Israel inajilinda na umasikini kwa kuwekeza kwenye elimu ya ubunifu wa teknolojia, hawana madini ardhi yao sehemu kubwa ni jangwa lakini kupitia Teknolojia wana uchumi wa dola bilioni 500 (Trilioni elf 1 na 500) kusanya nchi zote za Afrika Mashariki hatufikii. Kampuni yenye teknolojia kubwa ya umwagiliaji duniani ipo Israel, Kampuni nyingi zimeweka ofisi za ubunifu Israel, n.k.
Hizi ni nchi zenye uchumi mkubwa zaidi Mashariki ya Kati, Chanzo ni Wikipedia kwa kutumia takwimu za IMF shirika la fedha la kimataifa
View attachment 3118214
Israel inarushiwa makombora hawakimbilii kanisani kusema ni mipango ya Mungu kungoja kiama, wameumiza vichwa kubuni mitambo maalum ya kutungua makombora mengi (sio yote) kabla hayajatua,
View attachment 3118216
Nawaelezeaje wanangu kwamba Africa inalindwa na Mungu wa Israel kwenye Umasikini, Ujinga na maradhi wakati Israel inategemea zaidi Teknolojia kupunguza makali ?
View attachment 3118217