Nawaza mateso waliopata watu kwa kutongozana kabla simu hazijaja

Nawaza mateso waliopata watu kwa kutongozana kabla simu hazijaja

Sekta ya mapenzi kipindi hicho iliajiri kama sekta binafsi zaidi ya watu laki nane (maposta) kwaajir ya kupeleka barua na jumbe mbalimbali ijapokuwa zilikuwa sio ajira za kudumu pia malipo yake ilikuwa hayapo katika form ya kueleweke eg mtu anaweza kulipwa msosi kama ujira au fedha kiduchu

Sent from my using Tapatalk
 
Sekta ya mapenzi kipindi hicho iliajiri kama sekta binafsi zaidi ya watu laki nane (maposta) kwaajir ya kupeleka barua na jumbe mbalimbali ijapokuwa zilikuwa sio ajira za kudumu pia malipo yake ilikuwa hayapo katika form ya kueleweke eg mtu anaweza kulipwa msosi kama ujira au fedha kiduchu

Sent from my using Tapatalk
hakika na ujira ulikuwa mkubwa maana unaulipa kwa hisia pia
 
Shuleni tulikuwa tunaandika barua tunaiweka katikati ya daftari ya binti, wengi walipata misukosuko kwani baadhi ya mabinti waliozembea barua zilinaswa na walimu na wengine zilidondoka njiani bila wao kujua
hiyo nakumbuka kuna mabinti wawili waliniadhibiwa kisa mmoja kaniandikia barua kaweka kwenye daftari langu alafu takakusanya dah ilikuwa ishu mwalimu akaona
 
Kule vijijini tulikuwa tunaandika barua tunajificha kichakani tukisubiri binti anapokwenda au kutoka kuteka maji kisimani tunairusha barua njiani uso wa bahasha kwenye anuani yake ukiwa juu, akifika na kuiona anaichukua, ngoma ilikuwa kufuatilia majibu ya hiyo barua
hahaha
 
Nimeandika sana barua...hamna kitu kilikuwa kinauma kama niende posta nikute baba hajalipia sanduku limefungwa. Nadhani home walikuwa hawaelewi kwann nakaa na funguo ya posta
 
Makutano kwenye miti au vichaka au gheto kwa mshikaji. Watoto walikuwa ndio simu, unawatuma. Sasa mitoto mingine ilikuwa inaharibu, mzazi yupo bado kinasema "fulani anakuita pale kwenye mti", badala ya demu anakuja mzazi, si kwa mbio hizo
 
Siku hizi wanaume hakuna, wote tunajipanga nao foleni kununua chips mayai, wanaume wanasafisha kucha saloon doh, wanaume wanawekwa Heleni,
Zamani walikua hawavai hereni? huoni makabila yanayovaa hadi sketi leo hii wanaume? kuosha kucha mwanaume n dhambi? so wakae wachafu kisa wanaume? Chipsi zinaliwa na wanawake tu? maana ya balance diet ni nini? Tatizo la watu wengi saivi maisha wana ya complicate sana vitu vya kawaida ila mimacho itawatokaaaa kama vile huyo anaemshangaa ndio wakwanza kukifanya duniani...
 
Mbona ilikua simple


Unachora moyo unaotobolewa na mkuki na vijimaneno vichache unakua umemaliza shughuli.


Siku hzi ni mwendo wa mizinga tu!

Sent using Jamii Forums mobile app
mchoree asiyejua kusoma sasa, barua itaenda kusomwa mtaa wa 5. msomaji akivutiwa na mwandishi 'anabadili gia angani' anasema barua ni ya salamu toka kwa shangazi yako. kisha kwa muda wake anamjibia na kuuteka moyo wa msaka mwari.

mlengwa alieandikiwa anabaki gizani. na hapo ndipo utajua MAPENZI NI SAFARI, NAWE HAUNA NAULI!!
 
Shuleni tulikuwa tunaandika barua tunaiweka katikati ya daftari ya binti, wengi walipata misukosuko kwani baadhi ya mabinti waliozembea barua zilinaswa na walimu na wengine zilidondoka njiani bila wao kujua
1994 ilinihusu. sitaki kusimulia kabisa, naona chaji inaisha na Tanesco wamekata.
cc. mwl. Spenser Niboye
cc. Deus James Kagayo
 
Hivi mtoto mzuri akikuagiza umletee kiepe zege tatizo liko wapi? Au ndo kwenye foleni ukionekana unaagiza wewe nduo mlaji?
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] kuna wavulana mzazi aliwauliza unamwitia nini eti tunataka ku discuss physics, wakati yeye yupo form 4 binti form 1 [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Makutano kwenye miti au vichaka au gheto kwa mshikaji. Watoto walikuwa ndio simu, unawatuma. Sasa mitoto mingine ilikuwa inaharibu, mzazi yupo bado kinasema "fulani anakuita pale kwenye mti", badala ya demu anakuja mzazi, si kwa mbio hizo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji23][emoji23]ila henzi zile mademu walikua watamu mbaya japo kuwapata ilikua tabu
mchoree asiyejua kusoma sasa, barua itaenda kusomwa mtaa wa 5. msomaji akivutiwa na mwandishi 'anabadili gia angani' anasema barua ni ya salamu toka kwa shangazi yako. kisha kwa muda wake anamjibia na kuuteka moyo wa msaka mwari.

mlengwa alieandikiwa anabaki gizani. na hapo ndipo utajua MAPENZI NI SAFARI, NAWE HAUNA NAULI!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Simu zimesadia sana.. Vikwazo vilikuwa vingi sana..kuna vitu vilinipa shida sana..timing ya muda.. makaka wa binti..na majirani kwa umbea.. Sasa hivi unakula Dada wa mshikaji kimyakimya.
 
Kipindi cha nyuma 1985-2000 simu zilikuwa nadra sana,

Lakin pamoja na uchache wa simu, watu walitia maneno mpaka wenza wao wakawaelewa,

Kwa wale wa juzi juzi mmerahisishiwa kazi sana,

Mtu kipindi hicho anakaa Tabata anamfuatilia msichana wa makumbusho bila hata simu, inabidi apande gari akashuke mwenge atembee mpaka bamaga kwakuwa anahisi msichana yule atapita maeneo yale kama siku alivyomuona akipita nyuma,

Na anamkosa, anaamua kurudi home, kesho yake anatia kambi tena lakin hafanikiwi, hii ilileta hamasa kwamba hata akimpata maneno ni hapo hapo,

Watu wameng'atwa sana na Mbu wakiwasubiri kina Mwajuma wapite njia fulani kisa wameona anapita asubuhi,

Watu wameshinda mtoni wakiwasubiri akina hilda ili wapate nafasi ya kutema yao

Watu wameteseka mno,

Siku hizi wanaume hata kutongoza imekuwa shida neno linalotangulia ni NAOMBA NAMBA YAKE HIYO DADA,

hawana uwezo tena wa kumface mwana mke kumtemea cheche live,

Siku hizi wamerahisishiwa sana , mwanamke akikunyima namba ya simu unamuomba basi anayotumia tigo pesa haha anaachia mara moja

😀😀 kiongoz kipind icho nasikia walikua wanaweka barua mlangoni kisha wanaponda batini potelea mbal atoke mama baba watajua wenyewe
 
Niliwahi kupigwa mvua ya mawe giza limeshaingia halafu nyumbani mbali kinoma na natembea kwa miguu daaah!
 
Back
Top Bottom