Nauliza, Mwalimu Nyerere nchi ilimshinda kuongoza?

Nauliza, Mwalimu Nyerere nchi ilimshinda kuongoza?

Kuna mtu anahoji ni maono gani aliyokuwa nayo Mwalimu Nyerere.

Hiki kiswahili tunachotumia katika mijadala humu JF ni sehemu ya maono ya Mwalimu Nyerere, alihakikisha kila tarafa ya Tanzania kiswahili kinakuwa ni lugha ya mawasiliano. Hayo ni maono kwani yamechangia katika hii amani na umoja tulivyonavyo leo hii.

Malema mwanasiasa wa Afrika ya Kusini anapigia debe Afrika nzima kiswahili kiwe ni lugha ya mawasiliano ili tuweze kuwa na umoja wa bara zima ambao utatupatia urahisi wa sisi kwa sisi kuweza kuwasiliana na kuwa na bara moja lenye nguvu za kiuchumi.

Hayo ni maono ya Mwalimu Nyerere ya enzi hizo za awamu ya kwanza.
 
Wewe umeandika stori za kusoma vitabuni ambazo ziliandikwa kwa ajili ya kuwapamba Viongozi,Tofautisha viwanda alivyofitaifisha Nyerere na viwanda alivyovijenga. Ninachojua mimi baada ya Azimio la Arusha selikali ilitaifisha vitu vingi Sana, kumbuka hivi viwanda,makampuni zilikuwa na management zake,baada ya kutaifisha ilibidi waweke manegement za selikali ambazo watu wake hawana uzoefu taratibu zikaanza kupungua ufanisi mpaka kufa kabisa mfano kiwanda cha kusindika Nyama Tanganyika Pekers,kilikuwa kinaajiri zaidi ya wafanyaka 2000 kabla ya kupata uhuru na kilikuwa kinauza nyama iliyosindikwa inje ya inchi na kuiingizia Tanganyika pesa za kigeni,leo hii ni uwanjwa wa maombi,hapo wa kulaumiwa siyo Nyerere

Chukulia mfano mdogo South Afrika ya makaburu ilikuwa bora zaidi kuliko ya sasa,Nelson mandera hakuwa mjinga hakuna alichotaifisha kutoka kwa wazungu,lakini Mugambe alijikuta inaharibu uchumi wa Zimbabwe baada ya kutaifisha mashamba ya walowezi, kiuharisi aliyoyafanya Nyerere hayana tofauti na aliyoyafanya Mugabe
Walitaifisha kutokana na presha ya waliokuwa chini yao katika suala la kiuongozi.

Baada ya uhuru waingereza walimwambia Nyerere waijenge Kariakoo na sehemu kubwa ya jiji la Dar ili liwe ni jiji lenye kutazamika kimataifa, wazee wa kiswahili waliokuwa na nyumba zao Kariakoo walimbishia Nyerere pamoja na hao wazungu.

Waliwataka waingereza waondoke haraka bila hata ya kutimiza hiyo azma waliyomwambia Mwalimu Nyerere. Miaka mingi baadae watoto wa hao wazee wamekuja kuuza nyumba zile zile ambazo baba zao walishauriwa zijengwe upya kwa ajili ya kuwa na jiji la Dar lenye muonekano mzuri.

Hatuwezi kujua ni akili zipi haswa alizokuwa nazo Nyerere miaka hiyo ya awamu ya kwanza. Tukumbuke kielimu tulikuwa bado tupo nyuma sana. Mwalimu alikuwa na wigo mdogo wa washauri miaka ile ya uhuru.
 
Sunguratex, Mwatex, Mutex, UFI, Tamco, Tanganyika Packers na vingine vingi. Awamu zilizofuata ziliviua viwanda vyote japo ni kwa sababu ya presha ya IMF.
Kiwanda cha Tanganyika packers kilijengwa na mkoloni sawa na Willimson Diamond,Shirika la Usagishaji na Mazao N.M.C,Mamraka ya bandari, Tanzani Railways kuanzia Meli,Gari Mosh, Mabasi,Mpaka Malori,Posta na Simu,
Kiujumla tulirithi vitu vingi sana kutoka kwa mkoloni lakini tulishindwa kuviendesha,Sawa na kusema Africa pamoja na Tanzania,zingekubali uhuru wa bendera lakini wasingemfukuza mkoloni wangewachia wabaki kumiliki njia kuu za uchumi wakabaki wakusanyaji kodi tungekuwa mbali sana

,Nimetembelea inchi mbalimbali za Africa,utaona kwa macho yako uwekezaje waliofanya wakoloni ni tofauti walioendereza wale waliokuja kujiita wazalendo
Nitakupa mfano wa inchi moja inaitwa Mozambique, Mreno aliijenga vizuri sana kuanzia Miji,Mabarabara na kila kitu,Vita vya kupigania Uhuru vilipoisha chama cha Frelimo na selikali iliyoingia madarakani imeshindwa hata kujenga mita moja ya barabara na miji,kuendeleza pale alipoishia mkoloni,
Nenda Botswana,Namibia,South Africa, Angola,Zimbabwe, utaiona akili kubwa ya Mzungu iliyotumiaka jinsi miji yao ilivyo mizuri
 
K
Walitaifisha kutokana na presha ya waliokuwa chini yao katika suala la kiuongozi.

