Nchi hii hata watu wote wawe na Degree moja, haiwezi kuendelea

Nchi hii hata watu wote wawe na Degree moja, haiwezi kuendelea

Robert na. Ndiyo wale wanakimbiza moto nchi nzima Kwa Gharama kubwa huku wakishona mpaka sare za moto


Unanunua Ndege wakati watu hawana maji wala umeme.

Ungeweka kila nyumba iwe na maji na umeme alafu kila mwezi watu watalipia Huduma hizo kulingana na matumizi unafikiri ungekusanya Kodi kiasi gani?

Degree zinafundisha watu wawe Wabinafsi wapige 10 percent wajaze matumbo yao
 
Elimu haina tatizo na napingana na yeyote asemae kuna shida katika elimu, shida iko katika UBONGO wa mtu mweusi...

Jiulize Ni watanzania wangapi wamesoma nje ya nchi ambako kwa maelezo yako kuna mfumo mzuri wa elimu alafu Impact yao katika nchi iko wapi?
Hiyo ni argument ya kitoto sana,
Miaka mitatu ya kusoma nje ndio imfanye mtu awe na elimu?
Mtanzania definition ya elimu anapewa akiwa mtoto ni kuwa na maisha mazuri basi huko ulaya
wanaenda kutafata maisha mazuri sio elimu wangeenda kutafata elimu wangerudi wameelimika.
 
Hiyo ni argument ya kitoto sana,
Miaka mitatu ya kusoma nje ndio imfanye mtu awe na elimu?
Mtanzania definition ya elimu anapewa akiwa mtoto ni kuwa na maisha mazuri basi huko ulaya
wanaenda kutafata maisha mazuri sio elimu wangeenda kutafata elimu wangerudi wameelimika.
Hivi shule Kama IST hapa nchini wanatumia mitaala gani? Watu weusi hawasomi huko? Output yao katika nchi Ni ipi?

Usikurupuke, mtu mweusi ana matatizo...
 
Kwema Wakubwa!

Kwa tathmini zangu ninazoziamini kuliko kitu chochote kile. Nachelea kusema, nchi hii hata watu wote yaani wote milioni 60 tuwe na Degree moja moja na zaidi kamwe haiwezi kuendelea.

Kwa bahati nzuri Mimi ninayo hiyo degree hivyo ninachokiongea nakielewa vizuri Sana. Kama ningekuwa madarasa yangu ni madogo basi huenda ningeongea Jambo nisilo na Uelewa nalo.

Pengine naweza sema tena, nchi hii hata wote tungekuwa na PhD bado nchi hii isingeendelea.

Unajua Kwa sababu gani?

Sitaki kulijibu hili.
Lakini angalia wenye hizo degree mpaka maprofesa utaelewa nazungumzia Jambo gani.

Elimu tuipatayo ni Ile iliyopitwa na wakati,
Uliona wapi kitu kilichopitwa na wakati kikaendeleza nchi.

Elimu inayoua udadisi sio elimu,
Elimu inayofundisha ubinafsi sio elimu,
Elimu Inayomfanya mtu akariri badala ya kuelewa sio elimu,nilipokuwa nasoma degree nilikaririshwa mavitu ya watu wazamani mno ambayo Kwa akili ndogo tuu ningeweza kuayaeleza.

Embu assume ati uambiwe utoe maana ya istilahi "Lugha" au ueleze maana ya "mawingu" au ueleze Maana ya neno "udongo"
Mambo hayo ati mpaka umnukuu sijui Nani huko ambaye naye alitoa maana ya maneno hayo Kwa mtazamo wake.

Elimu za kidunia zinachekesha Sana. Yaani ukishindwa kuikariri maana hizo umefeli wakati huenda ukitoa maana yako ya kichwani ni Sawa kabisa na Ile Ile walioitoa HAO wahenga.

Elimu ya kunukuu watu waliopewa jina la utaalamu 🤣🤣🤣, elimu hii ndio inawafanya Vijana wasijiamini mpaka wapate mawazo ya watu wengine.

Unakuta liprofesa limepewa wizara serikalini, linatakiwa litoe maamuzi kuhusu Jambo Fulani ambalo kimsingi ni lawakawaida Sana. Yaani hata mtu ambaye shule hajaenda anaweza akalitathmini na kulitolea maamuzi. Lakini Kwa vile haiamini akili yake, utashangaa mpaka lifungue watu waitwao Wataalamu WA zamani huko, au aangalie nchi za Wazungu wamefanyaje.

