Nataka nizalishe kuku wa kienyeji laki moja ndani ya miaka mitatu

Nataka nizalishe kuku wa kienyeji laki moja ndani ya miaka mitatu

Hakuna kitu chochote kisicho wezekana chini ya jua ukiwa na nia na mazingira wezeshi.

Kuku elfu 100 kuwataja ni rahisi sana, lakini katika uhalisia nimradi mkubwa sana ambao unatakiwa kuwa na mtaji mkubwa sana wa hali na mali.

Nguvu kazi inayotakiwa kuwa kwenye huo mradi sio ndogo.

Kiufupi inawezekana lakini sio kwa wepesi kwa kiasi hicho na pia kwa muda huo na pia tegemea soko kusumbua pia.
 
Kuna kitu mkuu unakosea sana, hakuna aliekataa mazingira ya kijijini kuwa hayako favourable Kwa ajili ya ufugaji wa kuku na hasa free range system
Sasa mkuu, kwani mtu hua anaanza tu kuku laki moja ghafla bin vuu? Kama mtoa mada alivyosema kwa sasa ana kuku 15 na vifaranga 70 kadiri mradi unavyoendelea kukua ataendelea ku update figures zake kulingana na mradi unavyokua. Lakin kingne uwezo wa kuzalisha chakula upo kama atajipanga vzr. Ukiwa na eneo kubwa unaweza kutengeneza chakula mbala like kulima mboga kwaajili ya kula kuku.

Kulima chakuka kwaajili ya kuku like mtama / mahindi kutengeneza hydrophonic fodders, kutengeneza minyoo / funza kwaajili ya chakula. Hapo kwny chakula hapo ndipo pa kupatolea macho sabab akicheza vbaya hapo faida anaweza asiione.
 
Ni rahisi kusema haya, lakini uhalisia haupo hivyo, unayo safari ndefu kufikia idadi hiyo.
Anaweza akawa ndio mtu wa kwanza kufanya hivyo, kwanini ishindikane kama ana rasilimali za kufanyia hiyo kazi. Kuku laki moja si wengi kushindwa kuwafikia idadi hiyo kwa miaka 3.

Anahitaji kuwa na speed ya uzalishaji kubwa.
 
Endelea kujifurahisha na kufurahisha wengine, ila kiuhalisia ni kwamba Huwezi kuwa na kuku laki moja

Unawajua kuku laki 1 au unawaskia tu? Hiyo mashine unayosema ipo ya kusaga haina uwezo wa kuhudumia kuku laki 1 Kwa siku

Ni vizuri kama umeamua kukimbia Dar na kurudisha mpira Kwa goal kipa ila kama ndo umerudi na mawazo hayo basi muda sio mrefu utarudi Dar pamoja na kuku wa Mama

Kuanza na kuku 15 saizi unawaza kuwa na kuku laki 1, unadhani wafugaji wenzio walio kwenye tasnia kabla yako hawajui hayo madawa na chanjo?

Huwajui kuku vizuri wewe, Kwa sasa we furahia tu hao vifaranga 70 Kwa sababu wapo ndani ya uwezo wako na ata wafike 500 still wanaweza wakawa ndani ya uwezo wako

ila ukitaka kujua kuwa inawezekana unawaza ukiwa umeshiba sana au Una njaa sana basi Piga hesabu ya gharama ya kulisha kuku 5000 tu ndio utajua kuwa unaota ndoto ukiwa ndani ya Maji

Anyway, All the best mkuu
Akienda Bank au taasisi za kukopesha, kuku wanaweza tumika kama dhamana.
 
Sio kumkatisha tamaa ni kuelezana ukweli tu. Kuku laki moja wanahitaji mtaji mkubwa sana zaidi ya milioni 500. Sasa hiyo time aliyojiwekea kufikia hiyo idadi si sahihi unless awe na mtaji kama milioni 250 kwa sasa awekeze ili akizalisha afikie hilo lengo.
naofuga kuku wa mayai au wazalishaji vifaranga. Broilers ni faida za kawaida za kusukumia ndinga ila sio kuwa bilionea
Ila akiweka dhamira anaweza kufanikisha hili. Sababu mayai si lazima watage kuku wake tu anaweza kuchukua hata kwa watu baki akawa anatotolesha. Sasa mfano akiwa na kasi ya kutotolesha vifaranga vingi na kuvitunza hadi vikakua kuna possibility akakimbiza na kuifikia hiyo idadi nakuweza kuimudu ingawa ni kuku wengi sana kuwafuga.

