William J. Malecela
R I P
- Apr 27, 2006
- 26,584
- 10,400
Mwakalinga sawa Bro tupo wote One page Mkuu! SALUTE!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Zittos haters yaani you cant help yourselves mko very emotional na blind damn!
BR,
Ukichukulia mantiki ya kuwa Serikali fedha zake ni haramu kwa hiyo hazifai basi usitembee barabarani, usilipe kodi, usitake jambo lako lolote la kiserikali ufanyiwe nao. Hiyo ni kitu haiwezekani.
Inatakiwa hizo hizo fedha nasi tupewe au kusiwe na misaada yoyote kutoka Serikalini kwenda taasisi za kidini. Na sisi tunapiga hesabu za walipa kodi Waislaam, ikiwa watatupa zaidi ya hizo basi tutazirudisha, lakini wakitupa chini ya fedha ambazo tunalipia kodi, tunajuwa fungu letu linatoka kwenye fedha yetu ya halali.
Bibie,
Na wewe umeshaingia kwenye mtego wa wakristo kwamba MoU yao ni for social service, kuna variations kubwa sana katika meaning of social services??
Kwanza, Nitaeleza mimi nina own private hospital hapa Dar (private nimeajiri madaktari wazuri); tunatoa services bila kujali dini, kwa mantiki hii hospitali yangu haina tofauti yeyote katika kutoa service na hospitali ya kanisa (project) ni project kama yangu..ukizingatia bei charges e.g. diagnosis fee, consultation fee ziko sawasawa na za kanisa..ukitumia logic hiyo mimi nastahili ruzuku kutoka serikalini??? hivyo hivyo miradi ya kanisa iwe chuo au hospitali haina tofauti yeyote na project kama yangu hawastahili ruzuku hata kidogo. kwa hiyo madai ya waisalmu ni halali kwakuwa priority ya muislamu siyo biashara (kama kanisa) bali ni ibada kwanini asisaidiwe kutoka kwenye hazina ya serikali??
Pili, mtego mwingine ambao umeingia ukawa sawa na wakristo ni "kufikiri kuwa mahakama ya kadhi" ni kukomoana..hayo ni maneno ya kijahilia ambayo wanasema kuwa mahakama za kiislamu zinanyanyasa wanawake..sidhani kama uko sahihi kwenye hilo..
tatu, Kwa vigezo vyote vya kimantiki na ki-operation mahakama ya kadhi lazima kwanza itambulike kisheria (kikatiba), pili lazima iwe funded na serikali kwa kuangalia kesi ngapi zimeshughulikiwa na mahakama ya kadhi; kwa hiyo serikali inatakiwa ku-etablish kesi moja ina cost average ya shilingi ngapi kwenye mahakama zake?? hiyo itakuwa vey just way ya kutumia pesa za umma kwani kwani mahakama ya kadhi itakuwa imefanya kazi ambayo ingefanywa na mahakama zetu sasa hivi unaona logic bibie??
Usinchekeshe!
Ina maana waislam watanzania wao hawajiwezi hadi kuchangiwa? Hebu usituangushe.
Mtumai cha ndugu si hufa maskini?Mahakama ya kadhi tunachoionea mashaka ni kama itaweza kumaliza matatizo ya "kifikra' kwa wanaume wa kiislam hasa kwenye Ndoa.Huu umaskini uliokithiri utamalizwa vipi na hii mahakama? Tatizo ni umaskini wa fikra na mapato unaochangia wanawake wa kiislam kunyanyasika.Salma2015 kauliza maswali ya msingi na hakuna hata mmoja kaweza kujibu hizo hoja.Wanawake wa kiislam hawana tatizo na maagizo ya Kuran au ya Mtume.Wasiwasi ni utendaji kuanzia waumin wenyewe hadi watakaosimamia hizo mahakama.Enyi wanaume, mjue mnatuharibia ibada zetu kwa tabia zenu.Mnalazimisha wanawake wawe na tabia zisizoendana na Uislam kwa vile nyie hamtimizi maagizo.Mnabebesha wanawake mizigo mizito ya "hasira, wivu, chuki" ukiacha mingine ya familia . For you the intellectuals I would confidently say that
Ndoa kwenye uislam ni ibada.Allah kamuumba "mwanamke" kwa "mwanaume" waishi kwenye ndoa kwa lengo la kuwepo amani, utulivu, raha na faraja.Hivyo basi ndoa inatakiwa izae AMANI NA RAHA.Hii itawezekana kupatikana kama tu wote wanatimiziana wajibu unaowapasa vinginevyo kutakuwa na magomvi yatakayoharibu amani, utulivuna hatimaye kuharibu ndoa (Rejea Kur.30.21).Wanaume mmepewa onyo mkaambia Muogopeni Allah kwa jinsi mtakavyoshi na wake zenu, kwa sababu mumewaoa kwa trust ya Allah! Sasa kama nyie hata hili Onyo hamlizingatii, mnaweza kuwa na uhalali kudai mahakama ya Kadhi ili ati iwaamulie mambo ya ndoa?
