Nawezaje kuiokoa familia yangu na mateso ya jini huyu?

Nawezaje kuiokoa familia yangu na mateso ya jini huyu?

Naitwa Ododi 35yrs Mkazi wa Kimara Korogwe. Nipo kwenye ndoa kwa muda wa miaka 6 nimebahatika kupata mtoto 1 ambae anafikisha mwaka mmoja tangu kuzaliwa na kuja kwenye hii dunia yetu ukiachana na wengine 7 ambao wapo kwenye ulimwengu mwingine.

Najua unaweza usinielewe nikisema ulimwengu mwingine kuna watoto 7, ndio ninao si uongo ila hili sijambo nataka mnisaidie mawazo kwa leo.

Tuendelee na Mada tajwa.

Nia ya kuweka maandishi haya hapa chini ni vile nimekua nikipitia magumu mengi mimi pamoja na mke wangu na sasa naona mtoto pia anapitia shida nyingi, mke wangu amekua akiteswa sana na Kiumbe cha ajabu, amekua akikiona "fluently" Kikiwa na mapembe kama mbuzi kifupi ni kiumbe ambacho kina tisha sana, Ni kimekua kikimtesa, kumkaba, kumuingilia kivyovyote kikitaka, kinamfanya awe mgonjwa malanyingi, amekua hana nafasi ya kuwaza na kufikilia vyema.

Tatzo lilianza kabla ata sija funga nae ndoa, nakumbuka kuna siku nilimuacha nyumbani kwangu nikaenda kazini, ilipofika saa nane mchana alinipigia simu akilia sana, ikanibidi kurudi home. Nilipofika nilimkuta kalala chini hawezi ata kugeuka, alinambia kuna kiumbe cha ajabu kimemfata nakumbuluza nyumba nzima, amehangaika sana kuamka kashindwa lakini alikua macho anakiona na anasikia watu nje wakiongea nakupita ila pamoja na kupiga kelele hakuna alie sikia.

Mke wangu aliniita kwa majina yangu, na akasema alivyo kua akiona kipindi yule mdudu akimbuluza pale ndani ni kama amevunja vyombo vyote na TV, nikamjibu hakuna kitu chochote kilicho vunjika kila kitu kipo kama nilivyo acha asubuhi, Mke wangu aliinuka na kukaa kama dakika 20 bila kusema kitu, baadae akanambia anahisi maumivu makali sana kwenye mbavu, mgongoni, shingoni na mikononi.

Nilimvua nguo aliyo kuwa kaivaa juu kuangalia hizo sehemu anazopata maumivu, niliona mikwaluzo ya kucha alama za vidole, na zimevia damu sehem hizo zote, kiukweli sikuelewa nikamtafutia tu dawa za maumivu nikakaa kimya, ila cha ajabu usiku wake kile kiumbe kikaja tena, this time kilikua kinaongea ila mimi sikioni kikiniomba ni mpatie mwanamke wangu then chenyewe kinipe utajiri na mali nilikataa na nilisikia kikiondoka kinalia.

Ikapita muda maisha yakaendelea mpaka nikaja muoa huyu bibie, Safari ya ndoa haikua nyepesi nilipitia wakati mgumu sana kufanikisha zoezi la ndoa, matatizo ndo yakaanza mimba zinapotea juu kwa juu, Lile dudu likaanza mambo yake, mke akawa hawezi baki na nyumba itambidi akae nje mpaka nirudi na nikirudi hawezi enda kulala mpaka twende wote chumbani, nikama likawa linataka kumpa uchizi.

Siku moja kuna rafiki yangu akanipa wazo nijaribu kumtafutia Tiba kwa masheikh wa Pemba. Nikaomba likizo kazini ili niweze mtibia mke wangu, kazini nikapewa siku7 nikaona sawa, nikatafuta ndege mpaka Pemba mimi na mke wangu ili akafanyiwe visomo wamtoe huyo mdudu.. Mmh ndugu zangu ndo kama nikawa nimeenda kuwasha moto kwenye petrol station.