Na wanaweza hata kumpiga asipowapa chakula.
 
Ata kama mipango ni yake na sio yangu, ila kuna vitu vingine sio vya kumjaza mtu ujinga kisa nisimkatishe tamaa

Hebu tuwe serious, hivi wewe unawajua kuku laki 1 lakini au unataka tu kwenda na beat la mtoa mada umfurahishe?

Yani ulishe kuku laki 1 Kwa kutegemea mashine ya kusaga? Hebu acheni masikhara kwenye vitu vya msingi Aisee
Anaweza bwana. Kuku laki moja maana yake ni mafungu ya kuku 100 mara 1000. Akiweka malengo ya kuzalisha kuku 100 ndani ya muda huo mara 1000 anaweza kufika hiyo idadi na kuimudu kuilea.
 
Mleta mada ingawa idea yako imekaa kinadharia sana ila inaweza kutekelezeka kwa 90% with exceptions kama magonjwa ya mlipuko etec ambayo tuyatoe tukiamini ulinzi wa MUNGU upo juu yako.

Kuku laki moja ukiweka mkakati wa kuwapata kwa namna tofauti nje ya kuwazalisha mwenyewe tu kutokana na hao ulionao then itawezekana hadi hiyo miaka 3 ukaweza kutoboa na kuku hata elfu 80 au 90 which to me is goal attainable kuelekea kuku laki moja.

So my friend, ni kazi kubwa sana ila inawezekana na utaweza kumudu bila shida kukimbizia huu mradi wako. Cha msingi zingatia thamani ya pesa yako katika huo uwekezaji, mbinu utakazo tumia kwenye kufuga, na zaidi kabisa umakini ili usije pata loss sababu kuku 100,000 hawata takiwa kupata magonjwa yoyote.
 
Hakuna kitu chochote kisicho wezekana chini ya jua ukiwa na nia na mazingira wezeshi.

Kuku elfu 100 kuwataja ni rahisi sana, lakini katika uhalisia nimradi mkubwa sana ambao unatakiwa kuwa na mtaji mkubwa sana wa hali na mali.

Nguvu kazi inayotakiwa kuwa kwenye huo mradi sio ndogo.

Kiufupi inawezekana lakini sio kwa wepesi kwa kiasi hicho na pia kwa muda huo na pia tegemea soko kusumbua pia.
Kuku wakiwa wengi kiasi hicho soko ni uhakika cha msingi ni kulenga mteja sahihi kutokana ba utayari wa bei.
 
Mkuu unawazo zuri sana tena hadi nimependa arif,hizo ndio target za kiume unapoingia kufanya kitu unawaza mambo ambayo wengine wanaona Huwezi au unajitekenya mwenyewe.

lakini ukweli ni kwamba katika mawazo bora uliyonayo hilo nalipa no 1,target ni 100k chicken hauzwi kuku haliwi kuku mpka kufika Target,binafsi ni mfanyabiashara wa Gas wakati naanza nilisema nahitaji mitungi 1000 ndipo nianze kula faida ya Gas,

Nilionekana kama naota hivi,nilipokua naongea na wafanyakazi,wazazi wangu,na wale watu wangu wa Karibu lakini hivi sasa naelekea kufika tube 2000 nishafika buku kitambo saivi naitafuta 2000 by december iwe store. (inawezekana)

Shida ninayoiona kwako katika wazo lako ni 1, una wazo zuri lakini huna mikakati ya kukamilisha wazo lako,Kwa wingi huo wa kuku hutakiwi kuwaza Eneo,sijui dawa unazijua nk nk, unatakiwa uwaze namna ya kutengeneza chakula cha kuku wako,unatakiwa kujifunza namna ya kutengeneza dawa za kuku wako.

Project yako ni kubwa sana mkuu,kuku 100k ukirusha drone juu ukasema uwapge picha utasema ni Siafu wala hutosema ni kuku kwa namna watavyoonekana.

Hivyo basi nini ufanye ili ufanikishe hilo Wazo lako, kwanza unatakiwa uwe na uhakika wa chakula, Je pesa unayo? ni wazi pesa hauna hivyo unategemea ufugaji ukutoe, kwa project hiyo haitaki mtu type yako anaetemea kuku ndio wajilishe waljitunze,nk

Unahitaji kuwa mfanya biashara au mkulima,unaweza ukachagua kati ya kufanya biashara ya mazao au kulima mazao ambayo end product yake ni chakula cha kuku mfano Alizet au mahindi,nk

Ukiamua kuwa mfanyabiashara wa mazao ambayo end product n chakula cha kuku utatoboa, au uwe mkulima Lima alizeti lima mahindi,nk nk,ukisema ununue chakula chakuku Hutoweza nunua chakula cha kuku wa kienyeji.

