Nauliza, Mwalimu Nyerere nchi ilimshinda kuongoza?

Kweli Elimu ilikuwa bado ni ndogo na yeye Mwalimu alilijua hilo,
Ndio maana alikataa hata Madini ya dhahabu na mengineyo yasichimbwe kwa sababu waliokuwa wanahitaji kuchimba walitaka wapewe kwa masharti yao wawekezaji,

Mwalimu akawaambia acheni kwanza wenye Nchi wasome wajue thamani ya hayo Madini ili watakapokubali yachimbwe hawatakubali wapunjwe !
Bahati mbaya walipokuja hao wasomi waliokuwa wanasubiriwa Tukapigwa na kitu kizito kichwani !
 
Sunguratex, Mwatex, Mutex, UFI, Tamco, Tanganyika Packers na vingine vingi. Awamu zilizofuata ziliviua viwanda vyote japo ni kwa sababu ya presha ya IMF.
Tanganyika packers ya mzungu,aliitaifisha na ikamfia,umeorodhesha viwanda vya nguo,lakini watanzania walitembea uchi, viraka vitupu,walivaa magunia kipindi chake,hivyo viwanda vilizalisha nini!?..unaijua sukari guru?..ulifulia majani ya mpapai na mirenda kwa kuwa sabuni hakuna!?
 
Hivyo viwanda mbona vilishindwa kuzalisha bidhaa za mahitaji muhimu ya kila siku,hadi watu kutumia sukari guru,kuvaa magunia,sabuni tu za kufulia/ogea hazikuwepo?.. viwanda vilianza kumfia mwenyewe!?
Sikuwahi kuona watu wakivaa magunia!
Na Viwanda vyote vilikuwa vikifanya kazi japo ufanisi ulianza kupungua baada ya ile Vita ya Kagera !

Na Mabeberu wa IMF ndipo walipoona mwanya wa kumbana Mwalimu kwa sharti la kwamba kama anataka Mkopo ni lazima kwanza akubali thamani ya pesa ishuke kama walivyotaka wakubwa !
Mwalimu alikataa na akasema hawezi kukubali kugeuka jiwe!
 
Hata kumiliki gari, television TU ili kuwa ni msala mkubwa,
Acheni kumtetea huyo dictator, sasa tulitaka uhuru wa nini kama hatuwezi kumiliki uchumi wetu.
Na hii issue imepelekea mpaka leo wa tz kushindwa kumiliki rasilimali zao eg wildlife, minerals,gas.

Kila kitu kiko mikononi mwa rasi, na sio kwa wananchi kumiliki kupitia hisa .

Badala ya kuijenga nchi akakijenga chama kwa kutumia Kodi za wananchi masikini.
Niishie hapa
 
Vikwazo vya mabepari ndio vilimpelekea kung'atuka baada ya sera zake za ujamaa kufeli vibaya na kukosa msaada wowote baada ya former USSR kuanguka kwenye vita baridi. Ila foundation ya amani na mshikamano aliyotuachia watanzania inatosha kumkumbuka.

Hakuwa Rais fisadi na aliipenda nchi yake.
 
Hivyo viwanda mbona vilishindwa kuzalisha bidhaa za mahitaji muhimu ya kila siku,hadi watu kutumia sukari guru,kuvaa magunia,sabuni tu za kufulia/ogea hazikuwepo?.. viwanda vilianza kumfia mwenyewe!?
Kiujumla kama inchi ingemkuta mtu kama Magufuri,halafu akafanikiwa kukaa madarakani kwa mda mrefu,tungekuwa mbali Sana.
Angalia kwa miaka yote Nyerere aliyokuwa madarakani kamwachia Mwinyi inchi imechoka mbaya,hakuna mahitaji muhimu kalibu yote,kuanzia petrol,mafuta ya kula,sabuni,sukali,nguo kalibu kila kitu. Afadhali wenzetu waliokuwa wanaishi maeneo ya mipakani Kama, Kenya, Malawi,Zambia kwao hawakupitia changamoto kubwa
 
Hukuona watu wakivaa magunia!!..hata viraka hukuona?..unaona viraka siku hizi?!..unaujua mkasa wa akina mama kuwa uchi huko kusini kwenye ziara ya kiongozi mkubwa?.. viwanda vilishambuliwa na amini hadi ufanisi usiwepo baada ya vita?
 
Naamini ulikuwa mdogo kipindi kile !
Kulikuwepo na upungufu kidogo wa baadhi ya vitu tena haikuwa kwa nyakati zote!
Kipindi kile tulikuwa tukipata bidhaa zote kwa bei Elekezi iliyokuwa ikitolewa na tume ya bei !
Kwahiyo mambo kama ya sasa ya watu kukamuliwa bei na wanyonyaji hayakuwepo !

Na Mwalimu alituonya kwamba zitafika zama vitu vyote mnavyovitamani vijae madukani vitu vya anasa na kadhalika
Vitakuwepo madukani lakini wengi wenu hamtoweza kuvinunua mtaishia kuviangalia kwenye Vioo vya Madukani πŸ™„
Je ni kweli au sio kweli ???!! 😳😳
 
Kuwa na maarifa ni kitu kimoja na kuunganishwa na lugha moja ni kitu kingine.

Wakenya pia wanaongea kiswahili na siku hizi ni kizuri kwani wamekipa umakini huko mashuleni.

Malema hakuwa mjinga alipokipigia debe kiswahili kitumike afrika nzima. Lugha moja inarahisisha pia ulimwengu wa kiuchumi.
 
