Naungana na jamii ya kimataifa kutompa ushirikiano mheshimiwa Uhuru Kenyatta

Naungana na jamii ya kimataifa kutompa ushirikiano mheshimiwa Uhuru Kenyatta

Mimi sijaelewa ulichotaka kuwakilisha,ingawaje ninaona kama umewakilisha kitu cha muhimu sana....Ningefurahi kama ungeweza kutoa tafsiri ya terms ulizotumia ambazo wewe unazijua kabisa kwamba wengine wengi humu hatujui nini maana yake...hegemony,nihilist na neno zingine zote hizo.Asante sana kwa kunielewa

Kifupi.

Raila na Uhuru ni walewale tu. Wote watoto wa wabenzi.

Ashinde Raila au Uhuru tofauti nini?

Cha kufanya hapa ni kukubali matokeo na kurekebisha makosa kwenda mbele.

La sivyo watu watauana tena kwa kuwapigania mabwanyenye wawili na jamaa zao.

Watu wanazungumzia sana ukabila Kenya lakini hawazungumzii tofauti ya matajiri na maskini.
 
Wakenya wamefanya maamzi mazuri kwa utashi wao,marekani,wingereza na wengineo hawawezi kuwachagulia mtu wa kuwaongoza hata siku moja,ukiangalia siasa za fitina za odinga na wenzake ambao alikuwa amewapandikiza kumchafua kenyatta aonekane mkosaji,mbaya zaidi odinga alikuwa amejiamini kupita kiasi akijua wenzake wanamsindikiza kwenda ikulu,pole yake!
 
Japokua mimi ni si Mkenya ila niungane na Wakenya kwa kuamua kutumia haki yao ya msingi kumchagua mtu waliyempenda bila kufuata influence za Magharibi...kwa uelewa wangu mdogo wa siasa za Kenya hususan yale machafuko ya baada ya uchaguzi wa 2007 uliomwingiza Kibaki madarakani,Raila na Kibaki ndio walikua key players kwa hisani ya bwana Samwel Kivuitu aliyechezesha ngoma ambayo alishindwa kuhimili mirindimo yake,Mungu ampe hukumu ya haki kwa kua amekwisha kutangulia mbele ya hadi since February..

Yumkini Raila ndiye aliyeshinda uchaguzi ule wa mwaka 2007 si jambo la msingi nalosemea hapa ila reaction yake baada ya tume kumtangaza Mr Kibaki kua mshindi kwenye uchaguzi ule ilichochea ama kuhamasisha kwa namna moja ama nyingine wafuasi wake (Raila) of whom wengi walikua Waluo (im stand to be corrected) kuinuka juu ya wenzao Wakikuyu kwa kuwapiga na kuwaua ikifatana na uharibifu wa mali na makazi!

Wakati yote haya yakitokea si Raila,wala kibaki waliokemea 'kwa kumaanisha' ilihali mamia ya Wakikuyu/Wakalenjin wakiendelea kuteketea.Hapa ndipo ushiriki wa Kibaki unapokuja..

Kosa alilolifanya Uhuru ambalo limesababisha awe victim hadi leo ni nguvu kubwa aliyotumia kulipiza/kuzuia ndugu zake 'Wakikuyu' wasiendelee kuketeketezwa. Yatosha kusema tu kua kwa Jamii ya Wakenya esp. Wakikuyu/Waluo ambao hawakua upande wowote wanamwona Uhuru km Hero kwao ilihali jamii ya kimataifa ikimwona mhalifu wa kivita.

Watu wa kupeleka ICC ni pamoja Samwel Kivuitu (japo ameshafariki) Raila, na Mwai Kibaki! Wamarekani diplomatically wako sawa na Mataifa mengine na si haki kuwaamulia wenye taifa lao kwamba ni nani anafaa kuwa kiongozi. Tumeona sehemu nyingi duniani ambazo Mmarekani hana interest nazo akiachia zijiendeshe tu shaghalabaghala wakati huo huo akiwa mstari wa mbele kuamua masuala nyeti ya nchi zenye kumnufaisha kwa namna moja ama nyingine...

Viva Kenyatta,Kenya ipo mikononi mwako,kaa chini na jopo la wataalamu wa nchi yako wakushauri namna ya kujenga taifa lako na kuondoa hii mifarakano na mipasuko ya Kikabila!
 
