Nauliza, Mwalimu Nyerere nchi ilimshinda kuongoza?

Nauliza, Mwalimu Nyerere nchi ilimshinda kuongoza?

Sio kweli, Umbwe, Minaki, Iliboru, na nyingine nyingi zilikuwepo tangu awamu ya kwanza. Forodhani na nyingine za Dar pia zilikuwepo. usisahau juu ya umuhimu wa JKT iliyokuwepo kila mkoa na ya lazima kwa kila mtu kwenda.

Ilijenga taifa la wakakamavu wenye utayari wa kuishi kwa heshima tofauti na miaka ya sasa hakuna heshima yoyote ya kijamii.
Minaki ya wamisionari babu, nyerere hakujenga sekondari yoyote,hakukuwa na jkt kila mkoa,get your facts right bro,pawe na kambi ya jkt kila mkoa?..forodhani ni shule iliuotaifishwa
 
Mwinyi akiwa Rais alimwambia Mwalimu wewe Mwalimu ni mlima mimi Mwinyi ni Kichuguu tu
Kichuguu hakiwezi kushindana na Mlima 🙏🙏
Mwinyi alijuwa hadhi kubwa ya uongozi aliokuwa nao Mwalimu Nyerere. Na siyo yeye pekee aliye tambua hivyo.

Hawa wanao kuja hapa na kuibua vi-mada vya hovyo hovyo ni wajukuu wa wale walionyang'anywa maslahi yao kwa manufaa ya waTanzania; au kwa sababu zao za kiimani kama wazee wa Kariakoo.
 
Minaki ya wamisionari babu, nyerere hakujenga sekondari yoyote,hakukuwa na jkt kila mkoa,get your facts right bro,pawe na kambi ya jkt kila mkoa?..forodhani ni shule iliuotaifishwa
Zipo nyingi tu mkuu huko mikoani, kutaifisha maana yake zinatumiwa na watoto wa kizalendo. Ni mali ya walipa kodi baada ya kuwa zimetaifishwa,

Wewe labda mgeni, JKT Makutupora, JKT Mafinga JKT Buhimba, kule Kigoma, pia kulikuwa na JKT. Kila mkoa ulikuwa na JKT angalau moja.

Punguzeni chuki, kumchukia Marehemu ni kujitafutia laana zisizo na msingi.
 
Mwinyi alijuwa hadhi kubwa ya uongozi aliokuwa nao Mwalimu Nyerere. Na siyo yeye pekee aliye tambua hivyo.

Hawa wanao kuja hapa na kuibua vi-mada vya hovyo hovyo ni wajukuu wa wale walionyang'anywa maslahi yao kwa manufaa ya waTanzania; au kwa sababu zao za kiimani kama wazee wa Kariakoo.
Unaijua hadithi ya mwinyi ya kuoga bafuni na mwendawazimu kupitia nguo zako?..ulisikia alichokisema kwenye hotuba yake inayofichwa ya mikuki mitatu?..hapo alikua 'anamkoga' tu
 
Walitaifisha kutokana na presha ya waliokuwa chini yao katika suala la kiuongozi.

Baada ya uhuru waingereza walimwambia Nyerere waijenge Kariakoo na sehemu kubwa ya jiji la Dar ili liwe ni jiji lenye kutazamika kimataifa, wazee wa kiswahili waliokuwa na nyumba zao Kariakoo walimbishia Nyerere pamoja na hao wazungu.

Waliwataka waingereza waondoke haraka bila hata ya kutimiza hiyo azma waliyomwambia Mwalimu Nyerere. Miaka mingi baadae watoto wa hao wazee wamekuja kuuza nyumba zile zile ambazo baba zao walishauriwa zijengwe upya kwa ajili ya kuwa na jiji la Dar lenye muonekano mzuri.

Hatuwezi kujua ni akili zipi haswa alizokuwa nazo Nyerere miaka hiyo ya awamu ya kwanza. Tukumbuke kielimu tulikuwa bado tupo nyuma sana. Mwalimu alikuwa na wigo mdogo wa washauri miaka ile ya uhuru.
watu wengi wanamuona Nyerere kama nabii ,kwamba alipaswa kuanzisha na kumaliza yeye kila kitu .
wanasahau kuwa Nyerere ni mwanadamu japo na kwa zama zake alifanya makubwa sana

Kipindi tunapata uhuru, vitu vya msingi vilikuwa ni
1.Disunity
2.Ujinga
3.Ukabila
4.Decentralized Settlements
5.Udini
yote haya yakifanikiwa ndo huduma za kijamii zingefanikia kutolewa kwa watu wengi ndani ya muda mfupi

Nyerere alipokea nchi ikiwa bado ipo jehanam , asingeweza maliza kil kitu yeye binafsi

Alianzisha nia ila waliofuata wakabadili njia na ndo matokeo ya haya tunayaona sasa
1.Ufisadi
2.Utekaji
3.Mikopo ya hovyo
4.Mikataba ya hovyo
 
Zipo nyingi tu mkuu huko mikoani, kutaifisha maana yake zinatumiwa na watoto wa kizalendo. Ni mali ya walipa kodi baada ya kuwa zimetaifishwa,

Wewe labda mgeni, JKT Makutupora, JKT Mafinga JKT Buhimba, kule Kigoma, pia kulikuwa na JKT. Kila mkoa ulikuwa na JKT angalau moja.

Punguzeni chuki, kumchukia Marehemu ni kujitafutia laana zisizo na msingi.
Jkt ruvuma,rukwa,kagera,singida,kaskazini unguja,kusini,chakechake, kutaifisha siyo kujenga, acheni ujinga, hakuna anayemchukia bali ukweli uwekwe wazi
 
watu wengi wanamuona Nyerere kama nabii ,kwamba alipaswa kuanzisha na kumaliza yeye kila kitu .
wanasahau kuwa Nyerere ni mwanadamu japo na kwa zama zake alifanya makubwa sana

Kipindi tunapata uhuru, vitu vya msingi vilikuwa ni
1.Disunity
2.Ujinga
3.Ukabila
4.Decentralized Settlements
5.Udini
yote haya yakifanikiwa ndo huduma za kijamii zingefanikia kutolewa kwa watu wengi ndani ya muda mfupi

Nyerere alipokea nchi ikiwa bado ipo jehanam , asingeweza maliza kil kitu yeye binafsi

Alianzisha nia ila waliofuata wakabadili njia na ndo matokeo ya haya tunayaona sasa
1.Ufisadi
2.Utekaji
3.Mikopo ya hovyo
4.Mikataba ya hovyo
Acha uwongo wewe,disunity gani ilikuwepo nchini?..kariakoo kulikua na wanyamwezi kibao na makabila mengine wakiishi pamoja,tanga, morogoro makabila tofauti yslikuwepo,wahehe na watu wa tanga na tabora walikua na mafungamano tangu 1800 huko,wangoni na wahehe pia, nyerere kaacha ualimu kapewa nyumba magomeni aishi na alihudumiwa familia yake,hakubaguliwa mtu kuwa dini yake wala kabila,yeye ndiye aliyekua na agenda za dini
 
Huoni jinsi usivyo kuwa na akili?
Kutakuwaje na "ajenda ya siri..." kwa kiongozi ambaye hayupo tena, lakini wajinga wa aina yako bado mnahangaika na 'legacy' ya uongozi wake?
Nani ana ajenda hapa kama siyo nyinyi? Ajenda yenu ni nini?
Namna unavyo andika tu inaonyesha wazi wewe huna uelewa wala ufahamu wa kujadili jambo kama hili kwa kutumia akili zako mwenyewe.
Umehitimu wapi/chuo gani; kile cha Kariakoo kwa mzee Mohammed na wazee wake?
Mimi na wewe nani ambae hana akili? Nimetaja mambo ambayo yalikuwepo katika uongozi wake lakini wewe reply yako imejaa dhihaka na vijembe mwanzo mwisho, nilitegemea wewe mwenye akili upinge nilichoandika kwa mifano anuai. Katika uongozi wa teacher nchi haikutumbukia kwenye umasiki?, watu hawakukimbia nchini kwenda kuishi uamishoni?
 