Lini mtaweza kuzitumia akili zenu wenyewe enyi wasomi?"

Wasomi hawajiamini Kwa sababu wamefundishwa kutojiamini,

Kwa elimu hii tupewayo ukiwa na wasomi wengi basi jua fika kabisa taifa Lina idadi kubwa ya watu wasiojiamini, kwani shuleni ndivyo walivyofunzwa hivyo.

Kwa sasa hivi ni rahisi kumnyima haki msomi tena wa degree kuliko kumnyima mtu asiyesoma, mtu asiyesoma anatumia common sense yaani akili ya kuzaliwa tuu kujitetea na mazingira yake. Lakini wasomi wengi hawana hata hiyo common sense.

Msomi anasema Hana mtaji wa kuanzisha biashara lakini asiyesoma halalamiki hivyo,
Usoni imekaa mdomoni kuliko akilini huenda ndivyo walivyofunzwa.

Hata humu JF ati ili mtu aonekane Yuko na akili/ uwezo wake wakufikiri upo njema, utashangaa ati mtu akijifaraguza na kingereza ATI huo ndio usomi,🤣🤣🤣. Nacheka Kama MAZURI.

Msomi badala aumize kichwa kujua atatatua vipi changamoto ya Ajira iliyomo katika jamii yake yeye anakalia kulia Lia ati hakuna ajira. Pumbavu.

Degree nyingi zime-expire miaka mingi iliyopita.
Hazina tofauti na ngano au visasili vya Fasihi.
Labda iwe Kwa burudani tuu Kama Sanaa.

Elimu ambayo inamfundisha mtu Kumheshimu boss wake hata katika mambo ya Uhalifu uliona wapi elimu ya hivyo ikaendeleza nchi?

Elimu ambayo wasomi wanawategemea Wanasiasa 🤣🤣🤣 uliona wapi ikaendeleza nchi ndugu yangu?

Siku moja nikafanya utafiti huko kwenye vilinge Kwa waganga na waganguzi WA kienyeji, nikapata connection nyingi tuu nikikusudia kuchunguza mambo kadhaa.

Nikashangaa mpaka wenye degree wakienda Kwa waganga WA kienyeji🤣🤣🤣

Hivi degree hizi za kuamini waganga WA kienyeji ndio ziendeleze nchi hii, labda Kwenye ndoto.
Mtu na degree zake uketishwe Kwa waganga ati kujipatia Utajiri, sijui kupata kazi🤣🤣🤣 sijui kumfanya boss akuogope yaani vituko vitupu. Degree hiyo ndio iendeleze nchi hii. Thubutu!

Degree zilizofundishwa miujiza na maendeleo ya dezo, yaani maendeleo yanakuja kirahisi rahisi.
Nchi iendeleze na degree za wanaokimbizana kwenye maji ya upako Kwa hawa wajiitao manabii 🤣🤣🤣🤣.
Uende wakupe visakale vya wahenga wakiyahudi alafu ujifanye nawe utakuwa hivyo hivyo🤣🤣🤣.

Jamani tuache kudanganyana, hii nchi haitaendelea Kwa elimu hizi na Mchunguzi hata ipite miaka Buku.

Siku moja nilicheka kweli nimeona mtu aliyetengeneza Ndege ya kiwango cha chini Kabisa, walau yeye alitengeneza, nilipofuatilia elimu yake kumbe hata hajafika Kidato cha nne. Sasa wenye degree zao kuhojiwa wakaanza kunukuu sijui vifaa gani vya kitaalamu Kama walivyofundishwa huko vyuoni 😃😃😃.
Wewe na degree yako uprofesa wako umeshindwa kuunda hata baiskeli ya mabati ati unamkosoa mtu aliyeunda unda Ndege Kwa kuchanga vifaa mbalimbali sijui vya baiskeli, pikipiki au Gari.
Unamkosoa wakati wewe ukipewa walau Kama huyo wa aliyekimbia shule.

Nchi haitaendelezwa na wenye degree, wenye degree Hali zao nazijua, kwani Mimi ni mmoja wao.
Nje ya Ajira wengi wao ni Kama Masai bila some au rungu.

Aaargrrrrrrrhii!! Nilikuwa nataka kusema nini kwani?

Niishie hapa nasubiri povu la wenye degree.