Haya hili la Polygamy nalo ni suala lenye utata.Uislam umeweka msisistizo mkubwa kwa haki za watu - mume mke, na pia zile za Muumba.Kufuatana na Uislam,mke ni life partner and not a robot or husbands property that can be put out of commission or replaced at any time without any consideration, concern, shame or feelings!Uislam haumpi mwanaume yeyote yule a right to have more than one wife nor considers it is an act of piety.
Mtume mwenyewe alikuwa na mke mmoja tu for about twenty five years kabla ya kuoa wengine,na alimuoa huyu mke akimzidi mtume kwa miaka 15 years.Pigeni mahesabu ndipo mtambue "tamaa" haikuwa sababu ya msingi ya Mtume kuoa zaidi ya Bi Khadija. Hivyo basi kinyume na wanavyodhania wanaume wengi wa kiislam, monogamy is a norm and polygamy a rare exception in Islam. Kuhusisha dini na polygamy ni upotoshaji wa makusudi wa wale wenye kueneza huo utaratibu wa kuoa wake wengi.
Dini ya Kiislam ni dini ya haki kwa wote na siyo a smoke screen to deceive anyone and or hide behind it to protect personal desires or lust. Wanaume wengi wa Kiislam wanajitafutia uhalali wa vitendo vyao kwa kutumia verses za Kuraan conveniently and selectively bila kusoma ayah kamili na kuwa na uelewa wa kutosha. Ayah inayozungumzia kuoa zaidi ya mke mmoja ina context na imeelezwa uzuri kabisa: Marrying more than one wife was revealed after a battle in which many Muslim men were killed leaving behind helpless widows and orphans. The entire ayah (verse) of Surah (chapter) An-Nisa (The women 4:3), where Allaah The Almighty says; And if you fear that you shall not be able to deal justly with the orphan-girls, then marry other women of your choice, two or three, or four, but if you fear that you shall not be able to deal justly with them, then (marry) only one .
Sasa nyie wanaume wa Tanzania, miaka hii mna sababu gani zaidi ya tamaa zenu kuoa zaidi ya mke mmoja?
kila nikisoma post zako hapa nabaki kukuonea huruma tu..hauna pakutokea leo!
Hivi niwaulize.. kwa nini kila siku hapa lazima mtafuta mada inayohusu Waislaam wakati hakuna mada hata moja inayowahusu Wakristu... swala la Mahakama ya Kadhi mnalijengea ngome kana kwamba sijui waislaam wamewafanyia kipi tarabi. Nyie mchome misahafu, muwavue Hijabu wanawake zetu, mtuite dini ya mashetani, nchi zao zivamiwe na wakijilinda wanaitwa magaidi ili mradi basi Uislaam umekuwa tishio kubwa sana ktk maisha yenu maanake sioni mkiwafuata wahindu, Mabudha isipokuwa waislaam tu popote walipo..
Heee! Halafu tukisema Ukristu ni imani ya WATU mnachukia maanake sidhani kama hili lipo ktk biblia kwani nijuavyo biblia inasema mpende jirani yako kama unavyojipenda wewe...Je, haya ndio mapenzi yenyewe kweli....Ama kweli mafuriko yanatokea sii kwa bahati mbaya tumezidi roho mbaya!
