ni vyem kuhama huko hasa kam utategea kaz za watu wa zanzbr wata kunyanyasa
 
Back
Top Bottom