Kuku wa kienyeji wanakula na wanahtaji madini mengi hivyo chakula chao yabidi uwe wewe bnafsi ndio mtengenezaji,kadhalika na dawa ujue namna ya kutengeneza dawa tofaut tofaut, ukifanikisha eneo hilo basi kuku hao utawamudu bila mashaka hawatokushinda.

ila ukisema utaenda kununua chakula sikweliHuwezi fanikisha utashndwa tu,ukisema ukanunue dawa si kweli utaanguka Tu,anza na msingi wa kuku wako mahitaji makuu ni mawili, DAWA na CHAKULA eneo unalo,andaa mazingira ya chakula cha kuku either uanzshe biashara ya chakula cha kuku au uwe mtengenezaji wa dawa zao.

Fanya kama mimi,nina Plan ya kujenga DREAM HOUSE lakini siwezi sema nitaanza jenga sasa hv kidogo kidogo hadi ikamilike HAPANA,nikisema niweke hela bank pia ni kuchezea muda tu.

Nilichoamua kwasasa nimefungua biashara ya HARDWARE hii hardware inauza material zote nitakazokuja tumia ktk ujenzi waangu siku ikifika,kwasasa imeanza nauza vifaa yani kila unachokijua kuhusu ujenzi wangu nauza,naweka mdogo mdogo taratbu hela yangu inaendelea kujizungusha kuptia hii biashara,Lakini lengo langu si Biashara ya Hardware,lengo langu ni kuandaa mazingira yatakayoniwezesha kuja kujenga DREAM HOUSE yangu.

siwezi nunua kila kitu kwa reja reja,ila ukifanya biashara ya hardware utajua m,aterial zipi fake,zipi bora zinauzwaje zinapatkana vipi,nitajua mengi,Muda wangu ukifika nyumba nitakayojenga ama kwa hakika lazima waseme nimetoa mtu kafara.

Lakini kila kitu ni PLANS je umejiandaaje kupokea kuku Laki, usichukulie kuku Laki ukahisi wakifika Laki watakua laki Tu,Hao ni wazazi LAKI umeongelea watoto zao (vifaranga) wanaolalia,nk mzee kufika kuku Laki makadirio utakua na kuku sio chini ya 500k jumlisha na vifaranga, umejiandaaje kupokea hii project mzeee, usiangalie kirahisi juu juu.

Anza na Mzizi wa project yako

CHAKULA
DAWA
MAZINGIRA
WAFANYAKAZI
ULINZI
DHARURA

anzia huko chini kabla hata hujaanza kufuga hao kuku,ukishakamilisha hivyo vitu haya anza sasa Ufugaji wako,kama hujamilisha hivyo vitu usianze wala usijaribu.

utakua n sawa na baba anaetaka mpa mimba mke wake wakati hajaandaa mazingira ya namna huyo mtoto akija atakula nini,atasomaje,atavaa nini,nk nk usiwe na tabia hizo mazingira ya kijacho huandaliwa kabla hajaanza kutafutwa.

Mazingira ya project yako huandaliwa kabla hujaanza hiyo project. ASANTE kwa Muda wako, zaidi tu niseme komalia hapo hapo.
 
Sio kumkatisha tamaa ni kuelezana ukweli tu. Kuku laki moja wanahitaji mtaji mkubwa sana zaidi ya milioni 500. Sasa hiyo time aliyojiwekea kufikia hiyo idadi si sahihi unless awe na mtaji kama milioni 250 kwa sasa awekeze ili akizalisha afikie hilo lengo.

Mie nina kuku wanyamana wa mayai. Tuongelee wa nyama tu ambao ninao 8000 at a time na mtaji wake kwenye miundo mbinu yote kuanzia eneo mabanda, uzio, maji, miundombinu ya kulishia na nyumba ya wafanyakazi iligharimu around 60 milioni na lengo ni kufika kuku 15,000 ndani ya miaka minne. Tena hapo nimewekeza hela yangu na nina mpango wa kuchukua mkopo nimeshakamilisha business plan yenye kuonyesha costs, turn over na faida nitakayopata na expansion strategies. Kwa huyu wa kuku 70 na aweze kufika 100,000 ndani ya miaka mitatu ni ngumu sana unless uwe na mtaji kubwa sana wa kuanzia na mashine kubwa sana za utotoleshaji (incubator) pia inatakiwa eneo kubwa sana kama heka 20 mpaka 50 na linatakiwa liwe fenced kama ukifuga kwa mfumo wa kuwaachia (freerange).

