Uchaguzi 2020 Nawamegea siri: 'Bakuli la Lissu' lijazwe michango, linasaidia kuruka kiunzi kikuu mwaka huu

Uchaguzi 2020 Nawamegea siri: 'Bakuli la Lissu' lijazwe michango, linasaidia kuruka kiunzi kikuu mwaka huu

Sitaki niwachoshe kwa meneno mengi. Nawaambieni tu kwa kifupi na kwa uhakika. Bakuli la michango analolitembeza mgombea wa CHADEMA Tundu Lissu si la kubezwa au kumezwa. Yaweza kuwa ni kwa kujua au kutokujua, Lissu anaruka kikwazo kikuu kilichosukwa kwenye uchaguzi wa mwaka huu: ukata kwa vyama vya upinzani. Ukata tata ungewakata na kuwavuta wapinzani nyuma na kuwafanya washindwe kufanya kampeni.

Mipango kabambe ilishasukwa kitambo kuvifanya vyama vya upinzani mwaka huu kuandamwa na ukata wa kifedha. CCM yetu yenyewe, kwakuwa ina rasilimali za kutosha na kutisha na kwakuwa imejibanza kwenye koti la Serikali, ilijiandaa kujidai itakavyo kwenye kampeni hizi huku wapinzani wakishindwa kufanya kampeni. Mipango ilisukwa vyema. Kampeni zina gharama nyingi: usafiri, malazi,mavazi, chakula, vifaa vya sauti, majukwaa na kadhalika.

Mipango ya kuufanya ukata umee kwenye vyama vya upinzani ilianza miaka kadhaa iliyopita. Karibu kila chama kikubwa cha upinzani hapa nchini vikiwemo CHADEMA, ACT na NCCR-Mageuzi kina chama au vyama rafiki nje ya Tanzania. Marafiki hao wa nje husaidia vyama hivyo kifedha hasa kwenye harakati kama hizi za kiuchaguzi. Na hakukuwa na ubaya kuhusu kusaidiana huko. Lakini, mwaka huu misaada hiyo imepigwa pini. Imezibwa. Hakuna misaada tena. Ukata!

Lissu ajaziwe bakuli lake. Achangiwe. Hata mimi, kama mfuasi ninayejinafasi wa demokrasia ya vyama vingi, nimeshamchangia Lissu. Lazima tuwe na mgombea strong wa upinzani ili kutufanya tuchague vyema. Lazima mwaka huu mchuano mkali uwe kati ya Dkt. Magufuli na Lissu. Lazima tusikie sera za kila mmoja wao na tuamue. Bakuli la Lissu, hata kama litakejeliwa na kudhihakiwa, lina maana kubwa: linaruka mipango ya kidhalimu ya kutengeneza ukata kwa wapinzani.

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kigoma, Tanzania)
Ww mzee ,huwa sikuelewi philosophy yako.Unasema Lissu achangiwe.Pesa itoke wapi?Lissu anasema maisha ni magumu.Akawachangishe mabeberu wake sisi hatuchaongezewa mishahara toka 2015.
 
Wach
Wewe kweli mpumbavu ruzuku zimepigwa pini uliza credible sources utaambiwa.
a uzwazwa wewe. CDM wakidhulumiwa chochote bungeni huwa wanaweka wazi. Alidhulumiwa lissu kila mtu alijua, Lema kakatwa mafao yake kila mtu anajua. Kwanini ishu ya kutopewa ruzuku iwe siri. Hii inawezakana ni uzushi wa waandamizi wa CDM waliokula ruzuku bila kuifikisha sehemu husika sasa wanatafuta sababu. Yaani CDM wadhulumiwe ruzuku wafanye siri. Hiyo unayoiita reliable sijui credible source ni imekukamata wewe tuu kwa sababu ni kilaza na ambaye hujui siasa za chadema zinavyoendeshwa. Hii wangeifanya ni ajenda kwenye kampeni zao.
 
Nalazimika tu kujibu ingawa umenijibu kishabiki kuliko kiuchambuzi.

Hata vile nijibu kwa ujumla kuwa uwe mkweli na jasiri kuwauliza viongozi wa CHADEMA matumizi ya fedha za chama (ruzuku, michango ya wabunge, ada za wanachama, misaada ya vyama rafiki vya nje, nk}.

Kuna tuhuma dhidi ya Mbowe zilizotolewa na viongozi waandamizi waliokihama chama, hazijajibiwa hadi muda huu. Labda una majibu tofauti na madai yako kuwa zimetumika kwa shughuli za chama. Au ndiyo hayo ya tuhuma? Km inadaiwa kuwa watumishi wengi wa chama hawalipwi mishahara/posho.