Kama nilivyokwisha sema, MoU NI ISHU NJE YA HII MADA.Haihusiano na uanzishwaji wa mahakama za Kadhi.
Kwenye suala la mahakama ya Kadhi, nachukua msimamo wa Serikali ambapo MH.Rais, na viongozi wengine wa Serikali waliojadili na kuona busara ni kuachia suala hili liwe mikononi mwa Waislam wenyewe.
Kwamba naingia mtego wa wakristo, sijui kama ninauingia.Nina akili yangu timamu, nina uelewa wangu na pia ninatetea kile ninachoamini hata kama kitakuwa tofauti na wengine.
Kuna mwanazuoni mmoja aliwahi kusema kuwa, kama wote tutafikiri sawa, basi kuna ambaye hafikiri bali anadandia fikira za wengine.
Tatizo Mkandara ndugu yangu ni chuki na husda hamna lengine au kwa jina lengine Islamiphobia na Mswahili syndrome zinawasumbua achana nao. Mie siku hizi nimeacha kuchangia JF kwani I am wasting my time watoto wamekuwa wengi na watu wenye chuki bora niwe msomaji tu
kila unapozungumzia Mou huwa sioni point ya msingi zaidi ya mashindano ya kitoto...yani unachopigania kila siku ni 'hatukubali wanyang'anywe ili tukose wote' na sio inabidi na sisi tujipange tupate.
...........kwa hiyo hatutakaa kimya wakati kanisa linadhulma hela zangu BIG NO..tutapiga kelele kama ambavyo tunapiga kelele kuhusu RICHMOND na EPA..
Swadakta ni fardhi kuwa na mawazo na fikra tofauti lakini yote yakiwa na lengo la kujenga na si vinginevyo..
Swala la MoU linajirudia kwakuwa wenzetu (wakristo) na hata msimamo wa serikali kwa sasa unasema waislamu waanzishe wenyewe kisa wanaogopa "financing scheme and its legality" MoU ni precedent tosha kwamba serikali inaweza kufinance shughuli za kidini..ok
Sasa wewe tueleze how can mahakama ya kadhi become legal and how will it be financed??
Besides we have moral authority kudai serikali i finance mahakama ya kadhi kwasababu kazi ya hakimu wa kadhi courts ingefanywa na hakimu wa serikali sasa unaone hii ni goverment responsibility kuna shida gani serikali i-kiestablish average cost per case na wakawapa kadhi courts funds according to the number of cases???
Pamoja na kwamba unamawazo tofauti lakini umeegemea upande wa adui ambaye Allah "alishasema hawatakuwa radhi na waislamu hadi tuache kufuata amri zake".
Hivi niwaulize.. kwa nini kila siku hapa lazima mtafuta mada inayohusu Waislaam wakati hakuna mada hata moja inayowahusu Wakristu... swala la Mahakama ya Kadhi mnalijengea ngome kana kwamba sijui waislaam wamewafanyia kipi tarabi. Nyie mchome misahafu, muwavue Hijabu wanawake zetu, mtuite dini ya mashetani, nchi zao zivamiwe na wakijilinda wanaitwa magaidi ili mradi basi Uislaam umekuwa tishio kubwa sana ktk maisha yenu maanake sioni mkiwafuata wahindu, Mabudha isipokuwa waislaam tu popote walipo..
Heee! Halafu tukisema Ukristu ni imani ya WATU mnachukia maanake sidhani kama hili lipo ktk biblia kwani nijuavyo biblia inasema mpende jirani yako kama unavyojipenda wewe...Je, haya ndio mapenzi yenyewe kweli....Ama kweli mafuriko yanatokea sii kwa bahati mbaya tumezidi roho mbaya!
Wapi wewe Topical umepiga kelele kuhusu RICHMOND na EPA .
Nii vizuri usipoteze hii mada . Maana sasa unaonekana kutaka kuigemeza kwenye MoU ya Kanisa . Kuhsus "wenzenu" wakristu eti wanaogopa financing scheme sio kweli. issue ipo Kisheria.
