Ndoa na Mirathi: Nafasi ya Mahakama ya Kadhi kwa Wanawake

Ndoa na Mirathi: Nafasi ya Mahakama ya Kadhi kwa Wanawake

Status
Not open for further replies.
Baharia unampongezaje Zitto wakati Cigwiyemisi anaipigia chapuo? Cigwiyemisi si ndo Jumanne ama?
 
ni kweli wabunge waliacha taifa pembeni na kuanza kutetea imani zao ilikuwa ni aibu tupu na ukosefu wa uzalendo
 
NYC kiukweli kuna haja ya kutoa ufafanuzi how did it happen la 2changie kishabiki na hapo dhana ya great thinkers itakuwa imeminywa walajii...!wawaha watezhaga mwana mgoli komuwona kulibululu.lece ukamu wanzhe kijela kulibululu alayo...!
 
alietia aibu kuliko wote alikuwa Mwakyembe.....kwa mwalimu wa sheria kuongea utumbo aliongea ilikuwa aibu sana

alizungumza kama muwakilishi wa makanisa na sio mtaalamu wa sheria wa kuaminika.......sikutegemea kabisa
nilikuwa namheshimu mno Mwakyembe until siku hiyo......
 
Black Rose,
haki ninayoisema hapa, ni kwakuwa Waislam ni significant portion ya Wananchi wa Tanzania, wanavuja jasho na kuilipa kodi serikali, basi wana haki ya kugharimiwa kwa kiasi fulani katika shughuli zao za kijamii Kama wanavyofanyiwa wakristo wanaopewa mabillioni yatokanayo na kodi zetu sote, kwani hoja kuu ya Wakristo kukataa Mahakama hii ni kigezo cha gharama, as if kodi zote za serikali zinalipwa na Wakristo peke yao. Tukisema tuhoji uhalali wa mapato ya serikali, basi tutadumaa, kwa maana itabidi Waislam itabidi wote waache kazi serikalini, Kwa maana mishahara yao inatokana na vyanzo visivyo halali, tukatae huduma zote za serkali kwa sababu vyanzo vya mapato yake vingine si halali. Ndiposa nikahoji kwani sadaka na michango yote ya kuendesha na kujenga misikiti uhalali wake tunaujua? Kwa kuwa nchi yetu Ina interaction ya dini mbalimbali, basi Allah ni mwenye kuelewa zaidi na ni mwingi wa kusamehe na wala si mwenye kuikalifisha nafsi ila kwa jambo inaloliweza, na atatuhukumu kwa dhamira zetu na wala si kwa udhaifu wetu tu. Nia ya kutaka serkali igharimie kwa kiasi fulani ni kutaka kupunguza uzito wa gharama kwa watakaohitaji haki zao katika mahakama hiyo, hasa wanawake, waweze kuipata kwa gharama ndogo, hivi kweli BR huwaoni wajane walioolewa ndoa za kiislam wakafiwa na Waume zao wanavyodhulumiwa kwa kufukuzwa majumbani mwao, wakanyang'anywa kila kitu, wanatelekezwa na watoto mayatima, ndugu za mume wanafanya hivyo kwa kisingizio cha mila na desturi, State Courts ziko so corrupted asipokuwa na fedha za kutosha hataambulia kitu. Haki za mjane wa Kiislamu ni nyingi sana, sio ile thumni peke yake, bali inaanzia kwa Mali alizopewa na mumewe enzi ya uhai wake, maskani yake katika nyumba aliyoishi na mumewe, sustainance yake kipindi cha eda, custody ya wanawe aliozaa na marehemu, haki za wanawe ambao bado ni wadogo kujimiliki wenyewe nk nk, it's a very complex issue, state laws zilizopo hazikuSubstanciate haki hizi, badili yake zimeImply tu kuwa sheria za ndoa na mirathi za Kiislam zikubalike kwa waumini wake, matokeo ni kuwa Mahakimu wengi hawazijui sheria hizo, wengi wanaishia kutumia state laws pekee, na hivyo kuwakosesha haki waislam wengi, wake kwa waume, ndo maana ikadaiwa mahakama ya kadhi.
 
