Nataka kuuza nyumba, viwanja, gari na vitu vyote vya ndani nirudi bara kuanza upya kutoka Zanzibar

Nataka kuuza nyumba, viwanja, gari na vitu vyote vya ndani nirudi bara kuanza upya kutoka Zanzibar

Wazo langu ni kuuza hv vyote walau nipate 150M to 140M
Ushauri: Tuliza kichwa kwanza! acha papara, mhemko, hisia, uharaka na msukumo! Kumbuka: Akili na maarifa ndiyo huleta hela mpaka utajiri!

1000 ni ndogo ila pia ni nyingi! Bilioni moja ni nyingi lakini pia ni ndogo! Unatakiwa ufahamu si kila anaweza kuzalisha hela hasa kwa makuzi na malezi ya watoto wa Kitanzania!

Watanzania tumekuzwa hivi:

Kuzaliwa-nenda shule -ukasome kisha ufaulu -halafu uajiriwe serikalini-Halafu ufe!
 
Tuliza akili tajiri, kibinda unacho idea unazo ila acha pupa.

Yaani unataka kufanya biashara zaidi ya 4 kwa mkupuo kwa hela hiyo hiyo.

Anza na hiyo utakayoisimamia wewe, hizo frem nyingine kama utajenga, pangisha kwa watu wenginr ili wakuletee wateja kwenye hiyo biashara yako ya duka.
 
Kiukweli jamaa wa unguja hawapendi kabisaaa kuona mtu anayetoka bara anafanikiwa, sijui ni kwanini..??

Watakupa chakula ila sio mafanikio, ili ufanikiwe lazima uwe mjanja

Kingine, wanakemea sana watoto wa wenzao kuingiza wanawake/wanaume kwenye nyumba za kupanga... Lakini watoto zao hasa wa kike hawashindi nyumbani mwao, kutwa kushikana viuno beach, watoto wao wa kiume wanavuta sana bangi na sigara
 
Pia jibu swali la mdau, tunaambiwa zenji mtanganyika haruhusiwi kununua kiwanja, ww uliwezaje?

Ushauri wangu hiyo nyumba ifanye apartment, wakodshie wageni watalii, jinsi ya kuwapata najua unajua maana umekuwa nao. Tumia gari lako kama usafiri wa wageni poa kuwaleta na kuwatoa kwenye apartment yako.
konakona nyingi sana ndio unapata ardhi...
 
Yani nasikia kilo ya mbuzi ni 20000 ila wenye mabucha wananunua kwako elfu 11. Angalia Cha kufanya huku huku hata saplai mahitaji kwa mahoteli hasa matunda na vegetables. Ukiwa supplier unaishi vizuri mkuu sio bara kule kwenye fursa utakuja kuomba kazi yoyote humuhumu jf walahi
Ila ku supply nako changamoto saivi.....suppliers washakuwa wengi
 
Ushauri: Tuliza kichwa kwanza! acha papara, mhemko, hisia, uharaka na msukumo! Kumbuka: Akili na maarifa ndiyo huleta hela mpaka utajiri!

1000 ni ndogo ila pia ni nyingi! Bilioni moja ni nyingi lakini pia ni ndogo! Unatakiwa ufahamu si kila anaweza kuzalisha hela hasa kwa makuzi na malezi ya watoto wa Kitanzania!

Watanzania tumekuzwa hivi:

Kuzaliwa-nenda shule -ukasome kisha ufaulu -halafu uajiriwe serikalini-Halafu ufe!
Asante kwa ushauri 🙏
 
Ndugu wana JF poleni na kazi na mihangaiko ya maisha.

Mimi ni kijana wa miaka 29 mzaliwa wa Morogoro na kukulia DSM hasa maeneo ya Tandika! Nilipohitimu masomo yangu pale UDSM 2017 nilikuja Unguja mwezi wa 7 mwaka huo huo kujaribu bahati yangu, kilichonileta ni soka na alieniunganisha na hio timu ni rafiki yangu. Lkn ligi ya Unguja hailipi kwa mwaka huo ilikuwa ni kujitolea tu.

Mwishowe nikaongea na mwenye timu kuwa maisha ya soka yamenishinda narudi nyumbani, yule tajiri aliuliza kinachonisibu na mimi nikamueleza, Lkn alishangaa sana kusikia mimi ni muhitimu wa chuo kikuu na nimekosa kazi mpaka nimeamua kuja kucheza mpira ili nipate kula.

Yule tajiri alitokea kunielewa sana, akanambia nisiondoke na pale kwenye nyumba ya timu mtaani atanihamisha nitakaa peke yangu na atanitafutia kazi na kweli alitimiza, Mwaka uliofata yaani 2018 mwezi wa 8 niliajiriwa kwenye taasisi moja inayojishughulisha na masuala hapa Unguja.