Robert Heriel
TAIKON WA FASIHI
Kwa sasa Dar es salaam
Upo sahihi 100%

Eliminate yetu imeshindwa kabisa kusaidia Taifa hili. Hii leo Maprof huko vyuoni na kwenye research institutions wameshindwa kulisaidia taifa na badala yake 'wanajikomba' kwa wanasiasa kwaajili ya teuzi.

Hadi tutakapoacha kuamini ktk teuzi ndo tuishi, ndo utakuwa manzoni wa taifa letu kuinuka.

Wasomi wetu wanatufelisha big time
 
Hivi shule Kama IST hapa nchini wanatumia mitaala gani? Watu weusi hawasomi huko? Output yao katika nchi Ni ipi?

Usikurupuke, mtu mweusi ana matatizo...


🤣🤣🤣🤣

Ati mtu mweusi anamatatizo.

Ni kweli mweusi anamatatizo Kwa sababu anataka awaze Kama mtu mweupe, wakati yeye ni mweusi, anataka kufanya Kama mweupe wakati yeye ni mweusi.

Elimu haitamsaidia
 
Hiyo ni argument ya kitoto sana,
Miaka mitatu ya kusoma nje ndio imfanye mtu awe na elimu?
Mtanzania definition ya elimu anapewa akiwa mtoto ni kuwa na maisha mazuri basi huko ulaya
wanaenda kutafata maisha mazuri sio elimu wangeenda kutafata elimu wangerudi wameelimika.
Haya katika nchi za wazungu kuna watu weusi wengi wamepata Elimu kwa mitaala ya kule, nioneshe ni vitu gani vya kuonekana wamefanya katika jamii?

Akina Steve Jobs wanaweza kuanzisha kampuni Kama APPL kwenye Garage ya nyumbani tena hana Elimu ya Uhandisi, lakini mtu mweusi yake Ni Majungu, Uchawi, Uvivu, what a wasted race...!
 
Upo sahihi 100%

Eliminate yetu imeshindwa kabisa kusaidia Taifa hili. Hii leo Maprof huko vyuoni na kwenye research institutions wameshindwa kulisaidia taifa na badala yake 'wanajikomba' kwa wanasiasa kwaajili ya teuzi.

Hadi tutakapoacha kuamini ktk teuzi ndo tuishi, ndo utakuwa manzoni wa taifa letu kuinuka.

Wasomi wetu wanatufelisha big time


Mimi nawaoneaga huruma tuu, maana wengi hata hawaelewi elimu waliyonayo imelisaidiaje taifa, wanafikiri kuandika andika makaratasi ndio elimu hiyo
 
Hivi shule Kama IST hapa nchini wanatumia mitaala gani? Watu weusi hawasomi huko? Output yao katika nchi Ni ipi?

Usikurupuke, mtu mweusi ana matatizo...
Una draw conclusion based on generaliztion reasoning.
Tupe fact ya hicho unacho kisema utuambie na watu weusi walio ifanyia makubwa dunia wali-deviate vipi hiyo fact
kama ubongo wa muafrika unadefect.
Hata wakisomea wapi kama watoto mnawepeleka shule mkiwambia huko ndio watapata maisha
bora badala ya elimu focus yao itakuwa ni pesa tu.
 
Mi nikimuangalia dr Bashir na polepole tu, wanatosha kunifanya nikubaliane na wewe!
 
Haya katika nchi za wazungu kuna watu weusi wengi wamepata Elimu kwa mitaala ya kule, nioneshe ni vitu gani vya kuonekana wamefanya katika jamii?

Akina Steve Jobs wanaweza kuanzisha kampuni Kama APPL kwenye Garage ya nyumbani tena hana Elimu ya Uhandisi, lakini mtu mweusi yake Ni Majungu, Uchawi, Uvivu, what a wasted race...!
Huyo steve jobs umewahi soma kitabu chake chochote?
Au unaokoteza habari yule kaenda chuo, na baada ya kuacha chuo bado aliendelea kuiingia
class kusoma vitu alivyokuwa na mahaba navyo katika chuo hicho bora ulimwenguni.
Msingi mkuu wa elimu sio darasa ndugu yule alikuwa anajua maana ya elimu.
 
Una draw conclusion based on generaliztion reasoning.
Tupe fact ya hicho unacho kisema utuambie na watu weusi walio ifanyia makubwa dunia wali-deviate vipi hiyo fact
kama ubongo wa muafrika unadefect.
Hata wakisomea wapi kama watoto mnawepeleka shule mkiwambia huko ndio watapata maisha
bora badala ya elimu focus yao itakuwa ni pesa tu.
Wewe acha visingizio, Mtu mweusi ana matatizo full stop...

