Nawezaje kuanzisha Men Brotherhood? Kikundi cha wanaume cha kujengana?

Nawezaje kuanzisha Men Brotherhood? Kikundi cha wanaume cha kujengana?

View attachment 2962233View attachment 2962245
Wanaume kiasili ni wasiri na wasiopenda kuwa na urafiki au vikundi kama ilivyo wanawake. Pia wanaume wengi huweka vitu moyoni na sio rahisi kufunguka yanayowasibu, wengi hawaonyeshi hisia aidha za furaha au huzuni yaani ni stoic.

Lakini kwa upande mwingine mwanadamu ni kiumbe social anahitaji ile socialisation ili kuishi vizuri na kuweza kustawi hasa kisaikolojia na afya ya akili. Hii inaonyesha umuhimu wa kuwa na marafiki wenye common interest wa kujengana na kuweza kupeana motisha na ushauri mbalimbali katika maisha ya kila siku.

Kukosa hili husababisha upweke ambao athari zake hazina tofauti na uvutaji sigara. Hili linatokea hasa kwa wanaume kuanzia miaka 30 ambapo kila mmoja anakuwa bize na majukumu yake ya maisha.

Baadhi wanatumia vikundi vya unywaji, wengine vikundi vya michezo kama mpira, jogging, michezo ya magari katika namna ya kupata hiyo brotherhood ambayo husaidia utimamu wa mwanaume. Wengine hujiunga katika vikundi vya kifamilia n.k.

Lakini wengine duniani huko wapo kwenye vikundi vya siri (secret society) ambavyo vimekuwa vikubwa na powerful kiasi cha kuogopwa duniani.

Vile vile kuwa na umoja hurahisisha mambo mengi kwasababu ya mawazo tofauti na pia "network" ya watu mbalimbali. Wahindi wanatumia huu mfumo sana kwenye jamii yao na hata biashara ambapo asimilia kubwa ya biashara za wahindi wanatumia mfano benki ya exim ambayo ni ya wenzao vivyo hivyo kwa huduma nyinginezo.

Sasa je nawezaje kuanzisha Brotherhood, ya watu makini kwa ajili ya kupata ule ukomredi ( camaraderie) na kupeana changamoto na support katika maisha ya kila siku hapa nchini??

Je vikundi hivyo vipo tayari nchini?
Muwe wote mna vibunda so wengine muwageuze machawa wenu
 
Naam evelyn , binadamu pamoja na ubifsi tulio nao laiki hatujali haswa hisia za mtu, unaweza kuingia sehemu ilibupate faraja badala yake unapata frustrations na stress, heri ubaki mpweke.
Ila pia usikose kote kote, ukishindwa kijamii jiweke kwenye kikundi cha maokoto tu.... Hakuna kufatana wala kujuana. (Vinakuaga na msaada sana)
 
Ni cha wanawake tu labda
Ndio cha wanawake tu! Ila humo wote tuko serious na tunachokifanya. Kuna mtoto wa sister nakaa naye alipata komunio iliwekwa kamati km ya harusi na sikutoa mia yangu na nilipewa pesa zile chenchi zinazobaki kwenye kamati na zile za kutunzwa acha kabisaa!!
Sijutii kuwa na familia km ile ya…….!!!
Ukitokea msiba hata km kwenu mbali kiasi gani tunaenda
 
Basi nyie wote mliopo hapa nawaona kuwa mpo positive, ni watu wenye maono mazuri, mna life purpose na mnajali maisha yenu na ya wapendwa wenu, huu ndio msingi wa brotherhood yoyote ile, hivyo nawaalikeni kama founder members of The Saturday Brotherhood!

Karibuni katika brotherhood yetu! Tuna mambo mengi sana ya kushirikishana kati yetu na kuwashirikisha wengine pia. Maisha ni kushirikishana shida na raha. Kati yetu asiwepo hata mmoja mwenye lolote linalomtatiza akakaa kimya. Tushirikishane vipawa vyetu, hali zetu, mali zetu na hata changamoto zetu.

Brotherhood is all about udugu nje ya ule udugu wa vinasaba, udugu wa kuzaliwa. Ni udugu wa kifikra, kiimani, na kihisia.

Udugu wetu ambao kwasasa unaitwa jina la mpito, The Saturday Brotherhood utaongozwa na Duksi kama founder. Sisi wengine ni Co-founders. Karibu sana Duksi kuwa kiongozi wetu na hongera sana kwa wazo hili madhubuti!!!

Tunaweza kuanza kama a simple brotherhood na tunakua zaidi na kuwa chochote kile tunachopenda lakini tusisahau lengo letu la awali na la msingi, udugu.

Napendekeza kwamba tuwe na social group account kama vile WhatsApp au X (Twitter) na tuanze kushirikishana mengi. Kuna faidia kubwa sana katika udugu nasi tunapenda kuzijua faida hizo na kuzifaidi.