Ile taasisi ilinibadilishia maisha yangu sana kwani ndani ya muda mchache nilikuwa miongoni mwa wafanyakazi tegemezi pale kwenye taasisi, elimu yangu ikanisaidia kupata nafasi nzuri na mshahara mzuri zaidi kwani wengi wa waajiriwa walikuwa hawana elimu kubwa na wengi ni mabeach boy tu wa mtaani.

Maisha yalibadilika sana ndani ya muda mfupi safari za Dar, Arusha, Zenji kwa mwewe ilikuwa kawaida sana kwangu, nilipata pesa nyingi pia nje ya mshahara wangu, Nyingi zikiwa ni tips toka kwa wageni tukiwa safarini.

Mimi napenda sana watoto na wageni wengi wenye watoto walikuwa hawawezi kuniacha hivi hivi maana watoto wao walinipenda kwa muda mfupi na mara nilipojua hili shimo nililishikilia kweli kweli japo corona ilifanya taasisi ikayumba kidogo na baadhi ya wafanyakazi kupunguzwa lkn nashukuru sikuwa miongoni mwao.

Wakati wa corona mabosi walishindwana (Nasema mabosi kwa kuwa taasisi ni share older ya watu watano), Baadhi walitaka kampuni ifungwe kupisha janga la corona na wengine walisisitiza kazi ziendelee hata kama ni kwa hasara Ila jina la kampuni liwe midomoni mwa watu, Mvutano huu ulipelekea muanzilishi mmoja wa kampuni kujitoa na kudai share zake na akapatiwa na kuletwa share holder mwingine (Huyu aliyejitoa ndio aliyenipa kazi baada ya kuuganishwa na yule jamaa mwenye timu)

Kutokana na changamoto ya corona, mshahara ulipunguzwa sana na tukawa tunalipwa kama posho tu. Hali hii ilifanya niingie bank kucheki balance yangu na nikakuta nina namba nzuri tu kwenye account zote mbili (Ya Tsh na Dolar) nikaamua kununua viwanja vitatu hapa Unguja, nikanunua Alphard pia nikampa mtu aifanye private hire na nikawa nampa wageni wa pale kazini wanaotaka usafiri kwa siri kubwa maana hairuhusiwi taasisi ina magari yake pia inakodisha. Nilibakiwa na pesa kidogo sana kwenye acc kw ajili ya kula na matumizi madogo madogo maana ardhi ni ghali sana Unguja hasa maeneno jirani kama Kisauni, Mbweni, Kiembe Samaki, Chukwani, Fuoni, Kwerekwe nk!

Penye rizki hapakosi fitna wahenga walisema, kuondoka kwa yule bosi mmoja ikiwa kama kinga niliyokuwa nayo pale kwenye taasisi imeondoshwa na hapo nikaanza rasmi kuoneshwa mm sistahili kuwa pale, kwanza nikondolewa nafasi niliyopewa kwa kigezo kuwa mimi sijasomea masuala ya utalii japo hakuna yeyote aliyesomea wengi wamesomea lugha tu Kifaransa, Kipoland, Kirusi, Kitalina nk, kuondoshwa kwa hiki cheo kukafanya nibaki nategemea mshahara tu though haukuwa mdogo mana ni tarakimu 7 lkn nilipoteza pesa nyingi nilizokuwa napata kwenye kuandaa safari za ndege, hotel, chakula, sehemu wanazotembelea wageni nk

Wageni wengi walinizoea na walikuwa wanatoa recommendation nzuri dhidi yangu hiyo hata ofisini nikawa sikosi mia mia nje ya mshahara, lkn kadri muda ulivyokuwa unaenda nilianza kuona visa na mikasa, ubaguzi wa wazi wazi dhidi yangu! Mtu anakuchokoza kwa kukuita kafiri kisa tu muda wa kuswali umefika na wewe hujaenda kuswali ama hujasitisha huduma, wengine wanakuita ukawa timu pinzani, wengne wanasema aliyekuleta kaondoka wewe unafanya nini ilimradi tu ujibu ukatwe mshahara ama usimamishwe kazi nk

Haya tote yalianza kunikinaisha na ile kazi maana sasa nilikuwa simalizi miezi 6 bila adhabu kusimamishwa bila malipo ama kukatwa mahahara hata “Akijamba Mwantumu naambiwa nanuka mm” hii hali ilinikera sana. Lkn mtoto wa maskini hadeki niliendelea kuhustle kama kawaida nikijituma huku na kule na mwaka jana mwanzoni nilifanikiwa kujenga nyumba kwenye moja ya viwanja vyangu, Nyumba ya vyumba vinne viwili vikiwa ni master, jiko sebule na dining na stoo nikaipiga fence tamu sana nikaiacha ikiwa inahitaji finishing ndogo sana za ndani lkn rangi madirsha milango tiles mafeni gypsum tyr kifupi ni complete house

“Barabara hata iwe ndefu vipi haikosi kona kona, mwaka Jana mwez wa 6 yule dereva wangu nilimpa wageni 7 wanataka kuzunguka shamba (Shamba ni eneo nje ya mji hapa Unguja, Huko kuna mahotel na starehe nyingine nyingi) wale wageni wakaomba waongozane na mmoja wa mwenzetu pale ofisini, Hapo ndo kitumbua kiliingia mchanga kwani wakiwa njiani yule mwenzangu aliisifia gari kuwa inatunzwa vizuri iko fresh sana na yule dereva wangu ndipo akaropoka kuwa gari ya boss wako X hii.

Jamaa akachimbwa na yule mwanamke akamfungukia kuhusu nyumba na mengne mengi anayoyajua kuhusu mimi. Kesho yake nikaitwa na boss kuulizwa kwanini wageni hawakodi magari ya ofisi na badala yake gari fulani linaonekana kubeba sana wageni wa kampuni hasa wale wanaopita kwenye mikono yangu!

Nilijitetea sana kwamba yule jamaa bei zake ni nusu ya zetu na wageni wengi ni vishuka (hawana pesa) ndo maana nampa yeye kuiepusha taasisi na hasara lkn maelezo yangu hayakufaa kitu! Boss alikuwa anajua kila kitu na mwsho akanipa barua ya kunisimaisha kunifukuza kazi. Nilimsihi sana anisamehe lkn haikufua dafu sana alisistiza nilipokula na kuihujumu taasisi pametosha.

Wakati huu sikuwa na akiba yoyote bank maana ndo nilitoka kumalizia ujenzi nikabaki nasubiri pesa za kwenye gari niwe nakula lkn jamaa nae akwa analalamika kukosa wageni hivyo pesa ikazidi kuwa ngumu na tayari nilikuwa nawasaidia ndugu zangu wengi hivyo nikaanza kuona pengo sasa.

Nikauza kiwanja kimoja mwak jana mwezi 10 ili nijitafute lkn imeshindikana ile pesa nimeishia kuila tu na kusaidia ndugu! Sasa nimebakiwa na kiwanja kimoja ambacho nilikinunua 18M thamani kwa sasa inaweza kufika 25M mpk 22M, 20M ikawa bei ya chap kwa haraka, nina Alphard japo biashara haiendi nimechoka kugombana na madereva, na nina nyumba ambayo thamani yake inaweza kufika 100M kwa hapa Unguja.

Wazo langu ni kuuza hv vyote walau nipate 150M to 140M Kisha nikanunue nyumba 3 Tandika za 15M each, 2 nizipangishe na moja niifanyie ukarabati niweke flem zangu Tatu nifungue duka la chakula na mahitaji yote ya nyumbani na nje niweke genge, flemu ya pili nifungue glosary ya kawaida ya mtaani na nje niweke chips na flem ya Tatu nifungue mama lishe!

Hili ni wazo langu naomba ushauri zaidi hata ulio nje ya huu wana JF.

NAWASILISHA.
Uza viwanja ila nyumba usiuze nitafute inbox nikushauri unaweza kufanya nini?
 
Tuliza akili tajiri, kibinda unacho idea unazo ila acha pupa.

Yaani unataka kufanya biashara zaidi ya 4 kwa mkupuo kwa hela hiyo hiyo.

Anza na hiyo utakayoisimamia wewe, hizo frem nyingine kama utajenga, pangisha kwa watu wenginr ili wakuletee wateja kwenye hiyo biashara yako ya duka.
Asante sana kwa ushauri 🙏
 
Zanzibar bado fursa ni nyingi, hiyo nyumba uliyonayo inakupa pesa... Pangisha vyumba ama viwili, tumia kimoja.... Alphard ichukue mwenyewe piga kazi... Japo kwasasa ni low season... Tumia network uliyokuwa nayo wakati upo kazini... Huwezi kosa ya mafuta kwa siku
 
Kwa nini usendeshe gari yako mwenyewe,deal za kuchukua wagen toka airport to any hotel ziko wazi na nying znz,pili kwa nini usipangishe nyumba yako.watu wengi wanaofanya kazi za ma hotl znz hupanga chumba kimoja kimoja. Shamba anza ukulima kuliko kuuza.hivyo vitu ulivyonavyo ni asset nzuri maishan acha uoga.pambana jiajiri.hao ndugu wafike mahali waeleww unaanza upya.ww ni tajir tayar kuna watu hawana hata pa kulala,
 
Back
Top Bottom