Uchaguzi Mkuu 2015, CHADEMA kilikuwa kimejiandaa kifedha kwa kampeni ikiwa ni pamoja na mabango, TShirt, chopa, nk. Iweje leo kishindwe kumudu gharama za kampeni huku kina vyanzo vya uhakika {ruzuku + michango ya wabunge)?

Kuna vyama vingi tu vinashiriki Uchaguzi Mkuu huu visivyokuwa na ruzuku wala mapato kama CHADEMA, havitembezi bakuli.

Nashauri wafuasi wa CHADEMA, humu JF, waache unafiki kama wana nia nzuri ya kutaka kiwe Chama Tawala, ili isije baadaye kunung'unika kuwa hawakujua. Kuna ushahidi usio na mashaka kuwa CHADEMA hakiendeshwi kama chama cha siasa. Dai hili linakinyima uhalali wa kupewa ridhaa na wananchi kuongoza nchi.

Bila kumung'unya maneno, naomba kwa Mwenyezi Mungu awajaze ujasiri Watanzania kukiadhibu vibaya sana CHADEMA kwenye sanduku la kura ili viongozi wake warudi mezani kujenga chama upya kama chama cha siasa.
Sasa wewe unajaza tuhuma wakati ushahidi hauna, unataka nani approve kwa ajili yako? kuna msemo wa kisheria unasema ....who alleges must prove" sasa mpaka hapo umeshafeli, unaonekana una maneno mengi ya kuambiwa ambayo huna ushahidi nayo then unaniita mimi nimejibu kishabiki! halafu unataka niwe mpole kumeza hizi pumba zako!

Unazungumzia mazingira ya uchaguzi mkuu 2015, hujui leo tuko 2020, na hauoni hali halisi kiuchumi na kisiasa leo na 2015 ni tofauti? hujaona wapinzani wamezuiwa kupewa misaada na marafiki zao wa nje? unadhani lengo la serikali kufanya hivyo ni nini? yani huu ndio uchambuzi unaojidai nao!

Nimekwambia mwanzo, hata kam hiyo ruzuku ipo, ambayo ni milioni 200 na kitu kwa mwezi, itatosha nini kugharamia shughuli za chama nchi nzima? hivi unajua CCM wanachukua ruzuku ya bilioni 17 na bado wanaiba sehemu nyingine kuongezea?

Unasema kuna ushahidi usio na mashaka kuwa Chadema hakiendeshwi kama chama cha siasa....hivi wewe unajielewa kweli?! yani msajili yupo halafu aache Chadema iendeshwe kienyeji awe anatazama tu? na hizi sheria za mitego zilizopitishwa juzi kwenye bunge la Ndugai!upeo wako ni mdogo sana, na huu uchambuzi wako haujitoshelezi kabisa, hauna uthibitisho ni kelele tu.

Kama ukijibu, napenda ujibu kila aya niliyoandika hapo juu, usikwepe chochote, sitaki porojo hapa.

Mwenyezi Mungu sio mjinga wa kusikiliza hiyo sala yako ya kichovu.
 
Kwa nini msitumie pesa walizokuwa wanachangishwa wabunge kugharamia uchaguzi?
Unajua gharama za uchaguzi au unajiropokea tu?
ngoja nikupe mfano mdogo tu:.
kampein za CCM
MGARI yasiyopongua 60 kwenye msafara wa mgombea urais, makamu 50 na waziri mkuu 40 jumla ya magari 150 yanatumika kila siku kwa siku 60.
wastani wa chini mafuta kwa kila gari lita 80 kila siku unapata nini 150 x 80ltr x 1800 bei ya lita moja x siku 60 za kampeini 1,296,000,000/= kadirio la karibu 1.296B HIYO NI GHARAMA YA MAFUTA, ukiweka gharama za chakula na kulala kwa walioko kwenye hiyo misafara fanya watu wasiopungua 400 kwa siku wanalipwa posho ya sh 30,000 x 400 x 60 = 720,000,000 fanya 1B Kwa wastan wa chini kampeini za CCM hazitapungua B20 CHADEMA wanazo hizo hela je CCM nayo ina biashara gani ya kumiliki hizo hela, majibu unayo mwenyewe.
 
Unajua gharama za uchaguzi au unajiropokea tu?
ngoja nikupe mfano mdogo tu:.
kampein za CCM
MGARI yasiyopongua 60 kwenye msafara wa mgombea urais, makamu 50 na waziri mkuu 40 jumla ya magari 150 yanatumika kila siku kwa siku 60.
wastani wa chini mafuta kwa kila gari lita 80 kila siku unapata nini 150 x 80ltr x 1800 bei ya lita moja x siku 60 za kampeini 1,296,000,000/= kadirio la karibu 1.296B HIYO NI GHARAMA YA MAFUTA, ukiweka gharama za chakula na kulala kwa walioko kwenye hiyo misafara fanya watu wasiopungua 400 kwa siku wanalipwa posho ya sh 30,000 x 400 x 60 = 720,000,000 fanya 1B Kwa wastan wa chini kampeini za CCM hazitapungua B20 CHADEMA wanazo hizo hela je CCM nayo ina biashara gani ya kumiliki hizo hela, majibu unayo mwenyewe.
Unajua sheria ya uchaguzi inataka kiwango cha mwisho cha gharama za uchaguzi iwe sh ngapi? Unaropoka kama unaharisha.
 