Le Mutuz nakuunga mkono kumpongeza kamanda na wote waliopingamahakama ile ya kadhi.
 


Bold Nyeusi:
Hebu fafanua zaidi muktadha wa hiyo haki.

Nimejaribu sana kudodosa kuhusu hii MoU inayojadiliwa, bahati mbaya sijapata nakala yake.Nilichopata kutokana na kauli ile ya Mh.Rais ni kama vile waislam nao hawajakatazwa kusaini MoU na Serkali.Sasa kama milango iko wazi, kwanini hatutumii hiyo fursa na badala yake tunalumbana tu?

Binafsi ninavyoona, hatujachelewa.Tujaribu na kama tutaona hatusikilizwi na Serikali basi tudai "haki" hiyo kwa nguvu zote. Kwani ni ajabu serikali kusaini MoU na taasis nje ya serikali? Nadhani tunge explore options zote ndipo tudai support kwa lazima.

Bold Nyekundu: Mbona unanikwaza ? Nikidhani madai ya mahakama ya Kadhi ni kusudi tukamilishe ibada. Toka mwanzo nimekuwa nauliza " moral legitimacy " ya kudai mahakama ya kadhi na baadhi ya wachangiaji ( eg Topical na wengine) wakajibu ni kusudi kukamilisha matakwa ya Sharia.Sasa kama tutakuwa hatujali vyanzo halali vya mapato au mafungu ya kuanzisha nadhani tunakosa uhalali ule wa mwanzo.Tukichukua njia hiyo, tutadhihirisha hakika kwamba nia ya kuanzisha hivi vyombo ni "kukomoana" na siyo ibada.Tutakuwa tuna defeat argument yetu ya mwanzo.Nadhani lets stick to arguments zetu za "uhalali".Tusichanganye MoU for social services,ambazo zinaruhusu kuhudumia watu wa imani zote na establishment ya vyombo purely vya waislam.

Bibie,

Na wewe umeshaingia kwenye mtego wa wakristo kwamba MoU yao ni for social service, kuna variations kubwa sana katika meaning of social services??

Kwanza, Nitaeleza mimi nina own private hospital hapa Dar (private nimeajiri madaktari wazuri); tunatoa services bila kujali dini, kwa mantiki hii hospitali yangu haina tofauti yeyote katika kutoa service na hospitali ya kanisa (project) ni project kama yangu..ukizingatia bei charges e.g. diagnosis fee, consultation fee ziko sawasawa na za kanisa..ukitumia logic hiyo mimi nastahili ruzuku kutoka serikalini??? hivyo hivyo miradi ya kanisa iwe chuo au hospitali haina tofauti yeyote na project kama yangu hawastahili ruzuku hata kidogo. kwa hiyo madai ya waisalmu ni halali kwakuwa priority ya muislamu siyo biashara (kama kanisa) bali ni ibada kwanini asisaidiwe kutoka kwenye hazina ya serikali??

Pili, mtego mwingine ambao umeingia ukawa sawa na wakristo ni "kufikiri kuwa mahakama ya kadhi" ni kukomoana..hayo ni maneno ya kijahilia ambayo wanasema kuwa mahakama za kiislamu zinanyanyasa wanawake..sidhani kama uko sahihi kwenye hilo..

tatu, Kwa vigezo vyote vya kimantiki na ki-operation mahakama ya kadhi lazima kwanza itambulike kisheria (kikatiba), pili lazima iwe funded na serikali kwa kuangalia kesi ngapi zimeshughulikiwa na mahakama ya kadhi; kwa hiyo serikali inatakiwa ku-etablish kesi moja ina cost average ya shilingi ngapi kwenye mahakama zake?? hiyo itakuwa vey just way ya kutumia pesa za umma kwani kwani mahakama ya kadhi itakuwa imefanya kazi ambayo ingefanywa na mahakama zetu sasa hivi unaona logic bibie??
 


MgungaMiba,

..kuna thread ambapo nilitoa wazo kama lako, kwamba Waislamu waanzishe mahakama ya Kadhi halafu waandikishe MOU na serikali ili iweze kupata funds za kuiendesha.

..sasa kuna wachangiaji Waislamu walipingana na hoja hiyo wakidai kwamba ni lazima mahakama ya KADHI itumbukizwe ktk KATIBA ili hukumu zake ziweze kuwa enforced na DOLA.

