Naufunga mjadala: Zuchu ni mwandishi bora wa nyimbo kuliko Lady Jaydee

Naufunga mjadala: Zuchu ni mwandishi bora wa nyimbo kuliko Lady Jaydee

Mkuu, shikilia hapo sasa, kama unataka kufahamu anachokifanya Zuchu;
  • Mixing ya taarabu na singeli
  • Boosting ya matusi
  • Sauti inasaidiwa na vyombo

Show ya kwanza ya Jide naudhuria pale Diamond Jibilee, 2001, imeandaliwa na Clouds, nilipata wasaa wa kukaa naye meza moja aisee; itoshe kusema,
- Mleta mada anatafuta mileage kwenye thread yake na si vinginevyo!
Ana mahaba na Zuchu
 
Jide mara nyingi anaandikiwaga naamewahi kukiri domokaya ni moja kati ya mwandishi wake tofauti na Zuchu anaandika mwenyewe kwenye hili namuunga mkono mtoa mada but overall ukizungumzia kuhusu ubora wa kuimba Jide yupo by far zaidi ya Zuchu
Uha uhakika zuchu haandikiwi kijana?

Hebu acha kupotosha nenda dar ujue mengi sio kujifungia huko nachingwea
 
Sija soma komentii zote,ila samahani nakiri wewe ni mtoto wa 2000,unafananishaje maindi na pumbaa...lishangazi komando linaimbaa ujumbe toka ujazaliwa bro....sasa zuchu wako jimbo gani za ujumbe anazo nitajie bwana mdogo.japo mi ni hip hop and regge fun,si mchukii kwa kizazi chenu ni bora kwa nyie vijana wa ovyo so sorry to say that.
 
Jay Dee si kumlinganisha na Zuchu.
Jay Dee huyo anamzaa huyo Zuchu, heshimu amekaa kwenye game muda wote huo na bado anapambana na watoto wa 2000s.

Kitu ambacho hatuna uhakika Zuchu atafika hapo...

Kama ulishawahi ingia shows za Jay Dee utakiri Zuchu hawezi kufanya live performance kwa kuimba kama Jay Dee....
Nadhani hapa amezungumzia uandishi wa mashairi na si kitu kingine.
Kwenye uimbaji, performance na consistency kwenye game hiyo ni topic nyingine.
Jade alikuwa tishio sana,ana kipaji na ni fighter sana mpaka na ndiyo maana mpaka bado yuko relevant suala la je huyu bi mdogo atadumu kwa kipindi kirefu kama Jide,time will tell.
 
Uha uhakika zuchu haandikiwi kijana?

Hebu acha kupotosha nenda dar ujue mengi sio kujifungia huko nachingwea
Inasemekana 'eti' WCB kama hauandiki nyimbo zako mwenyewe hauwezi kuwa signed(hii ukitoa Queen Darlin ambaye alisainiwa kwa kigezo cha undugu).
Nobody can prove this lakini viongozi(managers) wa label ndivyo wanavyodai.
 
Jay Dee nilimshuhudia anafanya live performance yule dada anaimba aisee...

Mziki unapigwa umetulia unapiga fundo za vinywaji taratiiiib...

Sio unaniimbia 'kuna kitu kimoja sijui kinasimama kinataka kinyama.... Ptuuu.. upuuzi tu..
Chapati chapati 🤣🤣
 
We umeanza kusikiliza music majuzi nini?😀

Kwenye pen game hakuna msanii wa kike wa bongofleva amewahi kufikia uwezo wa Zuchu toka bongofleva izaliwe nasema hakuna.

Jide ni msanii mkali, anauwezo mkubwa kafanya hitsong nyingi namheshimu kwa ilo ila huu mjadala nimeuona uko kuwa Jide anaweza andika kumzidi Zuchu haupo sahihi.

Jide ni mkongwe ila ngoma nyingi ameandikiwa, Zuchu 97% ya ngoma zake anaandika mwenyewe.

Nafikiri mnaona uhandishi wa Zuchu hata wasanii wa kiume wengi hawamuwezi.

Nyimbo kama Raha, Kwaru, Nisamehe, Naringa ni uhandishi wa kiwango cha juu sana cha sanaa.

Huu mjadala usiendelee popote nimeumaliza rasmi.
 
Mtoa mada jitahidi kupunguza mahaba,uchawa,unafki,uzandiki na upambe katika mambo yanayomhusu komando .Hivi kulikuwa na umuhimu gani kumtaja mbona ungeweza kuandika bila kumtaja commando jide.

Eti asilimia tisini na Saba jide kaandikiwa hii asilimia umeipataje mkuu ?au ndio mahaba yanakufanya urahisishe kwenye namba Ili update Cha kuandika haraka haraka.mbona hujasema zuchu kaandikiwa asilimia ngapi?

Kuandikiwa Kwa msanii sio dhambi Ila dhambi ni kutokea chawa Kama wewe na kutoa takwimu feki Ili watu wamuone msanii wako ni Bora.Nakazia hata kama jide kaandika asilimia tatu mwenyewe basi katika hizo asilimia tatu kampita zuchu katika kazi zake zote alizoandika mwenyewe.
 
Back
Top Bottom