Hawa ni wahuni mkuu, wanadai wananchi wana halimbaya kiuchumi hapohapo wanawachangisha pesa sijui wanatuonaje Hawa watu.
Msikilize kilaza wa maccm na usomi wake uchwara.

"Ombi letu ni kwamba maji yetu hapa yaharakishwe kwa sababu, maji ya hapa yanatoka kama matope ni machafu sana, wananchi wa Kasulu hawana matatizo kabisa na ccm_tanzania na wamesema kura zote wanakupa wewe Meko"- Prof Ndalichako
 
Kwani ile michango waliokuwa wanakatwa wabunge kwa ajili ya uchaguzi iko wapi? Wananchi wana hali mbaya kwa nini muwachangishe?

Ilikuwa kwa ajiri ya kuimarisha chama ndiyo maana wamweza kuwa na mtandao nchi nzima hata baada ya kukaa mika mitano bila kuruhusiwa kufanya mikutano ya kisiasa.
 
Ilikuwa kwa ajiri ya kuimarisha chama ndiyo maana wamweza kuwa na mtandao nchi nzima hata baada ya kukaa mika mitano bila kuruhusiwa kufanya mikutano ya kisiasa.
Ofisi zimefungwa kila wilaya,wagombea udiwani na ubunge hawana hata vipeperushi. Hali ni mbaya sana, Mbowe alikula ruzuku na michango ya wabunge.
 
Sasa wewe unajaza tuhuma wakati ushahidi hauna, unataka nani approve kwa ajili yako? kuna msemo wa kisheria unasema ....who alleges must prove" sasa mpaka hapo umeshafeli, unaonekana una maneno mengi ya kuambiwa ambayo huna ushahidi nayo then unaniita mimi nimejibu kishabiki! halafu unataka niwe mpole kumeza hizi pumba zako!

Unazungumzia mazingira ya uchaguzi mkuu 2015, hujui leo tuko 2020, na hauoni hali halisi kiuchumi na kisiasa leo na 2015 ni tofauti? hujaona wapinzani wamezuiwa kupewa misaada na marafiki zao wa nje? unadhani lengo la serikali kufanya hivyo ni nini? yani huu ndio uchambuzi unaojidai nao!

Nimekwambia mwanzo, hata kam hiyo ruzuku ipo, ambayo ni milioni 200 na kitu kwa mwezi, itatosha nini kugharamia shughuli za chama nchi nzima? hivi unajua CCM wanachukua ruzuku ya bilioni 17 na bado wanaiba sehemu nyingine kuongezea?

Unasema kuna ushahidi usio na mashaka kuwa Chadema hakiendeshwi kama chama cha siasa....hivi wewe unajielewa kweli?! yani msajili yupo halafu aache Chadema iendeshwe kienyeji awe anatazama tu? na hizi sheria za mitego zilizopitishwa juzi kwenye bunge la Ndugai!upeo wako ni mdogo sana, na huu uchambuzi wako haujitoshelezi kabisa, hauna uthibitisho ni kelele tu.

Kama ukijibu, napenda ujibu kila aya niliyoandika hapo juu, usikwepe chochote, sitaki porojo hapa.

Mwenyezi Mungu sio mjinga wa kusikiliza hiyo sala yako ya kichovu.
Mwl Nyerere, Baba wa Taifa aliwahi kusema kwa lugha yake ya kuzaliwa akimaanisha "anayeficha ugonjwa mauti inamuumbua".

Si wajibu wangu kutafuta ukweli wa tuhuma dhidi ya M/Kiti wa CHADEMA kwa kuwa siyo mwanachama. Mimi kamwe nitakuwa mwanachama wa chama kinachoendeshwa kama SACCOS. Huo ndio ukweli mtupu.
 
Poa...ntachangia sana. Kwa kweli kupigwa risasi kwake mchana saa saba kumenifanya nimwonee huruma na hapohapo kanyimwa matibabu na ujira wake pia kanyang'anywa.
Sasa unamchangia hela ya kura au ya kampeni? Mbona bichwa maji unajichanganya.
 
Ndio ushangae SASA mambo ndio hivyo we jamaa unaonekana una uelewa wa mambo ila huelewa kinachoendelea na hii ni pengine umeajiriwa lumumba siku za karibuni kwa hiyo upo kwenye mazoezi ya namna ya kujitoa akili😎🙂😎😎😁😁
 
Back
Top Bottom