Visomo viliisha tuka rejea Dar es salam, Mambo yakawa mabaya zaidi, lile dudu ndo likaanza mkaba malanyingi kuliko mwanzo, sikukata tamaa nikaendelea kuhangaikia kwa mafundi mbali mbali ambao walidai wanaweza nisaidia mikoani huko bila mafanikio. Akiba yangu ikaanza kupungua kwa kasi sana sikumaliza mwezi kazini ni kapigwa chini.

Nikarejea sasa kukaa bila kazi hali ikawa mbaya sana, ilikua 2018 nilifedheeka sana kama mnavyoelewa maisha ya mjini ukiwa nacho alafu ghafla kikakata. Nikapata insomnia kwa muda maana nilikua silali usiku, mke wangu anaweza anza piga kelele anaona vitu mimi sioni usiku wamanane.

Usiku anapigakele za kuogopa vitu ambavyo mimi sioni, akidai amezungukwa na watu wa ajabu pale tulipo lala huku akijificha mgongoni kwangu, anadai kuna kitu wanamtoa tumboni anapiga kelele analia ni msaidie, imagine sioni chochote nabaki kama zuzu sielewi naanzia wapi, kuna muda alilia sana akasema wanamuuwa, alinistua sana kuangalia vizuri naona damu kitandani, nilipomwambia damu zina kutoka alipiga kelele moja na akazima.

Nilipata hofu nilipiga simu kwao nikawaelekeza juu ya yanayo endelea kwa mtoto wao, nilimkimbiza Botch Hospital alivyochekiwa Daktari akadai alikua na mimba inaonekana imeharibika.

ITAENDELEA
Nyie ni Waislam? Tuanzie hapa kwanza.
 
Baada ya kutoka hospital tulirejea nyumbani, na maisha yetu yakaendelea kama kawaida, nikaendelea kupigwa matukio kila siku, nikayumba sana kiuchumi. Alikuja mzee mmoja wa kisukuma huwa na fahamiana nae kwa muda akaniambia niende nyumbani Niliko zaliwa kweli nilifanya hivyo.



Inaendelea......

Kusoma Ilipoanzia

Sehemu ya Pili

-----

"NITAFUPISHA HAPA, IKUMBUKWE HII NI STORI YA MAISHA YANGU KABISA KWA MUDA WA MIAKA 7, NIMEKUA NIKUZUNGUKA HUKU NA KULE KUTAFUTA MSAADA KWA KIPINDI HIKO CHOTE. NILITAMANI KUELEZEA KILA STAGE NILIYOPITIA ILI MWENYE UWEZO WAKUSAIDIA MAWAZO AJUE NIWAPI ANAWEZA SAIDIA."

J3 Tumeamka nimeendelea na kazi za kila siku, Ila hapa kuna maisha kidogo yalikua tofauti, Wife alikua ananiambia vitu vingi na vinatokea, Mala nyingi akisema jambo na likatokea, Mfano nakumbuka alishanifanyia matukio mawili ndani ya siku 1, Siku hiyo alikua na mimba ya miezi kama minne nmetoka nampeleka pharmacy akanambia tu kiutani anatamani kuokota hela.

Basi nikawa namcheka tu nikapuuzia, tulipo kua tukirejea toka Pharmacy akanambia kachoka hawezi tembea nikaita Tax, wakati nakaribia kwenye Tax alinionyesha kibunda Kikiwa chini usawa mlango wa gari, akakiokota ilikua ni laki8, nilipata mshangao akacheka alafu hakusema kitu.

Tulipofika home alikuja rafiki yake kumuona, banda ya stori kadhaa akamwambia, leo atakama unaharaka vipi usipande bodaboda, akapuuzia alipokua akiondoka akadai kachelewa akaita boda, azikupita dakika 10 tunapigiwa simu wamedondoka kaumia vibaya.

