Ndege ya Rais yawasili tena Dubai ikitokea Dar es Salaam usiku huu! Kunani Dubai?

Atakuwa kaenda kukamilisha dili na waarabu maana leo redioni kwenye kipindi cha magazeti nimesikia bodaboda, bajaji, mama lishe wameandamana wakiunga mkono uwekezaji wa bandari na kwamba mwekezaji aje kuanza kazi pasipo kuchelewa, nchi ishakuwa saccos hii.​
 
Duh...!. haya mambo ya maximum transparency haya, mtu hata kwenda vakesheni tuu ujombani, kila mtu lazima ajue!. Mambo gani haya sasa?.

P
 
Mambo yamekuwa rahisi sana siku hizi, watu wanamtrack hadi mkuu wa nchi 😁

Anyway, huenda ndege imeenda matengenezo Dubai 😂😂😂, nimewaza namna "msemaji wa ndege ya rais" anavyojiandaa kulitolea ufafanuzi hili...
 
Wampe hata kandege kazuri basi…
Ile gulfstream ni ndege nzuri sana kama private jet. Kikwete alikuwa anapiga nayo safari za mbali kutoka Tanzania hadi New Zealand non-stop, kesho yake mke wake anakwenda Brazil nonstop. Kumbuka Mramba alisema angalau watanzania wale nyasi ile Gulfstream inunuliwe! Tatizo ni kwamba Tangu Magufuli alipoleta maboeing, mairbus na mabombadier ndipo ikaonekana kuwa haitoshi. Mwanzoni mwa utawala wake Mama Samia alikuwa kama amejimilikisha Airbus moja ambayo alikuwa anatumia kwa safari zote hata za ndani.
 

Anhaa
Nimekupata mkuu
 
Nyie ni kama bundi mara mseme Iko Saudia siku ya 8 Sasa mara Iko Oman mara saizi mnasema Iko Dubai yaani ni upuuzi tuu.

Tafuteni wajinga wenzenu ndio muwe mnaambizana huu utoto.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…