Baada ya uhuru waingereza walimwambia Nyerere waijenge Kariakoo na sehemu kubwa ya jiji la Dar ili liwe ni jiji lenye kutazamika kimataifa, wazee wa kiswahili waliokuwa na nyumba zao Kariakoo walimbishia Nyerere pamoja na hao wazungu.

Waliwataka waingereza waondoke haraka bila hata ya kutimiza hiyo azma waliyomwambia Mwalimu Nyerere. Miaka mingi baadae watoto wa hao wazee wamekuja kuuza nyumba zile zile ambazo baba zao walishauriwa zijengwe upya kwa ajili ya kuwa na jiji la Dar lenye muonekano mzuri.

Hatuwezi kujua ni akili zipi haswa alizokuwa nazo Nyerere miaka hiyo ya awamu ya kwanza. Tukumbuke kielimu tulikuwa bado tupo nyuma sana. Mwalimu alikuwa na wigo mdogo wa washauri miaka ile ya uhuru.
Kina Kambona walimshauri vizuri,lakini wanasema alikuwa hashauliki
 
Nimezaliwa miaka 1970, nimekutana na maisha magumu Sana, kulikuwa hakuna Sabuni, Sukari, Mafuta na hata nguo.

Watu walivaa magunia, kulikuwa hakuna vyakula na wakati tunapata uhuru aliikuta Tanganyika iko vyema kutoka kwa mkoloni nchi ikiwa vizuri.

Je, Uongozi ulimshinda?
Na mama pia nchi imemshinda hiii
 
K

Kina Kambona walimshauri vizuri,lakini wanasema alikuwa hashauliki
Alishaurika na alipenda sana mijadala. Ndiye aliyeanzisha msemo wa 'hoja haipigwi virungu'

Pia alitumia maneno haya ' nguvu ya hoja badala ya hoja ya nguvu'.

Suala la kina Kambona ni binafsi kwa maana ya ugomvi wa Mwalimu na Kambona, mafahari wawili.
 
Alifanya mengi sana mazuri na aliacha mengi sana mazuri ila walipokuja wasomi wazuri wakabomoa kila kitu na kuuza kwa bei chee kila kitu kilichokuwepo!
Kuanzia Viwanda mpaka mashirika ya Umma !
Kama huvijui Viwanda na Mashirika ya Umma yaliyokuwepo basi wewe utakuwa ni kijana uliyedanganywa na Wanyonyaji wa Mali za Umma !
Nchi ilitopea kwenye umasikini wa kutisha, alinusulika kupinduliwa mara mbili, yeye ndie muasisi wa kuzigeuza TISS na JWTZ kuwa matawi ya CCM, watu waliishi uhamishoni kwa kutofautiana nae mitazamo.

Hatuwepo wakati huo lakini rekodi zipo
 
Nchi ilitopea kwenye umasikini wa kutisha, alinusulika kupinduliwa mara mbili, yeye ndie muasisi wa kuzigeuza TISS na JWTZ kuwa matawi ya CCM, watu waliishi uhamishoni kwa kutofautiana nae mitazamo.

Hatuwepo wakati huo lakini rekodi zipo
CCM ilikuwa na chuo pale kivukoni tangu ilipoanzishwa mwaka 1977, ni sera ya chama sio Nyerere kama Nyerere.
 
Iko hivi nazani hata kesho ukiamka huwezi kumkoza mzee wa miaka 70,80 na kuendelea,au tafuta sehemu ya tukio husika lililowahi kutokea halafu waulize wahusika wa pale hasa wazee,utaupata ukweli no utafaidika kuliko kusoma vitabu vilivyoandikwa kwa kupotosha ukweli

And I tell exactly the same...that has never been a reliable way of passing on education or any important information from generations to generations. It is very backward. Africa has lost tremendous amount of knowledge because of using that same way to propel forward education.
Unachosema sio cha maana na haina maana mkisimuliana kwenye kahawa mnaambiana ukweli. Most of the time mnadanganyana sana.
Ndio maana wenzetu wote walioweka knowledge kwenye maandishi wanatupita mbali sana. Tusiendelee kudharau elimu na hasa kuandika. Hata wewe anza kuandika hata kwenye diary ili wajukuuu zako waje kusoma one of the days. Sio wasubiri kulishwa matango pori kwa porojo zisizoeleweka
 
Kuna mtu anahoji ni maono gani aliyokuwa nayo Mwalimu Nyerere.