Akawa ni mtu wa aina hiyo lakini lile tatzo lakukabwa halikuisha, Shida nyingine ikaja ata nikitongoza demu popote atajua hiyo kitu nayo imekua ikinivuruga sana.

Kuna sheikh mmoja yupo Ilala anaitwa sheikh Khalfan sikumoja baada ya dua alinambia tatzo la huyu jini wa mkeo ukisema uingize pesa yako kumtibu mkeo anakufungia kila kitu utaishiwa utakosa mpaka hela ya maji ya kunywa,

Na nikweli nakumbuka nimesha mpeleka wife kwingi nikifanya kutafuta tiba, basi nitapoteza kilakitu, yaani taishiwa na kazi tapoteza kabisa, Sasa ndugu zangu inawezekanaje kumuacha mwenzio akiugua kwa kuhofia hayo, Tatzo la hii michezo sio kama anakua kichaa au vipi hapana.

Ili niishiwe pesa tu naweza pata series ya wagonjwa, ndani ya mwezi mzima akaugua yeye, akaugua mama nyumbani wakawa wapokezana, ni mwendo wa hospital tu, imekua hivyo kwa muda sana.

.. Naomba niishie hapa kwa sasa, kwa mwenye uwezo au kujua wapi naweza pata njia ya kweli ya kutatua hili karibuni.
 
Naitwa Ododi 35yrs Mkazi wa Kimara Korogwe. Nipo kwenye ndoa kwa muda wa miaka 6 nimebahatika kupata mtoto 1 ambae anafikisha mwaka mmoja tangu kuzaliwa na kuja kwenye hii dunia yetu ukiachana na wengine 7 ambao wapo kwenye ulimwengu mwingine.

Najua unaweza usinielewe nikisema ulimwengu mwingine kuna watoto 7, ndio ninao si uongo ila hili sijambo nataka mnisaidie mawazo kwa leo.
Wewe toka mwanzo kwa nini ulishindwa kuijulisha familia yake
 
Ukitulia tu, mwisho wako hautakuwa mzuri kama utaendelea kuishi na huyo mkeo.
Mpeleke kwenye maombi;- jaribu kwenda arusha umpeleke ngurumo ya upako, kwa sababu kuna wengine hutoka nje ya nchi na kwenda pale kwa msaada.
 
Huko kwa waganga na mashekhe uchwara ndo umeenda kumuongezea madudu zaidi,kwasie wakristo huyo kabla hajafunguliwa anatakiwa afanye toba ya maagano aliyojiunga nayo ama yaukoo wao,then afanyiwe deliverence hicho kidude kitapigwa moto mpaka na aliyekituma wote watasambalatika . NB: Matatizo mnayataka wenyewe kwakupenda kwenda kwa waganga mnaacha kumtafuta Mungu mwenye nguvu kuliko hao waganga mashetani
 
Ushauri:
1. Nenda Kanisa la Kilutheri lililopo hapo Kimara pamoja na familia yako yote. Omba kumuona Mchungaji mueleze shida unayopitia, ataomba nawe na kuwapa sala ya toba. Baada ya hapo hakikisha mnashiriki maombi mara kwa mara familia nzima ili kama hilo dudu lilikuwa linasumbua pia mtoto liondoke kabisa. Hii huduma ni bure kabis
Nakazia hapa, wiki hii kuna maombi ya staili hii hapo K.K.K.T Kimara Korogwe kuanzia saa kumi na mbili jioni hadi saa mbili na nusu ni kila siku yataendelea hadi wiki ijayo hadi pasaka ukipata mda njoo nae hutajutia wala hutatumia hata senti.
 
Pole sana mkuu, kweli dunia ina mambo kama wasemavyo watu pori.
Najua wataalamu wa miziziology na tiba mbadara watakuja kukupa mwongozo.
 