Mimi hoja yangu hakujenga shule ya sekondari,kutaifisha alitaifisha hadi nyumba za kuishi za wahindi kariakoo na temeke,ni unyang'anyi wa kawaida tu
Ajenga zenu za chuki za kidini hazina mantiki yoyote. Alikuwa na wakati mgumu kuendesha nchi tofauti na hawa kina Mwinyi na wengine waliofuatia.

Wahitimu hawakuzidi kumi na tano nchi nzima, kwa maana ya shahada za chuo kikuu, taratibu akaanza kupata wasaidizi wenye elimu zenye kuweza kujenga nchi.
 
Nikisema uwezo wako wa kufikiri ni mdogo usidhani nabahatisha. Nimeweka hiyo mifano ya Kenya na Ethiopia kwa maksudi kabisa kuonyesha kuwa tatizo la njaa halikuwa kwa Tanzania pekee, na halikusababishwa na uongozi mbaya kama mnavyo taka kuaminisha watu. Lakini wewe hilo nalo huna uwezo wa kulitilia maanani.
Tatizo la njaa lilisababishwa na nini? Kama lilitokea kwa majirani zetu jr ni halali kutokea kwetu?. Uko Kenya sehemu kubwa ya ardhi yao haikubalinkilimo kama hapa kwetu, kwa wao kukumbana na tatizo la huaba wa chakula ni kawaida.

Reply zako unashambulia mtu binafsi badala ya kushambulia hoja.
 
Ajenga zenu za chuki za kidini hazina mantiki yoyote. Alikuwa na wakati mgumu kuendesha nchi tofauti na hawa kina Mwinyi na wengine waliofuatia.

Wahitimu hawakuzidi kumi na tano nchi nzima, kwa maana ya shahada za chuo kikuu, taratibu akaanza kupata wasaidizi wenye elimu zenye kuweza kujenga nchi.
Unajua nchi aliyoipokea mwinyi mpaka useme nyerere alichukua nchi ikiwa kwenye hali ngumu?..wazee walisema bora ya mkoloni,maana ilikua hovyo, ambulance kufuata wagonjwa ilishindikana wakati mkoloni alifanya
 
Unajua nchi aliyoipokea mwinyi mpaka useme nyerere alichukua nchi ikiwa kwenye hali ngumu?..wazee walisema bora ya mkoloni,maana ilikua hovyo, ambulance kufuata wagonjwa ilishindikana wakati mkoloni alifanya
Kukosoa ni kazi nyepesi sana. Nyerere alirithi nchi mbovu zaidi. Barabara ya kwanza ya lami ilijengwa mwaka 1956 na marehemu Kikenya, tumetoka mbali.

Haina tija yoyote kumsimanga marehemu asiyeweza kujitetea, alifanya kazi ngumu katika kuujenga msingi wa kitaifa.
 
Kukosoa ni kazi nyepesi sana. Nyerere alirithi nchi mbovu zaidi. Barabara ya kwanza ya lami ilijengwa mwaka 1956 na marehemu Kikenya, tumetoka mbali.

Haina tija yoyote kumsimanga marehemu asiyeweza kujitetea, alifanya kazi ngumu katika kuujenga msingi wa kitaifa.
Mkuu Mwalimu Nyerere anasimangwa na vijana wasiojua historia ya nchi hii na hata wae wasio na uwezo wa kuona mbali.
Mwalimu hstoria yake inajitetea yenyewe.
Mwalimu hakuwa mlafi
Mwalimu alikuwa na huruma
Mwalimu kwa fani yake ya ualimu alikuwa ana fundisha na kushawishi zaidi kuliko kitu kingine
Mwalimu hakuwa mbaguzi licha ya kutoka kabila dogo sana
Mwalimu hakujipendelea kimaslhi kujenga nyumba kwao wala barabra ya kwenda kwao.

Wengi humu hawajui kuwa Mwalimu hakuwa na barabara ya kwenda kujijini kwao kwa vile miaka yote ya Urais wake alikataa kujipendelea. Hata nyumba yake nzuri ya kwanza aijengewa na Jeshi kwa kulazimishwa.

Watu wengi walishindwa kwenda na filosofia ya Mwalimu kwa vile mioyo yao ilijaa mtamanio yao ya kujitajirisha kifisadi.
 
Back
Top Bottom