Tukifanikiwa katika hili, basi tutasajili brotherhood yetu na kuwa na utambulisho wa kisheria na kupanua shughuli zetu hata nje ya mipaka yetu! Tunaweza kuamua tunataka kufanya nini katika udugu wetu. Hakuna limit, lakini sisi tutachagua kilicho kizuri kwa watu wote na chenye kuleta manufaa zaidi.

Kwasasa tujuane zaidi, halafu tujue interests zetu na tuanze kushirikana tunu zetu. Baadaye tutatengeneza katiba ya udugu wetu.

Karibu kiongozi wetu Duksi, tafadhali endelea na kazi uliyoianza.

Karibuni The Saturday Brotherhood!

Asanteni

Fazili
Ili brotherhood iwe imara, iwe tu na waanaume pekee, wanawake kuchafua hali ya hewa ni dakika chache sana.....

Ikishakua imara, wake zenu nao mnawakutanisha wanakua na ka umoja kao pia inapendeza.
 
Ndio cha wanawake tu! Ila humo wote tuko serious na tunachokifanya. Kuna mtoto wa sister nakaa naye alipata komunio iliwekwa kamati km ya harusi na sikutoa mia yangu na nilipewa pesa zile chenchi zinazobaki kwenye kamati na zile za kutunzwa acha kabisaa!!
Sijutii kuwa na familia km ile ya…….!!!
Ukitokea msiba hata km kwenu mbali kiasi gani tunaenda
Heri ndugu yangu , ni mara chache sana kukutana na vikundi namna hio, ukiona au kusikia kinachopokea wanaume usisite kunijulisha naomba.
 
Hizi sie wachache wanaoweza, tuna mambo mengi sie
Mi nina kikundi kimoja cha kanisani cha wamama cha kusaidiana
Kwa kweli ni kizuri ni kama kikoba ila hakijakaa hivyo
Tunakutana mara moja kwa mwezi
Kina benefits nyingi sana
Mim sasa hivi nataka cha wafanya biashara sema nini uaminifu ndo naogopa
Haswa kikihusisha ela
Unamjua panda source?
Walizumianaga almost mil90
Wakamlipa lipa akaja akabaki anadai mil 90
Cha wafanya biashara wa china hicho
Kawachangia wenzie akawa wa mwisho kuja mzunguko wake wa mwisho hawataki kutoa ela mtu alikua anakunja 90M
 
Heri ndugu yangu , ni mara chache sana kukutana na vikundi namna hio, ukiona au kusikia kinachopokea wanaume usisite kunijulisha naomba.
Tatizo hivi ni vya wafanyabiashara tu! Kimoja ni mchanganyiko ila kiingilio kikubwa million 20 na mpk wakupitishe wakuchunguze sana.!!
 
Ili brotherhood iwe imara, iwe tu na waanaume pekee, wanawake kuchafua hali ya hewa ni dakika chache sana.....

Ikishakua imara, wake zenu nao mnawakutanisha wanakua na ka umoja kao pia inapendeza.
Hapana sio wote wanawake wanashida , ni wachache sana ila shida zao ndio zinafanya wanawake wengi waonekane changamoto, ukipata sehemu sahihi wakiwa wengi sahihi, wachache wabaya watakao ingia mnaweza kuwatoa.
 
Mi nina kikundi kimoja cha kanisani cha wamama cha kusaidiana
Kwa kweli ni kizuri ni kama kikoba ila hakijakaa hivyo
Tunakutana mara moja kwa mwezi
Kina benefits nyingi sana
Mim sasa hivi nataka cha wafanya biashara sema nini uaminifu ndo naogopa
Haswa kikihusisha ela
Unamjua panda source?
Walizumianaga almost mil90
Wakamlipa lipa akaja akabaki anadai mil 90
Cha wafanya biashara wa china hicho
Kawachangia wenzie akawa wa mwisho kuja mzunguko wake wa mwisho hawataki kutoa ela mtu alikua anakunja 90M
Mimi hivyo napendaga niwe wa kwanza sitaki utani na pesa kabisaaa!!!
 
Tatizo hivi ni vya wafanyabiashara tu! Kimoja ni mchanganyiko ila kiingilio kikubwa million 20 na mpk wakupitishe wakuchunguze sana.!!
Sema cha matajiri bwana, mtu mwenye biashara ya mtaji w milioni tano kushuka chini kwake si changamoto sana.
 
Mi nina kikundi kimoja cha kanisani cha wamama cha kusaidiana
Kwa kweli ni kizuri ni kama kikoba ila hakijakaa hivyo
Tunakutana mara moja kwa mwezi
Kina benefits nyingi sana
Mim sasa hivi nataka cha wafanya biashara sema nini uaminifu ndo naogopa
Haswa kikihusisha ela
Unamjua panda source?
Walizumianaga almost mil90
Wakamlipa lipa akaja akabaki anadai mil 90
Cha wafanya biashara wa china hicho
Kawachangia wenzie akawa wa mwisho kuja mzunguko wake wa mwisho hawataki kutoa ela mtu alikua anakunja 90M
Doh pole zake, uaminifu ni changamoto.
 
Back
Top Bottom