1.Mbinafsi na ukiwa mbinafsi naondoa asilimia 30% kabla hujawa mchawi.

Angalia Viongozi wako, hakuna anayewaza kuhusu vitukuu vya vitukuu vyetu vitaishije hapa, kila mtu anawaza leo, hakuna awazaye ya keshokutwa!

Hivi hata uongozi tu Ni wa kuwa na mitaala mingine?

Na akili za Viongozi wetu ndio akili zetu maana wao Ni taswira zetu...

Mtu mweusi bure kabisa...
 
Haya katika nchi za wazungu kuna watu weusi wengi wamepata Elimu kwa mitaala ya kule, nioneshe ni vitu gani vya kuonekana wamefanya katika jamii?

Akina Steve Jobs wanaweza kuanzisha kampuni Kama APPL kwenye Garage ya nyumbani tena hana Elimu ya Uhandisi, lakini mtu mweusi yake Ni Majungu, Uchawi, Uvivu, what a wasted race...!
hao kina Karl max na Enstein bila shaka hujui hata walikuwa weusi.
 
Kila siku watawala wanawaza kufanya yale yanawapa umaarufu wa muda mfupi ili wapate kura za wananzengo huku wakikipa kisogo kilimo chetu, sekta ambayo inaweza kutoa ajira nyingi na wana wa taifa hili kupata utajiri, kushiba, kuwa na akili timamu na kudhibiti magonjwa kwa kiasi kikubwa. Ardhi tunayo ya kutosha na yenye rutuba miongoni mwa nchi zilizo kusini mwa jangwa la sahara. Cha ajabu watawala hawataki kabisa kuliona hili na wakilifanya ni kwa hadaa tu ili wananzengo waendelee kuwa maskini ombaomba na kuburuzwa ktk chaguzi.

Mambo ni mengi ....
 
Huyo steve jobs umewahi soma kitabu chake chochote?
Au unaokoteza habari yule kaenda chuo, na baada ya kuacha chuo bado aliendelea kuiingia
class kusoma vitu alivyokuwa na mahaba navyo katika chuo hicho bora ulimwenguni.
Msingi mkuu wa elimu sio darasa ndugu yule alikuwa anajua maana ya elimu.
We jamaa Steve Jobs namfahamu nje ndani ebu tumuache, ebu fuatilia kampuni kama Toyota ama Nissan zilianzaje uje unambie...

Aisee ukiwa Mbinafsi=Mchawi huwezi kuwa na kiu ya uvumbuzi ambao ndo msingi wa maendeleo.
 
Wewe acha visingizio, Mtu mweusi ana matatizo full stop...

1.Mbinafsi na ukiwa mbinafsi naondoa asilimia 30% kabla hujawa mchawi.

Angalia Viongozi wako, hakuna anayewaza kuhusu vitukuu vya vitukuu vyetu vitaishije hapa, kila mtu anawaza leo, hakuna awazaye ya keshokutwa!

Hivi hata uongozi tu Ni wa kuwa na mitaala mingine?

Na akili za Viongozi wetu ndio akili zetu maana wao Ni taswira zetu...

Mtu mweusi bure kabisa...
Huko ulaya hayo mandeleo hajatokana na ngozi yao,
ni elimu tu.
Viongozi tulionao ni matokea ya elimu mbovu tuliyonayo na ndio wanaozalishwa najamii yetu.
 
We jamaa Steve Jobs namfahamu nje ndani ebu tumuache, ebu fuatilia kampuni kama Toyota ama Nissan zilianzaje uje unambie...

Aisee ukiwa Mbinafsi=Mchawi huwezi kuwa na kiu ya uvumbuzi ambao ndo msingi wa maendeleo.
Hahaha unamfahamu nje ndani?
Umesoma kitabu gani hicho kimekuaminisha hayo?
Huyo nimesoma vitabu vyake vingi kumhusu na bado siwezi kujiaminisha namjua huyo alikuwa ni true seeke wa eduction.
Huo uchawi ulaya kunahadi vyuo vinaufundisha sijui unaongelea uchawi upi?
Kama ni uchawi wewe ni mchawi namba moja unaleta imani zako ndio unataka iwe kweli
Tuambie ubongo wa mtu mweusi unauhusiano gani na uchawi na roho mbaya sio kuleta porojo.
kwa sababu najua hivyo vyote ni matokeo ya ujinga.
 
Back
Top Bottom