Uchaguzi 2020 Nchi imeamka ikiwa na huzuni kubwa sana, Kwamba wabunge wote Bara 100% wameshinda wa CCM

Uchaguzi 2020 Nchi imeamka ikiwa na huzuni kubwa sana, Kwamba wabunge wote Bara 100% wameshinda wa CCM

Hii inawezekana.

Kwakua waliojitokeza kupiga kura walikua wachache mno. Unaenda kupiga kura unakuta askari wapo kwenye difenda wanapiga stori, hakuna wa kumkamata wala kutuliza vurugu.

So inawezekana hivyo kwamba wamepita ndiyo ila wachaguaji walikua wachache. Kuingiza watu barabarani? Mwitikio wa watu kwenda barabarani utatoa picha kama kweli wapinzani walipigiwa kura nyingi za kustahili ushindi ama la..
Sio rahisi, kihivyo
 
Ila wapinzani nao wametia dosari sana hasa kile kipindi wanatoka bungeni na kususia vikao wananchi nasi tunachoka na njia hii ya kususia, tunawachagua wa kututete bungeni wao wanatoka bungeni

Akili kama hii ndio tatizo la nchi hii. Kwani hata waliobaki waliufanyia nini mpaka ukajiona ni bora leo kuliko mwaka 2014?? Hujui hata nyakati tulizopo, mbunge wa upinzani hawezi kuizuia kufanya chochote serikali kwa aina ya katiba tuliyonayo. Kimsingi, Bunge haliwezi kuizuia serikali kufanya chochote.

Nikukumbushe tu, bajeti na sheria kwa katiba yetu hupangwa na kutungwa na serikali na kuja kujadiliwa na kupitishwa na Bunge. Nchi wa wenzetu, Bunge ndio huwa chanzo cha matumizi na sheria. Serikali hutekeleza tu!!

Siko katika siasa lakini hata Bunge likiwa ni CCM tu, hakutaboreka kitu. Sana sana utaudhiwa zaidi kuliko ulivoudhiwa na habari ya wabunge wa upinzani kutoka nje. Watch my words!!
 
Msisingizie wïzi, maneno ya jpm na majaliwa ktk kampeni kuwa raia wanajichelewesha wenyewe na wao jpm na majaliwa wanataka connection ndio maneno chachu kwa wananchi. Wànanchi wamechagua maendeleo.

Mengine ni visingizio, ktk mkutano wa mbowe hai wananchi wa haî wanampiga maswali mazito mbowe anasingizia wametumwa, hii ngoma wapizaní wamelala. Watumie muda huu kujipanga.
Kwa bungeni ni upinzaní gani tutaumiss zaidi ya kugomea bajeti?

Màjimboni ni nini tutamiss wàkati hawajawã na mchango?
Tusikariri kuwa piga ua lazima wawepo wapinzani mia bungeni, zîto amekua na hoja zaidi ya wabunge wote wa upinzani.
 
Na uwezekano wa maandamano ni mdogo sana nchi hii labda sijui
Hapa kete kwa wapinzani iliyobaki ni kwenda kuishataki tume kwenye taasisi za kimataifa nchi ipigwe vikwazo,inyimwe misaada tuimbe wimbo mmoja
 
Kwa tulioshuhudia uporaji wa uchaguzi na wizi wa kura wa mchana kweupe, tutegemee kishindo kikubwa siku za usoni.
Time will tell
Sikuzote wanalalamika kuhusu wizi ata kama hakuna
 
2020/ 2025 itakuwa ni speed ya kimbunga kuhusu maendeleo ili wananchi waone kabisa upinzani ulikuwa unatuchelewesha
Ili 2025/2030
Wananchi wafanye mabadiliko ya katiba Tanzania iendeshwe kama China hakuna siasa wala kampeni Magu piga kazi mbaka sisi wenyewe tukuchoke tukwambie sasa nenda Chato kapumzike..
 
Mkuu Pagan Amum, ukweli lazima tuukubali na kuuheshimu kwama viongozi wa vyama vya upinzani, hasa wawakilishi wetu, hawakutenda kama tulivyowatarajia, katika kipindi cha utawala wa Serikali ya CCM.
√ Walipinga juhudi za maendeleo wakidai ni maendeleo ya vitu;

√ Mbaya zaidi walitumia lugha ya matusi, tuhuma za uzushi na kuhamasisha vurugu wakati wa kampeni; na
√ Isitoshe vyama vya upinzani, hasa CHADEMA, chama kikuu, na ACT-Wazalendo, viliwekeza nguvu zao zote kwenye wagombea Urais, ambao walishindwa kuwashawishi wapiga kura kwa hoja za kisera.

Kama ulivyosema afya ya kisiasa siyo nzuri sana uwakilishi kuwa wa chama kimoja cha siasa. Lakini kumbuka, CCM ina jinsi nzuri ya uendeshaji kudhibiti na kusimamia utekelezaji wa Ilani yake ya Uchaguzi kuliko vyama vingine vya siasa, ambavyo viongozi wake wamekuwa wakishutumiana kwa matumizi ya ruzuku na mali za chama
 
Ila wapinzani nao wametia dosari sana hasa kile kipindi wanatoka bungeni na kususia vikao wananchi nasi tunachoka na njia hii ya kususia, tunawachagua wa kututete bungeni wao wanatoka bungeni
Bado una akili fupi za kitoto sana kisiasa.
Fuatilia mabunge ya kidemokrasia duniani ndio utajua wabunge hufanya nini. Usikaririshwe ujinga kuwa eti mbunge kukaa ndani ya bunge ndio kukutetea!

Kutoka nje bungeni ni njia mojawapo ya kuwatetea watu kwa kuonyesha kutokukubaliana au kutokuridhishwa na mwenendo wa kibunge juu ya jambo fulani.

Katika mabunge ya jumuiya ya madola, wabunge wanaweza kushinikiza hoja zao kwa njia mbalimbali, ikiwemo kutoa hoja, kupiga kura, kushangilia, kuzomea, kupiga kelele, kutoka nje nk.

Mkiona hoja zenu hazipewi nafasi, kura zenu haziwezi kutosha na kupiga kelele hakutoshi, basi kususia kikao na kutoka nje ni njia muafaka.
 
Sasa unalia nini, wajumbe (wananchi) wameamua kuwa Tanzania si nchi ya mashoga....tunataka utawala bora utao peleka nchi yetu mbele zaidi. We unafikiri Chadema ingetupeleka wapi kama si kutubagua watanzania? Kile ni chama cha kikabila, hakikufai wewe wala mimi.
 
Back
Top Bottom