Hiki kiswahili tunachotumia katika mijadala humu JF ni sehemu ya maono ya Mwalimu Nyerere, alihakikisha kila tarafa ya Tanzania kiswahili kinakuwa ni lugha ya mawasiliano. Hayo ni maono kwani yamechangia katika hii amani na umoja tulivyonavyo leo hii.

Malema mwanasiasa wa Afrika ya Kusini anapigia debe Afrika nzima kiswahili kiwe ni lugha ya mawasiliano ili tuweze kuwa na umoja wa bara zima ambao utatupatia urahisi wa sisi kwa sisi kuweza kuwasiliana na kuwa na bara moja lenye nguvu za kiuchumi.

Hayo ni maono ya Mwalimu Nyerere ya enzi hizo za awamu ya kwanza.
Lugha inakuwa na maana kama unauchumi mkubwa,sasa wewe unajua kiswahili unaenda kuomba kazi kwa mtu anayejua kiingereza au kichina,kiswahili kitakusaidia nini?
Angalia wakenya walivyotupiga gape kimataifa kila sehemu wapo,sababu ya lugha ya kiingereza siyo kiswahili
 
You are Right 🙌
Wajanja na wasomi wazuri waliofuata baada ya Mwalimu walifaulu sana juzi-outsmart hujuma za Wazungu kwa kuwaita hao hao Wazungu waje wachimbe Dhahabu kwa kutugawia asilimia 3 ya mapato ya dhahabu itakayouzwa. 🙄

Tukaviuza Viwanda vyote vilivyokuwepo kwa Ushauri na masharti ya IMF kwamba Serikali isifanye Biashara !
Kukaviuza Viwanda vyote kwa Bei ya Bure kabisa. 🙄

Kisha wakaja wajanja na wasomi Zaidi wakawa-outsmart tena Wakubwa kwa kuingia mikataba ya Uchimbaji wa Gesi ambayo Kiongozi mmoja akaja kutuambia kwamba pale tulishapigwa hatuna chetu 😳🙄🤦🏽‍♂️

Kweli tumefanikiwa sana Kuwa-outsmart Wakubwa wa Dunia 🙌🤦🏽‍♂️
Kubolonga kwa wasomi waliofuata hakuondoi mabaya ya Nyerere, teacher na hao waliomfuata wote wamepuyanga ndio maana tupo hapa.
 
Nchi ilitopea kwenye umasikini wa kutisha, alinusulika kupinduliwa mara mbili, yeye ndie muasisi wa kuzigeuza TISS na JWTZ kuwa matawi ya CCM, watu waliishi uhamishoni kwa kutofautiana nae mitazamo.

Hatuwepo wakati huo lakini rekodi zipo
Kumbe kama ulikuwa umeshazaliwa kipindi kile basi itakuwa ulikuwa bado mdogo ! 🙏🙏
 
Uko sahihi kabisa. Binafsi nawaheshimu mno wazee kwa sababu hiyo. Kuna mzee fulani mitaa ya Ilala alikuwepo siku ya sherehe za uhuru huwa ananisimulia mno mikasa iliyotokea. Tatizo wazee wengi huwa kuna mambo wanaishia kuguna na kuelezea juu juu.
Wazee wanaogopa kusema mengi wanayoyajua na waliyoyapitia kwa sababu wameshawaona wenzao wakidhalilishwa na wenye kushika Hatamu za Uongozi Eti kwa sababu tu ya kuusema Ukweli !!

Acha waendelee kuukumbatia Uongo na kuwahujumu wanaosema Ukweli !
Lakini wajue Ukweli una tabia ya kujitokeza hadharani hata kama utafichwa kwa muda mrefu !
Iko siku utajitokeza bila kupingwa 🙏🙏
 
Wazee wanaogopa kusema mengi wanayoyajua na waliyoyapitia kwa sababu wameshawaona wenzao wakidhalilishwa na wenye kushika Hatamu za Uongozi Eti kwa sababu tu ya kuusema Ukweli !!

Acha waendelee kuukumbatia Uongo na kuwahujumu wanaosema Ukweli !
Lakini wajue Ukweli una tabia ya kujitokeza hadharani hata kama utafichwa kwa muda mrefu !
Iko siku utajitokeza bila kupingwa 🙏🙏
Umeongea ukweli
 
Alifanya mengi sana mazuri na aliacha mengi sana mazuri ila walipokuja wasomi wazuri wakabomoa kila kitu na kuuza kwa bei chee kila kitu kilichokuwepo!
Kuanzia Viwanda mpaka mashirika ya Umma !
Kama huvijui Viwanda na Mashirika ya Umma yaliyokuwepo basi wewe utakuwa ni kijana uliyedanganywa na Wanyonyaji wa Mali za Umma !
Hivyo viwanda mbona vilishindwa kuzalisha bidhaa za mahitaji muhimu ya kila siku,hadi watu kutumia sukari guru,kuvaa magunia,sabuni tu za kufulia/ogea hazikuwepo?.. viwanda vilianza kumfia mwenyewe!?
 
Back
Top Bottom