Nyerere anastahili heshima popote anapopewa mpaka leo hii. changamoto za dunia ile sio sawa na hizi za miaka ya sasa. Nchi nzima chuo kikuu kilikuwa kimoja tu.

Unasafiri kutoka Dar mpaka Tanga usiku kucha wakati ni mwendo wa masaa mawili tu.
 
Magufuli ni janga jingine,aliachiwa uchumi mzuri sana, uchumi ambao biashara zinafanyika kwa kasi,mzunguko wa pesa mkubwa,akaamua kuufikicha huo uchumi,mambo yakaanza kwenda arijojo, biashara zikafungwa kkoo na nchi mzima,akaona aite wafanybiashara ikulu, uchumi kuuharibu huchukua siku chache,kuujenga tunahangaika hadi leo
 
Alimdharau Kikwete na akataka kwa nguvu kubwa kuonyesha kwamba yote aliyoyafanya JK hayalingani na yale aliyoyafanya yeye. Ujuaji ulimzidi nguvu.
 
Hukuona watu wakivaa magunia!!..hata viraka hukuona?..unaona viraka siku hizi?!..unaujua mkasa wa akina mama kuwa uchi huko kusini kwenye ziara ya kiongozi mkubwa?.. viwanda vilishambuliwa na amini hadi ufanisi usiwepo baada ya vita?
Pesa yote ilielekezwa kwenye kumshughulikia Nduli !
Mpaka Magari binafsi baadhi yake yalikuwepo huko Front !
Kwahiyo kwa vyovyote vile Uchumi lazima ulitetereka na ndipo Mabeberu wakawa wamempata Mwalimu pale walipotaka kumpata !
 
Magufuli na yeye alikuwa na udhaifu wa kukosa uwiano katika maamuzi yake. Pia alikuwa na chembechembe za sadism, maumivu ya baadhi ya watu yalimfurahisha.
 
Unawapenda wananchiwako halafu wanalala njaa,si heri baba mpiga diri lakini
Hivi wewe unayakumbuka maduka ya Ushirika?kwa sisi wa vijijini ilikuwa inakuja Land Rover 09 imebeba sukari, mgambo na bunduki nyuma mnapanga foleni kwa ajili ya kupimiwa kilo mojamoja,kuna wakati sukali inaisha kabla wengine hawajapata

Yaani tumepitia maisha magumu nazani hata leo tukisimulia wanetu huwa wanaona kama hadithi vile
 
Umesema kweli tupu, inchi ilimshinda vibaya sana
Kama si mzee Mwinyi tungekuwa kama zimbabwe leo
 
Kwa umri wako mimi binafsi nilitegemea ungejua kilichotokea kwanza kwa experience to na pili kwa kusoma vitabu.
1970, mi niko la saba, namaliza primari.
Maisha ya kula mkate kwa Kenya Butter ilikuwa kwa sana.
Gramaphone za Grundig, magari za peugeot, vitanda vya Vono na sofa za wahindi ndio yalikuwa maisha.
1967, Mwalimu alitaifisha njia kuu za uchumi, mabenki viwanda, makampuni kama Bima, etc.
Wazalendo wakapata ajira kiuongozi na kukaa na mameneja wazalendo.
Kuanzia 70s Mwalimu alijenga viwanda vingi sana, vya tumbaku, chai, nguo n.k., makampuni ya mabasi KAMATA. UDA,RETCO Regional Transpot Corporations kila mkoa makapuni ya kusaga mazao NMC,Makampuni ya biashara mkoa, RTC, mameneja wazalendo.
Management ya viwanda na makampuni miaka ya kati ya 70s ilikuwa si nzuri, wizi kwa wingi kwenye mashirika ya umma.
Mashirika yalikuwa hayana mwenyewe na yakaanza kuzalisha losses.
Lossess zilifidiwa na ruzuku (kodi za wananchi)
1978, Idi Amin ndo akaja malizia kabisa katika downward decline ya uchumi.
Magari, malori, chakula, vijana wenye nguvu, ununuzi wa silaha nzito nzito ndio vikaumaliza uchumi kabisa.
1979, tuliposhida vita Mwalimu alitamka wazi kuwa itachukua miezi 18 kurudisha uchumi katika hali yake ya kawaida. Wachumi walmdanganya Malimi, hata baada ya miaka 18 hali ya uchumi na kushuka kwa thamani ya fedha za Tanzania ikawa hali ndio mbaya sana.

Wakati huo huo watu wakazaliana kwa wingi kugawana kile kidogo kilichopo. Wakti wa uhuru tulikuwa milioni 9, sasa miaka ya 70 tuko mara mbili au zaidi kufika miaka ya 80, mara tatu na zaidi.
Kiukweli hatuwezi kumlaumu Mwalimu kwa downward slide ya uchumi kutokana na ukweli kuwa wazalishaji waliendelea kuwa wachache na midomo ya kula kama mtoa mada iliendelea kuwa mingi sana.
Waalendo walikuwepo tena walishiriki kuyaua mashirika ya umma, sasa umlaumu Mwalimu kwa lipi?
 
Wewe kweli ulikuwepo nyakati zile πŸ™ŒπŸ‘
Wengine humu tunabishana nao wamelishwa matango pori !
 
Lawama lazima abebeshwe kama ambavyo kikwete, magu, na sasa samia wanavyolaumiwa,
Yaani lawama hazikwepeki kwa kuwa yeye ndio alikua kiongozi,
Inchi ilimshinda na hii ndio statement sahihi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…