Hakuna pepo awezae mtoa pepo wote ni kampuni moja awatupani, zaidi utapewa jini Mkubwa amtulize jini Mdogo baada ya mda itarejea tena hali.
Hakuna ushirika Kati ya mwanadamu na majini, Kazi ya jini ni kuuwa.
Ukiyakataa na kuyafurusha yasitawale maisha yako utakuwa salama.
 
Why mnarudi nyumba hiyo hiyo
Hebu Hama nyumba uone
Shida ni binti na sio nyumba.
Binti aliweka maagano au kwao binti anatoka ukoo wa kichawi,kiganga,kitemi au kichief ni rahisi kufatiliwa na roho wa chafu.
Mfano ugonjwa wa sicocell,kifafa chanzo ni uzao ukoo wa kichawi au uganga au wa kimaagano ya kichawi.
Kama nyumba ndo Ina vitimbi basi hio nyumba imejengwa juu ya madhabau ya kichawi,au zamani eneo hilo ilikuwa ni kilinge cha mganga au ilikuwa ni eneo la matambiko au ni lango la kuzimu au mmiliki wa nyumba hio ni agent wa kuzimu au ni member wa freemason ikiwemo nyumba hio imejengwa kwa pesa za shetani.
 
Naitwa Ododi 35yrs Mkazi wa Kimara Korogwe. Nipo kwenye ndoa kwa muda wa miaka 6 nimebahatika kupata mtoto 1 ambae anafikisha mwaka mmoja tangu kuzaliwa na kuja kwenye hii dunia yetu ukiachana na wengine 7 ambao wapo kwenye ulimwengu mwingine.
Mh. Mkimbilie Mungu ndio msaada sio waganga
 
Baada ya kutoka hospital tulirejea nyumbani, na maisha yetu yakaendelea kama kawaida, nikaendelea kupigwa matukio kila siku, nikayumba sana kiuchumi. Alikuja mzee mmoja wa kisukuma huwa na fahamiana nae kwa muda akaniambia niende nyumbani Niliko zaliwa kweli nilifanya hivyo.

Nikiwa nyumbani nilipelekwa sehem na uncle wangu, nikakaa pale kwa muda wa siku nne nikiwa naendelea na visomo, kuna Bibi alikuja nakunambia
Aisee! Pole sana mwamba.
 
Tunahakikishaje haya mambo yametokea kweli na.

1. Si hadithi ya mtu ya kutungwa tu.
2. Si matatizo ya akili ya mtu yanayotafsiriwa kama uchawi. Maana tushaambiwa Tanzania kuna watu wengi wana magonjwa ya akili hayajanyumbulishwa. Sasa tunajuaje haya nayo hayaingii humo?

Isije kuwa mtu ana kifafa cha aina yake hakijulikani vizuri, anaona double double mapicha ya kutisha, anajidhuru mwenyewe bila kujua, tunasema uchawi.
 
Wew jamaa cjajua ni dini gani ila naona tu hapo visomo na mashehe.. sasa basi nakushauri tafuta huu mwamba wa uzima YESU KRISTO hakuna tatizo lililoshindikana hapo upate tu sehemu sahihi..kua na imani..hakuna jina lingine chini ya mbingu wala popote liwezalo kuokoa zaidi yake..
 
unajua najiuliza mtu mpaka anapitia wakat mgumu kama huu na haon sululisho wakat ni jambo dgo sana hili, najiuliza ni kuwa spidi ya Yesu kutanganzwa duniani imepungua au watu wenye matatizo kama yako wanasikia lakini wanapuuza...?
.
nimegundua kuwa Yesu yupo kila mahali zaid ya robo tatu ya coment wamekwambia uende kwa Yesu na nauwakika mtaani ndio zaidi huwa unasikia habari za Yesu kuokoa watu.
.
Yesu alisema atakayekuikoa nafsi yake mwenyewe ataipoteza bali aipotezae nafsi yake kwa yeye(Yesu) ataokolewa.
.
uchaguzi ni wako..
 
Back
Top Bottom