Japokua mimi ni si Mkenya ila niungane na Wakenya kwa kuamua kutumia haki yao ya msingi kumchagua mtu waliyempenda bila kufuata influence za Magharibi...kwa uelewa wangu mdogo wa siasa za Kenya hususan yale machafuko ya baada ya uchaguzi wa 2007 uliomwingiza Kibaki madarakani,Raila na Kibaki ndio walikua key players kwa hisani ya bwana Samwel Kivuitu aliyechezesha ngoma ambayo alishindwa kuhimili mirindimo yake,Mungu ampe hukumu ya haki kwa kua amekwisha kutangulia mbele ya hadi since February..

Yumkini Raila ndiye aliyeshinda uchaguzi ule wa mwaka 2007 si jambo la msingi nalosemea hapa ila reaction yake baada ya tume kumtangaza Mr Kibaki kua mshindi kwenye uchaguzi ule ilichochea ama kuhamasisha kwa namna moja ama nyingine wafuasi wake (Raila) of whom wengi walikua Waluo (im stand to be corrected) kuinuka juu ya wenzao Wakikuyu kwa kuwapiga na kuwaua ikifatana na uharibifu wa mali na makazi!

Wakati yote haya yakitokea si Raila,wala kibaki waliokemea 'kwa kumaanisha' ilihali mamia ya Wakikuyu/Wakalenjin wakiendelea kuteketea.Hapa ndipo ushiriki wa Kibaki unapokuja..

Kosa alilolifanya Uhuru ambalo limesababisha awe victim hadi leo ni nguvu kubwa aliyotumia kulipiza/kuzuia ndugu zake 'Wakikuyu' wasiendelee kuketeketezwa. Yatosha kusema tu kua kwa Jamii ya Wakenya esp. Wakikuyu/Waluo ambao hawakua upande wowote wanamwona Uhuru km Hero kwao ilihali jamii ya kimataifa ikimwona mhalifu wa kivita.

Watu wa kupeleka ICC ni pamoja Samwel Kivuitu (japo ameshafariki) Raila, na Mwai Kibaki! Wamarekani diplomatically wako sawa na Mataifa mengine na si haki kuwaamulia wenye taifa lao kwamba ni nani anafaa kuwa kiongozi. Tumeona sehemu nyingi duniani ambazo Mmarekani hana interest nazo akiachia zijiendeshe tu shaghalabaghala wakati huo huo akiwa mstari wa mbele kuamua masuala nyeti ya nchi zenye kumnufaisha kwa namna moja ama nyingine...

Viva Kenyatta,Kenya ipo mikononi mwako,kaa chini na jopo la wataalamu wa nchi yako wakushauri namna ya kujenga taifa lako na kuondoa hii mifarakano na mipasuko ya Kikabila!

umesema hapa
 
Ppl bwana duu km nn vile!
Uchaguzi kina kushinda na kushindwa! Masuala yakutokubali matokeo kwa jumuia ya mataifa ni kutafuta kumwaga DaMu Kenya!
 
Inaonekana kuwa hauna msimamo,kisa wamarekani wamempinga Kenyatta na we masikini eti unampinga. Kumbuka kuwa nchi za magharibi zinaona hazitopata manufaa kwenye utawala wa Kenyatta, kila siku tunasema nchi kujitegemea kiuchum bila misaada kutoka nchi za magharb inawezekana zen we unaleta hoja za kipindi cha nyerere kutegemea misaada. Jipange
 
Heshima mbele,

Nimeshangazwa sana na maamuzi Wakenya waliyochukua, Naomba kuungana na jamii za kimataifa hususani Marekani ambayo tayari imetanabaisha kutoiunga mkono serikali ambayo Kenyatta atachukua nafasi kuiongoza.

Nawaza huyu bwana atainua vp uchumi,atafanya biashara na nani angali wamagharibi wameshaanza kumwekea ngumu.Sina uhakika asilimia mia moja kama haya maamuzi kweli yametoka mioyoni mwa Wakenya.

Hata kama siasa ya Kenya ni ya ukabila lakini ukabila gani unaoamini udhaifu wa mtu katika kupewa nafasi nzito kama hiyo?

Je ikitokea tuhuma zinazowakabili zikawafunga je nchi itaongozwa na nani?