..ukitumbukiza mahakama ya Kadhi ktk katiba basi hata wasio wa Islamu wanakuwa na mamlaka ktk kuamua utendaji kazi wa mahakama hiyo. ukizingatia kwamba Waislamu wanadai mahakama hiyo ni sehemu ya IBADA nadhani suala hilo linaweza kutuletea mtafaruku mbele ya safari.

Bila kutambilika kisheria (kikatiba) itakuwa sawa na bure..it does not work; its option but must be legal siyo vinginevyo
 
- People hivi karibuni nilipata bahati ya kuongea na Kiongozi mmoja Mkuu sana wa Serikali ya sasa. Tulikuwa tunajadili ishu ya Mahakama ya Kadhi.

- Mkuu akanielezea jinsi maajabu makubwa yaliyotokea Bungeni ishu ilpolepelekwa, I mean for the first time Wabunge wakawa hawana Vyama na very emotional anasema upande mmoja kulikuwa na Missanga na Mundhihir na the CUFs na huku kuna Mwakyembe na wengine!

- Anasema ilikuwa ni Mh. Zitto bila kujali Dini yake, aliyeokoa jahazi, kwa kweli kwa hilo Mungu akuzidishie sana Mheshimiwa na you have my respect.

MUNGU AIBARIKI TANZANIA!

Le Baharia William @..New York City, USA

Wabunge walikuwa very emotional kwasababu ya udini??

Wakristo wabunge hawataki mahakama ya kadhi (udini)

Waislam wabunge wanataka mahakama ya kadhi (udini)

Kwa ufupi anayekataa kwamba hakuna udini analea ugonjwa ambao utatuumbua siku si nyingi..
 
alichofanya Zitto ilikuwa ku play 'smart politics' tu
yeye ana ndoto za kuwa 'Rais' hapo baadae
asingeweza kuunga mkono wala kupinga jambo linalowagawa watu
while yeye anataka wote wamuone 'anafaa' kwa kuongoza....
Zitto hakusema anapinga wala kuunga mkono.....
alifanya siasa na kujiweka pazuri na leo mmeanza kumsifia....imelipa naona..
 
alichofanya Zitto ilikuwa ku play 'smart politics' tu
yeye ana ndoto za kuwa 'Rais' hapo baadae
asingeweza kuunga mkono wala kupinga jambo linalowagawa watu
while yeye anataka wote wamuone 'anafaa' kwa kuongoza....
Zitto hakusema anapinga wala kuunga mkono.....
alifanya siasa na kujiweka pazuri na leo mmeanza kumsifia....imelipa naona..

We call identity problem??? hajui anataka nini au anaamini nini??
 
alietia aibu kuliko wote alikuwa Mwakyembe.....kwa mwalimu wa sheria kuongea utumbo aliongea ilikuwa aibu sana


Unacheza na Pollonium 236?? akamuulize Alexander Litvinenko alivonyonyoka nywele ila ye alipewa 210 tu na KGB..hawa LTK wame muoverdose huyu
 
alichofanya Zitto ilikuwa ku play 'smart politics' tu
yeye ana ndoto za kuwa 'Rais' hapo baadae
asingeweza kuunga mkono wala kupinga jambo linalowagawa watu
while yeye anataka wote wamuone 'anafaa' kwa kuongoza....
Zitto hakusema anapinga wala kuunga mkono.....
alifanya siasa na kujiweka pazuri na leo mmeanza kumsifia....imelipa naona..

Kama ndivyo basi ana hali mbaya sana kwani Watz washaamka na wanaweka na kujua kila jambo linatokea kwa wakati huu na manufaa ya baadae.Zitto yupo smart but he zn smarter.Ila kwa alichokiifanya na kuweka msimamo wake kuhusu mahakama ya kadhi anastahili pongezi.
 
Zittos haters yaani you cant help yourselves mko very emotional na blind damn!

Kwasababu ana identity problem

Wanachadema hawamuamini kwasababu kama vile yuko ccm

Kwenye mahakama ya kadhi hajulikana yuko upande gani (yupo yupo)
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom