Natubu: Nilikuwa simuelewi Mwamposa, ila kwa idadi ya viwete walioponyeshwa Songea naanza kumuamini

Natubu: Nilikuwa simuelewi Mwamposa, ila kwa idadi ya viwete walioponyeshwa Songea naanza kumuamini

Mama mkwe anaugua kansa,anamwezi tangu aje hapa kaenda kwa mwamposa na kakutana nae kushikwa kichwa zaidi ya mara tatu ila mambo ni zero, juzi kaambiwa kina kongamano komboa familia kaja na gia akauze kiwanja apate pesa ya huko, nawangalia na wife alafu na baki hiiiiiii
Mwambie mama mkwe atumie juisi ya karoti na mbegu za maboga kwa wiki tatu halafu leta mrejesho hapa
 
Wengine wanabisha kwakuwa Ni wachawi au washirikina au hajawai kufuatilia miujiza inavyofanyika

Mwamposa hawezi kuwalipa wote wanao toa ushuhuda na ingekuwa ivyo wanaonunuliwa wangeshasema ukweli kwamba wamenunuliwa ili watoe ushuhuda
Swali kuna unayemjua kapona?
 
Hao waliojifanya vilema bomb lingetupwa hapo wangekimbia kabla ya kutibiwa kiujanja ujanja na mpigaji

Nakumbuka kuna jamaa hivi hivi alikuwa anawapanga watu waje kama vilema huko Kenya

Mwisho alipotapeli wengi akahama kwa Malaya wa Bar ila nao alipowatapeli waliita waandishi wa Habari

Jamaa waliingia kwenye show na baadae kina Dada wale walipoanza kuigiza wakabadili Gia na kumkashifu mchungaji
Endeleeni kuburuzwa na matapeli
Mkuu naikumbuka sana hii
 
Hakuna hospitali huko akafanye miujiza? Watu wanateseka mawodini na mtumishi yupo maeneo.
 
Kama kichwa cha habar hapo juu, ujio wa Mwamposa, Songea ni neema.

Umeleta uponyaji mkubwa sana, vilema wanatembea, vipofu wanaona, hiyo haina kupinga.

Mimi nilikuwa simuamini lakini kwasasa naanza kumuamini.

View attachment 2387081
Umetumwa siyo siri. Ila wajinga ndio waliwao nendeni mkaliwe mpaka mbakiwe na mifupa.

Ujinga upumbavu utapeli wa kiroho na kiimani mnazidi kuupigia debe kwa mafukara.

Mtayalipa hapa hapa duniani
 
Imani ndio dawa kinacchoponya ni iman na sio Mwamposa na inatakowa uwe na imani kweli kweli kuamini yan usi doubt hata dakika moja amini utapona hata ka unasali chumban kwako kikubwa uwe na moyo safi..,

Wengi sala zetu haziendi kwa kuwa tuna doubt na tunasali huku tuna dhambi....

Pamoja na kusema hivi ila naamin Mungu anaponya kupitia sisi binadamu huku dunian na sio muujiza wa Ghafla bin vuu ka enzi za Yesu.

Yaan ka ulikua mgonjwa ukasali kwa iman labda Mungu atakukutanisha na daktari mzuri, au ka ulikua huna kazi Mungu atakuongoza kwny connection, ka hvo ulikua kiwete Mungu atakuongoza kwa dokta mzuri wa mfupa ila mambo ya Ghafla bin vuu hayo aliweza Yesu tu...

TUJITAHD KUSALI KWA IMANI TUKIWA WASAFI BILA DHAMBI MUNGU ATATUONA HATA KA UNASALI CHUMBANI KWAKO
 
Back
Top Bottom