Wakenya mtashangilia leo ila kazi mnayo,time will tell.

kenya is about to bulid self sustained economy kama ya russia...hata tukijipanga vizuri afrika mashariki tunaweza kumaliza mahitaji yetu ndani kwa ndani
 
Wewe ni nani kuwamlia wa kenya? Tuwaache wakenya waendeshe nchi yao watakavyo!

Wewe kumbe huwajui hao waingereza na Marekani wana kwenda na mazingira!

Kwanza sijui kwanini Raila 0dinga akupelekwa ICC maana yeye ndio chanzo cha vurugu.
 
Heshima mbele,

Nimeshangazwa sana na maamuzi Wakenya waliyochukua, Naomba kuungana na jamii za kimataifa hususani Marekani ambayo tayari imetanabaisha kutoiunga mkono serikali ambayo Kenyatta atachukua nafasi kuiongoza.

Nawaza huyu bwana atainua vp uchumi,atafanya biashara na nani angali wamagharibi wameshaanza kumwekea ngumu.Sina uhakika asilimia mia moja kama haya maamuzi kweli yametoka mioyoni mwa Wakenya.

Hata kama siasa ya Kenya ni ya ukabila lakini ukabila gani unaoamini udhaifu wa mtu katika kupewa nafasi nzito kama hiyo?

Je ikitokea tuhuma zinazowakabili zikawafunga je nchi itaongozwa na nani?

Wakenya mtashangilia leo ila kazi mnayo,time will tell.

acha kuwatisha watu wazima,
 
Wild Fauna, fungua akili yako angalia mbali. Aliyepashwa kupelekwa ICC zaidi ni Raila akifuatiwa na Kibaki, hawa ndio kugombea kwao madaraka kulipeleka taifa kwenye machafuko. Uhuru alijitokeza kuzuia watu wa kabila lake wasimalizwe baada ya serikali kushindwa kuwapa protection. Jumuia ya kimaifa na hasa wazungu wanavyoliangalia hili suala la ICC ni tofauti ya Wakenya wanavyoliangalia, la sivyo Uhuru asingepigiwa kura zaidi ya millioni 6 na Wakenya.

I might be wrong, but this is my personal stand!!!

Tiba

Tiba, huo ndiyo ukweli wa hali halisi kisiasa Kenya. Kuendeleza kuwaabudu wazungu ni ugonjwa mbaya sana. Fikiria hata wenzetu Wakenya wameshalijua hilo wakati wao ndio tulidhani wanapatana nao zaidi. Sasa sisi ndiyo tumebaki kwenye ulemavu huo. Kenya sasa hivi iko mwendo kasi kwenye highway ya maendeleo na demokrasia ya kweli. Tanzania tumebakia kuwasema sema tu wakati hatuna chochote tulicho nacho cha kujivunia kuwazidi. Elimu iko juu na watu wamewaona Uhuru na Rutto ndiyo viongozi vijana ambao watafaa kuongeza kasi ya maendeleo nchini mwao. Angalia kilichotokea kwenye majimbo mengi, wameachana na viongozi wengi waliozoeleka na kuwachagua vijana wenye uwezo.
Hao Westerners watakaa kimya tu sasa, hawana la kufanya ila kutafuta njia muafaka ya maelewano.
Magharibi wana wasiwasi kwa sababu Uhuru ndiye aliyemshauri Kibaki (akiwa bado ni Waziri wa Fedha) aachane na tenda ya kujenga barabara kubwa muhimu kwa Kshs. bilion 60 na wakaenda kuwapa hiyo tenda China ambao wamekubali kuzijenga kwa bilioni 26 tu! Hawa jamaa wawili ni viongozi wachapa kazi sana na Wakenya wana imani nao. Sisi tujitahidi tuondoe huo ushetani wetu wa kung'oana meno na kucha kwa koleo kwanza kabla ya kuwajadili wenzetu vibaya.
Wenzetu wameshafikia kuwachagua Jaji Mkuu na IGP kwa kutangaza kazi zao na kuwachagua kwa uwazi. Hapo hatujafika ni kipi tulichonacho bora zaidi? Nawapongeza sana Wakenya kwa uchaguzi mzuri waliousimamia kwa amani.
 