Nilikuuliza swali kwenye therad yao ya "only intellectual " Je Wajaruo na wahatya na makabila mengine wakitaka au kuomba Sheria zao za mirathi ziingizwe kwenye mfumo wa Mahakama kuu ya Tanzania wewe kama ,mwanasheria mkuu uko tayari kumshaurii Rais akubali ? Ukajibu Its wrong kulingansha Uislam na wajaruo au wahaya. Nilitegemea mtu anayetetea kitu hicho aseme sawa tu hakuna shida
Lakini msipoteze hii mada ili tujifunze n kuelewa zaidi lakini issue ya kadhi sio cost issue ni ya sheria zaidi . Na hii mada imeletwa kwenye siasa mhhh tuone
Jibu linabaki lile lile kuwa huwezi kulinganisha hukumu za kihaya na kiislam??
a. Uislamu hauna kabila ni dini ya kabila zote na rangi zote
b. unaweka assumptions (wakiomba) kwa hiyo hiyo line of thinking siyo sawa) ..hawajaomba pengine hawataomba hadi milele kwasababu ni codified rules, no followers unlike ISLAM.
c. uislam ni dhambi kutohukuhukumiwa kwa mujibu wa Qur'an sidhani kama ni dhambi kutokuhukumiwa kihaya??
a. Uislamu hauna kabila ni dini ya kabila zote na rangi zote
Na Wala kabil halina dini. Vile vile Ni kosa kusema usilam ni dini ya Kabila zote Uislm ni uislam ma ulivyo ukristo .Uhaya , Uzaramo, Unymwezi ni kabila .So dini na bola Hizi ni demgrphic defition tfauti kabisa. hauna kimoj kiko ndani y ingine
Na kama kimoja kuwa ndani ya kingine basi ni utmaduni wa kabila ndio unameza dini Ndio maana utaona kwenye dini zetu kuna vitu watu tunafanya au kufuata n kuyaishi lakini ni utaratibu ulitokanana na utamduni wa makbila fulani na sio dini. Naturally kba hujawa muislam, Mrstu unakuwa mnyamwezi, mzaramu msambaaa.
b. unaweka assumptions (wakiomba) kwa hiyo hiyo line of thinking siyo sawa) ..hawajaomba pengine hawataomba hadi milele kwasababu ni codified rules, no followers unlike ISLAM.
Nakuuliza tena wewe kama mwanasehria Mkuu wa serikali wajaruo wanakuja na hoja sheria zao ziingizwe kwenye mfum wa mahaka y serikali. Utamshauri nini Rais. Toka wenye kona ya imani yako toa jibu la ki intelectual la kisheria la kitaifa .Ni wazi jibu utakalo toa ukiacha ushabiki halitofautini na lile alilotoa JK.
Makabila yetu hayaitaji followers unlike dini. Makabila Ni natural. Mimi nazunguza kabila langu na sijafundishwa darasani. kam niivyofundishwa imani ya kiristo. Na wewe nadhani ni hivyo hivyo unless uniambie wewe base ya idetity yako inaanzia kwenye dini. Itakuwa ajabu sana
c. uislam ni dhambi kutohukuhukumiwa kwa mujibu wa Qur'an sidhani kama ni dhambi kutokuhukumiwa kihaya??
Ndio imeshatolewa hoja kwa nn muendelee kutenda dhambi ya kutohukumiana kwa vgezo vya dini wakati sheria ya JMT kutambua ibada hiyo ipo. Mbona makundi mengine yanazo sheria hizo na yanatumika.
Kwenye makabia hakuna dhmabi dhambi ni dini .Huko wenye makabila kuna vitu wenyewe wanaita Mikosi. So ni kiasi cha muhusika kuamua tu sheria gani anaona itamtendea haki atumie. Kuna wajuro mzee mja alishiwa hata uzikwa kwa mwezi mzima sababu ya kesi kama hizi. Wazee wanataka mambo yaamuliwe kimila(kikabila) na mke anataka mambo yaamuliwe kwa taratibu za kiserikali.
Serikali Makini hawezi kufunga mlango wa kutoa haki kwa mujibu wa katiba ya JMT kama muhuska anaona mahakama ya kadhi au mahakama ya wajaruo au mahaama ya wahaya au mahakama ya wakristo haitmtendea haki.