Wazo la mtoa mada sio baya ila inabidi afanye research ya kutosha kuhusu nini kinahitajika, madawa, masoko, miundombinu na vitu vingine. Nigeria kuna jamaa mmoja anafuga kuku kama 10,000 hivi wa kienyeji mtafute youtube. Pia ingia "Farm Up" youtube ujifunze kwa huyo jamaa mganda ingawa yeye anafuga kuku wa mayai unaweza kujifunza kitu. Matajiri kwenye sekta hizi za ufugaji kuku ni wanaofuga kuku wa mayai au wazalishaji vifaranga. Broilers ni faida za kawaida za kusukumia ndinga ila sio kuwa bilionea
Unakuku wa ngp wa mayai
 
Anaweza bwana. Kuku laki moja maana yake ni mafungu ya kuku 100 mara 1000. Akiweka malengo ya kuzalisha kuku 100 ndani ya muda huo mara 1000 anaweza kufika hiyo idadi na kuimudu kuilea.
Kuku laki moja kwa miaka mitatu sio kazi rahisi hivyo
 
Ila akiweka dhamira anaweza kufanikisha hili. Sababu mayai si lazima watage kuku wake tu anaweza kuchukua hata kwa watu baki akawa anatotolesha. Sasa mfano akiwa na kasi ya kutotolesha vifaranga vingi na kuvitunza hadi vikakua kuna possibility akakimbiza na kuifikia hiyo idadi nakuweza kuimudu ingawa ni kuku wengi sana kuwafuga.

Na wanaweza hata kumpiga asipowapa chakula.
Time frame aliyojiwekea ni ndogo sana na pia hana mtaji zaidi ya hao kuku alionao. Angewekeza say milioni 200 kwa hiyo miaka mitatu angeweza kufikisha kuku laki moja ingawa bado ni ngumu. Ukiingia kwenye hii biashara ndio utaelewa
 
Time frame aliyojiwekea ni ndogo sana na pia hana mtaji zaidi ya hao kuku alionao. Angewekeza say milioni 200 kwa hiyo miaka mitatu angeweza kufikisha kuku laki moja ingawa bado ni ngumu. Ukiingia kwenye hii biashara ndio utaelewa
Uko sahihi,ufugaji na kilimo ni sayansi sio maneno,mtaji pia ni muhimu sana
 
Nakutakia kila lakheri katika ufugaji ila anza nao taratibu ujue mbivu na mbichi za hiyo biashara. Mimi ni mfugaji wa kuku wa nyama na mayai. Nionavyo mie kwenye mazao ya ufugaji kuku, wenye faida sana ni kuku wa mayai wanafuatia broiler lisha hawa kuku chotora kisha wa mwisho wa kienyeji
Samahani nakufuata PM,
 
Endelea kujifurahisha na kufurahisha wengine, ila kiuhalisia ni kwamba Huwezi kuwa na kuku laki moja

Unawajua kuku laki 1 au unawaskia tu? Hiyo mashine unayosema ipo ya kusaga haina uwezo wa kuhudumia kuku laki 1 Kwa siku

Ni vizuri kama umeamua kukimbia Dar na kurudisha mpira Kwa goal kipa ila kama ndo umerudi na mawazo hayo basi muda sio mrefu utarudi Dar pamoja na kuku wa Mama

Kuanza na kuku 15 saizi unawaza kuwa na kuku laki 1, unadhani wafugaji wenzio walio kwenye tasnia kabla yako hawajui hayo madawa na chanjo?

Huwajui kuku vizuri wewe, Kwa sasa we furahia tu hao vifaranga 70 Kwa sababu wapo ndani ya uwezo wako na ata wafike 500 still wanaweza wakawa ndani ya uwezo wako

ila ukitaka kujua kuwa inawezekana unawaza ukiwa umeshiba sana au Una njaa sana basi Piga hesabu ya gharama ya kulisha kuku 5000 tu ndio utajua kuwa unaota ndoto ukiwa ndani ya Maji

Anyway, All the best mkuu
Acha kukatisha tamaa,
Kinashundikana nini
 
Back
Top Bottom