swali ambalo najiuliza
immunite ambayo wataipata kama raisi na makamu wake itawasaidia icc?na
je wakipatikana na hatia icc itakuwaje?
Kwenye press confrence ya odinga amejaribu kuainisha mapungufu ya tume
ya uchaguzi na watafanya pertition kama mahakama itakuwa huru more 2
come

itakuwa kama rais wa sudan. lkn bda ya hapo, atafungwatu. kumb bwana slobogan milosovic,
 
Wakenya wamehamua tuwaache na Kenya yao kwani wao ndio wanaojua ni kwa nini wamemchagua Mh Uhuru Kenyetta kuwa rais wao. Hii naifananisha na mtu anaemlalamikia jiran yake kuwa kaoa mwanamke asiye faa je yeye ndio anaeishi nae au huyo mwenye mke. Tuwe makini tunapowazungunzia wenzetu kwa mahamuzi yao. Wao ndio wanaojua mbichi na mbivu za machaguo yao
 
Usamehewe kwa kuwa hujui usemalo. Ukipata nafasi ya kuzungumza na Wakikuyu ambao walikuwa wanachinjwa kama kuku kwenye zile vurugu za baada ya uchaguzi wa 2007, watakwambia kuwa Uhuru ni Mungu wao wa pili kwani bila kuingilia kati, wangeendelea kuchinjwa zaidi. Kwa wakikuyu Uhuru ni kama Musa aliyetumwa na Mungu kuwakomboa kutoka kwenye upanga wa Wajaluo. Siasa za Kenya ni ngumu kidogo.

Tiba

Siyo wajaluo waliokuwa wanawachinja wakikuyu Bali wakalenjini ndio waliwachinja wakikuyu. Hata hivyo nafikiri tuheshimu mahamuzi ya Wakenya na matumaini yangu ni kuwa jumuiya ya kimataifa pia itafanya hivyo. Kosa walilofanya Marekani na Uingereza ni kuwa hasi na Jubilee, hii iliwafanya Wakenya kuhamua ili kuwaonyesha kuwa wao ni taifa huru na wasingependa kuchaguliwa viongozi. Kudos Wakenya.
 
UHURU KENYATTA na ODINGA wote kwa pamoja hawakutakiwa kabisa kushiriki ktk uchaguzi huu wa KENYA maana wote ni wahusika wakubwa wa Ukabila nchini Kenya. Na nitasema wazi ya kwamba uchaguzi umekwisha lakini subirini mtakuja yaona yanayofuata wala sii muda mrefu, sura halisi za hawa watu zitajitokeza..


kenyatta yupo hivyo Tangu anaanza siasa na ataendelea kuwa hivyo. hafanyi siasa za kinafiki na kiubabaishaji kama wanavyofanya akina mbowe na slaa. hajawahi hata siku moja kumkashifu na kumtukana kiongozi aliye juu yake au mpinzani wake. Ni tajiri nambari moja Afrika ya Mashariki hivyo hakugombea kwa njaa bali ni kutaka kuwakomboa wakenya kutoka katika siasa za matusi. yeye ndiye aliyefanikisha kutuliza machafuko ya mwaka 2007. amelelewa na marais wote wa kenya kuanzia mzee kenyata ambaye ndiye baba yake, akaja mzee daniel arap moi na wakati moi anang'atuka kwenye siasa alikiacha chama cha KANU chini ya kijana mdogo uhuru kenyata. aidha ameshirikiana vizuri na Mzee Mwai KIBAKI mpaka mwisho wa uongozi wake> huyu jamaa usipime. hakamatiki
 
Kwa upande wangu simkubali Kenyatta! Vile vile siwapendi marekani na Uingereza wao ndio waliotufanya waafrika tuwe maskini kiasi hiki!

Uhuru nitamkubali pale atakapoweka msimamo wake juu ya mataifa haya wanyonyaji! Ningekuwa Rais wa Tanzania ningekuwa adui namba moja wa Marekani na Uingereza kwani hata bila wao tunaweza kuendelea kuliko sasa tuko nao lakini Nchi zetu haziendelei!

Otherwise,Tuheshimu haki ya kidemokrasia ya wakenya!
 
Hiv baada ya kubainika kuna mahackers na Uhuru akiwa 43% vipi kura zilirudiwa kutoka 0% kuja mpaka hii 50% ama ilikuwaje
 
Back
Top Bottom